Wanakiolojia wakichimba kwenye misingi ya maghofu ya monasteri huko Sweden
Barabara hii ya Pompei Italia ilifunikwa mwaka na majivu ya volkeno kwa muda wa miaka hadi kufunuliwa tena na wanakiolojia kuanzia
Arkiolojia kutoka Kiyunani zamani na neno usemi ni somo linalohusu mabaki ya tamaduni za watu wa nyakati zilizopita Waarkiolojia wanatafuta vitu vilivyobaki kwa mfano kwa kuchimba ardhi na kutafuta mabaki ya majengo makaburi silaha vifaa vyombo na mifupa ya watu

Tofauti na somo la Historia haichunguzi maandishi hasa ili kupata ufafanuzi juu ya mambo ya kale Historia ikiangalia habari arkiolojia huangalia vitu Waarkiolojia wanaweza kutumia maandishi na habari za historia wakiamua jinsi gani kuendelea na utafiti wao kwa mfano wachimbe wapi Lakini hutumia mitindo ya sayansi mbalimbali kuchunguza vitu vinavyopatikana kwa njia ya arkiolojia

Mfano bora wa arkiolojia ni utafiti wa mji wa Pompei huko Italia Habari za Pompei zimepatikana katika maandishi mbalimbali ya kiroma lakini mji uliharibika kabisa na kufunikwa na majivu ya volkeno Vesuvio mn mwaka bK Kuanzia mwaka wataalamu walianza kuchimba mahali pa mji mpotevu wakaipata Hadi leo sehemu kubwa ya mji umefunuliwa tena Chini ya majivu na udongo wa karne nyingi vitu vingi vimehifadhiwa vizuri ambavyo vingepotea kabisa visingefunikwa kwa mfano picha za kiroma kwenye kuta za nyumba zenye rangi nzuri kabisa Hata mabaki ya chakula yamepatikana yakachunguliwa

Afrika na Arkiolojia ujuzi wa arkiolojia ni muhimu sana kwa ajili ya historia ya Afrika Tamaduni nyingi za Afrika ziliendela bila maandishi hadi juzi au hata leo Habari zetu kuhusu utamaduni wa Zimbabwe Kuu au kuhusu uenezaji wa Wabantu hutegemea arkiolojia kwa kiasi kikubwa sana

Hivyo arkiolojia huongeza ujuzi wetu kwa kufunua ushahidi wa nyakati za kale wakati uleule kazi ya arkiolojia inahatarisha ushahidi huo kwa sababu kazi yake huondoa hifadhi ya udongo Katika karne za kwanza za arkiolojia mabaki mengi ya tamaduni za kale yameharibika kutokana na kufunuliwa kwao Kuepukana na tatizo hilo ni jukumu muhimu ya arkiolojia ya kisasa

The World Wide Web Library of African Archaeology Kiingereza

Sayansi

Daktari ma ni neno la asili ya Kilatini lililoingia Kiswahili kwa kupitia Kiingereza Hutumiwa na maana mbili

Mtaalamu aliyepata mafunzo maalum kwenye chuo kikuu ya kutibu maradhi au wagonjwa Mtu wenye ujuzi wa kutibu wanaitwa pia mganga wa tabibu ma

Kwa kufuata tabia za lugha nyingine daktari hutumiwa pia kama jina la heshima la mtu aliyepata shahada ya juu kabisa

Cheo

Historia ni somo kuhusu maisha ya binadamu na utamaduni wao wakati uliopita Mara nyingi neno historia pia ina maana ya maarifa yoyote kuhusu wakati uliopita yawe au yasiwe maarifa ya watu kwa mfano historia ya ulimwengu

Wanahistoria wanatoa maarifa yao kutoka maandiko ya zamani kutoka fasihi simulizi na kutoka akiolojia

Historia ya Afrika
Historia ya Amerika
Historia ya Australia
Historia ya Ulaya
Miaka
Vita



Kwa ujumla historia au tarehe ni kumbukumbu ya maisha ya mwanadamu duniani hasa ile tarehe iliyosajiliwa na kuhifadhiwa katika vitabu maandishi mbali mbali na simulizi au hekaya za mapokeo Ingawa historia iliyobebwa katika simulizi na hekaya huchukuliwa na baadhi kuwa haina nguvu kwa kukosa ithbati ya maandishi bado hivi ni vyanzo muhimu vya historia Mara nyingi historia iliyoko katika maandishi huwa imehifadhiwa katika simulizi na hekaya kwa muda mrefu kabla ya kuandikwa

Hapo kale bara la Afrika lilishuhudia matukio mengi ya harakati za mwanadamu kuliko mabara mengine ya ulimwengu Wataalamu wa athari wamegundua athari za binadamu zinazorudi nyuma kufikia hadi miaka milioni minne na athari za ustaarabu wa Wamisri huko Misri na Wafiniki huko Tunis na sehemu nyenginezo za Afrika ya Kaskazini katika karne ya tisa KK

Harakati za madola makubwa ya Warumi na Waarabu ziliweza kuonekana kabla ya karne ya nne BK na Waarabu walianza kuingia Afrika huko Habasha Ethiopia tangu karne ya saba BK na kutangaza dini yao na kuieneza katika maeneo mbali mbali ya Afrika pamoja na kuanzisha biashara na ustaarabu na utamaduni na kuimarisha mamlaka zao katika Sudan ya wakati huo tangu karne ya nane ya Kikristo

Himaya za Ghana Mali na Songhai zilikuwa zikijulikana kwa utajiri wao mkubwa na biashara stawi iliyokuwa ikifanyika wakati huo ya dhahabu na bidhaa nyinginezo Mwisho wa karne ya BK himaya ya Songhai ilikuwa na nguvu kuweza kuitia chini ya utawala wake mamlaka ya Mali Sehemu nyingine za kusini ya Afrika zilikuwa wakati huu hazijulikani sana na historia yake ilikuwa bado haijasajiliwa

Baina ya karne ya kwanza KK na karne ya kumi na sita BK Watu waliokuwa wakizungumza lugha ya Kibantu watokao sehemu za Nigeria na Cameroon ya leo ndio waliokuwa wameenea kwenye sehemu mbali mbali kusini mwa bara la Afrika wakiwa wameanzisha vijiji mashamba na mamlaka katika sehemu za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya leo za Luba na Mwememutapa lakini makundi ya wachungaji wanyama walianza kuhamia kusini katika karne za na na kukutana na Wabantu Ndipo walipoanzisha mamlaka zao za Bunyoro Buganda Rwanda na Ankole

Wazungu walianza kugundua bara la Afrika katika karne ya wakati Wareno walipokuja kwenye fukwe za bara la Afrika kutafuta njia nyepesi na ya amani ya kufikia India na kuweza kupata nafasi ya kushikilia biashara ya dhahabu na pembe na watumwa ambayo ilikuwa ikiendelea wakati huo katika bara la Afrika Katika mwaka Bartolomew Diaz alizunguka rasi ya matumaini mema cape of good hope na katika mwaka Vasco da Gama alifika ufukwe wa Afrika Mashariki na kuendelea mpaka India

Baada ya hapo Ureno alianzisha vituo vya biashara Afrika kufuatiwa na Waholanzi Waingereza Wafaransa na Wazungu wengineo na biashara ya Watumwa ikashika kani na kuwa na kasi na nguvu Wakati huu huu Waturuki walishikilia sehemu za kaskazini ya Afrika na Waomani wakashikilia ufukwe wa Afrika Mashariki Kati ya na Wazungu waliligawanya bara la Afrika baina yao na nchi zote zikawa chini ya utawala wa Wazungu isipokuwa Liberia na Ethiopia

Wafaransa wakachukuwa Afrika Magharibi na Kaskazini na kwa hivyo nchi za Afrika Magharibi Dahomey sasa Benin Guinea Mali Cote dIvoire Mauritania Niger Senegal na Upper Volta sasa Burkina Faso zilikuwa chini ya utawala wake Hali kadhalika Algeria Tunisia na Morocco zilitawaliwa na wao Aidha Wafaransa walitawala Togoland Somaliland Madagascar Comoro na Reunion

Waingereza nao wakatawala Afrika Mashariki na Kusini na kuwa sehemu ya Sudan na Somalia Uganda Kenya Tanzania chini ya jina la Tanganyika Zanzibar Nyasalanda Rhodesia Bechuanaland Basutoland na Swaziland chini ya utawala wao na baada ya kushinda katika vita huko Afrika ya Kusini walitawala Transvaal Orange Free State Cape Colony na Natal na huko Afrika ya Magharibi walitawala Gambia Sierra Leone the Gold Coast na Nigeria

Wareno wakachukuwa sehemu ya Guinea Angola na Mozambique na sehemu na visiwa fulani fulani huko Afrika ya Magharibi Wabelgiji wakachukuwa Kongo na RwandaUrundi na Wahispania wakachukuwa sehemu ya Guinea Spanish Sahara sasa Sahara ya Magharibina Ifni na sehemu fulani za Morocco Wajerumani nao wakachukuwa Togoland Cameroon na baadhi ya nchi katika Afrika ya Magharibi na Afrika ya Mashariki lakini baada ya vita vya kwanza vya dunia wakanyanganywa Wataliani wakachukuwa Libya Eritrea na sehemu ya Somaliland

Nchi ya kwanza kujitawala wenyewe katika Afrika ni nchi za Afrika ya Kusini zilizojiunga na kujiendesha wao wenyewe katika mwaka Misri katika mwaka wa walikuwa wanajiendesha wenyewe na Tangier katika mwaka wa Madola mengi ya Afrika yalianza kupigania uhuru katika miaka ya baina na na Wazungu wakasalimu amri na kuanza kutoa uhuru Libya wakajinyakulia uhuru katika mwaka wa Eritrea katika mwaka ikiwa imejiunga na Ethiopia Morocco katika mwaka wa na wakarudishiwa Tangier Katika mwaka huu wa Sudan na Tunisia vile vile walipata uhuru wao na Ghana katika mwaka wa Guinea katika mwaka wa na vile vile Morocco wakarudishiwa Spanish Morocco

Katika mwaka wa Ufaransa ukatoa uhuru kwa Cameroon the Central African Republic Chad Congo Brazzaville Cote dIvoire Dahomey Benin Gabon Madagascar Mali Mauritania Niger Senegal na Upper Volta Burkina Faso Vile vile katika mwaka huu huu wa Congo Kinshasa Nigeria Somalia na Togo zikapata uhuru wake na katika mwaka wa Sierra Leone na Tanganyika zikapata uhuru na Afrika ya Kusini ikawa Jamhuri Katika mwaka wa Algeria Burundi Rwanda na Uganda zikawa huru na zikafuatia Zanzibar Gambia na Kenya na katika mwaka wa Malawi Nyasaland na Zambia Rhodesia ya Kaskazini zikapata uhuru Baada ya miaka miwili katika mwaka wa Botswana Bechuanalandna Lesotho Basutoland zikajinyakulia uhuru Mauritius na Swaziland katika mwaka wa na vile vile Equitorial Guinea Uhispania ukairudisha Ifni katika mwaka wa katika mamlaka ya Morocco

Aidha katika mwaka wa Portuguese Guinea GuineaBissau ikapata uhuru wake na katika mwaka wa Angola Cape Verde Mozambique Sao Tome na Principe zikapata uhuru Uhispania vile vile ukaitoa Spanish Sahara Western Sahara na kuwapa Morocco na Mauritania katika mwaka wa lakini wananchi wa Sahara wakakataa kuwa chini ya nchi mbili hizi na kukazuka vita Mauritania ukaitoa sehemu yake na kuipa Morocco katika mwaka wa tatizo ambalo mpaka sasa linaendelea baina ya Morocco na Western Sahara na Umoja wa Mataifa unajaribu kutatua tatizo hili Waingereza wakawapa uhuru Seychelles katika mwaka wa na Ufaransa ukatoa uhuru kwa visiwa vya Ngazija Comoro

Katika mwaka wa Djibouti Afars na Issas iliyokuwa ikitawaliwa na Wafaransa ikarudi kwa wenyewe Rhodesia Zimbabwe ikapata uhuru katika mwaka wa na South West Africa iliyokuwa ikihukumiwa na Afrika ya Kusini ikapata uhuru katika mwaka na kuitwa Namibia
Ulaya Uingereza ukachukuwa visiwa vya St Helena na Ascension na Ufaransa ukaendelea kuhukumu Mayotte na Reunion Uhispania vile vile ukaendelea kutawala visiwa vya Canary na visiwa viwili vya Ceuta and Melilla vilivyoko karibu na Morocco vikabakia na Uhispania

Korotayev A Khaltourina D Introduction to Social Macrodynamics Secular Cycles and Millennial Trends in Africa Moscow URSS ISBN


Afrika

Hesabu ni somo linalohusika na idadi na jinsi tunavyoweza kuhesabu kwa kutumia kanuni zifuatazo Kujumlisha kutoa kuzidisha na kugawa

Hesabu ni sehemu ya hisabati

Hisabati

Jiografia ni somo la Dunia na vipengele vyake wakazi wake na maajabu yake Neno jiografia linatokana na maneno ya Kigiriki g Dunia na graphein kuandika Ina maana ya kuandika kuhusu Dunia Neno hili lilianza kutumiwa kwa mara ya kwanza na mwanasayansi mmoja aitwaye Eratosthenes KK

Sehemu za jiografia ni vitu kama mabara bahari mito na milima Wakazi wake ni watu wote na wanyama waishio juu yake Maajabu yake ni vitu vinavyotokea kama vile maji kujaa na kupwa upepo na tetemeko la ardhi

Burundi
Eritrea
Jibuti
Kenya
Komoro
Rwanda
Shelisheli
Somalia
Tanzania
Uganda
Uhabeshi Ethiopia

Gabon
Guinea ya Ikweta
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Zaire
Jamhuri ya Kongo
Kamerun
Sao Tome na Principe

Algeria
Libya
Misri
Moroko
Sahara ya Magharibi
Sudan
Tunisia

Angola
Botswana
Lesotho
Malawi
Mauritius
Msumbiji Mozambiki
Namibia
Afrika Kusini
Uswazi Swaziland
Zambia
Zimbabwe

Benin
Burkina Faso
Chadi
Cabo Verde
Ivory Coast
Gambia
Ghana
Guinea
Guinea Bisau
Liberia
Mali
Mauritania
Niger
Nigeria
Senegal
Sierra Leone
Togo

Kanada
Marekani au Maungano wa Madola ya Amerika
Meksiko au Maungano a Madola ya Mexiko

Belize
Guatemala
Honduras
El Salvador
Nikaragua
Kosta Rika
Panama
Meksiko mara nyingi huhesabiwa katika Amerika ya Kati kwa sababu za kiutamaduni

Antigua na Barbuda
Bahamas
Barbados
Dominica
Jamhuri ya Dominika
Grenada
Haiti
Jamaika
Kuba
Saint Kitts na Nevis
Saint Lucia
Saint Vincent na Grenadini

Argentina
Bolivia
Brazil
Chile
Ekuador
Guyana
Guyana ya Kifaransa
Kolombia
Paraguay
Peru
Surinam
Uruguay
Venezuela

Afghanistan
Kazakhstan
Kirgizistan
Mongolia
Tajikistan
Turkmenistan
Usbekistan

Siberia sehemu ya Urusi

Uchina pamoja na Taiwan
Japani
Korea Kaskazini
Korea Kusini

Brunei
Indonesia
Kamboja
Laos
Malaysia
Myanmar zamani iliitwa Burma
Philippines
Singapur
Thailand zamani iliitwa Siam
Timor Mashariki
Vietnam

Bangladesh
Bhutan
Uhindi au India
Maledivi
Nepal
Pakistan
Sri Lanka zamani iliitwa Ceylon

Armenia
Azerbaijan
Georgia
Irak
Israel
Yordani
Libanon
Palestina
Shamu au Syria
Uajemi au Iran au Persia
Uturuki

Bahrain
Kuwait
Muungano wa Falme za Kiarabu
Oman
Qatar
Saudia
Yemen

Jua
Utaridi Zebaki
Zuhura Ngandu
Dunia Ardhi
Mirihi Meriki Mars
Mshtarii Sumbula
Zohari Sarateni
Uranus
Neptun
Pluto

Nchi
Orodha ya nchi kufuatana na wakazi

Jiografia

Bendera ya Kiesperanto
Kiesperanto ni lugha ya kupangwa inayozungumzwa zaidi duniani kati ya lugha hizi Ilipangwa na Ludwik Lejzer Zamenhof myahudi aliyetoka mjini Biaystok nchini Urusi siku hizi ni sehemu ya nchi ya Poland Alitoa kitabu cha kwanza cha lugha hii mwaka baada ya kuitengeneza kwa miaka karibu kumi Nia yake ilikuwa kutengeneza lugha rahisi ili iwe lugha saidizi ya kimataifa lugha ya pili kwa kila mtu duniani Waesperanto wengine bado wanataka hiyo lakini wengine wanapenda kuitumia tu bila nia ya kuieneza duniani kote

Waesperanto wanakitumia Kiesperanto kwa ajili ya kukutana na wageni na kujifunza kuhusu nchi na tamaduni nyingine Siku hizi maelfu ya watu wanaitumia mara kwa mara ili kuwasiliana na watu popote duniani

Chunguzi za kitaalamu zimeonyesha kwamba Kiesperanto kinaweza kujifunzwa rahisi zaidi sana kuliko lugha asilia na pia kwamba kujifunza Kiesperanto kwanza kunarahisisha kujifunza kwa lugha nyingine

Kwa kuwa lugha ya kupangwa Kiesperanto hakiko katika familia yoyote a lugha Maneno yake yanatoka hasa lugha za Kirumi kama Kifaransa na Kilatini lakini pia lugha za Kigermaniki kama Kiingereza na Kijerumani na lugha za Kislavoni kama Kirusi na Kipolandi Maneno mengi yanaumbwa kwa kuunganisha mzizi wa neno moja na viambishi au kwa kuunganisha mizizi ya maneno mbalimbali Kwa mfano kuna kiambishi awali mal inayoonyesha kinyume bona ni zuri na malbona ni baya Kwa hiyo inawezekana kusema mambo mengi baada ya kujifunza maneno machache tu

Katika Kiesperanto kuna harufi na kuna sauti Kila harufi inaweza kutamka kwa sauti moja tu na kila sauti inaandikwa kwa serufi moja tu Harufi za Kiesperanto ni zifuatazo

a b c d e f g h i j k l m n o p r s t u v z

Irabu zote a e i o u zinatamka kama kwa Kiswahili

Kwa upande wa konsonanti b d f g h k l m n p r s t v na z zinatamka kama kwa Kiswahili c inatamka kama ts inatamka kama ch Matamshi ya yanafanana na matamshi ya j kwa Kiswahili ni sawasawa na matamshi ya j kwa Kiingereza inatamka kama j ya Kifaransa inafanana na sh ya Kiswahili lakini inatamka na sauti kama z inatamka kama sh inatamka kama w inatumika baada ya a na e tu tofauti kati ya au na a ni kwamba au inatamka kwa silabi mbili na a kwa silabi moja

Nomino majina zote zinahitimu kwa kiambishi tawali o kwa mfano arbo mti Wingi wa nomino unahitimu kwa oj arboj miti

Vivumishi vinahitimu kwa kiambishi tawali a kwa mfano alta refu Vivumishi kwa kawaida vinawekwa kabla ya nomino inayohusu lakini pia inaweza kuwa baada yake Wingi pia unaonyeshwa katika vivumishi kwa harufi j altaj arboj miti mirefu

Vitenzi vina viambishi tamati mbalimbali
i inatumika kwa vitenzijina kwa mfano fari kufanya
as inatumika kwa njeo ya wakati uliopo kwa mfano mi faras ninafanya
is inatumika kwa njeo ya wakati uliopita kwa mfano mi faris nilifanya au nimefanya
os inatumika kwa njeo ya wakati ujao kwa mfano mi faros nitafanya
us inatumika kwa hali a masharti kwa mfano mi farus ningefanya
u inatumika kwa hali ya kuamuru kwa mfano faru fanya li faru afanye

Maelezo mengine kuhusu Kiesperanto
Jifunze Kiesperanto
Tangazo la Praha la jamii ya kiesperanto
TANGAZO LA PRAHA LA JAMII YA KIESPERANTO Worddoc
esperantoafrikoorg
Jifunze lugha ya Kiesperanto

Lugha

Lugha ya kuundwa au lugha unde ni lugha ambayo msamiati na sarufi zake zimetungwa na watu badala ya kukua kama sehemu ya utamaduni wa umma fulani Kwa kawaida zinaundwa kwa ajili ya kuwasiliana kati ya watu sawasawa na lugha asilia Nyingi zinatengenezwa ili kuwa lugha saidizi za kimataifa lakini nyingine zinaundwa kwa ajili ya usiri au majaribio ya isimu au bila sababu fulani

Lugha ya kuundwa inayozungumzwa zaidi ni Kiesperanto

Mara chache lugha ya kuundwa maana yake ni lugha za kompyuta au za kuandaa programu angalia lugha asilia Kwa sababu ya utata huo watu wengi hasa Waesperanto hawapendi kutumia neno lugha ya kuundwa na badala yake wanasema lugha ya kupangwa Lakini msemo lugha ya kupangwa unatumika kwa lugha zile tu ambazo ziliungwa kwa ajili ya utumiaji wa kawaida baina ya watu

TUKI Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Massamba David Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Lugha
Isimu

Lugha kar ni utaratibu kwa ajili ya kuwasiliana kati ya binadamu au kati ya viumbe vyovyote venye akili

Mwaka wa ulikuwa Mwaka wa Lugha wa Kimataifa

Somo la lugha linaitwa maarifa ya lugha au isimu

Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zilizokua katika mpango maalum na zilizokubaliwa na jamii ya watu fulani ili zitumike katika mawasiliano

Mara chache neno lugha linatumika kwa taratibu za kuwasiliana za wanyama Lakini taratibu hizo ni tofauti sana Katika lugha za wanyama sauti moja ina maana moja tu Lakini katika lugha za binadamu sauti nyingi zinaunganishwa kutengeneza maneno na maneno mengi yanaunganishwa kutengeneza sentensi Hivyo mnyama ambaye anaweza kutengeneza sauti ishirini tofauti anaweza kusema mambo ishirini tu Kwa upande mwingine mtu ambaye anaweza kutengeneza sauti ishirini anaweza kusema mambo zaidi ya millioni

Kwa kawaida lugha ni sehemu ya utamaduni wa umma fulani Lugha ya aina hii inaitwa lugha asilia Lakini pia kuna lugha za kuundwa

Tangu siku za kwanza za binadamu lugha zimekuwa zikichipuka na kukuwa na kutangaa na kufa kama kiumbe chochote mwingine Kwa hivyo lugha zilizokuwepo leo ulimwenguni huenda baada ya karne nyingi kupita zikatoweka na kuzuka nyenginezo

Leo ulimwenguni mathalan kuna lugha karibu zikiwa katika bara la kaskazini na kusini ya Marekani zikiwa kwenye bara la Afrika katika bara la Ulaya katika bara la Asia na katika bara la Oshania Australia na nchi jirani nayo

Lugha ya Kiarabu
Lugha ya Kiesperanto
Lugha ya Kiingereza
Lugha ya Kiswahili
Lugha asilia
Lugha ya kuundwa

Lango la lugha

Mara nyingi lugha asilia maana yake ni lugha yoyote ambayo inaweza kuzungumzwa na watu na lugha za kompyuta na za kuandaa programu zinaitwa lugha za kuundwa

Lugha

Sayansi ni maarifa yanayopatikana kwa kufanya vitendo kutazama na kujaribu kweli zilizo bainishwa pasi kuthibitishwa

Kufikia kati kati ya Karne ya binadamu ameweza kukua kisayansi na hivyo kuvumbua tekinolojia zilizomwezesha kuruka na kuelea anga za juu kabisa za Dunia kwa mara ya kwanza na kuchunguza spezi

Kuna sayansi mbalimbali ambazo huainishwa katika

Sayansi Asili km
Biolojia
Jiografia
Zoolojia

Sayansi Umbile km
Fizikia
Hisabati
Kemia

Sayansi Jamii km
Arkiolojia
Elimu
Saikolojia
Siasa

Sayansi Tumizi km
Teknolojia
Uhandisi

Pia kuna sayansi zinahusu mada mbalimbali
Maarifa
Unajimu
Tiba

Msingi wa sayansi ni vitendo

Vitendo vya Kisayansi vina njia zake zinazotumikia kusimamisha kweli ya kisayansi

Namna ya kueleza jambo kisayansi huchimbuka toka Nadharia ama Udhanifu Halafu tena ili Kweli ikubalike hutoka kwenye udhanifu kwa kupitia kupitia majaribio rasmi hutengeneza dhana kamili ama nadharia kama ni shauri la kueleza mwenendo na tabia

Kwa hivyo asili ya njia ya kisayansi ni mtazamo unaokwenda sambamba na vitendo vinavyochunguzwa Kutoka mitazamo wanasayansi wanaumba nadharia Baadaye wanaangalia kama bashiri za nadharia ni kweli Isipokuwa kweli watakanusha nadharia hii Ikionekana kwamba mara nyingi sana nadharia ilibashiri ukweli na haijakosea itakuwa ni nadharia inayokubalika

Sayansi siku zote hutafuta kuongeza uelewa na kadri inavyowezekana uwezekano wa kumudu vipengele maalum vya Ulimwengu wa maumbile Mafanikio yake katika kufikia hapa hutoka katika shina la moja kwa moja tokea uwezo wake kuweka wazi misingi ya makanika ambayo hali asilia huchakata Hapa picha ya Mwako wa kibayo Bosheni ambao umekachiwa katika zao la tumbaku kwa kutumia Uhandisi ginetiki

Mara chache maarifa yatokanayo na sayansi yanaweza kuwa pingifu ya Hali ya kawaida Kwa mfano nadharia ya atomu inasema kwamba katika Jiwe Maada Yabisi kuna uvungu dutu tupu na kwamba atomi zinacheza katika nafasi ndogo katika jiwe ukifananisha na maada kimiminika Lakini kwa nadharia hii tunaweza kueleza mambo mengi hata kwa nini tunaweza kusema kwamba jiwe halina uvungu

Sayansi iliaanza kama udadisi wa mtu mmoja mmoja lakini kadri maarifa yanavyopanuka inakuwa vigumu kwa mtu mmoja kufanya mchango wakujitenga hivyo jumuiya zimebeba kusudi ambalo hapo mwanzo ilionekana kama ni shauku la mtu mmoja mmoja kama awali

Hii hufanya mkururo wa ugunduzi ama uvumbuzi kuwa ni sehemu ya historia ya Sayansi Majina na sifa kutajwa sambamba na shauri la aliyepelekea

Sayansi na Jamii huenda pamoja katika kuleta mabadiliko kwa kuwa mabadiliko huletwa na watu wenyewe

Katika dunia hii ya leo maendeleo ya watu hujidhihirisha sana kutokana na jinsi jamii husika ilivyopiga teke katika uwanja huu

Ingawaje haibanishwi wazi miongoni mwa sura ya mambo ya kidunia sayansi kwa kweli ni nguvu inayoweza kubadili maisha ya watu kwa wema lakini katika kilele chake cha mafanikio vyombo vyenye nguvu kimamlaka na fedha hushikilia baadhi ya matunda yake katika hali ya kibiashara na kiutawala zaidi

Wapo watu pia ambao hutumia sayansi kujaribu kuboresha maisha ya watu wote kwa ujumla Hivyo sayansi haibakii tu kuwa mikononi mwa wenye kushika dau kimifumo bali changamoto ya wote wenye kutaka kuleta maendeleo ya ujumla

Na hivyo roho ya uchunguzi ndio iliyoleta kuzaliwa kukua na kutapakaa kwa sayansi

Sayansi

Mwanamke wa Haki ni ishara ya idara ya sheria Haki inaonyeshwa kama mungu jike ambaye anabeba ishara tatu za utawala wa kisheria upanga unaoashiria nguvu ya mahakama mizani zinazoashiria upimaji wa madai yanayoshindana na kitambaa kinachofunika macho kuashiria kutofanya upendeleo

Sheria ni mfumo wa kanuni ambazo kwa kawaida hutekelezwa kupitia seti ya taasisi Inaunda siasa uchumi na jamii kwa njia mbalimbali na huratibu mahusiano baina ya watu

Sheria ya mkataba huongoza kila kitu kuanzia kununua tiketi ya basi hadi biashara katika masoko

Sheria ya mali inafafanua haki na wajibu unaohusiana na uhamisho wa jina la kibinafsi na mali ya kweli

Sheria ya Hifadhi inatumika kwa mali yanayotumika kwa uwekezaji na usalama wa kifedha huku sheria ya kukiuka wajibu inaruhusu madai ya fidia ikiwa haki au mali za mtu zinafanyiwa madhara

Ikiwa madhara ni kinyume cha sheria sheria ya jinai inatoa mbinu zinazoweza kutumiwa na taifa ili kumshataki mhusika

Sheria ya kikatiba inatoa utaratibu wa utungaji wa sheria ulinzi wa haki za kibinadamu na uchaguzi wa wawakilishi wa kisiasa

Sheria ya utawala inatumika kuangalia upya maamuzi ya vyombo vya kiserikali huku sheria ya kimataifa inatawala shughuli baina ya nchi huru katika zinazohusu mambo kama vile biashara vikwazo vya kimazingira na hatua za kijeshi

Akiandika mnamo KK mwanafalsafa wa Ugiriki ya Kale Aristotle alisema Utawala wa sheria ni bora kuliko utawala wa mtu yeyote binafsi

Mifumo ya kisheria inaelezea haki na majukumu kwa njia mbalimbali Tofauti ya jumla inaweza kufanywa kati ya maeneo yanayotawaliwa na mfumo wa sheria ya kiraia ambayo huandika sheria zao na yale yanayofuata sheria za kawaida ambapo sheria haijaundwa kwa utaratibu maalumu Katika baadhi ya nchi sheria ya dini bado hutumika kama sheria maalum Sheria ni chanzo kikuu cha uchunguzi wa kitaalam wa historia ya sheria falsafa ya sheria uchambuzi wa kiuchumi wa sheria au somo la kijamii kuhusu sheria

Sheria pia huibua masuala muhimu na magumu kuhusu usawa uadilifu na haki Katika usawa wake wa ajabu alisema mwandishi Anatole France mnamo mwaka sheria inakataza matajiri na mafukura kulala chini ya madaraja kuombaomba barabarani na kuiba mikate Katika demokrasia ya kawaida taasisi za msingi za kutafsiri na kuunda sheria ni matawi matatu makuu ya utawala ambayo ni mahakama isiyo na upendeleo bunge na serikali yenye kuwajibika

Ili kutekeleza na kutumia nguvu za kufanya sheria ifuatwe na kutoa huduma kwa umma urasimu wa serikali jeshi na polisi ni muhimu Vyombo hivyo vyote vya dola viliundwa na kutawaliwa na sheria taaluma ya kisheria iliyo huru na jamii yenye bidii zinajulisha na kusaidia maendeleo

Mifumo yote ya kisheria inahusu na mwaswala ya kimsingi lakini kila taifa inaainisha na kubainisha masomo yake ya kisheria kwa njia mbalimbali Tofauti ya kawaida ni kuwa sheria ya umma maneno yanayohusika kwa karibu na taifa na kuhusisha sheria ya kikatiba kitawala na ya jinai na sheria ya kibinfasi inayohusisha mkataba sheria ya kukiuka wajibu na mali Katikamifumo ya sheria ya kirai mkataba na kukiuka wajibu zinapatikana chini ya sheria ya majukumu huku sheria ya hifadhi inapatikana chini ya serkali za halali au mikataba ya kimataifa Sheria ya Kimataifa kikatiba kitawala jinai mkataba kukiuka wajibu na mali na hifadhi zinatambulika kama masomo msingi ya jadi ingawa kuna masomo zaidi ambayo yanaweza kuwa na umuhimu mkubwa zaidi wa kiutendaji

Ikitoa katiba ya sheria ya kimataifa ya umaa mfumo wa Umoja wa Mataifa ulikubaliwa wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia

Sheria ya kimataifa inaweza kuashiria mambo matatu sheria ya umma ya kimataifa sheria ya kibinafsi ya kimataifa au mgongano wa sheria na sheria ya mashirika makubwa ya kimataifa

Sheria ya Umma ya Kimataifa inajihusisha na uhusiano kati ya mataifa uhuru Vyanzo vya maendeleo ya sheria ya umma ya kimataifa ni desturi mwenendo na mikataba kati ya nchi huru Mikataba ya Geneva Sheria ya umma ya kimataifa inaweza kutengezwa na mashirika ya kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa ambao ilianzishwa baada ya kushindwa kwa Shirikisho la Kimataifa kuzuia Vita vya Vikuu vya Pili vya Dunia Shirika la Kimataifa la Ajira Shirika la Kimataifa la Biashara au Shirika la Fedha la Kimataifa Sheria ya kimatifa ya umma ina hadhi maalum kama sheria kwa sababu hakuna kikozi cha kimataifa cha polisi na mahakama kama vile Mahakama ya Kimataifa ya Haki kama tawi la kimsingi la Umoja wa Mataifa la mahakama halina uwezo wa kuadhibu kutokutii Hata hivyo miili michache kama vile WTO ina mifumo yenye ufanisi ya utatuzi wa kudumu na utatuzi wa mogogoro inayoambatana na vikwazo vya kibiashara

Mgongano wa sheria au sheria ya kibinafsi ya kimataifa katika nchi za sheria ya kiraia unahusisha maeneo ya kimamlaka ya kisheria ya mgogoro wa kisheria baina ya watu wa kibinafsi unafaa kusikizwa na sheria za maeneo gani ya kimamlaka ya kisheria ndiyo inayofaa kutumikaLeo biashra zinazidi kuwa na uwezo wa kusongeza minyororo ya ugavi ya mtaji na ajira kuvuka mipaka na pia kufanya biashara na kampuni za nchi za ngambo hivyo kulifanya swali kuhusu nchi ipi ndiyo inayomamlaka ya kisheria kuwa muhimu zaidi Idadi kubwa zaidi ya biashara zinachagua usuluhishi wa kibiashara chini ya Mkataba wa New York wa mnamo mwaka

Sheria ya Umoja wa Ulaya ndiyo ya kwanza kufikia sasa ambayo ni mfano wa mfano wa sheria kuu ya kimataifa Kutokana na mwenendo wa kuongezeka kwa ushirikiano wa kiuchumi Duniani mikataba mingi ya kikandahasa ya Umoja wa Nchi za Marekani ya Kusinizimeanza kuufuata mfano kama huu Katika Umoja wa Ulaya nchi huru zimekusanya mamlaka yao katika mfumo wa mahakama na taasisi za kisiasa Taasisi hizi zinapewa uwezo wa kutekeleza kanuni za kisheria dhidi ya au kwa nchi wanachama na raia katika namna ambayo haiwezekani kupitia sheria ya umma ya kimataifa Kama Mahakama ya Ulaya ya Haki yalivyosema katika miaka ya sheria ya Umoja wa Umoja wa Ulaya hujumiusha muundo mpya wa sheria ya kimataifa kwa ajili ya faida inayotegemeana ya kijamii na kiuchumi wa nchi zote wanachama

Azimio la Haki za Kibinadamu na za Raia ambalo kanuni zake bado zini thamani ya kikatiba

Sheria ya kikatiba na kiutawala zinasimamia mambo ya nchi Sheria ya kikatiba inahusisha uhusiano baina ya serikali bunge na mahakama na haki za kibinadamu au uhuru wa kiraia wa watu binafsi dhidi ya nchi Maeneo mengi ya kisheria kama vile Marekani na Ufaransa zina katiba moja iliyoandikwa kwa makini iliyo na Muswada wa Haki Katiba chache kama vile Uingereza hazina hati kama hiyoKatiba kwa ufupi ni zile sheria ambazo zinajumuisha mwili wa kisiasa kutoka kanuni sheria za uamuzi na mkataba Kesi kwa jina Entick dhidi ya Carrington ilionyesha wazi kanuni ya kikatiba inayotokana na sheria ya kawaifa Nyumba ya Bwana Entick ilifanyiwa upekekuzi na Afisa mmoja wa polisi aliyeitwa Carrington Wakati Bwana Entick alipolalamika mbele ya mahakama Afisa Carrington alidokeza kwamba kibali kutoka waziri wa Serikali Ali wa Halifax kilikuwa na mamlaka halali Hata hivyo hakukuwa na sheria iliyoandikwa au mamlaka ya kimahakama ambayo yalitoa uwezo huoHakimu mkuu Bwana Camden alisema

Mwisho mkubwa ambao ulifanya watu kuingia katika jamii ilikuwa kupata mali Haki hiyo imetunzwa na ni takatifu na haiwezi kuondolewa wakati wowote ambapo haijaondolewa au kufupishwa na sheria fulani ya umma kwa manufaa ya woteHakuna sababau inayoweza kupatikana au kutolewa kimya cha vitabu ni mamlaka dhidi ya mshtakiwa na aliyeathiriwa lazima atendewe haki

Kanuni ya kimsingi ya kikatiba ilitokana na John Locke inadokeza ya kwamba mtu binafsi anaweza kufanya isipokuwa kile ambacho kimekataliwa kisheria Sheria ya utawala ndiyo mbinu msingi ya kufanya mashirika ya umma yawajibike Watu wanaweza kutumia mapitio ya kimahakama kwa matendo au uamuzi uliofanywa na za halmashauri za mitaa huduma za umma au wizara za serikali kuhakikisha kuwa zinazingatia sheria Mahakama ya kwanza ya maalum ya kiutawala yalikuwa mahakama ya Conseil dtat yaliyoundwa mnamo mwaka wa wakati Napoleon alipochukua mamlaka nchini Ufaransa

Sheria ya jinai inayojulikana pia kama sheria ya kuadhibu inahusisha makosa na adhabu Kwa hivyo inapima ufafanuzi wa adhabu ya makosa yaliyopatikana kuwa na madhara yanaonekana kuwa na uwezo wa kusababisha uharibifu lakini kwa undani haifanyi uamuzi wa kimaadili kumhusu mkosaji wala kuwekea jamii vikwazo ambavyo vinakataza watu kimwili wasifanye makoa mwanzoni Investigating apprehending charging and trying suspected offenders is regulated by the law of criminal procedure Kesi ya kidhana ya uhalifu inatokana na ushahidi kuzidi shaka ya kuridhisha kuwa mtu ana hatia ya mambo mawili Kwanza mshtakiwa lazima awe amefanya kitendo ambacho kinatazamwa na jamii kuwa hatia au actus reus kitendo cha hatia Pili lazima mshtakiwa awe na dhamira ya kufanya uharibifu ya kufanya kitendoo fulani cha jinai au mens rea akili ya hatia Hata hivyo kwa kile kinachojulikana kama hatia za dhima kali actus reus haitoshi Mifumo ya jinai ya utamaduni wa sheria ya raia zinatofautisha kati ya nia katika dhana pana dolus directus na dolus eventualis na uzembe Uzembe hauna jukumu la jinai isipokuwa ambapo hatia fulani una adhabu yake maalum

Picha inayoonyesha kesi ya uhalifu kwa sababu ya uchawi katika eneo la Salem
Mifano ya uhalifu ni mauaji kushambulia udanganyifu na wizi Katika mifano maalum utetezi unaweza kutumika kwa vitendo maalum kama zile kuuwa ili utetezi wa kibinafasi au katika nyakati maalum kujitetea kuwa wazimu Mfano mwingine ni katika kesi ya karne ya ya Jamhuri dhidi ya Dudley na Stephens iliyopima utetezi wa kimahitaji Meli ya Mignonette iliyokuwa ikisafiri kutoka mji wa Southampton kuelekea mji wa Sydney ilizama Wafanyikazi watatu wa meli hiyo na Richard Parker kijana aliyekuwa na umri wa miaka walibaki katika meli iliyoundwa na vijiti Walikuwa na njaa na kijana yule alikuwa karibu kufa Kwa sababu ya kuwa na njaa iliyokithiri wafanyikazi hao walimuuwa kijana yule na kumla Wafanyikazi hao waliokolewa lakini wakafikishwa mahakamani huku wakiwa na hatia ya mauaji Walijitetea kwa kusema kwamba ilihitajika kwa lazima kwa wao kumuuwa kijana yule ili kuyaokoa maisha yao Bwana Coleridge akieleza kukataa kukubwa aliamua kuhifadhi maisha ya kibinafsi ni kwa kuzungumza kijumla wajibu lakini inaweza kuwa jukumu kuu kuyatoa maisha hayo kama kafara Wanaume hao walihukumiwa nyonga lakini maoni ya umma uliunga mkono haki ya wafanyikazi wale wa meli kuyaokoa maisha yao Mwishowe Ufalme ulipunguza hukumu zao hadi miezi sita gerezani

Makosa ya jinai yanatambulika si tu kama makosa dhidi ya waathirika binafsi lakini jamii pia Katika ngazi ya kimataifa nchi wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ambayo ilianzishwa kuwahukumu watu kwa hatia dhidi ya ubinadamu

Tangazo maarufu la kampuni ya Carbolic Smoke Ball lidai kuwa lingeweza kutibu homa Mahakama yaliamua kuwa tangazo hilo lilikuwa mkataba wa mtu yeyote

Sheria ya mkataba inahusu ahadi zinazowezwa kutendwa na inaweza kuandikwa kwa ufupi katika maneno ya Kilatinipacta sunt servanda ahadi lazima zitimizwe Katika maeneo ya kimamlaka ya sheria ya kawaida vipengele vitatu muhimu kuhusu utengenezaji wa mkataba vinahitajika kutoa na kukubali kutilia maanani na nia ya kutengeneza uhusiano wa kisheriaKatika kesi ya Carlill shisi ya Kampuni ya Carbolic Smoke Ball kampuni ya matibabu ilitangaza kuwa dawa yake mpya ya ajabu smokeball ingewatibu watu kutokana na mafua na ikiwa haingefaulu kuwatibu wanunuzi wangepata Watu wengi waliwasilisha kesi mahakamani ili wapate zao wakati dawa hiyo iliposhindwa kuwatibu Ikiogopa kufilisika Kampuni ya Carbolic ilijitetea kwa kusema kuwa tangazo lile lilikuwa mzaha tu na kwa hivyo halikuwa toleo lenye nguvu za kisheria Lilikuwa karibisho mchezo tu Lakini mahakama ya rufaa yaliamua kuwa kwa mtu mwenye kufikiria kwa kawaida kampuni ya Carbolic ilikuwa imefanya toleo Watu walikuwa wametoa kusudi la kununua bidhaa ile kwa kupitia shida bayana ya kutumia bidhaa yenye hitilafu Soma tangazo vile utakavyo na ulibadilishe tangazo hilo vile utakavyo alisema Hakimu Lindley haa kuna ahadi maalum ilitajwa katika lugha isyokuwa na utata wowote

Kutilia maanani knaonyesha ukweli kwamba vyama vyote katika mkataba vimebadilisha kitu fulani chenye maana Baadhi ya mifumo ya sheria ya kawaida ikiwemo Australi zinasonga mbali kutoka dhana ya kutilia maanani kama mojawapo ya mahitaji ya mkataba Dhana ya estoppel au culpa in contrahendo inaweza kutumika kuunda wajibu wakati mazungumzo kabla ya kuingia mkataba Katika maeneo ya kisheria ya kiraia kutilia maanani si lazima kwa mkataba kuwa na nguvu ya kisheria Nchini Ufaransa mkataba wa kawaida unasemekana kutokea ambapo kukutana kwa akili au kwa kuwa na nia zinazowiana Ujerumani ina mtazamio maalum kuhusu mikataba ambayo inayusisha sheria ya mali Kanuni ya dhana ya kiakili Abstraktionsprinzip wanayoitumia inamaanisha kuwa wajibu wa kibinafsi wa mkataba unaundwa kando na jina la mwenye mali yanayokabidhiwa Wakati ambapo mikataba inavunjwa kwa sababu fulani kwa mfano mnunuzi wa gari amelewa kiasi kwamba hana uwezo wa kisheria wa kufanya mkataba Wajibu wa kimkataba wa kulipa unaweza kuvunjwa tofauti na jina la mwenye gari Sheria ya kutajirika kusio kwa haki badala ya sheria tya mkataba basi inatumika kurudisha jina kwa mmiliki halali

Kesi ya McLibel Wahusika hawa wawili walifanya kesi ndefu zaidi katika historia ya Uingereza kwa uchapishaji wa kijikaratasi kilichokosoa mikahawa ya McDonalds

Sheria ya ukiukaji wa wajibu ambayo wakati mwingine huitwa kosa la jinai ni makosa ya raia Kuwa na kosa la ukiukaji wa wajibu mtu lazima awe amekiuka wajibu aliukwa anafaa kumtendea mty mwingine au kukiuka haki fulani ya awali ya kisheria mfano unaweza kuwa kumgonga mtu kimakosa na mpira wa mchezo wa kriketi Chini ya sheria ya uzembe ambayo ndiyo aina ya ukiukaji wa wajibu maarufu zaidi mtu aliyepatwa na madhara anaweza kuomba fidia kwa ya majeraha yake kutoka kwa mtu mwenye uwajibikaji Kanuni za uzembe zinaonyeshwa na kesi ya Donoghue dhidi ya Stevenson Rafiki mmoja wa Bi Donoghue aliagiza chupa isiyopenyeka nuru la pombe ya tangawizi iliyokusudiwa kutumika na Bi Donoghue katika mkahawa katika eneo la Paisley Baada ya kunya kunya nusu ya bia ile Bi Donoghue alimimina iliyosalia katika bilauri Mabaki yaliyooza ya konokono yalielea juu ya pombe Alidai kuwa alipigwa na bumbuwazi na kupata ugonjwa wa kuchomeka ndani ya matumbo na ilimbidi kumpeleka mtengenezaji pombe kwa kuruhusu kinywaji kuchafuka ovyo Nyumba ya Mabwana iliamua kwamba mtengezaji pombe aliwajibika kwa ugonjwa wa Bi Donoghue Bwana Atkin alikuwa na mtazamo maalum wa kimaadili na akasema

Dhima ya upuuzaji bila shaka ina msingi wake katika mawazo ya kijumla ya umma kuhusu makosa ya kimaadili amabyo mkosaji lazima alipe Kanuni ya kuwa unafaa kumpenda adui yako kisheria inakuwa haufai kumjeruhi jirani yako na swali la wakili nani ndiye jirani yangu linapokea jibu lenye vikwazo Lazima uwe na uwangalifu wa kuepuka na vitendo au visa ambapo hautendi lolote inapofaa ambavyo unaweza kutazamia kuwa vikamjeruhi jirani yako

Huu ulikuwa msingi wa kanuni nne za upuuzaji Bwana Stevenson alimdai Bi Donoghue wajibu wa kujali wa kuuza vinywaji salama yeye alivunja wajibu wake wa kujali madhara hayangefanyika isipokuwa kwa kuvunja kwake kwa wajibu wa kujali na tendo lake lilikuwa sababau ya karibu au haikuwa tokeo la mbali la madhara yaliyompata mtu fulani Chini ya dai la kero kelele hiyo inaweza kukomeshwa Ukiukaji wa wajibu pia inaweza kuhusisha vitendo vya kimakusudi kama vile ushambulizi vita au kuvuka na kuingia katka maeneo yaliyopigwa marufuku Sheria ya ukiukaji wa wajibu inayofahamika vyema ni ile ya kumharibia mtu jina ambayo inafanyika kwa mfano wakati gazeti linapochapisha madai yasiyokuwa na msingi ambayo yanaharibu sifa ya mwanasiasa fulani Ukiukaji wa wajibu ambao ni mbaya zaidi ni zile wa kiuchumi ambao huwa msingi wa sheria ya ajira katika baadhi ya nchi kwa kufanya vyama vya kibiashara kuwa na dhima kwa sababu ya migomo Wakati ambapo amri ya kisheria haipatiani kinga

Picha ya Bubujiko la Bahari ya Kusini mojawapo ya majanga ya kiuchumi yalilotokana na uvumi Janga hilo la kiuchumi lilisababisha kuundwa kwa kanuni kali kuhusu uuzaji wa hisa

Sheria ya Mali inatawala vitu vya thamani ambavyo watu huvitambua kama vyao Mali ya kweli wakati mwingine huitwa mali isiyohamishika inahusu umiliki wa ardhi na vitu vilivyojikita katika ardhi hiyo Mali ya kibinafsi inaashiria mambo mengineyo vyombo vinavyowezwa kusongeshwa kama vile tarakilishi magari mapambo na mikate au turathi haki kama vile akiba na hisa Haki ya in rem ni haki ya kipande maalum cha mali ikitofautishwa na haki in personam ambayo inaruhusu fidia kwa hasara lakini si kwa kurudishiwa kitu fulani Sheria ya ardhi inajumuisha msingi wa aina nyingi za sheria za mali na ndiyo ngumu zaidi Inahusisha mogeji mikataba ya kukodisha leseni maagano ruhusa na mifumo ya kisheria kwa usajili wa ardhi Kanuni kuhusu matumizi ya ardhi ya kibinafsi chini ya haki miliki sheria ya kampuni hifadhi na sheria ya biashara Mfano wa kesi msingi ya ya sheria nyingii za mali ni Armory v Delamirie Kijana wa kufagia chimni alipata pambo lenye mawe ya thamani Alichukua pambo lile kwa muundaji wa vifaa vya dhahabu ili thamani yake ikadiriwe Mwanafunzi wa muundaji wa vifaa vya dhahabu aliangalia pambo lile akaiba mawe yale ya thamani ma kumuambia kijana yule kuwa thamani yake ilkuwa nusu peni tatu na kuwa angeinunua Kijana yule alimwambia kuwa angepenga arudishiwe pambo lile kwa hivyo mwanafunzi wa muundaji vifaa alimrudishia pambo lakini bila mawe yale ya thamani Kijana yule alimpeleka mtengenezaji wa vifaa vya dhahabu kotini kwa jaribio la mwanafunzi wake kumdanganya Bwana Hakimu Mkuu Pratt aliamua kuwa ingawa kijana hangesemekana kuwa mumiliki wa pambo lile angefaa kutazamwa kama mpataji aliyefaa mpataji muwekaji hadi mumiliki wa kiasili anapopatikana Kwa kweli mwanafunzi na kijana yule wote walikuwa na haki ya umiliki wa pambo lile dhana ya kiufundi inayomaanisha kuwa kitu fulani kingeweza kumilikiwa na mtu fulani lakini nia ya kijana yule ya kumiliki ilitazamiwa kuwa bora zaidi kwa sababu ingeweza kudhihirishwa kuwa ya kwanza katika wakati Umiliki unaweza kuwa sehemu tisa kwa kumi ya sheri lakini si yote

Kesi hii hutumika kudhihirisha mtazamo wa mali katika maeneo ya kisheria ya kawaida kuwa mtu anayeweza kuonyesha dai bora zaidi la kipande cha mali dhidi ya chama kingine ndiye mumiliki Kwa kulinganisha mbinu ya kiklasiki ya sheria ya raia kuhusu mali iliendelezwa na Friedrich Carl von Savigny ni kuwa ni haki nzuri dhidi ya Ulimwengu Wajibu kama mkataba na ukiukaji wa wajibu hutazamwa kama haki nzuri dhidi ya watu binafsi Dhana ya mali inaibua maswala mengi zaidi ya kifalsafa na kisiasa Locke alidokeza kwamba maisha uhuru na nyumba zetu ni mali yetu kwa sababu tunamiliki mali yetu na tunachangayana ajira yetu na mazingira yetu

Mahakama ya Chancery London kipindi cha mapema cha karne ya

Usawa na amana ni mwili wa sheria ulioibuka nchini Uingereza kando na shera ya kawaida Sheria ya kawaida ilisimamiwa na mahakimu Bwana Chansela kwa upnade mwingine kama muwekaji dhamiri wa mfalme angeweza kupuuza sheria iliyotengenezwa na hakimu ikiwa alifikiria kuwa ilikuwa sawa kufanya hivyo Hili lilimaanisha kuwa usawa ulianza kufanya kazi zaidi kupitia kanuni bali si sheria ambazo hazikubadilika Kwa mfano ambapo mifumo ya sheria ya kawaida au sheria ya raia haiwaruhusu watu kugawa umiliki wa kutoka kwa udhibiti wa kipande kimoja cha mali usawa unaruhusu hili kupitia mpango unaoitwa amana Kudhibitiwa kwa mali na wenye amana ambapo kwa upande mwingine umiliki wenye manufaa au yenye usawa wa mali ya amana inashikiliwa na watu wanojulikana kama wadhamini Wadhamini wana wajibu kwa walengwa wao wa kuyachuna vyema mali waliyokabidhiwa Katika kesi ya awali ya Keech dhidi ya Sandford mtoto alirithi haki ya kokodisha katika soko katika eneo la Ramford mjini London Bw Sandford alikabidhiwa mali hayo hadi wakati ambapo mtoto angekomaa Lakini kabla ya hapo kipindi cha kukodisha kilikwisha Kabaila alikuwa inaonekana amemwambia Bw Sandford kuwa hakutaka mtoto yule awe na kukodisha kupya Lakini bado kabaila alikuwa amefurahi inaonekana kumpa Bw Sandford fursa ya kukodisha Bw Sandford aliichukua Wakati ambapo mtoto sasa Bw Keech alikuwa mkubwa alimpeleka Bw Sandford mahakamani kwa faida aliyokuwa akipata kwa kupata kukodisha kwa soko Bw Sandford alifaa kuaminika lakini alijiweka katika nafasi ya mgongano wa maslahi Bwana Kansela Bwana Mfalme alikubali na kumuamuru Bw Sandford kutoa faida ile na kumlipa Bw Keech Aliandika

Bila shaka Bwana Mfalme LC alikuwa na wasiwasi kwamba wadhamini huenda wakatumia fursa ya kutumia mali ya amana wenyewe badala ya kuyachunga Wadadisi wa kibiashara wanaotumia hifadhi walikuwa wamesababisha kuaguka kwa soko la hisa katika siku hizo Wajibu mkali kwa wadhamini ulijumuishwa katika sheria ya serikali na kutumika kwa wakurugenzi wa makampuni na maafisa watendaji wakuu Mfano mwingine wa jukumu la mdhamini unaweza kuwa kuwekeza mali vizuri au kuiuza Hii hasa ndiyo kesi kwa fedha za pensheni aina muhimu kwa zote ya amana ambapo wawekezaji ndio wadhamini wa akiba za watu hadi wastaafu Lakini amana pia zinaweza kuundwa kwa madhumuni ya hisani mifano maarufu ikiwa Makavazi ya Uingereza au Shirika la Rockefeller

Sheria huenea mbali kuliko masomo ya msingi hadi karibu kila eneo la maisha Ngazi tatu zimetajwa hapa ili kurahisiha majadiliano ingawa masomo mbalimbali hufanana na kutegemeana

Sheria na jamii
Chama cha wafanyikazi kilichoundwa na kikundi cha UNISON walipogoma

Sheria ya ajira ni somo la uhusiano wa mara tatu wa kiwandani kati ya mfanyikazi muajiri na chama cha wafanyikazi Hili linahusisha kupunguza kufanya biashara kwa pamoja na haki ya kugoma Sheria ya kuajiriwa kwa binafsi inaashiria haki za maeneo ya kazi kama zile usalama wa kazi afya na usalama au mshahara wa chini zaidi
Haki za kibinadamu haki za kiraia na sheria ya haki za kibinadamu ni maeneo muhimu katika kumhakikishia kila mtu uhuru na haki za kimsingi Haya yanapatikana katika maadiko kama vile Azimio la Ulimwenguni la Haki za Kibinadamu Mkataba wa Ulaya wa Haki za Kibinadamu iliyoanzisha Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu na Mswada wa Marekani wa Haki za Kibinadamu Mkataba wa Lisbon unafanya Mkataba wa Haki za Msingi za Umoja wa Ulaya uwe na nguvu za kisheria katika nchi zote wanachama isipokuwa Polandi na Uingereza
Utaratibu wa Kiraia na utaratibu wa jinai unahusisha kanuni ambazo mahakama lazima yafuate kadiri trial na rufaa zinapoendelea Yote yanahusu haki ya raia kupata kuhukumiwa kwa haki au kesi yake kusikizwa kwa haki
Ushahidi Sheria ya ushahidi inahusu vifaa vinavyofaa kutumika mahakamani ili kesi ijengwe
Sheria ya Uamiaji na sheria ya utaifa zinahusu haki za wageni kuishi na kufanya kazi katika taifa ambalo si lao na kupata na kupoteza uraia Yote yanahusu haki ya hifadhi na shida ya watu wasiokuwa na nchi
Usalama wa Kijamii Sheria ya usalama wa kijamii inahusu haki za watu kuwa na bima ya kijamii kama vile pesa zinazopewa watafuta kazi au faida za makazi
Sheria ya familia inahusu kesi za ndoa na talaka proceedings haki za watoto na haki za kuwa na mali na pesa ikiwa wenye kufanya ndoa watatengana

Sheria na biashara
Sheria ya kikampuni ilitokana na sheria ya amana ikitegemea kanuni ya kutenganisha umiliki na udhibiti Sheria ya kisasa ya kampuni ilianza na Sheria ya Kampuni za Pamoja za Akiba ya mwaka iliyopitishwa nchini Uingereza ambayo iliwapa wawekezaji mbinu rahisi ya usajili ili kupata dhima ya kupimika chini ya dhana ya mtu tofauti wa kampuni
Sheria ya kibiashara inahusu mkataba tata wa mkataba na mali Sheria ya shirika sheria ya bima bili za kubadilishana ufilisi na Sheria ya kuufungwa kwa biashara na sheria ya uuzaji zote ni muhimu na zinarudi nyuma hadi dhana ya Lex Mercatoria ya zama za kati Sheria ya Kuuza Bidhaa ya Uingereza na Kodi Sawa ya Biashara ya Marekani ni mifano ya kanuni za kibiashara ya sheria ya kawaida
Sheria ya maji na Sjeria ya Maji zinaweka muundo msingi wa biashara huru na biashara Duniani kote Baharini ambapo yamo nje ya eneo la udhibiti wa nchi fulani Makampuni ya meli yanafanya kazi kwa kutumia kanuni za kawaida za sheria ya biashara ambazo zimefanywa kuwa jumla kwa soko la kimataifa Sheria ya maji inajumuisha masuala muhimu kama vile kama vile kuokoa vifaa kutoka baharini lieni za maji na majeraha kwa abiria
Miliki Sheria inalenga aims at safeguarding creators and other producers of intellectual goods and services These are legal rights copyrights trademarks patents and related rights which result from intellectual activity in the industrial literary and artistic fields
Fidia inashughulika na kupata mapato ya mtu mwingine bali si fidia kwa hasara ya kibinafsi
Kutajirika isipofaa ndiyo nguzo ya tatu ya sheria ya raia pamoja na mkataba na ukiukaji wa wajibu Wakati ambapo mtu fulani ametajirishwa isipofaa au kuna kutokuwepo kwa msingi wa biashara kwa gharama ya mawingine tukio hili linazalisha haki ya fidia ili kugeuza faida hiyo

Sheria na vikwazo
Sakafu ya biashara ya Soko la Hisa la New York baada ya kuanguka kwa Wall Street mnamo mwaka wa kabla ya sheria kali zaidi za vikwazo vya kibenki vilipoanza kutumika

Sheria ya kodi inahusu kanuni kuhusu kodi ya thamani iliyoongezwa kodi ya kampuni kodi ya mapato
Sheria za kibenki na kanuni za kifedha zinaweka viwango vya chini zaidi kuhusu idadi ya mtaji ambao benki zinaweza kuwa nao na sheria kuhusu utendaji bora wa uwekezaji Hili ni kwa minajili ya kuhakikisha ulinzi dhidi ya taabu za kiuchumi kama vileKunguka kwa soko la Wall Street mnamo mwaka wa
Vikwazo vinashughulika na utoaji wa huduma za umma na usimamizi wa vifaa vya ummaSheria ya maji ni mfano mmoja Hasa tangu ubinafshaji uwe maarufu na uchukue usimamizi wa huduma kutoka kwa sheria ya umma makampuni ya kibinafsi ambayo hapo yalikuwa yakifanya kazi iliyodhitiwa na serikali hapo awali yamefungwa na vyeo mbalimbali vya wajibu wa kijamii Nishati gesi mawasiliano na maji zinadhibitiwa na viwanda katika nchi nyingi za OECD
Sheria ya mashindano nchini Marekani inajulikana kama sheria dhidi ya amana ni eneo linalozidi kubadilika ambalo lilianza katika kutokana na amri za Kirumi dhidi ya kuweka bei na mafundisho ya Uingereza ya biashara ya makini Sheria ya kisasa ya mashindano inatokana na sheria za Marekani dhidi ya biashara za magendo na dhidi ya ukiritimba Sheria ya Sherman na Sheria ya Clyaton ya mwisho wa karne ya Inatumika kudhibiti biashara zinazojaribu kutumia ushawishi wao wa kiuchumi kubadilisha biashra za sokoni bila kujali maslahi ya mnunuzi
Sheria ya mnunuzi inaweza kujumuisha chochote kuanzia kanuni kuhusu vifungu vya mikataba ambavyo si sawa hadi maelekezo kuhusu bima ya mizigo ya ndege
Sheria ya mazingira inazidi kuwa muhimu hasa katika mwanga wa Itifaki ya Kyoto na hatari inayoweza kutokana na mabadiliko ya hali ya anga Ulinzi wa kimazingira pia intumika kuwaadhibu wanaoharibu mazingira katika mifumo ya kisheria ya kiinchi

Kwa ujumla mifumo ya kisheria inaweza kugawanywa kati ya mifumo ya kisheria ya kiraia na mifumo ya kisheria ya kawaida Maneno sheria ya kiraia yanayoashiria mfumo wa kisheria hayapaswi kuchanganyishwa na sheria ya kiraia kama kundi la masomo ya kisheria ambayo ni tofauti na sheria ya umma au ya jinai Aina ya tatu ya mfumo wa kisheriainayokubalika bado na baadhi ya nchi ambazo zina utengano wa kanisa na taifani sheria sheria ya kidini ambayo ina msingi wake katika maandiko ya kidini Aina ya mfumo amabo nchi inatumia kutawala mara nyingi kudhamiriwa na historia yake uhusiano wake na nchi zingine au kushikilia kwake kwa viwango vya kimataifa Vyanzo ambavyo maneneo fulani ya kisheria hutumia kama kama zenye uwezo wa kuwa nguvu za kisheria ndizo sifa fafanuzi za mfumo wowote wa kisheria Hata hivyo uainishaji ni jambo la umbo kuliko maana kwani sheria sawa mara nyingi hutawala

Ukurasa wa kwanza wa toleo la mwaka wa la Sheria za Kinapoleoni

Sheria ya kiraia ni mfumo wa kisheria unaotumika katika nchi nyingi Duniani Katika sheria ya kiraia vyanzo vinavyotambulika kama kuwa na mamlaka ni haswa uundaji wa sheriahaswa sheria zilizoandikwa katika katiba au amri zinazopitishwa na serikalina tamaduni Sheria za kuandikwa zinapatikana hata katika miaka mingi ya awali huku mfano mmoja ukiwa Codex Hammurabi ya Kibabeli Mifumo ya sheria za kiraia ya kisasa inatokana na mazoezi ya kisheria ya Dola la Kirumi ambalo maadiko yake yalipatikana katika Ulaya ya Zama za Kati Sheria ya Kirumu katika siku za Jamhuri ya Kiruma na Dola la Kirumi lilitegemea sana utaratibu na ilikosa daraja la kitaaluma Badala uake mtu wa kawaida aliyeitwa iudex alichagukiwa kufanya uamuzi Kesi za awali hazikuripotiwa kwa hivyo sheria yoyote yenye msingi katika kesi iliyoibuka ilifichwa na hata kutotambulika Kila kesi ilikuwa ilimuliwe upya kutokana na sheria za nchi ambayo ni sawa na kupungua kwa umuhimu kinadharia wa uamuzi wa mahakimu kwa kesi za siku za usoni kwa mufumo ya kisheria siku za leo Katika kipindi cha karne ya NK katika Dola la Mashariki la Roma Kaisari Justinian I aliandika na kuzikusanya pamoja sheria ambazo zilikuwa zinapatikana hapo awali katika Roma ambapo kile kilichobakia kilikuwa sehemu moja juu ya ishirini ya kiwango cha maandiko ya kisheria kutoka awali Hili ikawa inafahamika kama Corpus Juris Civilis Kwa mujibu wa mwanahistoria mmoja wa kisheria Justinian alitazama kwa uangalifu hadi miaka ya dhahabu ya nyuma ya sheria ya Kirumi na alilenga kuirejesha hadi upeo wake wa karne tatu za awali Wakati uo huo Ulaya ya Magharibi ilitumbukia polepole katika Zama za Giza na haikuwa hadi karne ya ambapo wasomi katika Chuo Kikuu cha Bologna walipoyagundua upya maandiko yaliyokuwa yamepotea na kuyatumia kuzitafsiri sheria zao Maandiko ya sheria za kiraia yenye msingi unaofanana kwa karibu na sheria ya Kirumu sambamba na ushawishi mchache kutoka sheria za kidini kama vile sheria ya Kikanoni na sheria ya Kiislamu Leo cnhi ambazo zina mifumo ya kisheria ya kiraia ni kama vile Urusi na Uchina na maeneo mengi ya Marekani ya Kati na Marekani ya Kilatini Marekani inafuata sheria ya kawaida inayofafanuliwa hapa chini

Mfalme Yohana wa Uingereza anatia sahini Magna Carta

Sheria ya kawaida na usawa ni mifumo ya kisheria ambapo uamuzi wa mahakama yanakubalika wazi kuwa vyanzo vya sheriaMafundisho ya utangulizi au stare decisis Kilatini kwa kusimama kwa uamuzi unamaanisha kuwa sumauzi unaofanywa na mahakama yenye mamlaka kubwa yanafunga mahakama yenye mamlaka ya chini Mifumo ya kisheria ya kawaida hutumia amri mara chache sana zinazopitishwa na bunge lakini huenda zikafanya jaribio ambalo si la kitaratibu kuandika sheria zao kuliko katika mfumo wa sheria wa kiraia Sheria ya kawaida ina asili yake nchini Uingereza na imerithiwa na karibu nchi zote ambazo hapo awali zilihusika na Dola la Uingereza isipokuwa Malta Scotland na jimbo la Marekani la Louisiana na jimbo la Kanada la Quebec Katika Uingereza wakati wa zama za kati ushindi wa Norman ulisababisha kuungana kwa desturi mbalimbali za kikabila na hivyo basi kuunda sheria ya kawaida ya nchi yote Labda ikisukumwa na mazoea ya kisheria ya Kiislamu wakati wa Krusedi sheria ya kawaida iliendelea ambapo Mfalme wa Kiingereza alikuwa amefanywa kuwa dhaifu na gharama kubwa ya vita vywa kudhibiti sehemu kubwa za Ufaransa Mfalme Yohana alikuwa amelazimishwa na mabaroni wake kutia saini hati iliyoweka vikwazo kwa mamlaka yake ya kupisha sheria Mkataba huu mkuu au Magna Carta wa mwaka pia ulihitaji jopo la mahakimu wa Mfalme kufanya mikutano yao ya kimahakama na uamuzi wao katika mahali maalum badala ya kutoa haki ya kibepari katika maeneo yaliyokuwa magumu kutabiri kote Kundi la mahakimu walsomi na waliokolea walipata jukumu muhimu katika kuunda sheria chini ya mfumo huu na ikilinganishwa na wenzao Barani Ulaya mahakama ya Uingereza ilikuwa na urasimu mwingi zaidi Kwa mfano mnamo mwaka wa wakati ambapo mahakama kuu ya Ufaransa yalikuwa na mahakimu hamsini na wawili Mahakama ya Uingereza ya Maombi ya Kawaida yalikuwa na watano Mahakama haya yenye nguvu na yaliyoshikamana yalisababisha mfumo wa kikiritimba Kufuatana na hilo kadiri wakati ulivyopita idadi iliyoongezeka ya raia waliomba Mfalme kupuuza sheria ya kawaida na kwa niaba ya Mfalme Bwana Chansela alitoa uamuzi kufanya kile ambacho ni sawa kwa kila kesi Kuanzia wakati wa Thomas More wakili wa kwanza kuteuliwa kama Bwana Chansela mwili wa kimfumo wa usawa uliongezeka kando ya sheria ya kawaida yenye ukiritimba na ilianzisha Mahakama yake ya Chancery Mwanzoni usawa ulikosolewa kuwa ulikosa kukosa utaratibu na kuwa ulibadilika kulingana na urefu wa mguu wa Chansela Lakini baada ya muda iliunda kanuni hasa chini ya Bwana Eldon Katika karne ya mifumo hiyo miwili iliunganishwa pamoja Katika kuendeleza sheria ya kawaida na usawa waandishi wa kitaaluma wamekuwa na jukumu muhimu William Blackstone kuanzia kipindi cha alikuwa mwanachuoni wa kwanza kuelezea na kufunza usawa Lakini kwa kuelezea tu wasomi walitafuta melezo na miunso msingi walibadilisha polepole jinisi sheria ilivyofanya kazi

Sheria ya kidini inatokana na maagizo ya dini Baadhi ya mifano ni Halakha ya Kiyahudi na Sharia ya Uislamu ambazo zote mbili zinamaanisha njia ya kufuata huku sheria za Kanisa za Ukristo nazo hutumika katika madhehebu machache kama vile Kanisa Katoliki Kanisa la Kiorthodoksi na la Anglikana

Mara nyingi dini inadai kutobadilika kwa sheria kwa sababu neno la Mungu haliwezi kufanyiwa marekebisho wala kupingwa na mahakimu au serikali

Hata hivyo mfumo fasaha wa sheria kwa jumla unahitaji upanuzi upande wa binadamu Kwa mfano Torati au Vitabu Vitano vya Musa katika Agano la Kale Vitabu hivyo vina kanuni na sheria za msingi za Uyahudi ambayo baadhi ya jamii ya Kiisraeli huchagua kutumia Halakha ni kanuni ya sheria za Kiyahudi inayofanya muhtasari wa baadhi ya ufafanuzi wa kitabu cha Talmud Hata hivyo Sheria za Israeli zinaruhusu mlalamikaji kuchagua mbinu za kidini ikiwa tu anataka Mfano mwingine ni Korani ambayo ina sheria na inakuwa kama chanzo cha sheria zaidi kupitia ufafanuzi Qiyas kulinganisha Ijma kufikia muafaka na yaliyokwishatokea Hili hasa hupatikana katika mkusanyo wa sheria na falsafa ya kisheria inayojulikana kama Sharia na Fiqh
Kesi katika Dola la Ottoman mwaka wakati sheria ya kidini ilitumika chini ya Mecelle

Hadi karne ya Sharia ilitekelezwa kote katika Ulimwengu wa Kiislamu katika mfumo ambao haukuwa umeandikwa kwa ufasaha huku sheria ya Mecelle ya Dola la Ottoman katika karne ya ilikuwa ya kwanza kuandika vipengele vya Sharia Tangu miaka ya kati ya majaribio yamefanywa katika nchi nyingi kufanya sheria hizo zifanane zaidi na hali na dhana za kisasa

Katika nyakati za sasa mifumo ya kisheria katika mataifa mengi ya Kiislamu hutegemea sheria za kiraia na sheria ya kawaida na pia sheria na tamaduni za Kiislamu Katiba za baadhi ya nchi za Kiislamu kama vile Misri na Afghanistan zinatambua Uislamu kama sheria ya taifa hivyo kuyafanya mabunge katika nchi hizo yasiwe na budi kufuata Sharia Saudia inatambua Korani kama katiba na inatawaliwa kwa msingi wa sheria ya Kiislamu Iran pia imeshuhudia kurudi kwa sheria ya Kiislamu katika mfumo wake wa kisheria baada ya mwaka Katika miongo michache iliyopita mojawapo ya tofauti kuu ya harakati ya mwamko wa Kiislamu imekuwa wito wa kuirejesha Sharia wito ambao umeibua kiasi kikubwa cha maandishi na kuathiri siasa duniani

Mfalme Hammurabi anaonyeshwa mkusanyiko wa sheria na mungu wa jua wa Kimesopotamia Shamash ambaye pia anatambulika kama mungu wa haki

Historia ya sheria inashikamana kwa karibu na maendedelo ya ustaarabu Sheria ya Misri ya Kale iliyorudi nyuma mbali hadi mwaka wa KK ilikuwa na mkusanyiko wa sheria ambao huenda ilikuwa imevunjwa katika vitabu kumi na viwili Ilizingatia dhana ya Maat iliyokuwa na sifa ya mapokeo hotuba za kushawishi usawa wa kijamii na uaminifu Kufikia karne ya BC mtawala wa zamani wa Kisumeri UrNammu alikuwa ameandaa mkusanyiko wa sheria ambao ulihusisha kauli za kimjadala ikiwa basi Kufikia mwaka wa KK Mfalme wa Hammurabi aliboresha Sheria ya Babeli zaidi kwa kuikusanya na kuandika katika jiwe Hammurabi aliweka nakala kadhaa za jiwe lile kote katika milki ya babeli kama stelae ili watu wote waitazame hii ilikuja kufahamika kama Codex Hammurabi Nakala iliyobaki ambayo haijaharibika sana wa stelae hizi iligunduliwa katika karne ya q na wasomi kuhusu mambo ya milki ya Assyria wa Uingereza na tangu wakati huo imenakiliwa upya na kutafsiriwa katika lugha mbalimbali ikiwemo Kiingereza Kijerumani na Kifaransa

Agano la Kale lilianza mnamo mwaka wa KK na linachukua umbo la amri za kimaadili kama mapendekezo ya jamii nzuri Mjijimbo mdogo wa Kigiriki wa Atheni ya Kale na kuanzia karne ya KK ilikuwa jamii ya kwanza kuwa na msingi wake katika kuhusisha raia kwa upana isipokuwa wanawake na daraja la watumwa Hata hivyo Atheni haikuwa na sayansi ya kisheria na hapakuwa na neno la sheria isipokuwa kama dhana ya kiakili tu Bado sheria ya Ugiriki wa Kale ilikuwa na uvumbuzi mkubwa wa kikatiba katika kuendeleza demokrasia

Sheria ya Kirumi ilisukumwa sana na falsafa ya Kigiriki lakini maelezo yake ya kina yaliendelezwa na wanasheria wa kitaaluma na yalikuwa magumu sana Katika kipindi cha karne zilizopita kati ya kupanda na kushuka kwa Dola la Roma sheria imebadilishwa ili kukabiliana na hali za kijamii zilizokuwa zikibadilika na ilikusanywa na kuandkiwa vilivyo katoka wakati wa utawala wa Justinian I Ingawa ilipungua kwa umuhimu wakati wa Zama za Giza Sheria ya Kirumi iligunduliwa upya wakati wa karne ya wakati ambapo wasomi wa Zama za Kati walipoanza kutafiti mkusanyiko wa sheria za Kirumi na kayatumia mawazo yao Katika Uingereza ya Zama za Kati mahakimu wa Mfalme waliunda mwili wa utangulizi ambao baadaye ulijulikana kama sheria ya kawaida Lex Mercatoria ya Ulaya mzima iliundwa ili kuwapa wafanyabiashara uwezo wa kufanya biashara kwa kutumia viwango sawa vya mazoezi badala ya kutumia sheria za kimtaa zenye pande nyingi Lex Mercatoria mtangulizi wa sheria ya kisasa ya biashara ilihimiza uhuru wa mkataba na kuwekwa mbali kwa mali Kadiri utaifa ulipozidi katika karne za na ndipo Lex Mercatoria ilipozii kujumuishwa katika sheria za kimanispaa za nchi mbalimbali chini ya mkusanyiko mpya wa sheria za kiraia Mkusanyiko wa Sheria za Kinapolioni na sheria za Kijerumani ulikuwa na ushawishi mkubwa zaidi Ikitofautishwa na sheria ya kawaida ya Uingereza ambayo ina idadi kubwa ya sheria za kesi mikusanyiko ya sheria katika vitabu vidogo ni rahisi kuuza nje ili mahakimu waweze kuitumia Hata hivyo hivi leo kuna ishara kuwa sheria ya kiraia na sheria ya kawaida zinazidi kukaribiana Sheria ya Umoja wa Ulaya imekusanywa katika mikataba lakini huendelezwa kupitia utangulizi unaofanywa na Mahakama ya Ulaya ya Haki

Katiba ya nchi ya Uhindi ndiyo katiba ndefu zaidi iliyoandikwa kwa nchi ikiwa na Ibara Ibara ndogo na marekebisho mengi na maneno

Sheria ya Kiislamu na falsafa ya sheria zilianza katika kipindi cha Zama za Kati Mbinu ya kisheria ya utangulizi na kufikiria kupitia mlinganisho Qiyas iliyotumika katika sheria ya mapema ya Kiislamu ilifanana na na ile ya baadaye ya mfumo wa Sheria ya Kawaida ya Uingereza Hii ilitumika hasa katika shule ya Maliki ya sheria ya Kiislamu iliyopatikana sana katika eneo la Afrika Kasakazini Uhispania wa Kiislamu na baadaye Sicily ya Kiemereti Kati ya karne za na sheria ya Maliki iliendeleza taasisi nyingi zilizokuwa sambamba na taasisi za baadaye za sheria ya kawaida

Sheria ya kale ya Uhindi na Uchina zinawakilisha mapokeo tofauti ya sheria na kihistoria yamekuwa na shule huru za kinadharia na mazoezi Arthashastra ambayo pengine iliandikwa mnamo mwaka wa BB ingawa ina maadiko ya awali kidogo na Manusmriti BB yalikuwa mikataba ya uanzilishaji nchini Uhindi na ilikuwa na maandiko yanayofikiriwa kuwa uwongofu wenye mamlaka wa kisheria Falsafa kuu ya Manu ilikuwa kuvumiliana na Mfumo wa Vyama Vingi na ilitajwa kote katika eneo la Asia ya Kusini Mashariki Mapokeo haya ya Kihindu pamoja na sheria ya Kiislamu yalibadilishwa na na sheria ya kawaida wakati ambapo Uhindi ilifanywa kuwa sehemu ya Dola la Uingereza Malaysia Brunei Singapore na Hong Kong pia ilianza kutumia sheria ya kawaida Mapokeo ya Asia ya Kusini ya sheria yanaangazia mkusanyiko maalum wa ushawishi wa kidunia na kidni Ujapani ilikuwa nchi ya kwanza kuanza kuufanya mfumo wake wa sheria uwe wa kisasa sambamba na ule wa nchi za magharibi kwa kuagiza sehemu za mkusanyiko wa sheria za Ufaransa lakini hasa mkusanyiko wa sheria za Kijerumani Hili lilionyesha kwa kiwango fulani hadhi ya Ujerumani kama nguvu yenye uwezo mkubwa zaidi katika kipindi cha mwisho cha karne ya Pia sheria ya mapokeo ya Uchina ilifungua njia kwa kubadilishwa na nchi za magharibi kuelekea miaka ya mwisho ya nasaba ya Ching kupitia njia ya mkusanyiko wa sheria tatu za kibinfasi zilizokuwa na msingi katika muundo wa Ujapani wa sheria ya Ujerumani Leo sheria ya Kitaiwani inabaki na mshikamano wa karibu zaidi na mkusanyiko wa sheria kutoka kipindi hicho kwa sababu ya mgawanyiko kati ya wanataifa wa Chiang Kaishek ambao walitoroka kutoka sehemu hiyo na wakomunisti wa Mao Zedong waliopata ushindi wa kudhibiti bara mnamo mwaka wa Muundombinu wa sasa wa Jamhuri ya Watu wa Uchina ilishawishika pakubwa na Sheria ya Kisosholisti ya Wasovyeti inayopea sheria ya utawala umuhimu mwingi kuliko haki za sheria ya kibinafsi Kwa sababu ya kuongezeka kwa kasi kwa viwanda leo Uchina inapitia machakato wa wa marekebisho angalau katika nyanja ya haki za kiuchumi ikiwa si haki za kijamii na kisiasa Sheria mpya ya mkataba ya mwaka wa ilikuwa ishara ya kusonga mbali na kuwa na utawala mwingi Isitoshe baada ya mazungumzo yaliyodumu miaka kumi na mitano mnamo mwaka Uchina ilijiunga na Shirika la Biashara Duniani

Falsafa ya sheria kwa kawaida inaitwa jurisprudensi Jurisprudensi unaozidi kuongezka wenyewe ni falsafa ya kisiasa na unauliza sheria inafaa kuwa nini huku jurisprudensia ya uchambuzi inauliza sheria ni nini Jibu la kiutumikaji la John Austin linajibu kuwa sheria ni amri zinazoandamana na matishio ya vkwazo kutoka kwa mtawala ambaye watu wote wamezoea kumtii Mawakili wa sheria ya kimaumbile kwa upande mwingine kama vile JeanJacques Rousseau wanadokeza kwamba sheria inaangazia sheria isiyobadilika ya tabia ya kimaumbile Dhana ya sheria ya kimaumbile iliibuka katika falsafa ya Kigiriki ya zamani kwa wakati mmoja na kwa pamoja na dhana ya haki na iliingia mkondo wa utamaduni wa Magharibi kupitia maandiko ya Thomas Aquinas na maoni ya mwanafalsafa wa Kiislamu na mwanasheria Averroes

Hugo Grotius mwanzilishi wa mfumo uliotegemea dhana za kiakili pekee ya sheria ya kimaumbile alidokeza kuwa sheria inatokana na msukumo wa kijamiijinsi Aristotle alivyokuwa amesemana kufikiria Immanuel Kant aliamini kuwa amri ya kimaadili inahitaji sheria zichaguliwe kana kwamba zinafaa kushikilia kama sheria za ilimwenguni kote za kimaumbile Jeremy Bentham na mwanafunzi wake Austin wakimfuata David Hume waliamini kuwa hili liliongeza utata wa kilicho na kile ambacho kinafaa kuwepo Bentham na Austin walisisitiza kuwe na sheria ya uchanya na kuwa sheria ya kweli ni tofauti kabisa na maadili Kant pia alikosolewa na Friedrich Nietzsche ambaye alikataa kanuni ya usawa huku akiamini kuwa sheria hutokana na nia kwa nguvu na haiwezi fanywa kuwa ya kimaadili au utovu wa nidhamu

Mnamo mwaka wa mwanafalsafa wa Kiaustria Hans Kelsen alizidi na mapokeo ya uchanya katika kitabu chake Nadharia Safi ya Sheria Kelsen aliamini kuwa ingawa sheria ni tofauti na maadili inapewa ukawaida kumaanisha kuwa tunfaa kuitii Ingawa sheria ni taarfa chanya za ni km faini ya kuendesha kwa kurudi nyuma katika barabara kuu ni hii sheria inatuelezea kile tunachofaa kutenda Kwa hivyo kila mfumo wa sheria unaweza kudadisiwa kuwa na kanuni ya msingi Grundnorm ianyotupea amri ya kutii Mpinzani mkuu wa Kelsen Carl Schmitt alikataa uchanya na dhana ya utawala wa sheria kwa sababu hakukubali umuhimu wa kanuni za kidhana za Uchanya badala ya mitazamo na uamuzi bayana wa kisiasa Kwa hiyo Schmitt alipendekeza falsafa ya sheria ya maalum hali ya dharura ambayo ilikanusha kuwa kanuni za kisheria zingezunguka uzoefu wote wa kisiasa

Nadharia za Bentham za utumikiaji zilibaki kimya katika sheria hadi karne ya

Baadaye katika karne ya H L A Hart alimshambulia Austin kwa kurahisisha kwake kwa suala hilo na Kelsen kwa kutunga kwake kwa mambo ya kihadithi katika kitabu cha Dhana ya Sheria Hart alidokeza kuwa sheria ni mfumo wa kanuni zilizogawanywa kuwa kanuni za maadili ambazo ndizo za kimsingi na sheria za upili zinazowalenga maafisa kusimamia kanuni msingi Kanuni za upili zimegawanywa zaidi kuwa sheria za uamuzi kutatua migogoro ya kisheria kanuni za mabadiliko zinazoruhusu sheria kuwa tofauti na sheria ya utambuziinayoruhusu sheria kutambulika kama halali Wawili kati ya wanafunzi wa Hart waliendeleza mjadala Ktaika kitabu chake Dola la Sheria Ronald Dworkin alimshabulia Hart na wachanya kwa kukataa kwao la kufanya sheria iwe suala la kimaadili Dworkin anadokeza kuwa sheria ni dhana ya kitafsiri inayowataka mahakimu kupata suluhisho bora zaidi kwa mgogoro wa kisheria kwa mujibu wa mila zao Joseph Raz kwa upande mwingine anawataka alitetea mtazamo wa kichanya na kukosoa mtazamo wa Hart wa nadharia laini ya kijamii katika kitabu chake Mamlaka ya Sheria Raz anadokeza kuwa sheria ni mamlaka yanayotambulika kupitia vyanzo vya kijamii na bila kurejelea hoja za kimaadili Katika maoni yake uainishaji wowote wa kanuni zozote zaidi ya majukumu yao kama vifaa vya kimamlaka katika upatanisha ni bora yaachiwe elimu ya jamii badala ya falsafa ya sheria

Katika karne ya Adam Smith aliwasilisha msingi wa kifalsafa wa kuelezea uhusiano kati ya sheria na uchumi Taaluma hiyo ilitokana na mchango wa ukosoaji dhidi ya vyama vya wafanyikazi na sheria dhidi ya amana nchini Marekani Watetezi wa taaluma hii waliokuwa na ushawishi mkubwa zaidi kama vile Richard Posner na Oliver Williamson na kinachojulikana kama Shule ya Chicago ya wanauchumi na mawakili ikiwemo Milton Friedman na Gary Becker kwa jumla ni watetezi wa uouguzaji wa udhibiti na ubinafsishaji na ni maadui wa udhibiti wa serikali au kile wanachokiona kuwa vikwazo dhidi ya unedeshaji wa masoko huru

Richard Posner mmoja wa watetezi wa Chuo cha Chicago huandika blogu pamoja na Gary Becker mwanauchumi ambaye ni mshindi wa Tuzo la Benki ya Uswidi

Mchambuzi maarufu zaidi wa kiuchumi wa sheria ni mshindi wa Tuzo la Nobel la mnamo Ronald Coase ambaye makala yake makuu ya kwanza Hali ya Kampuni kulidokeza sababu za kuwepo kwa makampuni mbalimbali makampuni ubia nk ndiyo kuwepo kwa gharama za biashara Binadamu ambao hufikiria kawaida hufanya biashara kupitia mikataba ya bilaterala katika masoko wazi hadi wakati ambapo gharama ya biashara kunamaanisha kuwa kutumia makampuni ya kihalmasahhuri ili kuzalisha bidha ni ya ufanisi mwingi zaidiMakala yake makuu ya pili Shida ya Gharama ya Kijamii yalidokeza kuwa tunaishi katika Dunia bila gharama za kibiashara watu ambao huongea kuhusu gharama pamoja wanatengeneza mgao sawa wa rasilimali buila kujali jinsi mahakama yanavyoweza kuamua katika migogoro kuhusu mali Coase alitumia mfano wa kesi ya kero iliyoitwa Sturges dhidi ya Bridgman ambapo mtengenezaji peremende ambaye alipiga kelele nyingi na daktari mtulivu walikuwa majirani na walienda mahakamani ili wajue nani kati yao ndiye angefa kuhama Kwa hivyo sheria infaa kutazamia kile ambacho huenda kikafanyika na kuongozwa na ufumbuzi wenye ufanisi Wenye kuunda mipango serikalini wanaamini wazo kwamba sheria na vikwazo si muhimu au zenye ufanisi katika kuwasaidia watu Coase na wengine kama yeye walitaka mabadiliko ya mbinu ili kuweka mzigo wa ushahidi katika serikali iliyokuwa ikiingilia soko kwa kuchambua gharama za hatua

Somo la kijamii la sheria ni taaluma pana ya masomo inayotazama mwingiliano kai ya sheria na jamii na inahusiana kwa karibu na falsafa ya sheria uchambuzi wa kiuchumi wa sheria na masomo maalum zaidi kama somo la jinai Taasisi za The za ujenzi wa jamii na mifumo ya kisheria ni ameneo muhimu ya uchunguzi wa taaluma hii Mwanzoni wananadharia wa kisheria walishuku taaluma hii Kelesen alimshambuliwa mmoja wa waanzilishi wake Eugen Ehrlich ambaye alitaka kufanya wazi tofauti kati ya sheria ya uchanya ambayo mawakili wanajifunza na kutumia na aina zingine za sheria au kanuni za kijamii zinazodhibiti maisha ya kila siku na kwa jumla kuzuiwa migogoro isiwafikie mawakili mahakamani

Max Weber mnamo mwaka wa Weber alianza kazi yake kama wakili na antazamwa kama mmoja wa waanzilishi wa somo la jamii na somo la jamii la kisheria

Katika kipindi cha mwaka Max Weber alifafanua mbinu yake ya kisayansi ya sheria huku akitambua umbo la kimantiki ya sheria kama aina ya utawala ambao si chanzo cha watu lakini kwa dhana za kiakili Umantiki wa kisheria yalikuwa maneno yake aliyoyatumia kuelezea mwili wa sheria zinazoeleweka na zinazoweza kuhesabika na zilikuwa hatua ya kwanza ya maendeleo ya kisasa ya kisiasa na taifa la ukiritimba la kisasa na kuibuka sambamba na ubepari Wasomi wengine wa somo la jamii ni Hugo Sinzheimer Theodor Geiger Georges Gurvitch na Leon Petraycki Barani Ulaya na William Graham Sumner nchini Marekani

Sheria si mwili wa kanuni zisizobadilika bali ni machakato badilifu wa kanuni zinazobadilishwa kila wakati kuundwa na kupewa umbo ili kuambatana na hali fulani Mabadiliko yanafanywa kila wakati na taasisi mbalimbali katika jamii Taasisi kuu za sheria katika Demokrasia huru ni Mahakama huru mifumo ya haki bunge serikali yenye uwajibikaji na ukiritimba wenye uwezo na usiokuwa na ufisadi kiksoi cha polisi kudhibitiwa kwa jeshi na raia na taaluma ya kisheria yenye nguvu inayohakikisha watu wanapta haki na jamii ya kiraia mbalimbalineno linalotumika kuashiria taasisi za kijamii jamii na ushirikiano unaunda msingi wa kisiasa wa sheria

John Locke katika Maandiko Mawili kuhusu Serikali na Baron de Montesquieu katika Roho ya Sheria walitetea mgawanyo wa madaraka kati ya miili ya kisiasa ya bunge na serikali Kanuni yao ilikuwa kuwa hakuna mtu anayefaa kuwa na uwezo wa kuchukua mamlaka yote ya taifa ikitofautishwa na nadharia ya uimla ya Thomas Hobbes Leviathan Max Weber na wengine walibadilisha mawazo kuhusu taifa Jeshi la kisasa upolisi na mamalaka ya ukiritimba juu ya masiha ya raia wa kawaida husababisha matatizo maalum ya uwajibikaji ambayo waandishi wa awali kama vile Locke au Montesquieu hawangeweza kutabiri Mashirika ya kisasa ya kimataifa huzingatia umuhimu wa utawala wa sheria na utawala mzuri huku waandishi wengine hutafiti uhsusiano kati ya utawala wa sheria na utawala wa ufanisi katika nchi za kisasa

Mahakama ni idadi ya mahakimu wanaosikiza migogoro ili kuamua matokeo Nchi nyingi zina mfumo wa mahakama ya rufaa yanayojibu kwa mamlaka makuu ya kisheria Nchini Marekani haya ni Mahakama Kuu ya Marekani nchini Australia Mahakama Kuu ya Australia nchini Uingereza ni Mahakama Kuu ya Uingereza tangu tarehe Oktoba hapo awali yalikuwa Nyumba ya Mabwana nchini Ujerumani ni Bundesverfassungsgericht nchini Ufaransa ni Cour de Cassation Kwa nchi nyingi za Ulaya Mahakama ya Ulaya ya Haki nchini Luxembourg inaweza kuukataa umauzi wa kitaifa wakati ambapo sheria ya Umoja wa Ulaya inafaa Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu inayopatikana Strasbourg inawaruhusu raia wa nchi wanachama za Baraza la Ulaya kuleta kesi zao zinzohusiana na haki za kibinadamu mbele yake

Baadhi ya nchi huruhusu mamlaka yao makuu ya mahakama kukataa sheria wanayopata kuwa kinyume na katiba Katika kesi ya Roe dhidi ya Wade Mahakama Kuu ya Marekani ilipindua sheria ya jimbo la Texas iliyopiga marufuku kutoa msaada kwa wanawake wenye nia ya Kuavya mimba Marekebisho ya Kumi na Nne ya katiba ya Marekani yalikuwa yametafsiriwa kuwapa ya faragha na kwa hivyo haki ya mwanamke kuchagua kuavya mimba

Mahakama kinadharia yamefundwa na katiba kama tu miili ya bunge Katika nchi nyingi mahakimu wana uwezo tu wa kutafsiri katiba na sheria zingine zote Lakini katika nchi zasheria ya kawaida ambapo mambo si ya kikatiba mahakama pia yanweza kuunda sheria chini ya mafundisho ya utangulizi Uingereza Finland na New Zealand hutumia dhana ya uhuru wa bunge ambapo mahakama ambayo hayajachaguliwa hayawezi kupindua sheria iliyopitishwa na bunge la kidemokrasia Katika nchi za kikomiunisti kama vile Uchina mahakama mara nyingi hutazamwa kama sehemu ya serikali au kuwa chini ya bunge taasisi za kiserikali na watendaji mbalimbali basi wana ushawishi tofauti kwa mahakama Katika nchi za Kiislamu mahakama mara nyingi huchunguza ikiwa sheria za nchi zinafuata Sharia Mahakama Kuu ya Kikatiba ya Misri inaweza kuoinga sheria kama hizo Na nchini Iran Baraza la Ulinzi linahakikisha uwiano wa sheria zinazopitishwa na vigezo vya Uislamu

Chumba cha mjadala cha Bunge la Ulaya

Mifano maarufu ya bunge ni Majumba ya Bunge mjini London Kongresi mjini Washingtin DC Bundestag mjini Berlin na Duma nchini Moscow Parlamento Italiano mjini Roma na Assemble nationale mjini Paris Kwa kanuni ya serikali wakilishi watu hupigia kura wanasiasa ili watimize matakwa yao Ingawa nchi kama Israeli Ugiriki Uswidi na Uchina zina nyumba moja ya bunge nchi nyingi zina nyumba mbili za bunge kumaanisha kuwa zina nyumba mbili za kibunge zinazochaguliwa tofauti Katika nyumba ya chini wanasiasa wanachaguliwa kuwakilisha maeneo wakilishi bungeni Nymba ya juu kawaida huchaguliwa kuwakilisha majimbo katika mfumo wa majimbo kama vile nchii Australia Ujerumani au Marekani au upigaji kura tofauti katika katika mfumo wa umoja kama vile nchini Ufaransa Nchini Uingereza nyumba ya juu inachaguliwa na na serikali kama nyumba ya marudio Ukosoaji mmoja wa mifumo yenye nyumba mbili yenye nyumba mbili zilizochaguliwa ni kuwa nyumba ya juu na ya chini huenda zikafanana Utetezi wa tangu jadi wa mifumo ya nyumba mbili nni kuwa chumba cha juu huwa kama nyumba ya marekebisho Hili linaweza kupunguza uonevu na dhuluma katika hatua ya kiserikali

Ili kupitisha sheria idadi kubwa ya Wabunge lazima wapige kura ili muswada sheria inayopendekezwa upitishwe katika kila nyumba Kawaida kutakuwa na kusoma kwingi na marekebesho mengi yaliyopendekezwa na makundi tofaiti ya kisiasa Ikiwa nchi ina katiba inayofuatiliwa vyema idadi maalum ya mabadiliko katika katiba yanahitajika hivyo kufanya iwe gumu kubadilisha sheria Serikali kwa kawaida huongoza mchakato huo ambao unaweza kujumuisha Wabunge km nchini Uingereza na Ujerumani Lakini katika mfumo wa kiraisi serikali inachagua baraza la mawaziri kutawala kutoka kwa washirika wake kisiasa ikiwa wamechaguliwa au la km nchini Marekani au Brazili na jukumu la bunge linapunguza liwe kukubali au kukataa

Mikutano ya G inahusisha wawakilishi wa serikali ya kila nchi

Mtendaji katika mfumo wa kisheria hutumika kama kituo cha serikali cha mamlaka ya kisiasa Katika mfumo wa kibunge kama vile nchini Uingereza Italia Ujerumani na Ujapani mtendaji hujulikana kama serikali na huwa na wanachama wa bunge Mtendaji huchaguliwa na Waziri Mkuu au Chansela ambaye ofisi yake ina nguvu za chini ya imani ya bunge Kwa sababu uchaguzi wenye watu wengi huteua vyama vya kisiasa kutawala kiongozi a chama anaweza kubadilika katika kipindi kabla ya uchaguzi mwingine Mkuu wa Taifa ni kando na mtendaji na kimfano hupitisha sheria na huwa kama mwakilishi wa nchi Baadhi ya mifano ni Rais wa Ujerumani anayeapishwa na Bunge Malkia wa Uingereza wadhifa wa kurithi na Rais wa Austria anachaguliwa kwa kura ya wengi Mfano mwingine muhimu ni mfumo wa kirais unaopatikana nchini Ufaransa Marekani na Urusi Katika mifumo ya kirais mtrndaji huwa kama mkuu wa taifa na mkuu wa serikali na ana nguvu za kuchagua baraza la mawaziri pekee yake Chini ya mfumo wa kirais tawi la mtendaji ni kando na bunge ambapo haiwajibiki mbele ya bunge

Ingawa jukumu la mtendaji ni tofauti toka nchi moja hado nyingine kawaida itapendekeza wingi wa sheria na kupendekeza ajenda ya serikali Katika mifumo ya kirais mtendaji mara nyingi ana nguvu za kukataa sheria Mara nyingi mtendaji katika mifumo yote ana wajibu wa sera za mahusiano ya nje jeshi na polisi na urasimu Mawaziri au maafisa wengine wanasimamia ofisi za nchi kama vile wizara ya nje au wizara ya ndani Uchaguzi wa mtendaji tofauti kwa hivyo ina uwezo wa kupindua mtazamo wa nchi nzima wa serikali

Maafisa wa Marekani wa Forodha na Ulinzi wa Mipaka

Ingawa mashirika ya kijeshi yamekuwepo kwa muda mrefu kama serikali yenyewe dhana la kikosi cha polisi kilicho tayari ni dhana ya kisasa Mfumo wa Uingereza ya Zama za Kati ya mahakama ya jinai ya kusafiri au assize ilitumia kesi za maonyesho na unyongaji hadharani kufanya jamii ziwe na hofu na hivyo kudumisha udhibiti Polisi wa kwanza wa kisasa pengine walikuwa wale wa Paris wa karne ya katika mahakama ya Louis XIV ingawa Polisi wa Mkoa wa Paris ndio wanadai kuwa wao ndio waliokuwa wa kwanza kuvaa sare

Weber yu maarufu kwa kudokeza kwamba taifa ni lile ambalo linadhibiti kihalali utumizi wa kipekee wa vurugu Majeshi na askari wanalinda usalama kufuatana na amri ya serikali au mahakama Maneno taifa lililopangarayika yanaashiria taifa ambalo haliwezi kutekeleza au kulazimisha sera askari wao na majeshi hawana uwezo wa kulinda usalama na amani na jamii inaelekea vurugu pekee wakati serikali inapokosekana

Makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York yana watumishi wa kiserikali wanaotoa huduma kwa mataifa wanachama ya shirika hilo

Asili ya neno Urasimi ni neno la Kifaransa la ofisi bureau na neno la Kigiriki cha Zamani cha nguvu kratos Kama tu wanajeshi na polisi watumishi wa mfumo wa kisheria wa serikali na miili inayounda urasimu wake hufuata maagizo ya Mtendaji Mojawapo ya marejeo kwa dhana yalifanywa Baron de Grimm mwandishi wa Kijerumani aliyeishi nchini Ufaransa Mnamo mwaka wa aliandika

Roho halisi ya sheria nchini Ufaransa ni urasimu amabo marehemu Monsieur de Gournay alikuwa akilalamika sana kuhusu hapa ofisi makarani makatibu wasimamizi na wanaonuia kufanya kazi fulani hawaapishwi kufaidi maslahi ya umma kwa hakika maslahi ya ummayanaonekana kuanzishwa ili ofisi hizo ziwepo

Wasiwasi kuhusu utawala wa kiofisi bado ni kawaida na utendaji wa watumishi wa umma kawaida hutofautishwa na wa kampuni za kibinafsi zinazoendeshwa na lengo la faida Kwa kweli kampuni za kibinafsi hasa zile kubwa pia zina urasimu Mtazamo mbaya wa urasimu kando huduma za umma kama vile elimu afya na shughuli za polisi au uchukuzi wa umma ni kazi muhimu nchi hivyo basi kufanya urasimu wa umma chanzo cha nguvu za serikali Weber aliandika kuwa sifa za kawaida za urasimu wa kisasa ni kuwa maafisa wanafafanua lengo lake wigo wa kazi umefungwa na kanuni usimamizi unajumuisha wataalamu wa wataalamu wa kitaaluma amabo ambao husimamia kuanzia juu kuenda chini wakiwasiliana kupitia kuandika na kufunga uwezo wa wafanyikazi wa umma kufanya watakavyo kwa kutumia kanuni

Katika mifumo ya sheria ya kiraia kama ile ya Ufaransa Ujerumani Italia Uhispania na Ugiriki kuna aina maalum ya Karani wa sheria ya kiraia afisaa wa umma mwenye ufunzi wa kisheria anayelipwa fidia na wanaofanya biasharaa Hii ni picha ya karne ya ya karani wa sheria ya kiraia kama huyo ya mchoraji wa Kiflemi Quentin Massys

Hitimisho la utawala wa sheria ni kuwepo kwa taaluma ya kisheria yenye uhuru wa kutosha wa kuweza kuomba mamlaka ya mahakama huru haki ya usaidizi kusaidiwa na wakili mahakamani uanatokana na hitimisho hilinchini Uingereza kazi ya wakili inatofautishwa na ile ya mshauri wa kisheria Kama mahakama ya Ulaya ya Haki za Binadamu yanavyosema sheria inafaa kupatikana na kila mtu na waty wanfaa kutabiri jinsi sheria itakavyowaathiri Ili kudumisha utaaluma zoezi la sheria kawaida linachungwa na serikali au mwili huru kama vile chama cha mawikili baraza la mawakili au jamii ya sheria Mawakili wa kisasa wanapata utambulisho maalum wa kisheria kupitia taratibu maalum za kisheria km mafanikio katika mitihani yanahitajika na sheria ili kuwa na cheti maalum elimi ya kisheria inayompa mwanafunzi Shahada ya Sheria Shahada ya Sgeria ya Kiraia au Shahada ya Juris Doctor na zinawekwa ofisini kwa kutumia fomu za kisheria za kuapishwa kukubaliwa katika baraza la mawakili Nchi nyingi za Kiisalmu zina sheria sawa kuhusu elimu ya kisheria na taaluma ya kisheria lakini zingine bado zinaruhusu mawakili wenye mafunzo katika sheria ya Kiislamu ya jadi katika taaaluma ua sheria katika mahakama ya hadhi ya kibinasfi Nchini Uchina na katika nchi zingine za ulimwengu unaoendelea hakuna watu wa kutosha wenye mafunzo ya kisheria kufanya kazi katika mifumo ya mahakama iliyopo katika nchi hizo na kufuatana na hilo viwango rasmi si vikali sana

Baada ya kupata kukubalika wakili mara nyingi atafanya kazi katika kampuni ya sheria katika vyumba kama wakili wa kipekee katika wadhifa wa kiserikali au katika shirika la kibinafsi kama mshauri wa ndani Isitoshe wakili anaweza kuwa mtafiti wa kisheria anayepeana uatafiti wa kisheria unapoitishwa kupitia maktaba huduma ya kibiashara au kazi isiyokuwa na muajiri mmoja Watu wengi wenye mafunzo katika sheria walitumia utafiti wao katika taaluma nyingine tofauti kabisa Adhimu kwa zoezi la sheria katika mapokeo ya sheria ya kawaida ni utafiti wa kisheria kujua hali ya wakati wa sasa wa sheria Hili linahushisha kuchunguza ripoti za kesi majarida ya kisheria na sheria Zoezi la sheria pia inahusu kuandika hati kama vile kuiitia kwa mahakama brifu mikataba au amana Majadiliano na ujuzu wa kusuluhisha migogoro ikijumuisha mbinu za ADR pia ni muhimi kwa zoezi la sheria ikitegemea na aina ya taaluma

Maandamano mjini Washington DC wakati wa Harakati ya Haki za Kiraia ya Marekani mnamo mwaka wa

Dhana ya Kiripablikani wakati kulipokuwa na madaraja mbalimbali ya kijamii ya mashirika ya kijamii ilianzia wakati wa Hobbes na Locke Locke aliona mashirika ya kijamii kama watu wenye sheria sawa na mahakama kurejelea yenye mamlaka ya kuamua utata baina yao Mwanafalsafa wa Kijerumani Georg Wilhelm Friedrich Hegel alitofautisha taifa na mashirika ya kijamii burgerliche Gesellschaft katika kitabu chake Vipengele vya Falsafa ya Sawa Hegel aliamini kuwa mashirika ya kijamii na taifa zilikuwa kinyume kabisa katika mpangilio wa nadharia yake ya historia Taifa la kisasa lenye pande hizi mbilimashirika ya kijamii lilizaliwa tena katika nadharia za Alexis de Tocqueville na Karl Marx Siku hizi katika nadharia ya wakati wa baada ya kisasa za mashirika la kijamii lazima iwe chanzo cha sheria kwa kuwa msingi ambapo watu wanaunda maoni na kushwishi yale wanayoamini sheria inafaa kuwa Kama wakili wa Kiaustralia na mwandishi Geoffrey Robertson QC alivyoandika kuhusu sheria ya kimataifa

mojawapo ya vyanzo vyake vya kisasa inapatikana katika majibu ya kawaida ya wanaume na wanawake na mashirika yasiyo ya kiserikali amabyo wengi huunga kwa ukiukaji wa haki za kibinadamu amabyo wengi huona kwenye runinga wakiwa sebuleni nyumbani mwao

Uhuru wa kujieleza uhuru wa kujumuika na sheria zingine nyingi za kibinafsi zinawaruhusu watu kukusanyika kujadili kukosoa na kufanya serikali zao kuwajibika ambapo msingi wa demokrasia ya majadiliano inaibuka Watu wanapozidi kujihusisha mamlaka ya kisheria na na kuwa na uwezo wa kubadilisha jinsi mamlaka ya kisiasa yanapotumika maishani mwao ndivyo sheria inapozidi kuwa halali kwa watu Taasisi ambazo ni za kawaida sana za mashirika ya kijamii ni masoko ya kibiashra kampuni zenye malengo ya kupata faida familia vyama vya kibiashara hospitali vyuo vikuu shule mashirika ya msaada vilabu vya kujadili mashirika yasiyokuwa ya kiserikali vitongoji makanisa na vyama vya kidini

Haki za kibinadamu
Uchumi
Historia
Sayansi ya Kisiasa
Falsafa

Printed sources

See original text in Perseus program

Hamilton Michael S and George W Spiro The Dynamics of Law th ed Armonk NY ME Sharpe Inc ISBN

px Locke John

Online sources

Legal news and information network for attorneys and other legal professionals
Encyclopaedic project of academic initiative in Jurispedia
Legal articles news and interactive maps
WorldLII World Legal Information Institute
CommonLII Commonwealth Legal Information Institute
AsianLII Asian Legal Information Institute AsianLII
AustLII Australasian Legal Information Institute
BaiLII British and Irish Legal Information Institute
CanLII Canadian Legal Information Institute
NZLII New Zealand Legal Information Institute
PacLII Pacific Islands Legal Information Institute

Elimu jamii
Historia
Falsafa

Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika taifa mji au hata dunia mzima siasa ya kimatatifa Sehemu muhimu ya siasa ni majadiliano kati ya watu mbalimbali wenye nguvu au mamlaka

Katika dekokrasia kila mtu ana kiasi fulani cha nguvu na kwa hiyo siasa ya demoskrasia ina maana ya watu wote kujadiliana kuhusu maamuzi

Hapo chini mifumo mingine ya kisiasa huelezwa kifupi

Utawala wa Kifalme ni mfumo wa kiuongozi unaompa mamlaka ya dola na serikali Mfalme Katika mfumo huu madaraka hurithiwa na familia ya kifalme
Utawala wa Kiimla ni mfumo wa kiuongozi unaotoa madaraka yasiyo na mipaka kwa kiongozi Katika utawala huu watu binafsi hawana haki na uhuru wa kimaamuzi
Utawala finyu ni mfumo unaowapa wachache nguvu za maamuzi katika dola na serikaliNafasi ya wachache hawa hutokana na haiba na uwezo wao kiuchumi kijamii kijeshi au kutokana na mafanikio yao katika nyanja mbalimbali za maisha Mfumo huu ni nadra sana katika siku za hivi karibuni Pia waweza kuitwa utawala wa makabaila
Utawala wa Umma ni utawala unaotokana na jamii kuamua misingi ya kujiongoza Mfumo huu wa utawala hujulikana kama Utawala wa Kidemokrasia na umegawanyika katika sehemu nne
Demokrasia Baguzi ni aina ya Demokrasia inayojikita katika kulinda nguvu za kiuchumi zaidi
Demokrasia Duni ni aina ya demokrasia inayotokana na makundi ya watu na kisha kupitia makundi hayo watu kuunda serikali mf chama serikali
Demokrasia Endelevu ni aina ya demokrasia inayotoa fursa ya usawa na kupinga matabaka katika jamii
Demokrasia Shirikishi Katika aina hii ya Demokrasia wachache hupewa dhamana na wengi katika uwakilishi wa jamii katika maamuzi
Demokrasia ni mfumo unatoa fursa ya madaraka kwa umma moja kwa moja au kutokana na kuwakilishwa



Kibao cha Gilgamesh

Ushairi ni utungo wa kisanaa ulio na madhumuni ya kutumbuiza au kuelimisha Tena ushairi ni tawi moja la fasihi andishi Kinyume chake ni nathari

Inawezekana kutunga mashairi yenyewe au kutumia lugha ya kishairi katika aina nyingine za kisanaa kwa mfano tamthiliya au nyimbo

Ushairi una historia ndefu Kwa mfano mwanafalsafa Aristotle katika kitabu chake Ushairi Poetics kwa Kiingereza anachunguza matumizi yake katika hotuba tamthiliya nyimbo na futuhi

Shairi la Beowulf

Wamitila KW Kamusi ya Fasihi Istilahi na Nadharia Nairobi Focus Books

Fasihi

jamii

Makala katika jamii

Msaada

Simulia tatizo

Toka Wikipedia kamusi ya maandishi huru

Ukurasa huu umebadilishwa tarehe

All text is available under the terms of the GNU Free Documentation License

Kamusi elezo ya maandshi huru

Kuingia kwa watumiaji

watumiaji wapya tu

Tatizo limetokea wakati ulipojaribu kuingia Jaribu tena

umeshaingia

Lazima tarakalishi yako ipokee kuki ili uweze kuingia kwenye

Mambo yanayofuatwa na alama ni ya hiari Anwani yako ya baruapepe inawezesha watu wasiliane nako kwa kupitia tovuti bila ya kulazimishwa kwako kufunua anwani yako licha ya hayo anwani yako itaweza kutumika kwa kukupatia neno mpya la siri ukilisahau Jina lako halisi ukitaka kuliingiza litatajwa pamoja na kazi zako

inatumia kuki ili watumiaji waweze kuingia Tarakalishi yako inakataa kupokea kuki Tafadhali ondoa kizuizi hicho baadaye jaribu tena

ANGALIA Unakuwa unahariri nakala ya zamani ya ukurasa huu
Ukiendelea kuihariri mabadilisho yote yaliyofanywa tangu pale yatapotezwa

Tafadhali zingatia kwamba makala yote ya unayoyaandika yanafuata tazama kwa maelezo zaidi
Usipotaka maandishi yako yaweze kuharirishwa bure na kutolewa wakati wowote basi usiyaandike hapa
Unakuwa unaahidi kwamba maandishi unayoyaingia ni yako tu au uliyapata kutoka bure au ni mali ya watu wote USITOLEE MAKALA YALIYOHIFADHIWA HAKI ZAO ZA KUTUMIWA BILA KUPATA RUHUSA HALALI

Sura

Hisabati ni somo inayohusika na idadi upimaji na ukubwa Kwa ujumla ni somo inayohusika na miundo na vielezo

Hisabati inatimiza somo mbalimbali kama hesabu jiometria na aljebra

Chama cha Hisabati Tanzania Chuo Kikuu cha Dar es Salaam



Agano la kale
Arkiolojia
Biolojia
Bombwe
Daktari
Fasihi simulizi
Hadithi
Injili
Jenga
Jiografia
Kemia
Kiislamu
Kiswahili
Kiyahudi
Maarifa
Ngoma
Sheng
Sheria
Siasa
Teknolojia ya chuma
Usanifu
Ushairi

Maeneo penye wasemaji wa Kiswahili
Kiswahili ni lugha ya Kibantu yenye misamiati mingi ya Kiarabu inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki

Lugha hii ina utajiri mkubwa wa misamiati na misemo na mithali na mashairi na mafumbo na vitendawili na nyimbo Nayo inatumika katika mashule kufundishia elimu mbali mbali za dini na dunia na kuna vitabu vingi vilivyotungwa kwa kutumia lugha hii vikiwa vya hadithi au hekaya au riwaya

Lugha ilianza takriban miaka iliyopita katika mazingira ya vituo vya biashara vya pwani ambako wafanya biashara kutoka Uarabuni Uajemi na Uhindi walikutana na wenyeji Waafrika Lugha kuu ya kimataifa ya biashara hii ilikuwa Kiarabu Inaonekana ya kwamba lugha mpya ilijitokeza wakati wenyeji wa pwani waliokuwa wasemaji wa lugha za Kibantu walipopokea maneno mengi hasa ya Kiarabu katika mawasilaino yao Kwa hiyo msingi wa Kiswahili ni sarufi na msamiati wa Kibantu pamoja na maneno mengi ya Kiarabu Imekadiriwa ya kwamba theluthi moja ya maneno ya Kiswahili yana asili ya Kiarabu

Kando na Kiarabu kuna pia athira ya lugha mbalimbali kama Kiajemi Kihindi na Kireno Wakati wa karne ya Ishirini maneno mengi yalipokelewa kutoka Kiingereza

Kwa karne nyingi iliandikwa kwa herufi za Kiarabu sawaHili au lugha sawaHiliya
Sarufi ya kwanza pamoja na Kamusi iliandikwa mnamo na Dr Ludwig Krapf huko Rabai Mpya Mombasa

Kiswahili kilikuwa na lahaja nyingi kutokana na lugha mbalimbali za Kibantu zilizochangia mle Tangu karne ya lugha ilianza kuenea barani kwa njia ya biashara Wakati wa ukoloni wa Uingereza lugha ilisanifishwa kwenye msingi wa lahaja ya Unguja

Hakuna uhakika kuhusu idadi za wasemaji wa lugha idadi zinazotajwa zinatofautiana Wasemaji wa lugha ya kwanza wako labda kati ya milioni hadi na wasemaji wa lugha ya pili zaidi ya milioni sabini Idadi ya wasemaji wa lugha ya kwanza inakua kwa sababu lugha inaenea katika maeneo ambapo lugha nyingine zilikuwa lugha kuu na hasa katika miji ya Tanzania imekuwepo lugha kuu badala ya lugha za kikabila

Kati ya nchi ambapo Kiswahili kinatumika ni Tanzania Kenya Uganda KongoKinshasa Rwanda Burundi Msumbiji Somalia na visiwa vya Bahari Hindi kama Visiwa vya Ngazija Komoro

Kiswahili kimekuwa lugha rasmi katika nchi zifuatazo

Tanzania Lugha ya taifa ni lugha ya shule za msingi lugha ya utawala serikalini na mahakamani inatumika kote nchini kanisani kwenye misikiti kwa redio runinga na idadi kubwa ya magazeti

Kenya ni lugha ya taifa lakini Kiingereza ni lugha rasmi ya Kiutawala Kiswahili ni lugha ya kwanza ya mawasiliano kati ya wanachi wakikutana nje ya eneo penye kabila moja tu ni lugha inayofundishwa lakini si lugha ya kufundisha mashuleni ni lugha inayotumika na polisi na jeshi ni lugha ya kuhutubia wanachi mjini na kitaifa sehemu za ibada makanisani inatumia Kiswahili kuna gazeti moja tu la Kiswahili sehemu za programu redioni na kwenye runinga ni kwa Kiswahili Lugha inachanganywa mara nyingi na Kiingereza na lugha za maeneo au kikabila Hata hivyo baada ya rasimu ya katiba mpya kupitishwa mnamo tarehe Agosti Kiswahili sasa kitakuwa lugha rasmi sawa na Kingereza
Uganda imetangazwa kuwa lugha ya kitaifa tangu iliwahi kuwa lugha ya kitaifa wakati wa utawala wa Idi Amin wakati wa ukoloni ilifundishwa mashuleni ikaelekea kuwa lugha rasmi pamoja na Kiingereza lakini matumizi haya yalipingwa hasa na Waganda hivyo Waingereza waliacha mipango haya Ni lugha ya polisi na jeshi hali ambayo imeleta ugumu kwa lugha kukubalika na wanachi wengi kutokana na historia ya utawala wa kijeshi Uganda watu wengi bado hukumbuka hasa matusi ya wanajeshi waliowatesa wakisema Kiswahili Lakini kuna maeneo ya Uganda ambako Kiswahili kinatumika na watu wengi kama lugha ya sokoni na barabarani Wona UBC WBS tv

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Kiswahili ni kati ya lugha nne za kitaifa pia lugha ya jeshi katika mashariki ya nchi Kiswahili kimefika na misafara ya biashara ya watumwa na pembe za ndovu kutoka Zanzibar na pwani la Tanganyika Imeenea zaidi kati ya mchanganyiko wa wafanyakazi kwenye migodi ya Shaba

Kiasili Kiswahili kilikuwa lugha ya kwanza tu ya wakazi wa miji ya Waswahili kwenye pwani katika sehemu za pwani pia kijijini Baada ya kuenea kimekuwa lugha ya watu wengi mjini hasa Tanzania lakini pia Kenya

Kimeenea zaidi kama lugha ya mawasiliano na biashara pale ambako watu wa makabila mbalimbali wanakutana Pamoja na nchi zinazotajwa hapo juu Kiswahili kinatumika katika Kaskazini ya Msumbiji Kusini kabisa ya Somalia Mashariki ya Burundi Maeneo ya mpaka wa Tanzania kuna pia wasemaji kadhaa huko Malawi na Zambia

Tanzania na Kenya zilipokea wakimbizi wengi waliojifunza Kiswahili lakini hakuna uhakika kama bado kinatumika wakirudi Rwanda Sudan au Somalia

Lugha hii leo imekuwa na umuhimu mkubwa duniani kwa jumla na hasa Afrika kwa sababu ya kuenea kwake nchi mbali mbali na kukusanya kwake watu wa makabila na nchi kadha wa kadha wakaweza kufahamiana kwa lugha moja hasa ilivyokuwa ni lugha mojawapo katika lugha kubwa za Afrika ambazo zinachukuwa mahala pa lugha za kigeni zilizoletwa na Wakoloni kama Kifaransa Kiingereza Kitalia Kireno na kadhalika

Leo imekuwa inatumiwa katika kusambaza habari katika vituo mbali mbali ulimwenguni kama vile Sauti ya Amerika BBC Deutsche Welle Monte Carlo na nchi nyenginezo za Uchina na Urusi na Irani na kwengineko Aidha imekuwa ni mojawapo ya lugha muhimu zinazofundishwa katika vyuo vikuu nchini Marekani Uingereza Ulaya Urusi Uchina na barani Afrika

Lugha ina maendeleo inaweza kukua kukwama au kufa Athira nyingi hutokea bila mpangilio pale ambako wasemaji wanapokea maneno mapya wanaacha kutumia maneno mengine au hubadilisha kawaida ya matamshi au sarufi Haya yote hutokea pia katika uwanja wa Kiswahili

Kuna mzaha unaosimuliwa hasa Tanzania Kiswahili kilizaliwa Unguja kilikua Tanzania Bara kikafa Kenya na kuzikwa Uganda Hali halisi Kiswahili kina maendeleo yake katika nchi hizo zote labda zaidi Kongo Lakini itategemea pia juhudi za serikali kama umoja wa lugha utatunzwa kwa sababu kuna athari nyingi kutoka lugha za kila eneo zinazoingia katika ukuzi wa Kiswahili kwa namna zinazotofauitiana

Kuna taasisi zinazolenga kukuza na kuimarisha Kiswahili kama vile Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili TUKI kwenye chuo kikuu cha Daressalaam pamoja na idara za Kiswahili katika vyuo vikuu vingine vya Kenya na pia Uganda

Tanzania iko Baraza la Kiswahili la Taifa BAKITABaraza la kiswahili Zanzibar BAKIZA Kenya kuna Chama cha Kiswahili cha Taifa CHAKITA BAKITA na CHAKITA pamoja na wawakilishi kutoka Uganda wanaandaa kuundwa kwa Baraza la Kiswahili la Afrika Mashariki BAKAMA

Uchunguzi wa Kiswahili huendelea pia katika idara za vyuo vikuu vingi duniani kwa mfano katika Institut National des Langues et Civilisations Orientales mjini Paris Ufaransa Matumizi yake ni kwa njia ya lahaja za Kingwana

Kati ya shughuli muhimu ni kazi ya kukuza msamiati wa Kiswahili yaani kutafuta maneno mapya au kupanusha matumizi ya maneno yaliyopo ili kutaja mambo ya maisha ya kisasa yaliyobadilika Kutunga kwa kamusi za Kiswahili hupanusha elimu hiyo

Historia ya Kiswahili
Lahaja za Kiswahili

Ashton E O Swahili Grammar Including Intonation London Longmans
Hinnebusch T J Swahili Katika T Shopen mhariri Languages and Their Status uk Cambridge Massachusetts Winthrop
Hinnebusch T J and S M Mirza Kiswahili Msingi wa Kusema Kusoma na Kuandika Lanham MD University Press of America
Nurse D and Hinnebusch T J Swahili and Sabaki A Linguistic History Berkeley and Los Angeles University of California Press
Ohly Rajmund Warsaw Wydawnictwa Uniwersytetu warszawskiego
Jzyk suahili
Zarys gramatyki Wybr tekstw
Teksty suahili w pimie arabskim wraz z wiczeniami i wprowaeniem metodologicznym
Literatura suahili
Ohly R KraskaSzlenk I and Podobiska Z Jzyk suahili Warsaw Wydawnictwo Akademickie Dialog
Wald B Swahili and the Bantu Languages Katika B Comrie mhariri The Worlds Major Languages uk New York Oxford University Press
Whiteley W Swahili The Rise of a National Language London Methuen
Zawawi S Kiswahili Kwa Kitendo An Introductory Course New York Harper Row

Kiswahili lugha moja ya Tanzania Kiingereza
Jifunze Kiswahili Kiingereza
Kamusi Hai ya KiswahiliKiingereza
Kamusi ya Kiswahili Kiingereza
Tovuti kwa Kiitaliano yenye maelezo mafupi kuhusu lugha ya Kiswahili Kozi kwa mtandao na Kamusi ya Kiitaliano Kiswahili
Mwana Simba Kiswahili Hakuna matata KiingerezaKifaransa
Swahili LiteraturFasihi ya Swahili KijerumaniKiswahili
WoerterbuchKamusi KiswahiliDeutsch DeutschKiswahili KijerumaniKiswahili
Vitabu vya Kiswahili na Kijerumani SwahiliBuecher und bungen

Afrika
Lugha za Tanzania
Waswahili


Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Main Page bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Mat bytes
Kiesperanto bytes
Lugha bytes
Hisabati bytes
Lugha iliyotengenezwa bytes
Ngoma bytes
Fasihi bytes
Kemia bytes
Jiografia bytes
Maarifa ya lugha bytes
Dini bytes
Sheng bytes
Historia bytes
Majenzi bytes
Kiswahili bytes
Daktari bytes
Siasa bytes
Lugha asilia bytes
Kiislamu bytes
Mathayo bytes
Jenga bytes
Hesabu bytes

alarabiyya Kiarabu

Lugha ya Kiarabu ni mojawapo ya lugha muhimu sana duniani kwa sababu ya kutumika kwake kama lugha ya kidini kwa mamilioni ya Waslamu duniani na kwa kutumika kwake na zaidi ya nchi ishirini na mbili zilizokuwemo ndani ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu mbali na kuwa ni lugha kale iliyokuwa na athari na taathira kubwa juu ya lugha nyingi ulimwenguni na juu ya ustaarabu na utamaduni wa watu na makabila tofauti tofauti duniani

Kiarabu kwa kawaida huandikwa kwa herufi za Kiarabu

Lugha hii ambayo leo imekubaliwa kama ni mojawapo ya lugha rasmi katika Umoja wa Mataifa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Mkutano wa Kilele wa Kiislamu ni lugha yenye utajiri mkubwa wa misamiati maneno na ufasihi mkubwa wa misemo na udhibiti mkubwa wa sarufi na nahau Ni lugha iliyokusanya aina nyingi za mithali na mafumbo na ina utamaduni mkubwa wa nyimbo na mashairi na misemo nayo inakubaliwa na watu wengi duniani kuwa ni lugha yenye utamu wa matamshi na uzuri wa lafdhi

Kwa kuwa Qurani Tukufu na Hadithi za Mtume Muhammad na Mashairi ya zama za Ujahili ndio yenye kudhibiti lugha hii isiteteleke na kubadilika na kupotea kama nyingi katika lugha za ulimwengu leo baada ya miaka zaidi ya elfu imebakia thabiti kama ilivyokuwa wakati ilipoteremshwa Qurani na mabadiliko yoyote yaliyotokea hayana uhusiano na lugha yenyewe ya Kiarabu bali yana uhusiano na lahaja na vilugha mbali mbali zinazotumika na Waarabu fulani katika sehemu fulani ya nchi au mji Ama lugha rasmi ya Kiarabu basi imedhibitika kulingana na Qurani na Sunnah ili maandishi haya yaendelee kufahamika milele na milele

Leo Kiarabu kinazungumzwa na watu ya zaidi ya milioni kama lugha yao ya kwanza na ni lugha ya sita ulimwenguni kwa wingi wa idadi ya wanayoitumia kila siku katika maisha yao baada ya Kichina na Kihindi na Kihispania na Kiingereza na Kibengali Umuhimu wa lugha hii unazidi kukuwa kila siku kwa sababu ya kutumika kwenye maeneo ya katikati ya ulimwengu baina ya mabara ya kale Ulaya na Asia na mabara mapya ya ulimwengu Amerika ya Kaskazini na Kusini
Ramani inaonyesha nchi ambako ni lugha rasmi ya pekee kijani au lugha rasmi pamoja na lugha nyingine buluu

Kiarabu pamoja na lugha ya Kiebrania ya Wayahudi na Kiaramu na Kiamhari Ethiopia zinatokana na asili moja ya lugha ya Kisemiti Kuna lugha nyingi vile vile ambazo zinatokana na asili hii kama Kiashuri na Kifinisia na Kibabili na kadhalika Baadhi ya hizi lugha zimekufa au kuwa na wazungumzi wachache na kwa hivyo umuhimu wake umekuwa si mkubwa kama ulivyo umuhimu wa lugha ya Kiarabu

Kuna aina tatu kubwa za lugha hii ya Kiarabu Kiarabu Fasihi ambacho kilikuwa kikitumika zama za Ujahili kabla ya kuja Uislamu na kuendelea kutumika baada ya kuja Uislamu katika Qurani na Sunnah za Mtume Muhammad Kiarabu Mamboleo ambacho kinatumika katika maandishi na mazungumzo rasmi baina ya Waarabu wote kwa jumla na Kiarabu Lahaja ambacho kinatumika na watu maalumu katika sehemu fulani za nchi au vijiji na ni lugha ya mahali tu kama vile Kiyemeni au Kimasri au Kishami au Kimaghribi na lugha hizi au lahaja hizi zinakuwa zinatafautiana sana baina yao katika misamiati na matumizi

Nigeria

NigerChad na Africa ya Mashariki

Kiarabu ni katika lugha ya zamani sana nayo pamoja na lugha nyenginezo za Kisemiti zilikuwa zikitumika katika nchi za Mashariki ya Kati Kiarabu ambayo tarehe yake inarudi nyuma zaidi ya miaka ni lugha kubwa yenye misamiati mengi sana na utajiri mkubwa wa maneno na misemo Lugha Fasihi ilianza kuwa na nguvu zaidi baada ya kuteremshwa Qurani kwa lugha hio na kuhifadhiwa Hadithi za Mtume Muhammad na kuwa ndio chanzo cha lugha zote nyinginezo za Kiarabu zilizokuweko wakati huo

Fasihi ya Kiarabu isiyo na tabia ya kidini ilikuwa hasa Ushairi Washairi kama Abu Nuwas Omar Khayyam Hafiz ibn Qayyim alJawziyyah kukumbukwa hadi leo Masimulizi kama Alfu Lela U Lela hayakuwa fasihi yenyewe hata kama yamepata maarufu katika nchi za Ulaya

Maandishi mengine ya Kiarabu yaliyokuwa muhimu sana ni maandiko ya falsafa na sayansi Waarabu walitafsiri maandiko ya Wagiriki wa Kale wakaendeleza ujuzi wao Katika karne zilizopita Ulaya ilipokea sehemu kubwa ya elimu yake kutoka kwa Waarabu

Tangu karne ya na katika karne ya fasihi ya Kiarabu imepata uamsho mkuu Khalil Jibran wa Lebanon yuko kati ya washairi wanaosomwa zaidi kimataifa Nagib Mahfuz wa Misri ni mwandishi Mwarabu wa kwanza aliyepokea Tuzo ya Nobel ya Fasihi mwaka


Lugha za Kisemiti
Lugha za Algeria
Lugha za Irak
Lugha za Lybia
Lugha za Mauretania
Lugha za Misri
Lugha za Moroko
Lugha za Sudan
Lugha za Tunisia
Lugha za Syria

Uislamu kwa Kiarabu alislam ni dini inayotokana na mafunzo ya Mtume Muhammad Wafuasi wa imani hiyo huitwa Waislamu na wanakadiriwa kuwa milioni hivi Hivyo ni dini ya pili duniani yenye wafuasi wengi baada ya Ukristo mwenye wafuasi milioni

Imani ya Waislamu ni kumwamini Mungu mmoja tu anayeitwa Allah Wana kitabu kitakatifu cha Kurani ambayo wanaamini ilifunuliwa kwa Muhammad kutoka mbinguni kupitia malaika Jibrili ni kawaida kusema Kurani iliteremshwa kwa Muhammad

Pamoja na Kurani kuna mafundisho ya Sunna na Hadith ambayo ni maneno ya mtume Muhammad na masimulizi juu ya matendo yake ambayo pengine hutazamiwa kama mwongozo katika Uislamu

Allah kama Mungu pekee ni muumba wa kila kitu Kurani inasisitiza kwamba hana mshirika hana baba wala mwana hakuzaa wala hakuzaliwa na hana mwanzo wala mwisho

Pamoja na amri mbalimbali kuna mfumo wa sheria za kidini zinazoitwa kwa jumla sharia inajumlisha maagizo kuhusu mambo mengi ya maisha uchumi na siasa

Muhammad alizaliwa mnamo mwaka BK kama mtoto wa mfanyabiashara mjini Maka uliopo kwenye Bara Arabu

Kufuatana na mapokeo ya Kiislamu malaika Jibril alimtokea alipokuwa na umri wa miaka yaani mnamo mwaka Kutoka kwa malaika alipokea maneno ya Kurani na ufunuo huu uliendelea hadi mwisho wa maisha yake

Mtume alitangaza yale aliyosikia kwa wafuasi wake na maneno ya Kurani yalianza kukusanywa tayari wakati wa maisha ya mtume Baada ya kifo chake mwaka khalifa wa tatu Uthman ibn Affan alikusanya aya zote na kuziweka katika umbo kamili na Waislamu wanafundisha ya kwamba umbo hili halikubadilika tena na ni sawa na yale aliyotangazwa mtume

Ujumbe uliohubiriwa na Muhammad huko Maka ulipata wasikilizaji wachache lakini viongozi wengi wa Quraishi waliokuwa kabila muhimu ya Maka waliwaona kama hatari kwa Maka na mwaka Waislamu walipaswa kutoka Maka wakahamia Yathrib mji wa jirani

Uhamisho huu unaitwa hijra na tangu khalifa wa pili Umar ibn alKhattab ni chanzo cha kalenda ya Kiislamu

Mjini Yathrib mtume aliendelea kuwa kiongozi wa kisiasa na wa kijeshi Alifanya mapatano na watu wa Yathrib iliyoitwa baadaye madinat annabi ikajulikana kwa kifupi kama Madina

Kutoka Madina mtume alianza kushambulia misafara ya watu wa Maka akawashinda mara kadhaa Wakati huohuo aliwafukuza Wayahudi wa Yathrib

Mwaka viongozi wa Maka walilazimishwa kufanya mapatano na Waislamu na mwaka jeshi la Waislamu iliingia mjini Maka

Mtume alipoaga dunia mwaka sehemu kubwa ya Bara Arabu ilikuwa chini ya Uislamu tayari

Uislamu unawafunza wafuasi wake mambo mengi yanayohusiana na maisha ikiwa yale yanayohusu ibada kama Swala Zakat Saumu na Hija ambazo pamoja na kauli ya Shahada Nakiri kwa moyo na kubaini kwa ulimi kwamba hakuna Mola apasaye Kuabudiwa kwa haki ila Allah na Muhammad ni Mtume wake huitwa nguzo za Uislamu au yale yanayohusu maingiliano baina ya wanadamu yakiwa maingiliano ya kijamii kama ndoa na talaka na ujirani mwema au ya kiuchumi kama biashara au ya kisiasa kama kawaida za kumchagua kiongozi wa dola au ya uhusiano baina ya mataifa mbali mbali ulimwenguni

Uislamu unatazamwa kuwa mfumo kamili wa maisha ya binadamu kiimani kimaisha kisiasa kijamii na kiuchumi

Ibada katika Uislamu ni vile vitendo ambavyo Muislamu anamfanyia Mwenyezi Mungu peke yake kwani ibada yoyote haitakikani iwe na ushirikina ndani yake na wakati itakapokuweko aina yoyote ya shirki basi ibada ile inakuwa haina maana wala thawabu wala ujira wowote ni kazi ya bure

Kwa hiyo kila Muislamu anatakikana wakati anapofanya ibada yake afanye kwa ajili ya Mola wake aliyemuumba akampa kila aina ya neema na kumtukuza kuliko viumbe vingine vyovyote kwa kumpa akili fahamu na elimu

Nguzo tano za Uislamu
Nguzo za Uislamu ni tano na katika madhehebu ya Wasunni wanafundishwa jinsi inavyoonyeshwa hapo chini

Washia hawahesabu shahada kati ya nguzo tano wakiona shahada pamoja na imani ya Kiislamu ni msingi kwa nguzo tano halafu wanaongeza kama nguzo ya tano

Nguzo hizo ziliwekwa taratibu katika mwaka ulioonyeshwa katika mabano shahada sala tano zaka saumu hija

Shahada Nguzo ya kwanza katika Uislamu hujumuisha kutoa kauli mbili Hakuna Mola apasaye Kuabudiwa ila Allah na Muhammad ni Mtume wake Kauli hizo hutolewa pale mwanadamu anapoingia Uislamu
Salat kwa Kiarabu ni sala inayofuata utaratibu maalumu mara tano kila siku Asubuhi mchana alasiri jioni na usiku Kabla ya kuingia katika ibada hii Mwislamu anapaswa kufanya wudhu ambayo ni tendo la kutakasa mwili kwa maji au kama hakuna kwa kutumia vumbi badala yake Salat ina maneno yake na pia namna ya kusimama au kujinama Salat hii ni tofauti na dua au sala ya kuomba kwa hiari
Zakat Nguzo ya tatu ya Uislamu nayo ni ibada inayomuelekeza Mwislamu kuwaangalia Waislamu wenzake kwa hali na mali na kushughulikia mahitaji yao ya maisha kwa kutoa fungu la mali yake na kuwapa wale walio maskini na wasiojiweza ili nao waweze kuishi vizuri
FungaSwaum Wakati wa mwezi Ramadani kila Mwislamu anapaswa kufunga chakula na kinywaji chote kuanzia asubuhi hadi jioni Watoto na wagonjwa hawapaswi kutekeleza wajibu huu Waislamu wanaona maana ya ibada hii kumkurubisha Mwislamu na Mola wake na kumfanya amche na kumuogopa zaidi kwani saumu humsaidia Mwislamu kufahamu shida na taabu ambazo wale wasiokuwa na uwezo wanazipata wakiwa na njaa na hawana cha kukila na kwa hivyo huingiwa na huruma na kuwa na moyo wa kutaka kuwasaidia na kuwaondoshea shida hizo
Hija Kar alhajj Kila Mwislamu mwenye uwezo anatakiwa kufika Maka mara moja katika maisha yake wakati wa mwezi DhulHija Nguzo hii inawapa fursa Waislamu ulimwenguni kukutana na wenzao na kujua hali zao na kupata nafasi ya kuomba maghfira na msamaha kwa madhambi yao katika mkutano mkubwa kabisa wa wanadamu ulimwenguni

Uislamu umeweka kawaida mbali mbali katika maisha wakati watu wanataka kuweka uhusiano fulani baina yao ili mambo yaende vizuri na uhusiano uzidi kuwa mwema baina yao Katika maingiliano yaliyowekewa kawaida na nidhamu katika Uislamu ni mambo yanayohusu

Nikaha au ndoa baina ya Waislamu
Biashara na mambo yanayohusu uchumi
Uhusiano wa kijamii baina ya watu katika mtaa au kijiji au mji au nchi
Uhusiano wa kimataifa baina ya madola mbali mbali yakiwa ya kiislamu au yasiyokuwa ya kiislamu

Kuna mielekeo mikubwa miwili ndani ya Uislamu ambayo ni vikundi vya Wasunni na Washia

Kundi kubwa ni Wasunni waliopata jina kutokana na Sunna kawaida ya mtume takriban asilimia ya Waislamu wote huhesabiwa humo Kati yao kuna madhehebu ambao ni Hanafi Maliki Hanbali na Shafii Tofauti katika mafundisho si kubwa zinahusu hasa sharia na fikh

Kundi dogo zaidi ni Washia ambao wamegawanyika kati yao katika vikundi vingi Washia walijitenga na Wasunni baada ya makhalifa wanne wa kwanza kuhusu swali ni nani anayefaa kuongoza Waislamu Washia ni wale waliosisitiza sharti awe mtu kutoka ukoo wa Muhammad kupitia binti yake Fatima Vikundi vya Washia vinatofautiana juu ya viongozi hawa Jumuiya kubwa ya Washia ni Ithnashara walio wengi huko Uajemi Irak na Lebanoni

cennet Uislamu Kurasa za pekee
Islam Blog

Uislamu

Quran kwa Kiarabu ni kitabu kitukufu cha Uislamu Quran inatazamiwa na Waislamu kama Neno la Allah Mungu Kitabu hiki kwao ni tofauti kabisa na maandiko ya vitabu vya dini nyingine kwa maana hicho kinaaminika kwamba kimeandikwa moja kwa moja na Mwenyezi Mungu kupitia mtume wake wa mwisho Muhammad

Imeandikwa na kusomwa kwa lugha ya Kiarabu pekee kwa zaidi ya miaka

Kadiri ya Qurani Mungu alimuambia Muhammad Na namna hivi tumekufunulia Qurani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Makka na walio pembeni mwake

Lakini kwa vile leo Waislamu walio wengi ulimwenguni hawajui Kiarabu maana halisi ya Quran hutolewa kwa lugha nyingine hivyo kupelekea wasomaji kuelewa vyema yale maneno ya Kiarabu kwenye Quran yana maana gani Vitabu hivyo ni kama kamusi kwa ajili ya Quran hawavisomi hivi kama moja ya sehemu ya Quran tukufu na Waislam ili kuwa badala ya Quran ya Kiarabu

Waislamu wengi wanaamini kwamba tafsiri ile siyo ya Quran tukufu na wala siyo ya kweli ni kopi ya Kiarabu tu iliyotolewa kwenye Quran ya kweli

Sura ya kwanza ya Quran tukufu Sura hii imeandikwa kwa Kiarabu

Waislamu wanaamini kwamba Quran tukufu mtume Muhammad alipewa na malaika Jibrl kwenye pango la mlima Hira kwa kipindi cha zaidi ya miaka ishirini na tatu hadi mauti wake ilipomfikia

Quran tukufu haikuwa kitabu cha maandiko wakati wa uhai wa mtume Muhammad iliwekwa kwa mawasiliano ya kimdomo tu Bimaana watu walihifadhi kichwani

Mtume labda hakuwa anajua kusoma wala kuandika lakini kwa mujibu wa Waislamu swahaba wake Abu Bekr alikuwa akiandika maandiko yale juu ya kitu fulani wakati huo mtume Muhammad yu hai Pale Abu Bekr alipokuja kuwa khalifa ameileta Quran na kuwa kitabu kitakatifu

Uthman ambaye ni khalifa wa tatu ameondoa vipengele ambavyo vilikuwa havihusiani na Quran tukufu

Kuna sehemu katika Quran ambayo inafanya kuwa na sura Kila sura ina namba tofauti ya mistari

Kwa mujibu wa mafunzo ya Kiislam sura kati ya hizi zimeshuka mjini Makka sura kati ya hizi zimeshuka mjini Madina

Miongoni mwa sura zilizoshushwa mjini Medina ni pamoja na AlBaqara Al Imran AlAnfal AlAhzab AlMaida AnNisa AlMumtahina AzZalzala AlHadid Muhammad ArRad ArRahman AtTalaq AlBayyina AlHashr AnNasr AnNur AlHajj AlMunafiqun AlMujadila AlHujraat AtTahrim AtTaghabun AlJumua AsSaff AlFath AtTawba AlInsan

Katika Quran tukufu inasomwa kwamba Wayahudi na Wakristo pia huamini Mungu wa kweli Dini hizi pamoja na Uislamu huitwa za Abrahamu kwa sababu ya mahusiano haya

Kuna baadhi ya kurasa za Quran zinazoelezea habari za mambo ya watu wa katika Biblia Kwa mfano watu wa katika Biblia waliotajwa kwenye Quran ni pamoja na Adamu Nuhu Abraham Lutu Ismaili Yakobo Yosefu Haruni Musa mfalme Daudi Solomoni Elisha Yona Yobu Zakaria Yohane Mbatizaji Bikira Maria na Yesu

Hata hivyo kuna tofauti za muhimu kabisa baina ya Uislamu na toleo la Biblia katika kuelezea habari za aina moja Kwa mfano Quran tukufu inaelezea kwamba Yesu Kristo si Mwana wa Mungu kama jinsi Wakristo wanavyoamini kwa Waislamu alikuwa nabii tu anayeheshimiwa kwa jina la Isa bin Mariamu

Uislamu unafundisha kwamba haya yanatokea kwa sababu maandiko ya awali ya Biblia yamepotea na hivyo kuna baadhi ya watu wameyabadilisha Lakini nje ya Quran hakuna uthibitisho wa fundisho hilo

Historia ya uandishi wa Qurani

Tarjuma ya Qurani Tukufu Kwa Kiswahili na Sheikh Ali Muhsin AlBarwani
Online Quran Project kwa Kiarabu na tafsiri zaidi ya katika lugha pamoja na Kiswahli

Misahafu
Uislamu

Hadithi au Sunnah ni maneno na vitendo ambavyo Mtume Muhammad alikuwa akisema au akifanya katika kipindi chake cha utume Hadithi hizi ni moja ya miongozo ya imani kwa Waislamu Hadithi hizi zinajumuisha pia mambo aliyoyaona au kuyasikia katika muda wa utume wake akalinyamazia kimya au akawa hakulipinga na akalikubali

Muhammad aliishi miaka kama arobaini bila kuwa na imani ya Mungu pekee Kisha Mwenyezi Mungu akamletea mjumbe kutoka kwake aitwaye malaika Jibrili anayeaminika kuwa ndiye aliyempa aya zilizoko katika msahafu wa Waislamu Kurani Inaelezwa kuwa Jibrili alimpa Muhammad aya hizo kwa muda wa miaka ishirini na tatu mpaka alipofariki dunia akiwa na umri wa miaka

Hadithi za Mtume Muhammad zimekusanywa katika vitabu vingi sana na wanazuoni mbalimbali wa Hadithi lakini vitabu vya hadithi ambavyo ni muhimu na vinategemewa na wengi katika Uislamu ni hivi vifuatavyo

Sahih AlBukhari
Sahih Muslim
Sunan AnNasai
Sunan AtTirmidhi
Sunan Ibn Majah
Sunan Abu Daud
Muwatta Ibn Maalik
Musnad Ahmad bin Hanbal

Mtume Muhammad alikuwa hapendelei Hadithi zake ziandikwe wakati mmoja na Kurani yasije yakachanganyika maneno yake na yale ya Mwenyezi Mungu na kwa hiyo Hadithi zilichelewa kuandikwa mpaka baada ya kufariki kwake dunia kwa muda mkubwa kidogo na kwa sababu hii Hadithi zikatawanyika sehemu mbalimbali kulingana na usahihi wake au udhaifu wake au uwongo wake

Kuna Hadithi aina nne kulingana na fahamu na kutegemewa kwa msimulizi wa hiyo Hadithi Hadithi Sahihi Hadithi Hasan Nzuri Hadithi Dhaifu na Hadithi Maudhuu Hadithi ya Uwongo Vile vile kuna aina nyingine za Hadithi zilizogawanyika kwa mujibu wa mambo mengine kama kwa mujibu wa wapokezi au mfululizo wa wasimulizi au idadi ya wasimulizi katika kila sehemu ya mfululizo au kwa mujibu wa simulizi lenyewe na msimulizi wake

Hadithi Sahihi huwa imesimuliwa kutegemewa ukweli wake na dini yake na mtu ambaye anafahamu nini anasimulia na kuieleza hadithi kama alivyoipokea kutoka kwa Mtume Muhammad
Hadithi Hasan au Nzuri huwa inajulikana asili yake na wasimulizi ni watu maarufu
Hadithi Dhaifu huwa ile isiyofikia daraja ya Hasan kwa sababu ya upungufu wa mmoja katika wasimulizi au mfululizo wa wasimulizi haufikii mpaka kwa Mtume unakatika kwa mojawapo ya Masahaba au mmoja katika wasimulizi si wa kutegemewa na kuna kasoro fulani katika mambo haya
Hadithi Maudhuu ya Uwongo ni ile hadithi iliyobuniwa ikatiwa katika Hadithi za Mtume na huwa kawaida inakwenda kinyume na Qurani au Hadithi nyinginezo Sahihi au Hasan au kutonasibiana na maneno yake Mtume au kuwa msimulizi wa Hadithi hii ni mwongo au kuwa msimulizi hakukutana na yule ambaye amesema amepokea kwake katika mfululizo wa wasimulizi waliotajwa au kuweko kasoro fulani katika maelezo au matukio yaliyotajwa ndani ya Hadithi hio

Hadithi Qudsi ni ile hadithi ambayo Mtume Muhammad ameisimulia kutoka kwa Mola wake
Hadithi Marfuu ni hadithi iliyopokewa na mfululizo wa wasimulizi na kufikishwa mpaka kwa Mtume
Hadithi Mauquf ni ile hadithi iliyosimuliwa na masahaba lakini wasiseme kuwa wameipokea kutoka kwa Mtume mwenyewe
Hadithi Maqtuu ni ile hadithi iliyokatika silsila au mfululizo wake

Uislamu
Misahafu

Sanamu ya Kristo mkombozi huko Rio de Janeiro Brazil ni sanamu ya Yesu kubwa kuliko zote zilizopata kutengenezwa

Ukristo ni dini inayomwamini Mungu pekee kama alivyofunuliwa na Yesu Kristo mwanzilishi wake

Dini hiyo iliyotokana na ile ya Wayahudi inayolenga kuenea kwa binadamu wote na kwa sasa ni kuu kuliko zote duniani ikiwa na wafuasi zaidi ya bilioni mbili

Kitabu chake kitakatifu kinajulikana kama Biblia Ndani yake inategemea hasa Injili na vitabu vingine vya Agano Jipya

Chimbuko la Ukristo ni kuwepo kwa mtu aliyezaliwa takriban miaka iliyopita huko Mashariki ya Kati katika kijiji cha Bethlehemu kilichopo hadi hivi leo kwenye mipaka ya Palestina naye alikuwa akiitwa Yesu wa Nazareti au mwana wa Yosefu mchonga samani mama yake akifahamika kwa jina la Bikira Maria

Ukristo ni matokeo ya utume wa Yesu uliopokewa na waliomwamini kuwa ndiye Masiya yaani Mpakwamafuta Kristo kwa Kigiriki mkombozi aliyetimiliza ahadi za Mungu kwa uzao wa Abrahamu

Utabiri wa kuja kwake ulianzia katika bustani ya Edeni pale Mungu alipomwambia mwanamke uzao wako utamponda kichwa nyoka yaani shetani

Musa mwanamapinduzi aliyewakomboa watu wa Israeli kutoka utumwani Misri takribani miaka kabla ya kuzaliwa kwa Yesu ndiye nabii wa kwanza kutabiri wazi ujio wa Masiya au Kristo Kumbukumbu la Torati hususan mstari Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zenu na nitatia neno langu kinywani mwake na atasema nao yote niliyomwamuru

Kuja kwake kulitimia katika Agano Jipya ambalo ni ukamilifu wa yote yaliyotabiriwa katika Agano la Kale Kwani Musa alitumwa kuanzisha Agano la Kale kama maandalizi ya Agano Jipya akikabidhi mifumo mingi ya nje na ndani kwa watawala na waamuzi waliomfuatia watakaoshikilia Agano la kusubiri Masiya wakishirikiana na manabii na makuhani

Yesu alizaliwa miaka kama baada ya Abrahamu Vitabu vya Injili vinaeleza matukio na mafundisho ya Yesu ambayo ndiyo mwongozo wa imani hiyo Maisha na kazi ya Yesu yameibua mambo mengi katika historia Ndiyo sababu kalenda iliyoenea duniani huhesabu miaka kutoka ujio wake huu ni mchango mmojawapo wa Ukristo

Hotuba ya Mlimani na Carl Heinrich Bloch Hotuba ya Mlimani inachukulika na Wakristo kuwa utimilifu wa Torati iliyotolewa na Musa katika Mlima Sinai

Yesu alifanya ishara za kustaajabisha au miujiza Matokeo ni kwamba watu wengi wakamwamini Nikodemu mshiriki mmojawapo wa baraza la Sanhedrini ambayo ilikuwa pia mahakama kuu ya Kiyahudi alivutiwa na kutaka kujua zaidi kuhusu siri ya miujiza hiyo na ujumbe kutoka kwa Mungu kwani yeye alihamasika kuona ishara zile kutoka kwa Mungu
Yesu akamjibu kwamba hakika mtu hawezi kuingia ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili kwa maji na Roho
Pia akajieleza kuwa mpatanishi wa ulimwengu wa dhambi na Mungu na kwamba kila anayemgeukia kwa imani hatapotea bali atarithi uzima wa milele Kristo ni mfano wa nyoka wa shaba aliyetengenezwa na Musa Yohana Hesabu

Akiwa akitembea kando ya Ziwa la Galilaya Yesu alikuta umati wa watu umekusanyika Basi akapanda mashua na kuenda mbali kidogo na ufuoni akaanza kuwafundisha kuhusu Ufalme wa Mbingu kupitia mfululizo wa mifano
Mmojawapo ni hili lifuatalo Ufalme wa Mbingu ni kama punje ya haradali ambayo mtu anaipanda Ingawa ni mbegu ndogo sana inakua na kuwa mti wa mboga kubwa kuliko yote Inakua mti ambao ndege wanauendea wakipata makao katika matawi yake Mathayo Marko Luka Zaburi Isaya

Mtume Paulo anazungumza hivi kuhusu Kristo

Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu ila si hekima ya dunia hii wala ya hao wanaotawala dunia hii wanaobatilika bali twanena hekima ya Mungu katika siri ile hekima iliyofichwa ambayo Mungu aliazimu tangu milele kwa utukufu wetu ambayo wenye kutawala dunia hii hawaijui hata moja maana kama wangalijua wasingalimsulubisha Bwana wa utukufu Lakini kama ilivyo andikwa
Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia
wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu
mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho maana Roho huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuaye ila Roho wa Mungu Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu makusudi tupate kuyajua yaliyokirimiwa na Mungu Nayo twayanena si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamnu bali yanayofundishwa na Roho tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu maana kwake ni upuzi wala hawezi kuyafahamu kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote wala yeye hatambuliwi na mtu Maana Ni nani aliyefahamu nia ya Bwana amwelimishe Lakini sisi tunayo nia ya Kristo Wakorintho

Jumuia ya Wakristo inaitwa Kanisa lililotajwa na Yesu katika Mathayo

Wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu Wala milango ya kuzimu haitalishinda

Ujio wa Roho Mtakatifu

Mara baada ya Yesu kwenda zake katika tukio linalotajwa kupaa kwake mbinguni wafuasi wake wakarudi Yerusalemu yapata mwendo wa sabato na walipoingia huko wakapanda ghorofani walipokuwa wakikaa Petro na wenzake
Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwapo wote mahali pamoja Ukaja upepo toka juu kama upepo wa nguvu ukienda kasi ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi Kukatokea na ndimi zilizogawanyikana kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao Wote wakajazwa na roho mtakatifu wakaanza kusema kwa lugha nyingine kama Roho alivyo wajalia Matendo ya Mitume

Hii ilifuatiwa na Petro na wenzake kuanza kuhububiri ufufuko wa Bwana Yesu na hatimaye kugusa wengi Matendo ya Mitume

Ustawi wa Jumuia ya kwanza ya wafuasi wa Kristo

Na watu walipokuwa wakidumu katika fundisho la mitume na katika ushirika na matendo mengine wengi wakaona ishara nyingi basi nao wakauza mali zao na vitu walivyokuwa navyo na kugawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu wakila pamoja na kushiriki kwa moyo mweupe

Hivyo ndivyo jumuia ilivyozaliwa na kufahamika kama Kanisa Matendo ya Mitume

Kukutanika na kushiriki mafumbo makuu kushukuru na kusifu pamoja na uwepo wa karama za Roho Mtakatifu hufanya Kanisa liwe hai

Mtume Paulo akiandika waraka

Mitume wa Yesu walienea toka Yerusalemu hata Lida Yafa Kaisaria Damasko nk na kuanzisha jumuia nyingi Nazo jumuia kwa bidii za waamini wa mwanzo zikafika Foinike Kipro Antiokia ambako waliitwa Wakristo kwa mara ya kwanza kutokana na waamini wa mataifa mengine kuwazidi wale wenye asili ya Kiyahudi Matendo

Imani na desturi za mikusanyiko hiyo zilitapakaa na hivyo kuanza kusuguana na mapokeo ya jamii mbalimbali zilipopenya Hii inatokana na ukweli kwamba watu wengi wa siku zile tayari walikuwa na imani zao walizokuwa wakizitunza Basi ukaja wakati ambao Wakristo wakaanza kukosoana kuhusu dhamira zao na huduma Ndiyo asili ya nyaraka mbalimbali ambazo zinaunda sehemu muhimu wa Agano Jipya

Viungo ni vingi ila mwili ni mmoja

Mtume Paulo anazungumza hivi

Maana kama vile mwili ni mmoja nao una viungo vingi na viungo vyote vya mwili ule navyo ni vingi ni mwili mmoja vivyo hivyo na Kristo Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja kwamba tu Wayahudi au kwamba tu Wayunani ikiwa tu watumwa au tu huru nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja Wakorintho

Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa wa kwanza mitume wa pili manabii wa tatu waalimu kisha miujiza kisha karama za kuponya wagonjwa na masaidiano na maongozi na aina za lugha Je wote ni mitume Wote ni manabii Wote ni waalimu Wote wanena kwa lugha Wote wafasiri Takeni sana karama zilizo kuu Hivyo nawaonyesha njia iliyo bora Wakorintho

Juu ya Wafu Ufufuko wa Miili na Utukufu Wake

Mtume Paulo anazungumza hivi kuhusu wafu ufufuko wa miili ya utukufu na roho kwa Kanisa la Korintho

Lakini labda mtu atasema Wafufuliwaje wafu Nao huja kwa mwili gani Ewe mpumbavu uipandayo haihuiki isipokufa nayo uipandayo huupandi mwili ule utakaokuwa ile chembe tupu ikiwa ni ngano au nyingineyo lakini mungu huipa mwili kama apendavyo na kila mbegu na mwili wake Nyama yote si nyama moja ila nyingine ni ya wanadamu nyingine ya hayawani mingine ya ndege nyingine ya samaki Tena kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali na fahari yake ile ya duniani ni mbali Kuna fahari moja ya Jua na fahari nyingine ya Mwezi na fahari nyingine ya Nyota maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota Kadhalika na ufufuo wa Wafu Hupandwa katika uharibifu hufufuliwa katika kutoharibika hupandwa katika aibu hufufuliwa katika fahari hupandwa katika udhaifu hufufuliwa katika nguvu hupandwa mwili wa asili hufufuliwa mwili wa Roho

Ikiwa uko mwili wa asili na wa roho pia uko Ndivyo ilivyoandikwa mtu wa kwanza Adamu akawa nafsi iliyo hai Adamu wa mwisho ni Roho yenye kuhuisha Lakini hautangulii ule wa Roho bali ule wa asili baadaye huja ule wa roho Mtu wa kwanza atoka katika nchi ni wa udongo Mtu wa pili ni atoka mbinguni Kama ilivyo yeye wa udongo ndivyo walivyo walio wa udongo na kama alivyo yeye wa mbinguni ndivyo walivyo walio wa mbinguni Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni Ndugu zangu nisemayo ni haya ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa mungu wala uharibifu kurithi kutokuharibika

Angalieni nawaambia ninyi siri Hatutalala sote lakini sote tutabadilika kwa dakika moja kufumba na kufumbuawakati wa parapanda ya mwisho maana parapanda italia na wafu watafufuliwa wasiwe na uharibifunasi tutabadilika Maana Sharti uharibikao uvae kutokuharibika nao huu wa kufa uvae kutokufa Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika na huu wa kufa utakapovaa kutokufa hapo ndipo ndipo litakapokuwa lile neno lililioandikwa

Mauti imemezwa kwa kushinda
Ku wapi ewe mauti kushinda kwako
U wapi ewe mauti uchungu wako

Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu za dhambi ni torati Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana Wetu Yesu Kristo Wakorintho

Hivyo imani katika ufufuko una sura isiyo ya kimaada tena una fahari kama mambo ya mbingu yenye kudumu zaidi na milele yake

Wajibu wa Wakristo

Mtume Paulo anasema hivi kwa Wafilipi

Basi wapendwa wangu kama vile mlivyotii siku zote si wakati mimi nilipokuwapo tu bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu kutaka kwenu na kutenda kwenu kwa kutimiza kusudi lake jema Yatendeni mambo yote pasipo manunguniko wala mashindano mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama wala udanganyifu wasio na hila kati ya kizazi chenye ukaidi kilichopotoka ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu mkishika neno la uzima nipate sababu ya kuona fahari katika Kristo ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure Naam hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu nafurahi tena nafurahi pamoja nanyi nyote Nanyi vivyo hivyo furahini tena furahini pamoja nami Wafilipi

Katika historia ndefu ya Ukristo yalitokea mafarakano mengi waamini wa Yesu wakizidi kutofautiana Makundi makubwa zaidi ni Kanisa Katoliki Makanisa ya Waorthodoksi na madhehebu ya Uprotestanti

Zaidi ya nusu ya Wakristo wote wanashikamana katika imani na sakramenti chini ya maaskofu wenye ushirika kamili na yule wa Roma ambaye kwa kawaida anaitwa papa Kati yao umoja unazingatiwa sana

Wakristo wengi walioishi upande wa mashariki wa Dola la Kirumi na ngambo ya mipaka yake walitengana na Wakatoliki hasa katika karne V na karne XI Hata hivyo msimamo wao wa imani si tofauti sana kwa kuwa wanachanga mapokeo ya awali ya Kanisa la Mitume na la Mababu

Utitiri wa madhehebu ya Kiprotestanti ndio wenye tofauti kubwa zaidi kati yao wenyewe na kati yao na Wakristo waliotajwa kwanza Hiyo ilitokana na msimamo wa msingi wa kutaka kila mmoja aweze kutafsiri Biblia alivyoielewa bila ya kutegemea mapokeo wala mamlaka ya Kanisa

Mama Teresa wa Kolkata
Kutokana na historia ya Kanisa kuwa na mchanganyiko wa mazuri na mabaya wengine wanahisi kuwa halina maana sana Hali hii inajionyesha hasa pale ambapo waamini wengi wameacha kwenda kanisani isipokuwa siku ya Krismasi na Pasaka au kwenye harusi na misiba

Pia kutokana na mgawanyiko wa madhehebu kumekuwa na mkanganyiko kuhusu kazi ya Kanisa la leo

Wakatoliki Waorthodoksi Waanglikana Wamethodisti Walutheri na wengineo wanafuatilia desturi kama walivyozipokea Mtiririko wa ibada zao huandikwa na hujulikana kama Liturugia

Madhehebu mengine hasa yale ya Kipentekoste huwa na ibada ambazo hazijaandikwa kitabuni kiongozi wa ibada wa siku hiyo huja na madondoo yake na mtiririko wa ibada huenda kama Roho atakavyoongoza siku hiyo Kwa sababu hiyo husema kwamba hawafuati desturi au mapokeo Ukiangalia zaidi utaona kuwa ibada zao pia huwa na mtindo na mtiririko fulani kama vile kuimba mapambio ya harakaharaka wakiwa wanapiga makofi kucheza na kurukaruka Mapambio hayo hufuatiliwa na mengine ya taratibu wakiinua mikono kuabudu Inawezekana kusema hao nao wana utaratibu au liturugia yao ingawa haijaandikwa kwenye vitabu

Upande mwingine wanakanisa wanajaribu kuonyesha jitihada zao katika jamii ikiwa ni pamoja na kuleta amani na maendeleo na kutoa misaada ya kijamii Kuna uwezekano kwa madhehebu kadhaa kubadilisha mkazo wao kuutoa kwenye imani tu na kuuweka kwenye huduma za jamii au elimu hii inafanya yaonekane kama moja ya mashirika ya hisani

Binadamu wa karne ya wanahitaji jibu litakalosaidia kuwakwamua kutoka matatizo yao Wenye dini mbalimbali hususan Wakristo wanadai kujua ufumbuzi wa matatizo makuu ya binadamu ingawa wachache tu wameweza kuonyesha dhahiri matatizo yaliyotatuliwa kabisa kwa dini Wakati mwingine wanadini wenyewe wamekuwa chanzo cha matatizo badala ya kuyatatua

Jibu linaweza kupatikana katika maneno ya Yesu mwenyewe aliposema kwamba wafuasi wake ni chumvi ya dunia ambayo ilete ladha katika maisha ya watu lakini kama chumvi hiyo inapoteza ladha yake haifai kitu isipokuwa kutupwa na kukanyagwa kwa dharau Hivyo changamoto ya Wakristo ni kufuata vema mafundisho ya imani yao ili kukidhi hitaji la nyakati hizi la kuishi kwa amani furaha na upendo duniani kote

Ni imani ya Wakristo lakini pia ya Waislamu kwamba Yesu atarudi duniani kwa utukufu ingawa jambo hilo linatafsiriwa kwa namna tofauti

Ukristo na Uyahudi

Ni wazi kuwa Ukristo unahusiana zaidi na dini ya Kiyahudi kwa sababu unatokana nayo na kutumia vitabu vyake vitakatifu Tanakh Haiwezekani kumuelewa Yesu kwa kumweka nje ya mazingira ya Kiyahudi

Dini hizo mbili zilitengana moja kwa moja miaka hivi baada ya Yesu kuaga dunia Ni kwamba Wayahudi katika mkutano wa Jabneh mwaka hivi BK waliamua kuwatenga kama wazushi wananchi wenzao waliomuamini Yesu hasa baada ya kuona hawakusaidia vita vya ukombozi dhidi ya wakoloni Warumi vilivyosababisha maangamizi ya Hekalu na mji wa Yerusalemu mwaka BK Tangu hapo Wakristo hawakushiriki tena ibada pamoja na Wayahudi wakazidi kuzingatia sakramenti ya Kumega Mkate katika Siku ya Bwana Jumapili siku inaposadikika Yesu alifufuka badala ya Sabato Jumamosi siku ya pumziko ya Wayahudi Kabla ya hapo Wakristo wa Kiyahudi walikuwa wanashika siku zote mbili

Ukristo na Ubuddha

Hakuna uhusiano wa kihistoria kati ya Yesu na Ubuddha Hata hivyo mambo kadhaa yanafanana

Yesu alifundisha kuhusu nidhamu mbili zinazompelekea mtu kuwa mwadilifu na hatimaye kuurithi utukufu wa kiroho ambao karama yake ni uzima wa milele hizo ni kumpenda Mungu kwa moyo wako wote na kwa akili yako yote na jirani yeyote kama unavyojipenda mwenyewe Buddha alifundisha hali ya kutodhuru viumbe hai wowote tena kuwa na moyo mkuu wa mapenzi kwa vitu vyote Hii ni miongozo inayolenga mtu atambue tabu anazodumisha yeye mwenyewe kwa matendo yake na upeo ulio na mipaka katika maisha yake ya kila siku

Baada ya hili mafundisho ya Kristo yanatofautiana katika kuchukulia hali hii Kwa mujibu wa Kristo dhambi matendo yenye kukosea kanuni za kiroho na hata za kimaumbile hufutwa na Kutubu wakati katika mafundisho ya Buddha makosa yote yanatokana na kotokuwa makini Hivyo kwa mujibu wa Buddha njia pekee ya kumkomboa mtu na shida zake ni kufuata mwongozo wa Nguzo Nane ambazo humweka katika hali ya kuweza kuamka kiroho wakati utulivu wa kimwili na kiakili unapofikiwa Haya ndiyo yanayofanya Ubuddha kuwa ni njia inayojali sana nidhamu ya mtu kimatendo wakati Ukristo hufuata sana moyo wenye kukiri makosa na kutafuta uadilifu wa kweli wa kiroho Huu ni uzuri wa pekee kutoka kwenye mafundisho ya Yesu Tubuni kwa kuwa saa ya ukombozi ni sasa

Jingine lenye tofauti ni kuwa Kristo hufundisha kuhusu Upendo kwamba ni Mungu kwa kuwa Upendo una maana kuliko hekima yote ya mwanadamu nao ndio unaounganisha na kutunza vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana Hilo hutambulika kupitia Kristo ambaye hujidhihirisha kwa yule mwenye kupokea Roho wa Mungu Upande wa Buddha hukanusha nafsi na pia Mungu akisema Ni Buddha mwenye ufahamu wa milele tena hana nafsi isipokuwa Utupu na ni wenye furaha isiyo kifani izidiyo yote yenye kufanyika ulimwenguni yaani Nirvana kila mtu ni Buddha aliyesahau asili yake ya ndani kabisa

Ukristo na Uislamu

Ukristo na Uislamu vinafanana zaidi kwa sababu Muhammad alifahamu Wayahudi na Wakristo wengi katika nchi yake na katika safari zake Dini hizo zinajulikana kwa kushika imani katika Mungu Pekee muumba wa vitu vyote

Mafundisho ya msingi ya Uislamu ni unyenyekevu kwa Mola mmoja aitwaye Allah mwingi wa rehema na mwingi wa fadhila nguzo ya Uislamu ni kumuabudu Katika Uislamu unyenyekevu wa mtu katika kumcha Mola kwa ibada na swala humpa kukirimika na kuhifadhika kwa Mola wake mwenye fadhila ambaye atamtunuku haki yake Naye mnyenyekevu kwa Mola ataishi kuona utukufu mwingi wa Mola wenye kutajwa katika Kurani kwa majina ya Allah Kati ya sifa na utukufu huo ulio na majina mengi baadhi yake ni Al Rahman kwa Kiarabu mwenye rehema Al Nur Mwenye Nuru nk Hayo hufanana na neno la Nuru ya Bwana rehema na ukombozi kuwa utukufu wa Mbingu katika mwongozo wa Kikristu

Pia Uislamu unafundisha udugu miongoni mwa Waislamu yaani mzizi wa neno linalotumika sana katika Kuran Waly Wala Wilayat Mawla Awla katika kueleza jinsi Mwislamu apasavyo kuishi karibu na mwenzake Nalo husisitiza upendo na kulindana kwa heri na pia kuepushana na shari Hilo linafanana na upendo ambao katika Ukristo ndio adili kuu kuliko yote

Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika kama sina upendo mimi si kitu kabisa Wakorintho

Lakini katika Ukristo upendo hauna mipaka wala masharti Unatakiwa kuenea kwa maadui pia na kusamehe kila mara kufuatana na mfano wa Baba wa Mbinguni

Mwislamu kadiri ya wingi wa unyenyekevu na usafi wa moyo wake huakisi sifa za Mola wake Uislamu hufundisha kuhusu vita vya ndani ambavyo muumini hupigana na nafsi yake yenye matamanio ya chini ambayo huzaa chuki dhuluma wivu na maovu mengine ili kuishinda kwa utukufu wa Mola na kudumisha dini mwongozo yake katika ngazi zote za maisha Kabla yake Yesu alihimiza wote wafuate mfano wake wa upole na unyenyekevu wa moyo akitoa kielelezo katika Heri Nane za hotuba ya mlimani Tofauti ya msingi ni kuwa kwa mujibu wa Kristo ni kwa neema ya imani katika Neno la Uzima kwamba mtu hukombolewa kutoka matamanio yake ya kibinadamu mbali ya kwamba anapaswa kujitahidi asije akapotewa na neema hiyo na kurudia utumwa wa dhambi

Dini


Swahili wikipedia logo gfdl by node

Nembo

Oct Pteron uploaded Afrikaramaniyaduniapng
Sep Node ue uploaded Wikipng Swahili wikipedia logo GFDL Translated text by node This logo is a trademark of the Wikimedia Foundation
Sep Hashar uploaded Wikipng new logo
Sep Node ue uploaded Swwikilogopng Swahili wikipedia logo gfdl by node

new logo

Nembo
Wikipedia

nchi ambako Kiingereza ni lugha rasmi lakini si lugha ya kwanza ya watu wengi Kiingereza kipo pia kati ya lugha rasmi za Umoja wa UlayaKiingereza ni lugha ya Kigermanik cha Magharibi iliyokua nchini Uingereza Leo zaidi ya wasemaji milioni mia nne duniani wanazumgumza Kiingereza kama lugha ya kwanza Watu wengi wanazumgumza Kiingereza kama lugha ya pili kwa sababu ni lugha muhimu sana kwenye nyanja za sayansi na uchumi wa kimataifa

Kiingereza ni lugha rasmi ya pekee katika nchi za Uingereza Marekani Australia New Zealand Jamaica na nchi zingine Kiingereza ni lugha rasmi pamoja na lugha nyinginezingine katika nchi nyingi kwa mfano Kanada na Kifaransa India na Kihindi na lugha za majimbo Ireland na Kigaelik Philippines na Kitagalog

Nchi nyingi za Afrika zinatumia Kiingereza kama lugha rasmi lakini ni Waafrika wachache isipokuwa Waafrika Kusiniwanaosema kuwa ni lugha ya kwanza Nchi hizo ni Afrika Kusini Ghana Gambia Lesotho Liberia Kamerun Kenya Namibia Nigeria Sierra Leone Swaziland Zambia na Zimbabwe Kiingereza kinazumgumzwa pia nchini nyingine za Afrika ambapo sio lugha rasmi Lugha nyingi za Afrika zimeazima maneno ya Kiingereza Maneno haya yamerekebisha sauti ya lugha nyingine kwa mfano Kiingereza train Kiswahili treni

Lugha ya Kiingereza kilianzia huko Uingereza kutokana na kuingiliana kwa lugha mbalimbali hasa lugha za kale za Ujerumani Denmark na Ufaransa

Kusini ya kisiwa cha Uingereza ilikuwa sehemu ya Dola la Roma hadi mwanzo wa karne ya tano Wenyeji walitumia lugha ya Kikelti pamoja na Kilatini ya Waroma hasa mjini

Baada ya kuondoka kwa Waroma kisiwani makabila kutoka Ujerumani wa Kaskazini na Denmark walianza kuvamia kisiwa Katika mwendo wa karne mbili waliteka sehemu kubwa ya Uingereza isipokuwa sehemu za magharibi kama vile Cornwall na Wales na sehemu za Kaskazini penye Waskoti Wavamiaji walileta lugha zao za Kisaksoni na Kianglia Ujerumani wa Kaskazini zilizounganika kuwa lugha ya Kiingereza cha Kale Inaonekena ya kwamba wenyeji walio wengi walianza kutumia lugha ya watawala wapya wengine waliuawa au walihamia sehemu zisizo chini ya WaangliaSaksoni

Lugha hii iliathiriwa mara mbili Kwanza ndio Wadenmark waliojaribu kujenga ufalme wao kisiwani Waliteka sehemu za Uingereza ya Magharibi Kiasi cha maneno kutoka lugha yao kimeingia Kiingereza cha kale kama Wales

Mwaka jeshi la Kinormandy kutoka Ufaransa wa Kaskazini walivamia na kuteka Uingereza Wanormandy walikuwa wa asili ya Skandinavia lakini walikuwa wameshaanza kutumia lugha ya Kifaransa cha kale Wanajeshi hawa walikuwa mabwana wapya wa Uingereza wakitumia Kifaransa chao cha Normandy Kwa karne kadhaa lugha mbili zilitumika kandokando Kiingereza cha KiangliaSaksoni cha watu wa kawaida na kile Kifaransa cha Kinormandy cha tabaka ya watawala Kwa jumla watawala walianza kutumia lugha ya raia lakini lugha hii ilibadilika pia kwa kupokea maneno mengi kutoka kwa Kifaransa Kuna makadirio ya kwamba zaidi ya theluthi moja ya maneno yote ya Kiingereza ni za asili ya Kifaransa

Kipindi hiki cha kuingiliana kati ya Kifaransa cha mabwana na lugha ya kawaida kimeleta Kiingereza cha Kati Hadi leo asili ya maneno kutoka Kijerumani na Kifaransa ni wazi kabisa Mfano mzuri ni maneno tofauti ya wanyama kadha na nyama yao ngombe huitwa cow sawa na Kijerumani wa Kaskazini Kau lakini nyama yake ni beef kutokana neo la Kifaransa kwa ngombe boeuf vilevile sheep kwa mnyama ya kondoo na mutton kwa nyama yake Kijerumani ya Kaskazini Schaap Kifaransa mutton vilevile swine pork nguruwe und calf veal ndama Wakulima wafugaji walitumia lugha yao kwa mnyama mabwana wasiogusa mnyama lakini kula nyama yake waliendelea kutumia neno la kifaransa kwa ajili ya mnyama yuleyule Maneno yote mawili yaliingia katika Kiingereza cha Kisasa lakini kwa mambo mawili tofauti

Kiingereza cha kisasa kimeanza na tafsiri ya Biblia ya William Tyndale baadaye na washairi wakuu kama William Shakespeare Teknolojia ya uchapaji vitabu ilisambaza lugha hii nchini kote na kupunguza athira ya lahaja mbalimbali Wakati ule Kiingereza kilipokea pia maneno mengi kutoka lugha za Kilatini na Kigiriki zilizokuwa lugha za taaluma na sayansi hadi karne ya kote Ulaya

Kiingereza cha kisasa cha leo kimeendelea kurahisisha lugha Lakini urekebisho wa tahajia umeshindikana hadi leo hata kama kulikuwa na majaribio mbalimbali Kutokana na historia yake Kiingereza kimebaki na tahajia isiyolingana na matamshi ya maneno Mwandishi George Bernhard Shaw alionyesha tatizo hili kwa pendekezo la dhihaka Neno la fish samaki liandikwe ghoti gh kama sauti ya f katika cough o kama sauti ya i katika women na ti kama sauti ya sh katika nation

Tangu karne ya idadi kubwa ya wasemaji wa Kiingereza hawakuishi tena Uingerezea bali Marekani Wakati wa karne ileile Kiingereza kilikuwa lugha ya utawala katika maeneo makubwa ya koloni za Dola la Uingereza Baada ya koloni kuwa nchi huru mara nyingi Kiingereza kimeendela kuwa lugha rasmi za nchi hizi

Kutokana na matukio haya yote Kiingereza kimekuwa leo lugha ya kwanza ya mawasiliano duniani hata kama si lugha yenye wasemaji wengi wa lugha ya kwanza

en Muhtasari kuhusu Kiingereza kwenye Ethnologue
Kamusi Hai ya Kiingereza Kiswahili Kiingereza
en More than English words recorded by a native speaker
en ReRomanization of English

Kiingereza
Lugha za Kigermanik
Lugha za Ulaya
Lugha

Afrika duniani

Afrika ni bara la pili duniani kwa ukubwa likiwa na eneo la kilometa mraba na wakazi bilioni mwaka Asia ndiyo bara pekee kubwa kushinda Afrika

Afrika kutoka sateliti
Neno Afrika limetokana na lugha ya Kilatini ya Waroma wa Kale Waroma kwa jina hilo hawakumaanisha bara lote bali eneo katika Tunisia ya leo tu Asili yake ni kabila la Afrig lililoishi sehemu zile

Wakati huo Wagiriki wa Kale walitumia zaidi jina la Libya kwa ajili ya nchi kusini ya Bahari ya Mediteraneo Maeneo ya ndani kuelekea kusini mara nyingi yaliitwa kwa jina la Ethiopia linalomaanisha nchi ya watu weusiweusi kwa Kigiriki aithiops aliyechomwa na jua

Katika ramani za kale kutoka Ulaya maneno yote matatu ya Afrika Lybia na Ethiopia yanapatikana yakitumika kama jina la bara Jina la Afrika limekuwa kawaida kuanzia karne ya BK

tazama makala Lugha za Afrika

Zaidi ya lugha elfu za Kiafrika zinazungumzwa katika Afrika leo

Lugha za Kibantu kwa mfano Kiswahili ni lugha muhimu katika Afrika ya Kusini Afrika ya Kati na Afrika ya Mashariki

Kiarabu ni lugha muhimu Afrika ya Kaskazini

Lugha za Ulaya zinazumgumzwa pia hasa Kiingereza Kifaransa na Kireno

Kiafrikaans ni lugha ya pekee ya Afrika Kusini yenye asili ya Ulaya

Tazama makala Orodha ya nchi za Afrika

History of Africa Marco Notari for Africa
Maria Petringa Brazza A Life for Africa ISBN

Historia ya Afrika
Maziwa ya Afrika


Bara

Kuki

Kuki ni tafsiri ya muda ya neno la Kiingereza cookie

Maana yake asili ni biskuti lakini neno la kuki linatumika ili kompyuta yenye kurasa za tovuti iweze kuwasaliana na watazamaji
Programu za tovuti hizi inahifadhi habari kadhaa za mtazamaji au mtumiaji km jina la mtumiaji neno la siri ruhusa mapendekezo kwenye kompyuta ya mtazamaji mwenyewe Hivi mtazamaji anatambuliwa kila wakati anaingia kwenye tovuti hii

Pendekezo la kuki limepelekwa mbele na Mradi wa Kilinux Linux na Open Office kwa Kiswahili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Mradi wa kampuni ya Microsoft ya kuswahilisha programu ya Windows umependekeza kutumia neno kidakuzi pamoja na kuki

Orodha ya maneno ya tarakishi ya mradi wa Kilinux kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Intaneti

Panzi ni aina ya mdudu anayekula mimea Panzi waainishwa katika nusuoda Caelifera ya oda Orthoptera Wanachupa mbali kwa kutumia miguu yao ya nyuma ambayo ina nguvu sana Wengi wanaweza kuruka angani Panzi wana vipapasio vifupi kuliko mwili wao Panzi wakubwa na ambao wanajikusanya kwenye makundi wanaitwa nzige

Panzi jike wana maumbile yanayowawezesha kuchimba ardhi na kutaga mayai yao ndani ya vibumba Vibumba vya mayai huweza kuwa na mayai kumi na tano hadi zaidi ya mia moja Mayai ya panzi aina nyingi huingia kwa diaposi kupitia majira ya baridi au kiangazi Hali ya hewa ikiwa nzuri mayai yaendelea kupevuka halafu tunutu wanatoka Tunutu panzi wachanga waambua ngozi zao mara tano mpaka mara saba kufuatana na aina yao Kila hatua ya ukuaji ni kubwa kuliko ile iliyotangulia Wakati wa uambuaji wa mwisho panzi mkubwa atokea na kuwa mpevu ndani ya siku au wiki chache

Kuna wadudu ambao wanafanana na panzi lakini wana vipapasio virefu kuliko mwili wao Aina moja kati yao anaitwa nsenene na huliwa na watu Jike ana umbile kama mfuo kinachofanana na kitara Anataga mayai juu ya au ndani ya mimea

Panzi huliwa sehemu nyingi duniani kwa sababu wana virutubisho protini vingi Wanajeshi huambiwa wakamate panzi na kuwala wakipungukiwa chakula

ImageAcanthacris ruficornis citrinajpgAcanthacris ruficornis citrina
ImageAcorypha clara malejpgAcorypha clara
ImageAcorypha unicarinata femalejpgAcorypha unicarinata

ImageAcrotylus blondelijpgAcrotylus blondeli
ImageAiolopusthalassinusjpgAiolopus thalassinus
ImageHeuschrecke gro jpgAnacridium aegyptium

ImageBrachycrotaphus tryxalicerus femaleJPGBrachycrotaphus tryxalicerus
ImageCannula gracilis femalejpgCannula gracilis
ImageCatantops sylvestris malejpgCatantops sylvestris

ImageChirista compta malejpgChirista compta
ImageCryptocatantops haemorrhoidalis malejpgCryptocatantops haemorrhoidalis
ImageEucoptacraanguliflavamalejpgEucoptacra anguliflava

ImageRomalea micropterajpgRomalea microptera
ImageLocust Stethophyma grossum malejpgStetophyma grossum dume
ImageLocust Stethophyma grossum femalejpegStetophyma grossum jike

Panzi na jamaa
Wanyama wa Biblia

Nzige ni jamii ya panzi wenye uwezo wa kujikusanya kwenye makundi makubwa na kuruka umbali mrefu kwa pamoja Nzige wanapokuwa wametawanyika mmoja mmoja huishi kama panzi wa kawaida Wanapozaliana na kuongezeka idadi hujikusanya katika makundi Makundi ya tunutu husafiri kuelekea upande mmoja na kula majani wanakopitia Makundi ya nzige wakubwa huweza kufikia idadi zaidi ya bilioni na huruka umbali mrefu na kuharibu mazao wanakotua

Anacridium melanorhodon
Anacridium m melanorhodon Nzigemiti wa Kisaheli
Anacridium m arabafrum Nzigemiti wa Kiarabu
Anacridium wernerellum Nzigemiti Mabawameusi
Dociostaurus maroccanus Nzige wa Maroko
Locusta migratoria Nzige msafiri
Locustana pardalina Nzige kahawia
Nomadacris septemfasciata Nzige mwekundu
Schistocerca gregaria Nzigejangwa

Calliptamus italicus
Chortoicetes terminifera
Nomadacris succincta
Schistocerca americana

FileAnacridium melanorhodon arabafrumjpgNzigemiti wa kiarabu
FileLocusta m migratorioides femalejpgNzige msafiri
ImageSGR layingjpgNzigejangwa

FileCalliptamus italicusjpgItalian locust

Panzi na jamaa
Wanyama wa Biblia

Mtume Muhammed jinsi alivyotengeneza Kaaba huko Makka picha mnamo mwaka kutoka Asia ya Kati
Mtume Muhammed jinsi alivyosali mbele ya Kaaba katika picha za Kiosmani uso wa mtume hufichwa mara nyingi tangu karne ya BK

Muhammad kwa Kiarabu Mwenye kusifika sana jina kamili kwa kirefu ni Muhammad bin Abd Allh bin Abd alMualib alHshim anaaminika katika dini ya Uislamu kuwa ni mtume wa mwisho wa Mungu Allah kwa binadamu

Muhammad alizaliwa yatima kwani baba yake alifariki kabla yeye hajazaliwa Hakuishi sana na mama yake Amina kwa kuwa naye alifariki dunia Muhammad akiwa na umri wa miaka sita

Baadaye akachukuliwa na babu yake Abdul Muttalib na kuishi naye kwa muda wa miaka miwili kisha babu yake naye akafariki

Kazi ya kumlea Muhammad ilimwangukia ami yake Abu Talib ambaye ndiye aliyeishi naye mpaka ukubwa na kumuoza na kumpa himaya wakati alipoanza kazi ya kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa watu

Kadiri ya hadithi za Kiislamu ilipokua karibu atadhihiri Mtume mapadri wa Kinasara na makuhani wa Kiyahudi waliokuwa wakikaa Bara Arabu walikuwa wakiwatahayarisha majirani wao wa Kiarabu waliokuwa wakiabudu sanamu wakiwaambia Karibu ataletwa Mtume katika nchi yenu hii abatilishe hii ibada yenu mbovu ya sanamu Walipoambiwa hivi wale Waarabu waliwauliza jina la Mtume huyo wakawajibu kuwa jina lake litakuwa Muhammad Kwa hivyo kila mwenye kusadiki hayo alimwita mwanawe Muhammad

Lakini hayakusikilizana majina haya ila kwa baadhi ya Waarabu waliokua wakikaa Shamu tu na Najran Yaman ambako mapadri wengi walikaa na vilevile katika Madina ambayo nusu ya wakazi wake walikuwa Wayahudi

Hata lilipoanza kutangaa jina la Mtume waliokuwa wamekwisha kuitwa kwa jina hilo walikuwa wachache tu Bara Arabu nzima

Inasemekana Mtume aliinukia tangu utotoni kwake juu ya sifa zake nzuri na ukomavu wa akili ya kiutu uzima hakupata kufanya vitendo vya utoto umri wake wala kuazimia kuvifanya ila mara mbili tu ambazo mara mbili zote hizo Mwenyezi Mungu alimhifadhi navyo

Kitendo chenyewe alichokiazimia kukifanya mara mbili zote hizo na Mwenyezi Mungu akamhifadhi nacho ni kutaka kwenda kukesha katika ngoma za arusi mbili za marafiki wake waliooa katika mji wa Makka

Lakini Mungu alimpa usingizi mkubwa katika masiku yote hayo mawili hata hakuweza kufumbua jicho wala kunyanyua miguu kwenda mahali Hajapata kuhudhuria hata mara moja katika ibada za kuabudu sanamu wala kula chakula kilichochinjwa kwa ajili yao Moyo wake ulichukizwa na hayo na mambo mengine yaliyo mabaya

Tangu udogo wake Mtume aliondokea na sifa nzuri ambazo hapana hata mmoja katika hirimu zake aliyekuwa nazo zote Kila sifa zinazohesabiwa kuwa ni njema na Waislamu ndizo alizokuwa nazo tangu utoto wake

Mkewe Aisha alipoombwa kutaja kidogo sifa za Mtume alisema hivi Sifa zake ni zile sifa nzuri zinazosifiwa na Qurani na katika Qurani zimetajwa chungu ya sifa zilizo nzuri

Mtume mara nyingi alikuwa akisema Sikupata kufanya hata siku moja yale mambo waliyokuwa wakiyafanya makafiri Kwa hivyo yeye hakupata kuabudu sanamu kulewa kuzini kucheza kamari wala hakumdhulumu mtu kitu chake na kama haya

Lakini alikuwa msemakweli mwaminifu mpole na mwenye haya na sifa nyingi nyinginezo bora kama hizi Watu wa Makka walikuwa wakimsifu kwa tabia zake hata wakampa jina la Muhammad AlAmin mwaminifu Alikuwa hatajikani ila kwa jina la AlAmin

Wakubwa na wadogo walikuwa wakimheshimu na kumpa amana zao kuwawekea hata baada ya utume

Makureshi ni watu wa biashara kila Kureshi alipata kufanya kazi hii

Safari moja baadhi yao walipokuwa wakienda Yaman katika biashara zao baba yake mdogo wa pili Bwana Zubeyr alimshauri ikiwa atapenda kusafiri Mtume aliridhia akenda naye mpaka Yaman wakakaa huko muda wa siku tatu tu kisha wakarejea wakati huu Mtume alikuwa mtoto wa miaka tisa

Hata alipotimia miaka mwaka alisafiri tena pamoja na baba yake mdogo mwingine Bwana Abu Talib safari hii waliazimia kwenda Shamu lakini walipofika Busra mji wa kusini kabisa katika nchi ya Shamu walikutana na padri jina lake Bahyra ambaye alimkataza asisogee na mwanawe zaidi kuliko hapo akamwambia Mtoto huyu namwona ana alama zote za Mtume aliyetabiriwa kuwa atakuja basi naona ni hatari kubwa akienda Shamu asije akauawa na Wayahudi huko Nakusihi sana urejee naye au umpe mtu mwaminifu arejee naye nawe uende katika biashara zako Abu Talib alimpa mtu arejee naye Makka naye akaendelea na safari yake

Huyu padri Bahyra alikuwa mwanachuoni wa Kinasara na alimbashiri Mtume lakini hakuwahi kumwamini alipoanza utume ila mwanafunzi wake Salman AlFarsy Mwajemi mara alipopata habari ya kupata utume wake alisilimu na aliusaidia Uislamu katika mambo mengi

Baada ya kutimia miaka Mtume aliingia katika kufanya biashara ndogondogo yeye na mwenziwe Saib bin Yazid lakini biashara yao walikuwa wakiifanyia katika miji iliyokuwa karibu na Makka tu Alipata sifa kubwa ya uaminifu na ukweli katika biashara zake hizi Mshirika wake huyu alisilimu siku ilipotekwa Makka na Mtume alifurahi sana kwa kusilimu rafiki yake huyu

Muhammad hakuwa akihudhuria sikukuu za Wapagani tangu kufahamu kwake Alikuwa akipenda kukaa peke yake Kufanya haya kulikuwa kukimwonjesha raha kubwa kuliko kutoka mbele za watu akaona yale mambo yao mabaya aliyokuwa akiyachukia Kila usiku ukicha alikuwa akizidi kuyachukia Lakini alikuwa hajui la kufanya

Hata alipotimiza miaka hakuweza tena kustahimili kuona zile ibada za sanamu na tabia mbovu walizokuwa nazo wenziwe ilivyokuwa hana la kufanya katika kuzizuia alifanya shauri kuuacha mji wa Makka na kwenda porini kukaa

Akapata pango zuri katika Jabal Hira Kaskazini ya Makka inapata maili toka huko Makka Akawa akikaa huko kwenye Jabal Hira kwa muda wa wiki nyingi kisha hurejea Makka kuja kumtazama mkewe wanawe na jamaa zake wengine na vile vile kwa ajili ya kuchukua chakula kinapokuwa kimekwisha

Wakati mwingine akikaa siku nyingi sana huko porini hata humpasa mkewe Khadija kwenda kumsikiliza na mara nyingine alikuwa akifuatana naye pamoja na watoto wao

Alidumu katika hali hii muda wa miaka miwili na kitu

Baadaye alisimulia kuwa katika mwezi wa Ramadhani Jumatatu katika mwaka wa unusu wa umri wake alimuona mtu kamsimamia mbele yake bila ya kumuona wapi katokea akamwambia Soma Mtume akamjibu Mimi sijui kusoma kwani sijapata kujizunza Akaja akamkamata akambana akamwambia tena Soma Mtume akamjibu jawabu yake ileile Hata mara ya tatu akamwambia Soma Iqraa Bismi Rabbik akamsomea sura ya mpaka kati yake kisha Mtume akaisoma kama alivyosomewa Hii ndiyo sura ya kwanza kushuka katika Qurani ingawa haijawekwa mwanzo

Mara yule mtu malaika akaondoka machoni pake asimwone kaenda wapi naye akarejea kwake hofu imemshika

Alipofika nyumbani Khadija alidhani ana homa akamfunika nguo gubigubi akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka Homa ilipomwachia alimweleza Khadija yote yaliyomtokea naye akamtuliza moyo wake akamyakinishia ya kuwa hapana lolote baya litakalomzukia

Mara Bibi huyu akaondoka akaenda kwa jamaa yake Waraqa bin Naufal akampa habari yote iliyompata mumewe Naye akamwamrisha amwite na Mtume akaenda akamweleza habari yake yote Bwana Waraqa akamwambia Huyo ndiye Jibril aliyemshukia Nabii Musa na Nabii Isa Basi jibashirie kuwa wewe ni Mtume wa Umma huu Nami natamani kuwa hai nikuone unavyosimama kuwatengeneza jamaa zako Inshaalla nitakuwa mkono wako wa kulia

Wakarejea kwao hofu yote imemtoka Baada ya kuazimia kuwa hatakwenda tena kule pangoni

Pale pale akaondoka akenda pangoni mwake ili aonane na malaika tena ingawa alikaa huko muda mrefu

Siku ile ya kupata Utume inawafiki mwezi wa Desemba

Huyu Waraqa hakuwa akiabudu dini ya sanamu bali alikuwa Mkristo alipokuwa akisoma vitabu aliona kutatokea Mtume mwingine ndiyo maana alipohadithiwa habari ile mara moja akaamini kuwa aliyemjia Mtume ni Jibril

Muhammad aliishi Makka kwa muda wa miaka arubaini katika hiyo akiwa ni mtu wa kawaida kabla ya kupewa utume na akiwa ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu

Maisha yake Makka yalikuwa ya taabu tangu utotoni mwake kwani alizaliwa yatima kisha alipokuwa katika ujana wake alikuwa akifanya kazi ya kuchunga mbuzi na kondoo wa watu wa Makka kwa vijipesa kidogo mpaka alipofika umri wa miaka ishirini na tano akapata kazi ya kumfanyia biashara Khadija bibi mtukufu wa Kikureshi ambaye baadaye alikuja kuwa mkewe na kuzaa naye aghlabu ya watoto wake

Katika miaka aliyoyaishi hapo Makka baada ya kupewa utume Muhammad alipata kila aina ya mateso na masumbuko juu ya nafsi yake na juu ya wafuasi wake naye alisubiri na kustahimili kila aina ya taabu na shida kwa ajili ya Mola wake mpaka Mwenyezi Mungu alipompa amri ya kuhama mji huo na kuelekea Madina

Katika muda huu alipokuwa Makka wengi katika jamaa zake na watu wa makabila mengine wa matabaka mbalimbali za jamii waliingia dini yake

Mwaka Wakureshi wakiona hasara katika mafungamano yao na Waarabu wengine wenye kuabudu miungu mingi kwa dukuduku zao zilimfanya Muhammad ahame pamoja na sahibu wake Abubakar Assiddiq na wafuasi wake hivi akaishi Yathrib mji ambao ulikaliwa na Waarabu na Wayahudi pamoja na ambao baadaya ukaitwa Madinat alNabi yaani Mji wa Nabii kifupi Madina

Mwaka huo ukawa wa kwanza katika Kalenda ya Kiislamu inayotumika tangu wakati wa halifa Omar ibn alKhattb hadi leo

Mtume Muhammad baada ya kupewa amri ya kuguria Madina aliondoka na kuhamia mji huo ambao ulimpokea na kumkubali na kumsaidia na kumtukuza na kumlinda na maadui

Ingawa Wayahudi wa Madina walikataa kumsadiki kuwa nabii kama wale wa Biblia aliendelea kuhubiri huko na tangu mwaka wa kwanza alitunga Hati ya Agano iliyokubaliwa na Wamadina wote ndiyo asili ya Umma jamii ya waumini

Mtume Muhammad aliishi Madina kwa muda wa miaka mingine akitangaza dini ya Mwenyezi Mungu na huko watu wengi na makabila mbali mbali ya Kiarabu yaliingia dini ya Uislamu kwa makundi makundi

Wakati huohuo alianza kushambulia misafara ya Wamakka wapagani na kuwashinda kwanza huko Badr akashindwa huko Uhud hatimaye akapata ushindi mkuu huko Madina katika vita vya handaki hapo alifukuza na hatimaye akaangamiza kama wasaliti Wayahudi wote wa Madina na wanaume wote wa Waqurayza wakati wanawake wao pamoja na watoto wakauzwa kama watumwa huko Syria

Mwaka Muhammad akiwa na nguvu za kutosha aliweza kurudi Makka na kuiteka akairudisha Kaaba ambayo ndiyo kibla cha Waislamu wote ulimwenguni katika mambo ya Sala na Hija

Hata hivyo akarudi kuishi Madina na kutoka huko akaeneza kazi yake ya kisiasa na ya kidini katika Hijaz yote Baada ya ushindi wake huko Hunayn dhidi ya Waawazin na wenzao aliteka au kusilimisha vijiji mbalimbali vya maana upande wa uchumi au wa vita kwa mfululizo wa mapigano kwenye Wadi alqura

Kwa jumla alihudhuria vita akiua kwa mkono wake mtu mmoja tu

Akiendelea kuishi Madina alinadhimu kwa Sharia na hukumu nyingi maisha ya jamii ya Waislamu huko na kuweka chanzo cha dola ya kiislamu ulimwenguni

Sharia na hukumu hizo zinapatikana katika kitabu kitakatifu cha Qurani ambacho leo Waislamu wote ulimwenguni wananadhimu maisha yao kulingana nacho

Ingawa Kurani inaruhusu wake tu Muhammad alisema ana idhini ya kuvuka kiwango hicho Jumla alioa wake ambao majina yao yamepangwa hapa chini kufuatana na tarehe ya ndoa

Khadija binti Khuwaylid tangu hadi kifo chake Januari ambaye aliwahi kuolewa na waume wawili na kuwazalia watoto Katika maisha mazuri ya ndoa alimzalia Muhamad mabinti Ruqayya Umm Khulthm Zaynab na Fatima mbali na watoto wa kiume Qsim na Abd Allah ambao lakini walikufa wakiwa bado wadogo

Sawda binti Zama tangu Machi aliyewahi kuolewa na mume mmoja

Aysha binti Abu Bakr tangu Januari aliyeolewa na Mohamed akiwa na umri wa miaka

Hafsa binti Umar tangu Novemba aliyewahi kuolewa na mume mmoja

Zaynab binti Khuzayma tangu Juni hadi kifo chake Agosti

Hindi Umm Salama binti Abi Umayya tangu Februari aliyewahi kuolewa na mume mmoja na kuachiwa watoto wengi Alikuwa mtoto wa kambo wa shangazi ya Mohamed

Zaynab binti Jahsh tangu Juni aliyeachwa na mume wake Alikuwa binamu wa Mohamed

Juwayriya binti Al Harith tangu Desemba

Ramla Umm Habba binti Abi Sufyan tangu Agosti alipoachana na mumewe aliyeingia Ukristo

Safiyya binti Huyay tangu Septemba ambaye alikuwa Myahudi akatekwa nyara katika vita vya Khybar

Maymuna binti Harith tangu Februari aliyekuwa na umri wa miaka

Kati yao wa kwanza tu alimzalia Muhammad watoto lakini wana wote walifariki kabla ya baba yao isipokuwa Fatma aliyekufa miezi sita baada yake

Aliwaoa pia lakini bila ya kulala nao Asma binti Al Numan mkoma na Amra binti Yazid aliyekataa katakata ndoa hiyo akapewa mara talaka

Mbali na wake rasmi Kurani inaruhusu kuwa na masuria wasio na idadi dht alyamn waliomilikiwa na mkono wa kuume yaani watumwa hasa waliotekwa vitani Muhammad alikuwa nao kati yao Marya Mkristo alimzalia mtoto wa kiume Ibrahim aliyefariki mdogo sana kwa huzuni kubwa ya baba yake aliyemfuata kaburini muda mfupi baadaye

Visivyotolewa na Waislamu
Muhammad article on Enyclopaedia Britannica Online
Muhammad Legacy of a Prophet PBS Site
Muhammad Legacy of a Prophet UPF Producers Site
Encarta Encyclopedia
Encyclopedia article on Mahomet
William Muir The Life of Mahomet
The Hero as Prophet A passionate championship of Prophet Muhammad as a Hegelian agent of reform by Carlyle Thomas On Heroes and the Heroic in History Lincoln Nebraska University of Nebraska Press

Vilivyoandikwa na Waislamu
ArRaheeq AlMakhtum The Sealed Nectar
PDF version of ArRaheeq AlMakhtum
The Life of Muhammad by Muhammad Husayn Haykal
About the Prophet Muhammad University of Southern California

Uislamu
Watu wa Kurani
Mitume katika Uislamu

A kipitishoumemkuu kuonyesha Ifekti ya Meissner
Fizikia kutoka kigiriki physikos maumbile na physis kiumbo ni sayansi inayohusu maumbile ya Dunia ambayo inahusu asili ya viungo vya ulimwengu

Ni taaluma kutoka shina la sayansi yenye kushughulika na Maada na uhusiano wake na Nishati

Tangu zama za nyuma kabisa wanafalsafa ya asili walijaribu kueleza mafumbo kama vile mienendo ya sayari na asili ya maada Na Mlengo huu ulijulikana hapo mwanzo kama Fizikisikut eng Physics ikiandikwa Physike kuiga dhana ya Aristotle Kuibuka kwa Fizikia kama tawi la sayansi lenye kujitegemea toka kwenye shina falsafa asilia kulitokana na mapinduzi ya kisayansi ya karne ya na na kuendelea mpaka pambazuko la Sayansi ya Kisasa mnamo mwanzo wa karne ya Nyanja hii imekuwa ikiendelea kutanuka kulingana na kukua kwa tafiti na kupelekea gunduzi mbali mbali kama vile modeli sahili ya chembe za kimsingi na uelezi uliotanuka wa historia ya ulimwengu sambamba na mapinduzi ya tekinolojia mpya kama silaha za kinyuklia na semikonda Leo hii Utafiti unaendelea katika mikondo mipana ya ki mada kuhusisha mpitishoumemkuu katika joto la hali ya Juu Ukototiaji wa Kikwantumu utafutaji wa Higg Boson na jitahada za kuendeleza Nadharia ya Mtuazi wa Kikwantumu Uliokitwa katika Mitazamo na vitendo na pia seti zilizojisheheneza kwa nadharia zinazodhihirishwa kwa Hisabati nzuri Fizikia imefanya mchango mwingi katika sayansi tekinolojia na falsafa

Ugunduzi katika Sayansi umegusa kote ndani ya Sayansi Asilia na Fizikia inaelezwa kama Sayansi ya Msingi kwa sababu nyanja zingine kama Kemia na Baiolojia huchunguza mifumo ambayo tabia zake husimama toka kwenye kanuni za Fizikia Kemia kwa mfano ni sayansi ya dutu iliyofanyika na atomu na molekyuli kwa wingi mmoja lakini tabia za kampaundi za kikemia zinatathminiwa kwa tabia za kimaumbile za molekyuli zinazochipukia kwayo

Fizikia ya vitendo inahusiana kwa karibu na Uhandisi na Tekinolojia Mwanafizikia anayejihusisha na msingi wa utafiti hufanya muundopicha na kisha kufanya vitendo kwa kutumia vyombotekichi kama kikazanishio mwendo wa chembe na Biru na angali mwanafizikia anayejihusisha na tafiti zilizotendewa kazi huvumbua tekinolojia kama vile Upigaji Picha Kiusumaku Mtetemiazi Kut eng MRI Magnetic Resonance Imaging na tranzista za sifa mbali mbali

Fizikia ya kinadharia ina uhusiano wa karibu na hisabati ambayo huipa lugha ya nadharia za kimaumbile Aghalabu ni kweli kwamba shauri la kwanza la Nadharia ni kupembua mahusiano katika sura ya ki ulimwengu inayo shahibiana na yatendekayo kazi ingine ya umuhimu sawa ni kufanyiza kanuni za mahusiano kimahesabu Matumizi ya hisabati katika nadharia huwakilisha dhana ya kimawazo katika mchakato wa kuibua mhitimisho muhimu kutoka kwenye hali ya Udhanifu uliopitia sheria rasmi za ukokotoaji Hata hivyo nafasi ya hisabati katika nyanja ya Fizikia ya Kinadharia inapelekea kwamba si tatizo la mwanafizikia ya kinadharia ku chetua kidhibitihakikivu cha kihesabu na kwa kweli kabisa mahitaji yaliyokaza sana kwenye hesabu mara nyingi hupingana na kweli za kimaumbile Mwanafizikia ya Kinadharia maranyingi vile vile huegamia katika ufuatiliaji tathmini wa kinamba na uchocheaji picha wa kompyuta na hivyo kuona matokeo yake na ndio maana kompyuta na kuprogram kompyuta imekuwa na uwanda mpana wenye sura mbali mbali katika kufanya modeli za kimaumbile Kwa kweli nyanja ya Hisabati na Ufuatiliaji tathmini kikompyuta ni uwanja uliochangamka katika utafiti Fizikia ya kinadharia mara nyingi huhusiana na falsafa na metafizikia ambapo inaangukia upande wa mawazo ya kufikirika kama vile Spesi za vizio wakadhaa na yunivesi sambamba

atomu za haidrojeni chache za kwanza obiti za elektroni zilizooneshwa kwa sura ya mkatizo zikiwa zimetiwa rangi alama densiti ya uwezekanivu

Ingawaje mwanafizikia husoma aina mbali mbali za mafumbo ya maisha kuna baadhi ya nadharia zinatumika kwa wanafizikia wote Kila moja ya hizi nadharia imejaribiwa kwa idadi ya vitendo na kuhakikishwa makadirio sahihi ya asili iliyopo ndani ya mizingo yenye kukubadilika umakini Kwa mfano nadharia ya

Fizikia
Sayansi

Bara Arabu

Bara Arabu ni ile sehemu ya dunia iliyoko baina ya Bara la Afrika na Bara la Asia ambayo sehemu kubwa yake imezungukwa na bahari upande wa magharibi na Bahari ya Shamu upande wa kusini na Bahari ya Hindi na mwengine wa Mashariki na Ghuba ya Uajemi Sehemu za Kaskazini mwa Bara Arabu imepakana na nchi za ufalme wa Jordani na jamhuri ya Iraq

Kwa sababu ya makame hakuna mito ya kudumu katika bara hili ijapokuwa kwenye sehemu mbali mbali kunapatikana chemchemu na vijito vya maji ambavyo huzidi wakati wa msimu wa mvua katika majira ya baridi Sehemu kubwa ni jangwa tu Bara Arabu ina milima upande wa Magharibi na Kusini mwake lakini kila ukiteremkia Mashariki unakutana na ardhi tambarare mpaka kufikia kwenye Ghuba ya Uajemi

Eneo la Bara Arabu kwa jumla ni kilomita muraba ikiwa Saudia inakalia sehemu nne katika tano ya jumla ya maeneo yake na sehemu iliyobakia ambayo ni moja katika tano inakaliwa na nchi zilizobakia zote zikiwepo pembezoni mwa Saudia kwenye bahari ya Ghuba ya Uajemi na bahari ya Waarabu na bahari ya Shamu

Nchi zilizokuweko kwenye bara hili ni Bahrain Kuwait Oman Qatar Saudia Muungano wa Falme za Kiarabu na Yemen Sita za mwanzo zikiwemo kwenye Baraza la Ushirikiano wa Nchi za Ghuba zina mfumo wa kifalme katika utawala wake na ya mwisho ni Jamhuri ya Yemen Nchi hizi zina historia ndefu inayorudi nyuma kabla ya kuja Uislamu na ustaarabu mbali mbali ulipatikana katika maeneo mbali mbali ya nchi hizi Katika ustaarabu mashuhuri wa nchi hizi ni ule ustaarabu wa nchi ya Yemeni ambao ulikuwa ukijulikana kuwa ni ustaarabu wa Sabaa zama za Balqis malkia wa Yemen wa wakati huo

Kuna miji mingi katika Bara Arabu lakini miji mikuu ya madola mbali mbali ya Bara Arabu ni Riyadh mji mkuu wa Saudia ijapokuwa kuna miji mashuhuri na mitukufu katika Saudia kama Makka na Madina Mji mkuu wa Yemeni ni Sanaa lakini mengine muhimu ni Aden Hudeidah Taez Mukalla Shibam na Seyun Ama mji mkuu wa Oman ni Maskat lakini kuna miji mengine mashuhuri yenye tarehe kubwa kama Salala Sohari Nizwa na Rustaq Mji mkuu wa Falme za Kiarabu ni Abu Dhabi na mengine mashuhuri ni Dubai Sharjah Ajman RasalKhayma UmmulQuwain na Fujairah Kuwait mji mkuu wake ni Kuwait na Qatar mji mkuu wake ni Doha na Bahrain ni Manama

Nusu Kisiwa cha Bara Arabu kina jangwa kubwa la Rub al Khalikusini mwake na AnNafud kaskazini mwake Ni sehemu ya ulimwengu ambayo haina mvua nyingi na ukame ndio tabia ya nchi zilizokuwemo katika bara hili na kwa hivyo hali ya hewa huwa ni joto sana katika majira ya joto kufikia hadi daraja C katika baadhi ya sehemu zake na kufikia daraja hadi C katika baadhi ya sehemu nyengine katika majira ya baridi

Idadi ya wakaazi wa nchi hizi saba kwa ujumla inafikia wakiwemo asilimia wenyeji na asilimia wageni Wenyeji au wananchi wa nchi hizi aghlabu yake ni Waarabu lakini pia kuna Wajemi Mabulushi Wahindi Mabangladeshi Wazungu Mapakistani Waafrika na kabila nyenginezo

Nchi zote saba zilizokuwepo kwenye Bara Arabu ni za kiislamu na aghlabu ya Waislamu wake ni wa madhehebu ya Sunni lakini pia kuna madhehebu ya Shia na Ibadhi kwenye baadhi ya nchi hizi Asilimia ya wananchi wa nchi hizi ni Waislamu lakini vile vile kuna wafuasi wa dini nyenginezo katika wakazi wake kama Mayahudi Mabaniani Wakristo na kadhalika

Kiarabu ndio lugha inayotumika kwenye nchi hizi saba na ndio lugha rasmi ya nchi hizi lakini Kiingereza karibuni kimeanza kutumika sana kwa sababu ya kuwepo dharura ya kutumia lugha hii katika biashara mawasiliano baina ya wananchi na wageni na katika uhusiano wa kimataifa baina ya nchi mbali mbali ulimwenguni

Bara Arabu ina aina nyingi ya madini na nishati Kuna dhahabu fedha chumvi na kadhalika Inajulikana hasa kwa akiba zake kubwa za mafuta ya petroliamu na gesi jambo lililofanya hizi nchi kutegemea zaidi mali asili hizi kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi zao na maendeleo mengine ya nchi

Hapo zamani watu wa nchi hizi wakitegemea sana uvuvi ufugaji wa wanyama kama mbuzi kondoo ngombe ngamia na farasi Aidha walikuwa wakilima na kupanda mitende matunda ngano na shayiri na kwa hivyo bidhaa zao walizokuwa wakisafirisha nje zilikuwa zaidi ni tende buni samaki na papa wakavu na ngozi za wanyama

Rasi za Asia
Asia

Neno Mwenyezi Mungu kwa lugha ya Kiswahili linatumika kwa Muumba wa kila kitu Mwenye kuabudiwa kwa haki kinyume na neno mungu ambalo lina maana chochote au yeyote anayeabudiwa ikiwa kwa haki au si kwa haki Kwa hivyo Mwenyezi Mungu ni Muumba wa mbingu na ardhi na kila kilichomo baina yake naye ni Mlezi wa viumbe vyote na Mpaji riziki kwa kila chenye uhai ulimwenguni

Mwenyezi Mungu katika dini na mila nyingi duniani ni yule anayestahiki kuabudiwa kwa haki ikiwa peke yake bila kushirikishwa na chochote au kwa kushirikishwa na viumbe vyengine kwa nia ya kuwa hawa viumbe vyengine vinamkurubisha naye Hii ni kwa sababu kila dini au mila ina namna yake ya kumsawiri Mwenyezi Mungu na njia gani sahihi ya kumuabudu na kwa kuwa hakuna itifaki baina ya hizi dini mila na madhehebu kuhusu Mwenyezi Mungu na namna anavyotakikana kuabudiwa hizi tofauti chungu nzima zimetokea

Uislamu kwa mfano unaeleza kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja tu hana mshirika hana mwanzo wala mwisho hakuzaa wala hakuzaliwa na wala hapana yeyote mwenye kufanana au kushabihiana naye naye ni Mola wa ulimwengu huu wote na Muumba wa kila kitu Kwake Yeye inatoka riziki ya kila kiumbe na Yeye ndiye Mwenye kuhuisha na Mwenye kufisha Marejeo ya viumbe vyote wakishakufa na kufufuliwa ni kwake Yeye tu siku ya Kiyama Yeye pekee ndiye Mwenye kuhukumu viumbe siku ya malipo na ndiye atakayewapa waja wake ujira na thawabu na kuwatia Peponi kwa mema waliyoyafanya au kuwatia adabu na kuwapa adhabu na mateso na kuwatia Motoni kwa maovu waliyotenda hapa duniani

Ukristo unakubaliana na Uislamu katika mengi ya sifa hizi za Mwenyezi Mungu za kuumba kuhuisha na kufisha kuruzuku kufufua kuhukumu na kulipa ya kheri kwa mwenye kufanya kheri na ya shari kwa mwenye kufanya shari lakini aghlabu ya madhehebu za Kikristo ijapokuwa si zote zinampa Mwenyezi Mungu sifa ya utatu na kumsifu kuwa ni Mungu Baba na Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu na kuwa wote hawa watatu wanashirikiana katika Uungu na kuwa ni kitu kimoja Uislamu kwa upande wake unakataa katakata masala ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu chochote na kwa hivyo ni Mmoja tu wala hana mshirika wa aina yoyote

Dini nyenginezo kadhalika zina tasauri na fikra nyengine kuhusu Mwenyezi Mungu Kuna wale wanaoabudu viumbe mbali mbali wakichukulia kuwa wanamwakilisha Mwenyezi Mungu kama kuabudu masanamu nyota jua ngombe wanyama mbali mbali mizimu miti panya moto viumbe wenziwao malaika na majini na kadhalika Dini na mila hizi pengine huchukulia kuwa vitu hivi vinatusaidia kutufikisha kwa Mwenyezi Mungu na kuwa bila ya vitu hivi ibada zetu haziwezi kufika Ama wengine huwa na imani kuwa vitu hivi ndio Mola mwenyewe wa kuabudiwa na kuombwa na kutakwa msaada

Kama tulivyoeleza Mwenyezi Mungu ana sifa mbali mbali kwa mujibu wa dini na mila na madhehebu tofauti tofauti na kila watu wanamsifu Mwenyezi Mungu kwa namna ambayo wanavyomjua wao kulingana na mafunzo ya dini na mila zao Hii ni kwa sababu watoto tangu wazaliwapo hufunzwa na wazee wao habari za Mwenyezi Mungu na namna ya kumuabudu na mafunzo haya hubakia katika mawazo na fikra zao na kukuwa nayo mpaka ukubwani mwao

Waislamu wanafunzwa tangu utotoni mwao kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja tu peke yake hana mshirika naye ndiye mwenye kufaa kuabudiwa kwa haki bila ya kushirikishwa na chochote katika viumbe vyake na kuwa Yeye ni wakutegemewa katika kila kitu na kuombwa msaada na kuombwa msamaha wakati wa makosa na madhambi Yeye hana kitu kilichofanana naye hakuzaa wala hakuzaliwa hana mwanzo wala mwisho Mwingi wa rehema na Mwenye kurehemu Mtoa riziki Mwenye kuhuisha na Mwenye kufisha Hukumu yote ni yake siku ya Kiyama Mtukufu na Mkubwa Bwana na Mola wa walimwengu wote Yeye tu ndiye Mwenye kustahiki kuabudiwa na Yeye tu ndiye Mwenye kufaa kuombwa na kutakwa msaada

Dini

Ardhi
Dunia wakati mwingine pia ardhi ni mojawapo ya sayari zinazotembea katika anga ya ulimwengu Kuna sayari nane zinazolizunguka jua dunia yetu ikiwa sayari ya tatu katika mfumo wa jua na sayari zake Masafa baina yake na jua ni kilomita milioni Dunia huchukua siku kulizunguka jua na masaa kuuzunguka mhimili wake Dunia ina upana wa kilomita

taz makala Muundo wa dunia
Tabaka za ganda la dunia
Muundo wa dunia yetu ni ya tabaka mbalimbali zinazofuatana kutoka nje kwenda ndani Kila moja ina tabia yake

Kila ukiingia ndani dunia inazidi kuwa moto mpaka ukifika ndani kabisa daraja ya harara hufikia nyuzi C

Dunia yetu ni sayari pekee inayojulikana mpaka sasa ambapo binadamu na viumbe vingine vinaweza kuishi Hapa kuna sababu mbili
dunia yetu ina umbali na jua unaofaa kwa maisha kwa sababu sayari zilizoko karibu zaidi na jua km Zuhura zina joto kubwa mno na sayari zilizoko mbali zaidi kama Mrihi ni baridi mno
dunia yetu ina angahewa yenye asilimia ya naitrojini asilimia ya oksijini na asilimia ya aina nyenginezo za hewa na kwa sababu hii uhai na maisha yanamakinika katika ardhi kinyume na sayari nyenginezo

Sehemu kubwa kabisa ya dunia inafunikwa na bahari kwani takriban asilimia ya uso wake unafunikwa na maji ya bahari na kutokana na maji yote yaliyokuwepo ardhini asilimia ni maji ya bahari na asilimia ni maji matamu Theluthi inayobaki ni nchi kavu kwenye mabara mbalimali na visiwa vingi

Sura ya dunia ni kilomita mraba ikiwa nchi kavu imechukuwa eneo la kilomita mraba na maji yamechukuwa eneo la kilomita mraba

Mabara makubwa ni Asia Afrika Amerika Kusini na Amerika Kaskazini Australia na Ulaya

Hewa iliyoko juu ya ardhi vile vile ina tabaka mbalimbali na kila tabaka ina kazi yake Hewa kwa jumla ina masafa ya kiasi cha kilomita au maili kuendea juu na baada ya hapo unaingia kwenye anga ya nje Hewa hii ndio inayotukinga sisi viumbe na madhara ya jua na mnururisho wa angani ambao unaingia anga la dunia na kuteremka chini

Madhara ya ongezeko la joto Duniani

Sayari
Dunia

Asia
Asia ni bara kubwa kabisa kuliko mabara yote mengine ya dunia Bara hili lina eneo la kilomita za mraba maili za mraba ambalo ni sawa na asilimia ya ardhi yote Wakazi wa bara la Asia ni kwa mujibu wa makisio

Bara la Asia lina nchi na visiwa mbali mbali vya madola mbalimbali Mlima mrefu kabisa ulimwenguni ambao ni mlima wa Everesti wenye urefu wa mita futi ulioko Nepal pia uko kwenye bara hili Kadhalika nchi zenye wakazi wengi zaidi ulimwenguni China na India pia ziko kwenye bara hili

Ziwa kubwa kabisa ulimwenguni bahari ya Kazwini Caspian Sea lenye eneo la kilomita za mraba maili za mraba vile vile liko Asia kati ya ya nchi hizi Azerbaijan Urusi Kazakhstan Turkmenistan na Uajemi

Bara la Asia linaweza kugawanywa katika sehemu zifuatazo

Bara
Asia

Ukurasa huu unahusu imani ya Uislamu kumhusu Yesu kadiri ya Kurani Ingawa Waislamu wanakiri pia vitabu vitakatifu vya Torati Zaburi na Injili katika ibada wanatumia Kurani tu na kwa kawaida ndiyo chanzo chao cha habari juu ya watu na matukio ya kabla yake

Kitabu hicho kilichoandikwa miaka hivi baada ya Kristo kina aya zinazomhusu lakini hakileti mfululizo wa habari za maisha yake wala za mafundisho yake maalumu

Kwao Nabii Isa ni mtume anayeaminiwa kuwa mmojawapo wa mfululizo wa mitume na manabii watukufu wa Mwenyezi Mungu walioletwa ulimwenguni kuwapasha wanadamu ujumbe wa upweke na umoja wake ili wamuabudu Yeye peke yake akiwa ndiye Muumba na Mruzuku wao hapa duniani Mitume na Manabii hawa wameletwa katika zama mbalimbali na kwa watu kaumu na umma mbalimbali na mfululizo huu ulianza na Adamu baba wa wanadamu wote hadi Mtume Muhammad akiwa ndiye wa mwisho

Yeye ni miongoni mwa mitume wakubwa ambao Mwenyezi Mungu amewasifu kwa subira yao na ustahimilivu wao mkubwa Manabii Nuhu na Ibrahimu na Musa na Isa na Muhammad Tena ni miongoni mwa Mitume waliopewa Kitabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kiitwacho Injili Masihi Isa bin Mariamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Neno lake tu alilompelekea Mariamu na ni Roho iliyotoka kwake sura ya aya Wakristo wanamuita kwa kawaida Yesu Kristo

Nabii Isa alizaliwa na bibi Maryam kimiujiza kwani alizaliwa bila ya baba kwa amri ya Mola wake ambaye alimtuma malaika Jibrili kumtangazia kupata kwa mtoto mtukufu Baada ya kuzaliwa Nabii Isa alisema utotoni mwake akiwa bado mchanga ukiwa ni muujiza mwingine kwa watu ili kuwaonyesha kuwa yeye si mtoto wa kawaida na kuwa mamake hana dhambi ya kuja kwake bila ya baba Huu ni mfano mmoja katika mifano minne ya uumbaji aliyotuonyesha Mwenyezi Mungu kwani Mwenyezi Mungu alimuumba Adamu bila ya baba wala mama na akamuumba Hawa bila ya mama na akamuumba Isa bila ya baba na akaumba wanadamu wote waliobakia kutokana na baba na mama

Habari za kuzaliwa kwake Nabii Isa zinapatikana katika Kurani surat Maryamu kuanzia aya

Na mtaje Maryamu katika Kitabu pale alipojitenga na jamaa zake mahali upande wa mashariki Na akaweka pazia kujikinga nao Tukampelekea Roho wetu akajifananisha kwake sawa na mtuMaryamu akasema Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe ukiwa ni mcha Mungu Malaika Akasema Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako ili nikubashirie tunu ya mwana aliyetakasika Akasema Nitampataje mwana hali mwanamume yeyote hajanigusa wala mimi si kahaba Malaika akasema Ni kama hivyo Mola wako Mlezi amesema Haya ni mepesi kwangu Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu na Rehema itokayo kwetu na hilo ni jambo lililokwishaamuliwa Basi akachukua mimba yake na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende akasema Laiti ningelikufa kabla ya haya na nikawa niliye sahaulika kabisa Pakatangazwa kutoka chini yake Usihuzunike Hakika Mola wako amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji Na litikise kwako hilo shina la mtende utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu Basi kula na kunywa na litue jicho lako Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga kwa hivyo leo sitasema na mtu Akenda naye mwanawe kwa jamaa zake amembeba Wakasema Ewe Maryamu Hakika umeleta kitu cha ajabu Ewe dada yake Harun Baba yako hakuwa mtu muovu wala mama yako hakuwa kahaba

Akawaashiria mtoto Wakasema Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi Mtoto akasema Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu Amenipa Kitabu na amenifanya Nabii Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo Na ameniusia Sala na Zaka maadamu ni hai Na nimtendee wema mama yangu Wala hakunifanya niwe jeuri mwovu Na amani iko juu yangu siku niliyo zaliwa na siku nitakayo kufa na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai Huyo ndiye Isa mwana wa Maryamu Ndiyo kauli ya haki ambayo wanaifanyia shaka Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana Subhanahu Yeye ametakasika Anapolihukumia jambo basi huliambia tu Kuwa Likawa

Nabii Isa aliletwa kwa wanadamu kufikisha ujumbe kwao wa kuwafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja hana mwenzake na kuwa Yeye pekee ndiye mwenye kustahili kuabudiwa kwa haki na ujumbe huu ndio ujumbe uleule uliotumwa kwa Mitume na Manabii wote kwa wanadamu ili kuwaongoza naye alikuja kutilia mkazo na kusisitiza jambo hili na kuzipa nguvu tume za Mitume na Manabii waliopita Kadiri ya sura ya aya ya alisema ni msadikishaji wa yale yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati na ili niwahalalishieni baadhi ya yale mliyoharimishiwa na nimewajieni na Ishara kutoka kwa Mola wenu kwa hiyo mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii Alitabiri kuwa baada yake atakuja Mmoja ambaye atawafundisha wanadamu ukweli wote na kuwaongoza kwenye haki na kuwaeleza kila wanalolihitaji katika maisha yao Ujumbe wake ulikuwa ni wa mwisho kabla ya ule wa Mtume Muhammad ambao ndio wa mwisho kabisa kwa wanadamu wote

Mwenyezi Mungu ameleta Mitume na Manabii wengi ulimwenguni lakini alichagua baadhi yao na kuwateremshia vitabu vya uongozi na sharia na hekima kwa wafuasi wao Katika vitabu vilivyoteremshwa kwa Manabii mbalimbali ni Taurati kwa Nabii Musa Zaburi kwa Nabii Daudi Injili kwa Nabii Isa na Qurani kwa Nabii Muhammad Kitabu cha Nabii Isa kiliteremshiwa Wayahudi ambao ndio walengwa wake wa kwanza wa Nabii Isa kama ilivyothibitishwa na Qurani wakati aliposema

Enyi Wana wa Israili Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu ninayethibitisha yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati na mwenye kubashiria Mtume atakayekuja baada yangu jina lake ni Ahmad Lakini alipowaletea hoja zilizo wazi walisema Huu ni uchawi ulio wazi

Nabii Isa alipewa na Mwenyezi Mungu miujiza mbalimbali kumsaidia katika kazi yake ya kutangaza dini ya Mwenyezi Mungu kwani ilikuwa ni kawaida kwa Mtume au Nabii kuonyesha miujiza kwa watu au kaumu yake ili awathibitishie kuwa yeye kweli ni mjumbe aliyeletwa na Mola wa ulimwengu huu Mitume waliotangulia kabla ya Nabii Isa kama Nuhu na Ibrahim na Musa na wengineo wote walikuja na miujiza mbalimbali Baadhi ya miujiza ya Nabii Isa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu ni kuumba ndege kutokana na udongo kuponyesha vipofu wakaweza kuona na kuwaondoshea ukoma wale wenye ukoma na kuhuisha mtu aliyekufa na kuwateremshia wafuasi wake chakula kutoka mbinguni ili iwe ni dalili kwao wote

Muhammad alikuta Wakristo au Manasara wakiwa wamehitilifiana katika imani yao kuhusu Nabii Isa kwani wote walimkiri kuwa Mwana wa Mungu lakini kwa wengi hii ilikuwa na maana kuwa yeye ni Mungu aliyejifanya mtu isipokuwa wachache walitafsiri tofauti Makundi ya namna hiyo yalitengana baada ya Nabii Isa kuondoka ulimwenguni na kuwaachia wafuasi wake waendeleze kazi yake ya kutangaza dini ya Mwenyezi Mungu Wafuasi waliokuja baada ya wale kumi na mbili waliokuwa pamoja naye walitoa fikra na mawazo yao kuhusu Isa hivyo baada ya muda waligawanyika makundi mbalimbali

Waislamu pamoja na Wakristo wanaamini kuwa Isa atarudi tena ulimwenguni kukamilisha kazi yake aliyoiacha baada ya kupaa kwenda kwa Mola wake na haya yanaelezwa katika vitabu vya dini vya Kiislamu na vya Kikristo lakini wanahitilifiana kuhusu namna na njia aliyoondokea ulimwenguni Waislamu wanasema kuwa Isa alichukuliwa na Mola wake na kupandishwa kwake mbinguni baada ya Wayahudi kutaka kumuua na kwa hivyo hawakuweza kumuua wala kumsulubu Wakristo kwa upande mwingine wanaamini kuwa aliwahi kusulubiwa na kuzikwa kisha akafufuka siku ya tatu Muhimu hapa ni kujua kuwa atarudi tena duniani kukamilisha kazi aliyopewa na Mwenyezi Mungu

Dini
Uislamu
Manabii katika Uislamu
Watu wa Kurani

Bara au kontinenti ni sehemu kubwa ya dunia iliyochomoza juu ya bahari ambayo kikawaida hukaliwa na watu na kuwa juu yake milima na mimea na wanyama na kila aina ya viumbe Sehemu hii ya dunia ndio inayojulikana kama bara na sehemu nyingine ya dunia ni ile iliyoko chini ya bahari

Kwa kawaida duniani huhesabiwa mabara saba mengine yakiwa makubwa na mengine madogo

Bara la Afrika
Bara la Asia
Bara la Amerika ya Kaskazini
Bara la Amerika ya Kusini
Bara la Antaktika
Bara la Ulaya
Bara la Australia

Mara nyingi visiwa vya Pasifiki hujumlisha pamoja na Australia kama
Australia na Pasifiki
na kuhesabiwa kama bara

Kuna mahesabu tofauti yanayojumuisha Amerika ya Kaskazini na Amerika Kusini kuwa bara moja au kinyume chake Amerika ya Kati hutazamiwa pekee Ulaya na Asia hutazamiwa pia kuwa bara moja la Eurasia

Eneo la dunia yote kwa jumla ni kilomita mraba ikiwa nchi kavu imechukuwa eneo la kilomita mraba na maji yamechukuwa eneo la kilomita mraba Eneo la maji kulingana na eneo la nchi kavu ni asilimia na nchi kavu kilomita mraba ni asilimia Maji ya bahari yamechukuwa eneo la kilomita mrabaambalo ni asilimia na maji yaliyobakia matamu ni asilimia tu

Mabara jinsi yanavyoonekana hukaa juu ya mabamba ya gandunia ambayo ni vipande vikubwa vya mwamba vinavyounda uso wa dunia Mabara tunavyoyajua yanalingana kila moja na bamba lake na kila bamba ina mwendo wake wa polepole Hii ni sababu ya kwamba baada ya miaka mingi uso wa dunia utaonekana tofauti kuliko leo

Kijiolojia bara haliishi kwenye pwani pale bahari inapoanza Bara linaendelea chini ya uso wa bahari kama tako la bara

Mabara na mabamba yao ni kama ifuatayo Afrika Bamba la Afrika Antaktika Bamba la Antaktika Australia Bamba la Australia Ulaya na sehemu kubwa ya Asia Bamba la UlayaAsia Amerika Kaskazini pamoja na Siberia Bamba la Amerika ya Kaskazini na Amerika Kusini Bamba la Amerika ya Kusini Mabamba madogo yamejitenga ingawa nchi juu yao inaonekana kuwa sehemu ya bara lingine Mfano wake ni Bara Hindi iliyokuwa kama bara ndogo au kisiwa kikubwa zamani lakini tangu miaka milioni imejisukuma chini ya bamba la AsiaUlaya na kuikunja hadi kutokea kwa milima ya Himalaya

Kwa jumla miamba ya sehemu za mabara ni mipesi kushinda miamba ya chini na hii ni sababu ziko juu ya miamba mingine

Bara la Asia lina nchi huru
Bara la Afrika lina nchi huru
Bara la Amerika ya kaskazini lina nchi huru
Bara la Antaktika halina wakazi wa kudumu wala nchi huru hata moja ijapokuwa nchi kama zinadai kumiliki sehemu fulani za bara hili
Bara la Australia au Oshania lina nchi huru
Bara la Ulaya au Uropa lina nchi huru

Kwa hivyo kwa ujumla kuna madola katika mabara yote ya ulimwengu mara huzidi kukitokea na mgawanyiko wa nchi au hupungua kukitokea umoja au muungano wa nchi


Jiografia

border cellpadding cellspacing stylemargin em em em background fff border px aaa solid bordercollapse collapse fontsize


aligncenter colspan styleborderbottompx solid gray
Wito Uhuru na Umoja

Lugha rasmi Kiswahili kwa dhati

Mji Mkuu Dodoma

Makao ya Serikali Dar es Salaam

Serikali Jamhuri

Rais Jakaya Kikwete

Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Eneo km

Wakazi Julai

Wakazi kwa km

Uhuru kutoka Uingereza tar Desemba

Pesa Shilingi ya Tanzania

Wakati UTC

Dini za wakazi Ukristo Uislamu Dini za jadi

Wimbo wa Taifa Mungu ibariki Afrika

colspan alignright Tanzania katika Afrika

colspan alignright Ramani ya mikoa ya Tanzania


Tanzania ni nchi iliyoko Afrika ya Mashariki Imepakana na Uganda na Kenya upande wa Kaskazini Bahari Hindi upande wa mashariki Msumbiji Malawi na Zambia upande wa kusini Kongo Burundi Rwanda na Uganda upande wa magharibi

Nchini Tanzania kuna lugha za kikabila zaidi ya mia moja Hakuna lugha rasmi ya sheria Lakini Kiswahili ni lugha ya kitaifa ya Tanzania Kiswahili kinatumika kama lugha baina ya watu wa makabila mbalimbali na kwa mambo ya rasmi kwa hiyo Kiswahili ni lugha rasmi ya dhati Baada ya uhuru Kiingereza iliyokuwa lugha ya kikoloni kabla ya uhuru iliendelea kutumika kwa mambo kadhaa rasmi na kwa hiyo ilichukuliwa lugha rasmi ya dhati pamoja na Kiswahili Lakini utumizi wa rasmi wa Kiingereza imepungua katika milongo iliyopita na sasa utumizi huu karibu umekwisha Kwa hiyo siku hizi ni kawaida zaidi kuchugulia Kiswahili kama lugha rasmi ya dhati ya pekee

Tanzania ni nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki

Mji mkuu Dodoma Makao makuu ya serikali Dar es Salaam miji mikubwa mingine Mbeya Arusha

kuhusu historia ya maeneo ya Tanzania kabla ya angalia makala za Tanganyika Zanzibar na Afrika ya Mashariki ya Kijerumani

Jina Tanzania limeundwa kutokana na majina ya TANganyika na ZANzibar pamoja na athira ya jina la kale la Azania

Nchi hizo mbili zilikuwa zote chini ya utawala wa Uingereza hadi kupata uhuru lakini hazikuwa makoloni ya kawaida Zanzibar ilikuwa na hali ya nchi lindwa kutokana na mikataba kati ya masultani wa Zanzibar na Ufalme wa Uingereza Tanganyika iliwahi kuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani hadi Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia halafu ikawa chini ya Uingereza kama eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa iliyoweka Tanganyika katika ngazi B ya maeneo ya kudhaminiwa

Tanganyika na Zanzibar zilikuwa nchi mbili tofauti hadi zilipoungana na kuwa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Kiongozi wa Tanganyika Mwalimu Julius Nyerere alikuwa Rais wa kwanza na kiongozi wa mapinduzi ya Zanzibar Abedi Amani Karume akawa Makamu wa Kwanza

Tanzania chini ya Rais wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi iliruhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa Tanzania na kuanza mpango wa kurekebisha uchumi kuendana na masharti ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani

Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa aliendeleza mfumo wa uchumi wa soko huria ambapo mashirika ya umma yanabinafsishwa

Tarehe Desemba Kikwete Jakaya Kikwete ameapishwa kuwa Rais wa nne wa taifa

Tanzania ni moja kati ya nchi maskini duniani ambazo zimefanikiwa kufutiwa madeni katika mpango wa kusamehe madeni wa Kundi la Nchi Nane

Tangu muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka Tanzania imefuata miundo ifuatayo
Nchi inatawaliwa na serikali ya muungano ikitekeleza sheria zinazotolewa na bunge la Tanzania
Tanganyika au Tanzania bara haina serikali au bunge la pekee
Zanzibar Unguja na Pemba ina serikali na bunge lake zinazoratibu mambo yasiyo ya muungano

Mambo yafuatayo yalikubalika kuwa shughuli za muungano
Mambo ya nje
Jeshi
Polisi
Mamlaka ya dharura
Uraia
Uhamiaji
Biashara ya nje
Utumishi wa umma
Kodi ya mapato orodha
Bandari Usafiri wa anga Posta na Simu

tazama Orodha ya makabila ya Tanzania

Watu wa Tanzania hawaenei sawasawa Katika maeneo makavu sana kunaishi mtu mmoja tu kwenye kilomita moja ya mraba km lakini sehemu zenye rutuba za bara kuna watu kwa kila kilomita ya mraba Hatimaye huku Unguja kuna watu kwa kilomita ya mraba Zaidi ya asilimia themanini huishi vijijini Dar es Salaam ni mji mkubwa kabisa wenye watu karibu milioni tatu

Kuna makabila zaidi ya Makabila yenye watu zaidi ya milioni moja ni Wasukuma Wanyamwezi Wachaga Waha Wagogo Wahaya na Wamakonde

Idadi kubwa sana ya Watanzania ni Wabantu Nje ya hao kuna Waniloti kwa mfano Wamasai na Wajaluo ambao wengi wao zaidi wanaishi Kenya Kundi lingine ni makabila ya Wakushi wanaoishi kaskazini mwa Tanzania hao ni makabila ya Wairaqw Wafiome na Wasi Kuna vikundi viwili vya Wakhoisan wanaofanana na makabila ya Botswana na Namibia majina yao ni Wasandawe na Waburunge Hatimaye kuna Wahadzabe wachache ambao utafiti wa DNA umeonyesha hivi karibuni wana uhusiano wa asili na Watwa wa nchi za Afrika ya Kati

Ingawa kila kabila lina lugha yake lugha ya taifa ya Tanzania ni Kiswahili ambacho ni mojawapo kati ya lugha za Kibantu Hali hii imesaidia sana kukubaliwa kwa Kiswahili nchini kwa sababu idadi kubwa ya Watanzania ni wasemaji wa lugha za Kibantu

Nchi haina dini rasmi na katiba ya Tanzania inatangaza uhuru wa dini kwa wote Mara nyingi idadi ya wafuasi wa dini hutajwa kuwa theluthi moja Waislamu theluthi moja Wakristo na theluthi moja wafuasi wa dini za jadi Lakini tangu uhuru swali la dini ya wananchi halijaulizwa tena katika sensa kwa hiyo kadirio la theluthitheluthi halina msingi halisi bali ni zaidi azimio la kisiasa

Waislamu hudai mara nyingi ya kwamba wenyewe ni sehemu kubwa ya Watanzania angalau zaidi ya nusu Kamusi ya World Christian Encyclopedia yataja Wakristo kuwa Waislamu kuwa na wafuasi wa dini za jadi kuwa

Kwenye visiwa vya Zanzibar idadi ya Waislamu huaminiwa kuwa takriban

habari za undani zaidi katika makala ya Usafiri wa Tanzania

Usafiri nchini Tanzania ni hasa kwa njia ya barabara Mengine ni reli na ndege Kwenye maziwa makubwa na pwani la Bahari Hindi kuna pia usafiri kwa meli

Hadi sasa idadi ya barabara za lami si kubwa Kuna hasa njia nzuri kati ya Dar es Salaam Mbeya katika kusinimadharibi Dodoma katika kitovu cha nchi Arusha Tanga katika kaskazinimashariki KusiniMashariki na Magharibi ya nchi kwa jumla haina barabara nzuri na mawasiliano ni magumu

Shirika mbili za reli zahudumia Tanzania ni TRC Shirika ya Reli Tanzania Tanzania Railways Corporation na TAZARA TanzaniaZambia Railways Corporation TRC imetawala reli ya kati kuanzia Dar es Salaam hadi Kigoma halafu reli ya Tanga kati ya Tanga na Arusha Tazara imeunganisha Dar es Salaam na kusini ya nchi hadi Zambia Zote hazikutunzwa vizuri na usafiri unakumbwa na huduma mbaya pamoja na ajali

Huduma kwa ndege zatumia hasa nyanja za ndege penye barabara ya lami kwa ajili ya ndege hasa Julius NyerereDar es Salaam Kilimanjaro ArushaMoshi na ZanzibarKisauni

Tembo

Kati ya wasanii wa Tanzania ni hasa wajume wa ubao na wachoraji waliojulikana kimataifa

Mabombwe ya Kimakonde yamesifiwa tangu mwanzo wa karne ya Wamakonde wengi wamehamia Daressalaam au Arusha wanapohudumia soko la watalii pia soko la nje

Tangu miaka ya uchoraji wa tingatinga umejulikana uliopata jina kutoka kwa Edward Tingatinga naye mtu wa Umakonde

Mahali pafuatapo katika Tanzania pamepokelewa katika orodha ya UNESCO ya Urithi wa Dunia

mwaka wa kukubaliwa jina la mahali

Hifadhi ya Taifa Ngorongoro
Hifadhi ya Taifa la Serengeti
Maghofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara
Hifadhi ya Taifa Selous
Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro
Mji Mkongwe wa Jiji la Zanzibar Unguja
Michoro ya Kondoa


Nchi za Afrika

Uhindi pia India ni nchi katika bara la Asia Ni nchi ya kidemokrasia kubwa duniani Kufuatana na idadi ya wakazi ni nchi ya pili duniani baada ya China Kufuatana na eneo ina nafasi ya saba duniani Imepakana na Pakistan China Nepal Bhutan Bangladesh na Myanmar Mji mkuu ni New Delhi

Wakazi walio wengi hufuata dini ya Uhindu Takriban ni Waislamu hivyo Waislamu wa Uhindi ni jumuiya ya pili katika dunia ya kiislamu baada ya waislamu wa Indonesia Dini nyingine ni Ukristo Usikh Ubuddha na Ujain

Lugha ya kitaifa ni Kihindi ambacho ni lugha ya KihindiKiulaya Kiingereza hutumiwa kama lugha ya kiutawala ya kitaifa pia kwenye ngazi ya majimbo Kuna lugha kubwa na lugha nyingi zisizo na wasemaji wengi sana Katika kusini ya Uhindi watu husema lugha kama Kikannada Kitelugu Kitamil na Kimalayalam Katika kaskazini husema hasa Kipunjabi Kibengali Kigujarati na Kimarathi

Kiutawala Uhindi ni shirikisho la jamhuri lenye majimbo ya kujitawala pamoja na maeneo ya shirikisho

tazama pia Uhindi wa Kiingereza

Majimbo ya Uhindi

Tovuti rasmi
India Travel

Nchi za Asia

Ramani ya Afrika Mashariki
Afrika ya Mashariki ni sehemu ya bara la Afrika ambayo iko upande wa mashariki ikipakana na Bahari ya Kihindi Afrika ya Mashairiki ina nchi kadhaa ambazo ni Kenya Uganda Tanzania Rwanda Burundi Msumbiji Somalia Sudan Jibuti na Ethiopia lakini nchi mashuhuri zaidi katika sehemu hii ni Kenya Uganda Tanzania Rwanda na Burundi kwa sababu ya kutumia lugha moja katika mawasiliano yao baina ya wananchi wa sehemu hii yaani Kiswahili

Aghalabu ya nchi za Afrika ya Mashariki zinazungumza lugha ya Kiswahili kama ndio lugha ya mawasiliano kati yao kwani katika nchi hizi kuna makabila mengi sana na kila kabila lina lugha yake ambayo kawaida inatumika nyumbani baina ya watu wa kabila moja lakini wakitaka kuwasiliana na makabila mengine mara nyingi hutumia lugha ya Kiswahili na hii ni kwa sababu lugha hii ndio iliyoenea zaidi na kufahamika zaidi katika eneo hili la dunia

Wakazi wengi wa Afrika ya Mashariki ni wasemaji wa lugha za Kibantu sehemu ya Kaskazini wasemaji wa lugha za Kihamiti ni wengi Waoromo Wasomalia Katika Ethiopia kuna wasemaji wa lugha za Kisemiti

Afrika ya Mashariki inatajwa na sayansi kuwa mahali ambako watu wa kwanza duniani walipopatikana

Majina ya miji ya Afrika ya Mashariki imetajwa mara ya kwanza katika Periplus ya Bahari ya Eritrea katika karne ya kwanza bK

Mara nyingi hata nchi zifuatazo huhesabiwa kuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki

Malawi Zambia na Zimbabwe wakati mwingine zinehesabiwa kuwa sehemu ya Afrika ya Kusini au ya Afrika ya Mashariki zamani zilikuwa pamoja kama Rhodesia ya Kusini Rhodesia ya Kaskazini na Unyasa katika Shirikisho la Afrika ya Kati

Komori Morisi Shelisheli Mayotte na Runion ni visiwa vidogo vya Bahari Hindi vinavyohesabiwa kuwa sehemu za Afrika ya Mashariki

Nchi za Afrika ya Mashariki hasa Kenya Uganda na Tanzania ni nchi ambazo ni karibu tangu zamani Zimeshirikiana historia zote zimekaliwa hasa na makabila yanayotumia lugha za Kibantu Kenya na Uganda wana pia idadi muhimu ya wakazi wasiotumia lugha za Wabantu Katika nchi zote tatu lugha ya Kiswahili imekuwa lugha muhimu ingawa kwa daraja mbalimbali Wakati wa ukoloni zilitawaliwa na Uingereza iliyoacha taasisi na taratibu mbalimbali zilizosaidia kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wakati wa uhuru

Tanzania Kenya na Uganda zina ukubwa wa eneo la maili za mraba Tanzania ikifuatiwa na Kenya na Uganda upande wa mashariki nchi hizi zimepakana na bahari ya hindi na upande wa kaskazini mashariki zimepakana na Somalia upande wa kaskazini zimepakana na Ethiopia na Sudani upande wa magharibi ni Kongo na jamuhuri ya Rwanda na Burundi kusini ni Zambia Malawi na Msumbiji

Nchi hizi zimepitiwa na mstari wa ikweta umepita Kenya na kusini mwa Uganda Kenya na Tanzania zina ukanda wa pwani wenye bandari za Mombasa Tanga Bagamoyo Daressalaam Zanzibar Kilwa na Mtwara

Afrika ya Mashariki

Simu
Simu kutoka kar sim inayomaanisha waya ni chombo cha umeme Mamtumizi ya simu ni kwa ajili ya watu wawili waliokatika sehemu mbili tofauti na wanaweza kuongea Bimaana ni chombo cha mawasilianoanga Awali simu ilihitajika iuanganishwe na nyaya Lakini leo hii simu inaweza kutumwa kwa kutumia redio Hii nayo inaitwa nyayatupu siwaya au simu bila waya

Watu wengi wanaamini kuwa sumu iligunduliwa mnamo na Alexander Graham Bell Alikuwa mtu mwenye umri wa miaka aliyeishi nchini Marekani akiwa kama Muuskoti Lakini Antonio Meucci alianzisha na kuanza kutoa matumizi ya simu toka kunako mwaka wa huko Marekani

Mawasiliano
Simu

Kiido ni lugha ya kupangwa Inafanana sana na Kiesperanto lakini haizungumzwi na watu wengi kama Kiesperanto

Wikipedia ya Kiido

Lugha

Mtumiaji

Mungu ni jina linalotumika kwa yeyote anayesadikiwa katika dini mbalimbali kuwa na uhai wa hali ya juu

Kati ya wafuasi wa dini hizo wengi wanaona Umungu kwa jinsi ulivyo au unavyofirika haukubali mgawanyiko Hasa katika Uyahudi Ukristo na Uislamu wanasisitiza umoja wa Mungu kuwa ndio msingi wa imani yao Kwao Mungu anafahamu yote na kutaka hasa uwepo wa viumbe Tena kwa hiari yake alipenda kujifunua kwa binadamu kielelezo ni IbrahimuAbrahamu aliyefanywa rafiki yake na baba wa waamini wote

Kumbe dini nyingine zinakubali kuwepo kwa miungu mbalimbali wawili au zaidi Hasa dini nyingi za jadi zinaamini uwingi wa miungu Dini kubwa duniani inayosadiki miungu mingi ni Uhindu Pia katika sehemu za Afrika ya Magharibi ibada za miungu mingi inaendelea hadi leo

Dini
Teolojia

Volkeno

Volkeno pia volkano zaha ni mahali ambako lava inatoka nje kwa uso wa ardhi Mara nyingi lakini si kila mahali volkeno ni mlima Volkeno huwa na kasoko yaani shimo ambako lava na gesi inatoka nje

Volkeno ni dalili ya kwamba mahali pake ganda la dunia si nene sana hivyo joto la ndani linapata njia ya kutoka nje Volkeno huanza katika tambarare Lava hutoka katika hali ya kiowevu ikipoa haraka inaganda kuwa mwamba na hujenga mlima wa kuzunguka shimo la kasoko yake Milima ya aina hii inaweza kukua sana Mfano wa volkeno kubwa ni Kilimanjaro Miamba yake yote ilijengwa na lava iliyotoka ndani ya dunia

Volkeno nyingi hutokea pale ambako mabamba ya ganda la dunia vinaachana au kusukumana Hivyo volkeno hutokea hasa kwenye mistari ya kukutana kwa mabamba haya

Sababu nyingine ya kutokea kwa volkeno ni kuwepo kwa chumba cha magma ndani ya ganda la dunia

Mlipuko wa volkeno ni hatari sana kwa ajili ya wanadamu na mazingira Kuna mifano ya vifo vingi vilivyosababishwa na volkeno Hasara inategema kama miji iko karibu na volkeno au la na kama serikali zina huduma za kutazama volkeno na kuonya watu watoke mapema wakati dalili za kwanza zinatokea

Kati ya mifano ya milipuko makali inayojulikana zaidi ni

mlipuko wa volkeno ya Vesuvio Italia Iliharibu miji ya Pompei na Herkulaneo mwaka BK
mlipuko wa volkeno ya Krakatau Indonesia mwaka Ilirusha vumbi nyingi angani kiasi kilichoonekana kote duniani
mlipuko wa volkeno Nevado del Ruiz Kolumbia mwaka uliua watu kutokana na kuyeyusha theluji na barafu mlimani na kusababisha mafuriko ya ghafla

Ol Doinyo Lengai ni volkeno ndogo iliyolipuka Tanzania kaskazini mwaka

Volkeno

Kiazi cha kizungu kiazi ulaya kiazi mviringo au mbatata ni mmea wa chakula ulioko katika familia ya Solanaceae Chakula ni sehemu nene za mizizi yake yenye wanga vitamini na madini Sehemu bichi zinazoonekana juu ya ardhi haziliwi ni sumu

Viazi hivi ni chakula muhimu kimataifa ni chakula kikuu katika nyingi Asili ya mmea iko Amerika ya Kusini ilipolimwa na Maindio

PichaSolanum tuberosum JPGMaua
PichaSolanum tuberosum JPGTunda
PichaVarious types of potatoes for salejpgViazi sokoni
PichaPreparedPotatoesjpgViazi mezani

Mnavu na jamaa
Mbegu za mimea
Chakula

px
px
Seattle ni mji katika jimbo la Washington ncha ya magharibi na kaskazini ya Marekani Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa mji una wakazi wapatao milioni wanaoishi katika mji huu Mji upo m kutoka juu ya usawa wa bahari

Seattle ni bandari ya uziwa Seattle na Mombasa Kenya ni mijindugu

Mji umejulikana kimataifa hasa kwa sababu hadi ilikuwa makao makuu ya kampuni ya Boeing inayojenga ndege za abiria na mizigo

Miji ya Marekani
Washington

Swahili Let us all pull together
imagemap Kenya orthographic projectionsvg
nationalanthem Ee Mungu Nguvu Yetu O God of All Creation
officiallanguages Kiingereza na Kiswahili
other languages gKky Luhya Luo Maasai Meru Embu Arabic Somali Hindi and numerous others
demonym Kenyan
capital Nairobi
latd latm latNSS longd longm longEWE
governmenttype Semipresidential Republic
leadertitle President
leadertitle Prime Minister
leadername Mwai Kibaki
leadername Raila Odinga
largestcity Nairobi
areakm
areasqmi arearank th
areamagnitude E
percentwater
populationestimate
populationestimateyear
populationestimaterank th
populationcensus
populationcensusyear February
populationdensitykm
populationdensitysqmi populationdensityrank th
GDPPPPyear
GDPPPP billion
GDPPPPpercapita

Jamhuri ya Kenya ni nchi inayopatikana Afrika Mashariki Iko katika ikweta kando ya Bahari ya Hindi Kenya imepakana na Ethiopia eneo la kaskazini Somalia kaskazini mashariki Tanzania kusini Uganda na Ziwa Victoria magharibi kisha Sudan kaskazini magharibi Mji mkuu ni Nairobi Eneo la Kenya ni asilimia ya nchi ya Ufaransa au Texas Idadi ya watu imeongezeka katika miaka ya hivi karibuni na kukaribia milioni Kenya ina mbuga mbalimbali wanamoishi maelfu ya wanyama pori wa kila aina

Jina Kenya linatokana na Mlima maarufu wa Kenya ulio wa pili kwa urefu barani Afrika Waingereza walilitamka jina hilo kama ingawa matamshi ya wenyeji na yaliyokusudiwa katika maendelezo asiliKenia yalikuwa Enzi ya Jomo Kenyatta kuwa raisi wa Kenya miaka ya matamshi ya Kiingereza yaani yalikubalika na kutumiwa sana kwa sababu jina lake lilidumisha matamshi asilia ya wenyeji Kabla ya mwaka wa eneo linaloitwa Kenya liliitwa Himaya ya Uingereza Afrika Mashariki kwa hivyo hapakuwa na haja kutaja neno mlima uliporejelea mlima huo

Mabaki yaliyopatikana Afrika Mashariki yaonyesha kuwa viumbe mfano wa sokwe waliishi eneo hili miaka milioni iliyopita Uchunguzi wa hivi juzi karibu na Ziwa Turkana waonyesha kuwa viumbe aina ya Homo habilis walioishi miaka milioni na iliyopita na Homo erectus walioishi miaka milioni na miaka iliyopita huenda ndio wazazi wa viumbe wa kisasa homo sapiens walioishi Kenya enzi za barafu kuu kuisha barani Katika mwaka wa uvumbuzi uliofanywa na mtafiti maarufu Richard Leakey na Kamoya Kimeu huko Ziwa Turkana ulikuwa wa mifupa ya mvulana Mturkana iliyohusishwa na Homo erectus miaka millioni iliyopita Utafiti wa awali wa viumbe hawa unahusishwa na Mary Leakey na Louis Leakey ambao ndio waliohusika na uchunguzi wa mwanzo wa kiakiolojia huko Olorgesailie na Hyrax Hill Baadaye utafiti wa Olorgesailie uliendelezwa naye Glynn Isaac

Site wa Msikiti Mkuu wa Gedi ambayo dates kutoka karne ya
WazungumzaKikushi kama walivyoitwa naye Schloezer kutoka Afrika kaskazini waliingia eneo linaloitwa Kenya miaka ya kabla ya kuzaliwa kwa kristo Wafanyi biashara wa Kiarabu walianza kuja pwani ya Kenya mwaka wa BK Ukaribu wa Kenya na Uarabuni kuliraisisha ukoloni na Waarabu na Waajemi walianza kuishi eneo la pwani karne ya Hata hivyo baadhi ya walioitwa Waarabu katika eneo la Afrika Mashariki walikuwa ni machotara WaafrikaWaarabu Katika milenia ya kwanza wazungumzaji wa Kinailoti na Kibantu waliingia katika eneo hili na sasa Wanailoti ni robo tatu ya Wakenya wote kwa jumla Pwani ya Kenya imekuwa makao ya jamii ya wahunzi na jamii ya wakulima wadogo wadogo wawindaji na wavuvi ambao walikuwa mhimili wa uchumi kwa kushirika katika kulimo uvuvi utengenezaji chuma na kufanya biashara na nchi za kigeni Mwanabaharia Mreno Duarte Barbosa wa karne ya alidai kuwa Mombasa ni bandari nzuri na yenye shughuli nyingi mashua nyingi na hata meli kubwa ajabu ambazo zote hutoka Sofala na nyingine kutoka Cambay Melinde na nyingine zinazoabiri hadi kisiwani Unguja

Karne kadha kabla ya ukoloni upwa wa Kenya wanakoishi Waswahili ulikuwa sehemu ya eneo la mashariki mwa Afrika liliofanya biashara hasa ya watumwa na pembe za ndovu na Waarabu na Wahindi Inasemekana kwamba kabila la Wameru lilitokana na watumwa waliotoroka utumwa Uarabuni miaka ya Mwanzoni wafanyi biashara wengi walitoka milki za Uarabuni lakini baadaye wengine wakatoka Unguja kama Tippu Tip

Kiswahili ambayo ni lugha ya Kibantu iliyokopa msamiati wa Kiarabu Kiajemi na mwingine kutoka Mashariki ya Kati na Asia Kusini baadaye ilikua na ikawa lingua franca ya kibiashara kwa jamii mbalimbaliKiswahili ambayo ni lugha ya Kibantu iliyokopa msamiati wa Kiarabu Kiajemi na mwingine kutoka Mashariki ya Kati na Asia Kusini baadaye ilikua na ikawa lingua franca ya kibiashara kwa jamii mbalimbali Katika mwaka wa utawala wa Malindi ulimkaribisha msafiri na mvumbuzi maarufu kutoka Ureno
Vasco da Gama

Seaport Mombasa chini ya Malindi ina reli ya Nairobi kituo kusini ya Naivasha Nyeri bonyeza ramani to enlarge

Wareno walikuwa Wazungu wa kwanza kuzuru eneo la Kenya ya sasa Vasco da Gama alikuwa amezuru Mombasa mwaka wa Safari ya Vasco da Gama ilifaulu alipofika huko India na jambo hili liliwawezesha Wareno kufanya biashara moja kwa moja na Mashariki ya Mbali kupitia bahari na hivyo kutatiza mitandao ya kibiashara ya awali ya nchi kavu na baharini kama njia za biashara ya viungo zilizotumia Ghuba la Uajemi Bahari Nyekundu na misafara iliyofika hadi eneo la mashariki ya Mediterranean Jamhuri ya Venisi ndiyo iliyotawala maeneo ya biashara kati ta Uropa na Asi Baada ya njia za kawaida za nchi kavu hadi India kufungwa na Waturuki wa Ottoman Ureno ilitarajiwa kutumia njia ya barabarani iliyotumiwa kwanza na Vasco da Ghama ili kuvunja ukiritimba wa Venice Utawala wa Wareno hapa Afrika Mashariki ulijihusisha haswa na pwani iliyokaribia Mombasa Kuwepo kwa Wareno Afrika Mashariki kulianza rasmi baada mwaka wa wakati manowari za Wareno zikiongozwa na Don Francisco de Almeida zilipokishinda Kilwa kisiwa kilicho katika eneo ambalo sasa ni Tanzania kusini

Kuwepo kwa Wareno Afrika Mashariki kuliwawezesha kudhibiti biashara katika Bahari ya Hindi na kulinda njia za baharini zinazounganisha Uropa na Asia Manuari zao za kivita zilikwamiza biashara za maadui wao magharibi mwa Bahari ya Hindi na walitoza kodi ya juu bidhaa zilizosafirishwa kupitia eneo hili kwani walitawala bandari zote na njia kuu za meli Kujengwa kwa ngome iliyoitwa Fort Jesus Mombasa mwaka wa kulikusudiwa kuimarisha utawala wao katika eneo hili lakini ushawishi wao ulikatizwa na kuja kwa Waingereza Waholanzi na Waarabu wa Omani katika eneo hili karne ya Waarabu kutoka Omani ndio waliokuwa tisho kuu la utawala wa Wareno Afrika Mashariki na waliizingira ngome ya Wareno wakazishambulia meli zao za kivita kisha kuwafukuza Wareno waliobaki kutoka pwani ya Kenya na Tanzania kufikia mwaka wa Kufikia wakati huu ufalme wa Ureno haukuwa na haja na njia ya bahari ya biashara ya viungo kwani faida yake ilikuwa imepungua sana Utawala wa Wareno ulibakia tu katika bandari na maeneo ya kusini mwa Msumbiji hadi mwaka wa

Kutawaliwa kwa pwani ya Kenya na Tanzania na Waarabu kutoka Omani kuliifanya miji hii iliyojitawala hapo awali iwe chini ya uangalifu mkali wa wageni kuliko ilivyokuwa katika enzi za utawala waWareno Waarabu wa Omani kama wareno waliowatangulia waliweza kutawala eneo la pwani tu bali si eneo la bara Hata hivyo kuanzishwa kwa mashamba makubwa ya mikarafuu kuongezeka kwa biashara ya utumwa na kuhamishwa kwa makao makuu ya Waomani hadi Zanzibar mwaka wa na Seyyid Said kulisababisha waomani kuimarisha utawala wao katika eneo hili Utawala wa Waarabu katika bandari kuu zote pwani ya Afrika Mashariki uliendelea hadi Uingereza ilipoamua kumaliza biashara ya utumwa na uanzishaji wa utaratibu wa kufanya kazi kwa malipo ukaanza kushinikiza utawala wa Waomani Kufikia mwisho karne ya kumi na tisa biashara ya watumwa katika bahari zote kuu ilikuwa imeharamishwa na Waingereza na Waarabu wa Omani hawakuwa na uwezo wa kupingana na jeshi la wanamaji la Uingereza lililokuwa likitekeleza amri hiyo Waomani waliendelea kuwepo visiwani Unguja na Pemba hadi mapinduzi ya mwaka wa lakini kuwepo kwa Waarabu wa Omani nchini Kenya rasmi kulisitishwa wakati Wajerumani na Waingereza walipozithibiti bandari zote kuu na kuanzisha mahusiano ya kibiashara na viongozi mashuhuri waliokuwa wenyeji miaka ya Hata hivyo urithi waliouachwa Afrika Mashariki ungali unaonekana kupitia kwa vizazi vyao vipatikanavyo pwani ya Kenya na ambavyo vinaona kuwa asili yao ni Oman Vizazi hivi hata waleo humiliki utajiri mwingi na ndio wenye ushawishi mkubwa wa kisiasa katika jamii za pwani ya Kenya
Reli ya KenyaUganda karibu na Mombasa kuhusu

Hata hivyo wanahistoria wengi hushikilia kuwa historia ya ukoloni nchini Kenya ilianza wakati Wajerumani walipoanza kutawala mali ya Sultan wa Unguja iliyo pwani mwaka wa ikifuatwa na kuja kwa kampuni ya Imperial British East Africa Company mwaka wa Uhasama wa kwanza baina ya wabepari ulikatizwa wakati Ujerumani ilipoiachia Uingereza sehemu ya pwani iliyomiliki Hii ilifuatia kujengwa kwa reli iliyounganisha Kenya na Uganda Baadhi ya makabila ya Kenya yalipinga ujenzi huu haswa Wanandi wakiongozwa na Orkoiyot Koitalel Arap Samoei kwa miaka kumi kuanzia hadi lakini hatimaye Waingereza waliijenga reli hii Inaaminika kuwa Wanandi walikuwa kabila la kwanza kuwekwa kwenye maeneo yaliyotengewa Waafrika ili kuwazuia kutatiza ujenzi wa reli Wakati wa ujenzi wa reli Wahindi wengi wenye ujuzi waliingia nchini ili kuchangia katika ujenzi Wakati wa ujenzi wa reli kupitia mbuga ya kitaifa ya Tsavo Wahindi wengi na wenyeji Waafrika walivamiwa na simba wawili waliojulikana kama walawatu wa Tsavo Wahindi hawa na vizazi vyao baadaye walibakia nchini Kenya na kuunda kitovu cha jamii za Wahindi zijulikanayo kama Ismaili Muslim na Sikh

Mnamo Agosti Vita vya Kwanza vya Dunia vilipoanza magavana wa British East Africa kama eneo hili lilivyojulikana na German East Africa walifikia makubaliano ili kuepusha makoloni yao machanga na uhasama Hata hivyo Luteni Kanali Paul von LettowVorbeck alichukua mamlaka ya majeshi ya Ujerumani akiwa na kusudi la kutwaa raslimali nyingi iwezekanavyo za Uingereza Jeshi la Uingereza likiwa limemtenga na Ujerumani von Lettow aliendesha kampeni iliyofaulu ya vita vya kuvizia wakila walichopata wakiteka bidhaa za matumizi za Uingereza na kuepuka kushindwa Mwishowe alisalimu amri na akajisalimisha nchini Zambia siku kumi na moja baada ya mapatano ya kusimamisha vita kutiwa sahihi mwaka wa Waingereza walitumia jeshi la Wahindi kumfukuza Lettow na walihitaji wachukuzi wengi ili kubeba vifaa vya matumizi hadi bara kwa miguu na hivyo kutatua shida kuu ya uchukuzi Kundi la wanajeshi wachukuzi liliundwa na kuwajumuisha Waafrika na kuchangia katika uhamasishaji wao wa muda mrefu kisiasa

Mwanzoni mwa karne ya wakulima Waingereza na Wazungu walituama katika nyanda za juu katika eneo la kati walikoondokea kuwa matajiri kwa kulima kahawa na chai Kufikia takribani walowezi waliishi katika maeneo haya na walikuwa na ushawishi mkubwa wa kisiasa kwa sababu ya uwezo wao wa kiuchumi Maeneo haya yalikuwa makao ya watu milioni moja wa kabila la Wakikuyu na wengi wao hawakuwa na ithibati ya kumiliki mashamba kwa mujibu wa Waingereza lakini mashamba haya yalimilikiwa na kabila hili kabla ya Wazungu kufika na waliishi kama wakulima wanaohamahama Ili kuendeleza matakwa yao walowezi waliwakataza kilimo cha kahawa na kuwalazimisha kulipa kodi ya nyumba na maskwota walipewa mashamba madogo baada ya kuwafanyia kazi Wakikuyu wengi walihamia mijini kwani mashamba yao hayangeweza kutosheleza mahitaji yao

Mwaka wa Horace Hector Hearne akawa mkuu wa sheria nchini Kenya alitoka Ceylon alikoshikilia wadhifa huo huo na alifanya kazi katika Mahakama Kuu mjini Nairobi Alihudumu katika wadhifa huo hadi alipoteuliwa kama Hakimu wa Rufaa katika Mahakama ya Rufaa ya Afrika Magharibi Usiku wa tarehe Februari wakati Mfalme George VI alipoaga dunia Hearne alimsindikiza Malkia Elizabeth mke wa mwana mfalme wa Edinburgh kama alivyokuwa wakati huo kwa dhifa ya kitaifa hotelini Treetops ambayo sasa ni kivutio maarufu cha watalii Hapa ndipo alipouanzia umalkia Alirudi Uingereza mara moja akiandamana na Hearne

Kuanzia Oktoba mpaka Disemba Kenya ilikuwa katika hali ya hatari kufuatia uasi wa Mau Mau dhidi ya utawala wa Uingereza Gavana aliomba na kupata msaada wa wanajeshi Waingereza na Waafrika pamoja na Kings African Rifles Mnamo Januari Meja Jenerali Hinde aliteuliwa kuwa mkuu wa oparesheni ya kuzima uasi Hali hii haikuimarika kwa kukosa uchunguzi kwa hivyo Jenerali George Erskine aliteuliwa kuwa kamanda msimamizi wa majeshi ya kikoloni mnamo Mei akiungwa mkono hasa na Winston Churchill

Kutiwa mbaroni kwa Warhi Itote aka General China tarehe Januari na kuhojiwa kwake kulipelekea Waingereza kuuelewa vyema usimamizi wa Mau Mau Oparesheni Anvil iliyoanzishwa tarehe April ilipangwa na jeshi kwa wiki kadhaa baada ya kukubaliwa na kamati kuu ya vita Wakati wa oparesheni hii mji wa Nairobi ulidhibitiwa na wanajeshi na wakaazi wake walihojiwa huku wafuasi wa Mau Mau wakikamatwa na kupelekwa vizuizini Mnamo Mei walinzi wa nyumbani walitambulika kirasmi kama askari wa usalama Askari hawa wa nyumbani ndio waliounda kikosi cha kupambana na mikakati ya Mau Mau kwani walikuwa Waafrika waaminifu na si majeshi ya kigeni kama Jeshi la Uingereza na Kings African Rifles Kufikia mwisho wa hali ya hatari askari hawa walikuwa wamewaua Mau Mau ambayo ni asilimia ya waasi wote Kukamatwa kwa Dedan Kimathi huko Nyeri tarehe Oktoba kuliashiria kushindwa kwa Mau Mau na kukamaliza vita

Waafrika walichaguliwa moja kwa moja katika bunge la uwakilishi kwa mara ya kwanza mwaka wa Licha ya Waingereza kutamani kuwakabidhi mamlaka wapinzani wasio na siasa kali wa Kiafkrika ni chama cha Kenya African National Union KANU kilichoongozwa na Jomo Kenyatta kilichounda serikali punde tu kabla ya Kenya kupata uhuru tarehe Disemba Mwaka uo huo jeshi la Kenya lilipigana na Vita vya Shifta dhidi ya kabila la Wasomali waliokusudia kuiona NFD imejiunga na Jamhuri ya Somalia Mashifta walililemea jeshi la Kenya lakini baadaye walishindwa mwaka wa

Kenya ilitia saini mkataba na nchi ya Ethiopia mwaka wa unaodumu mpaka leo kwa kuhofia mashambulizi kutoka kwa jeshi la Somalia lililokuwa na nguvu zaidi Eneo la NFD nchini Kenya halijaendelea kutokana na kiangazi na mafuriko Hata hivyo wakimbizi wanabiashara wa Kisomali waliotajirika wamebadilisha mtaa wa Eastleigh uliokuwa wa mabanda na kuufanya kuwa ngome ya kibiashara katika sehemu kubwa ya mashariki mwa mji wa Nairobi

Tarehe Disemba Kenya ilitangazwa kuwa jamhuri huku Kenyatta akiwa rais wa kwanza Mwaka wa Kenyatta alifariki na Daniel arap Moi akawa rais Daniel arap Moi alidumisha urais kwa kuchaguliwa bila kupingwa katika chaguzi za mwaka wa uchaguzi wa ghafla na zote zikiwa zilifanyika chini ya katiba ya chama kimoja Uchaguzi wa ulifanyika mwaka mmoja mapema kutokana na njama ya kupindua serikali iliyokosa kufaulu mnamo tarehe Agosti

Mapinduzi haya yaliyotibuka yalipangwa na askari mwanahewa wa cheo cha chini Bwana Hezekiah Ochuka na kuendelezwa hasa na wanahewa Jaribio hili lilizimwa kwa haraka na wanajeshi waaminifu wakiongozwa na Jeshi la Nchi Kavu General Service Unit GSU kikosi cha polisi wenye hadhi ya kijeshi na baadaye polisi wa kawaida Hata hivyo raia kadhaa walijeruhiwa na wengine kuuawa Tukio hili lilisababisha kuvunjwa kwa kikosi chote cha wanahewa huku wengine wakiachishwa kazi na wengine wakishtakiwa kwenye mahakama ya kijeshi

Katika uchaguzi wa kura za mlolongo zilianzishwa ambapo wapiga kura walitakiwa kupiga foleni nyuma ya wagombea uchaguzi wanaowapenda badala ya kutumia kura ya siri Jambo hili lilionekana kama kilele cha enzi ya ukiukaji mkubwa wa kidemokrasia na likasababisha msukumo mkuu wa mageuzi ya kikatiba Vipengele vilivyokuwa na utata kikiwemo kile kilichoruhusu chama kimoja pekee cha kisiasa vilibadilishwa miaka iliyofuata Katika uchaguzi wa kidemokrasia wa vyama vingi wa miaka ya na Daniel arap Moi alichaguliwa tena Kulingana na katiba mwaka Moi hakuruhusiwa kuwania urais na Mwai Kibaki wa chama cha upinzani cha National Rainbow Coalition NARC akachaguliwa kuwa rais Uchaguzi huu ulitambulikana kuwa wa kidemokrasia na wachunguzi wa humu nchini na wa kimataifa na hivyo kuwa chanzo cha mageuzi makubwa ya kidemokrasia nchini Kenya

Tarehe Novemba ilitangazwa kuwa sikukuu ya kitaifa kusherehekea ushindi wa Barack Obama ambaye babake alikuwa Mkenya kama rais wa Marekani

Katika sehemu za mashambani kama wilayani Kisii visa vya kuchoma watu wakidaiwa kuwa wachawi vinaongezeka Waathiriwa hasa ni wanawake wakongwe Mnamo Mei watu waliuwa na nyumba kuchomwa

Kufikia mwaka wa eneo linaloitwa Kenya lilijulikana kama koloni la Uingereza la Afrika Mashariki Mwaka wa koloni la Kenya liliundwa na kupatiwa jina linalotokana na Mlima Kenya na linatamkwa kinj

Saa uhuru mwaka Jomo Kenyatta alichaguliwa kama rais wa kwanza Awali alikuwa alishika jina hili kutafakari ahadi yake ya kumkomboa nchi yake na matamshi yake ya jina lake ulisababisha katika matamshi ya Kenya katika Kiingereza kubadilisha nyuma ya makadirio ya awali uliotokea matamshi

Maandamano haya yalibadilika kuwa ghasia zilizosababisha kuharibiwa kwa mali Viongozi mashuhuri wa Afrika wakiongozwa na aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Kimataifa Kofi Annan walisuluhisha mzozo huu wa kisiasa kwa amani Kundi la Annan liliungwa mkono na Umoja wa Mataifa Jumuia ya Ulaya Muungano wa Nchi za Afrika Serikali ya Merikani na nchi zingine maarufu ulimwenguni kote Kwa habari zaidi rejelea Ghasia nchini Kenya

Annan aliomba usaidizi kwa kamati yake ya upatanishi kutoka kwa shirika la kushughulikia mizozo la Uswizi lijulikanalo kama Kituo cha Mazungumzo ya Kihisani yaani Centre for Humanitarian Dialogue

Tarehe mwezi wa Februari Kibaki na Odinga walitia sahihi mkataba wa kuunda serikali ya muungano ambapo Odinga angekuwa waziri mkuu wa pili nchini Kenya Kulingana na mkataba huu rais angeteua baraza la mawaziri kutoka pade zote mbili za PNU na ODM kulingana na wingi wa wabunge wa kila chama bungeni Mkataba huu ulieleza kuwa baraza la mawaziri litajumuisha Makamu wa Rais na manaibu wawili wa Waziri Mkuu Baada ya majadiliano bungeni ilipitishwa kuwa muungano huu utadumu hadi mwisho wa kipindi cha bunge ama chama kimoja kikijitoa kwenye muungano kabla ya kipindi cha bunge kuisha

Ofisi hii mpya ya waziri mkuu itakuwa na nguvu na mamlaka kuratibu na kusimamia shughuli za serikali Vile vile itaongozwa na mbunge aliyechaguliwa ambaye pia atakuwa kiongozi wa chama au muungano wa vyama wenye idadi kubwa ya wabunge bungeni Ulimwengu ulimshuhudia Annan na kamati yake iliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na mwenye kiti wa muungano wa nchi za Afrika Jakaya Kikwete walipowaleta pamoja wapinzani hawa sugu kwenye sherehe za kutia sahihi mkataba huu Sherehe hizi zilionyeshwa moja kwa moja kwenya televisheni ya kitaifa kutoka kiingilio cha Jumba la Harambee mjini Nairobi Wawakilishi wa PNU na ODM walianza majadiliano ya kina kuhusu ugavi wa mamlaka tarehe mwezi wa Februari Wabunge wa Kenya kwa pamoja waliidhinisha mkataba wa ugawaji mamlaka tarehe mwezi wa Machi ili kuiokoa Kenya iliyoaminika kama mojawapo ya nchi thabiti na iliyoendelea barani Afrika Mkataba huu uliunganisha PNU iliyoongozwa na Kibaki na ODM ya Odinga kisha kupelekea kuundwa kwa serikali ya muungano vyama vyote viwili vikiwa na mamlaka sawa

Mnamo tarehe Aprili Rais Kibaki aliitangaza baraza la mawaziri wa serikali hii ya muungano ikijumuisha waziri mkuu na makamu wake wawili Baraza hili lilijumuisha pia manaibu wa mawaziri na lilitawazwa katika Ikulu ya Nairobi tarehe Aprili huku Dkt Kofi Annan na viongozi wengine mashuhuri wakishuhudia

Mikoa ya Kenya

Kenya ina mikoa minane kila mmoja ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa anayeteuliwa na rais Mikoa mkoa umoja imegawanywa katika wilaya Kulingana na sensa ya mwaka kulikuwa na wilaya Wilaya zimegawika kuwa tarafa Tarafa hizi nazo zimegawika kuwa mitaa kisha kugawika kuwa mitaa midogo Mji wa Nairobi umenufaika kuwa eneo la kiutawala la mkoa Serikali husimamia utawala wa wilaya na mikoa Mikoa hii ni

Mkoa wa Kati
Mkoa wa Pwani
Mkoa wa Mashariki
Mkoa wa Nairobi
Mkoa wa Kaskazini Mashariki
Mkoa wa Nyanza
Mkoa wa Bonde la Ufa
Mkoa wa Magharibi

Serikali ya mitaa huendelezwa kupitia kwa mabaraza ya miji Maeneo mengi ya mijini huwa ni mji manisipaa au baraza la mji Serikali za mitaa katika maeneo ya mashambani huitwa serikali za wilaya Madiwani wa mitaa hii huchaguliwa katika uchaguzi wa madiwani unaofanywa wakati mmoja na uchaguzi mkuu

Maeneo ya uwakilishi bungeni yamegawanywa kwa sababu ya upigaji kura Kuna maeneobunge nchini Kenya

Mlima Kenya ni kilele cha juu kabisa katika Kenya saa Kenya ni jina lake baada ya mlima
Kenya ni nchi ya kwa ukubwa duniani ikifuata Madagascar

Twiga katika Mbuga ya wanyama ya Kitaifa ya Nairobi na upeo wa macho wa Nairobi nyuma yake
Kenya ina eneo kubwa linaloishi wanyama wa pori likiwemo Masai Mara ambapo nyumbu na wanyama wengi wala nyasi hushiriki katika uhamaji kila mwaka Takribani nyumbu huangamia kila mwaka katika uhamaji huu wa kutafuta lishe wakati wa kiangazi Wale wanyama wakubwa watano wa Afrika wanapatikana Kenya simba chui nyati kifaru na ndovu Wanyama wengine wengi wa pori na ndege hupatikana katika mbuga za kitaifa na hifadhi za wanyama hawa nchini Mazingira ya Kenya yanatishiwa na kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu na athari zake

A route katika Mashariki Tsavo National Park

Kenya ni nchi yenye jua Ina joto na unyevunyevu sehemu za pwani joto kiasi sehemu za bara na ni kame katika sehemu za kaskazini na kaskazini mashariki mwa nchi Hata hivyo kuna mvua nyingi kati ya mwezi wa Machi na Aprili na mvua ya kadri kati ya Oktoba na Novemba Halijoto huwa juu miezi hii yote

Katika nchi hii jua huwaka mwaka mzima na nguo za majira ya jua huvaliwa mwaka mzima Hata hivyo huwa na baridi usiku na pia asubuhi na mapema

Mvua ya masika hunyesha kuanzia Aprili hadi Juni Mvua ya vuli nayo hunyesha kuanzia Oktoba hadi Disemba Wakati mwingine mvua hii huwa nyingi na aghalabu hunyesha wakati wa alasiri na jioni Majira ya joto jingi ni kuanzia Februari hadi Machi nayo ya baridi ni Julai hadi Agosti

Uhamaji wa wanyama wa kila mwaka hasa uhamaji wa nyumbu hutokea Juni hadi Septemba na hushirikisha mamilioni ya wanyama Tukio hili huwavutia sana wapigaji picha za sinema

shilingi note kutoka depicting kishaRais Daniel Arap Moi

Baada ya uhuru Kenya iliendeleza ukuaji wa kiuchumi haraka kupitia kwa uwekezaji wa umma kuhimiza uzalishaji wa kilimo na kushawishi uwekezaji wa watu binafsi na wageni katika viwanda Pato la taifa lilikua kwa asilimia kuanzia hadi Uzalishaji wa kilimo ulikua kwa asilimia kila mwaka kwa kipindi hicho ukiwa umechochewa na ugawaji upya wa mashamba kuanzishwa kwa kilimo cha mimea iliyoimarishwa na kuanzisha mashamba mapya

Hata hivyo kati ya na ukuaji wa kiuchumi wa Kenya ulipungua Kupungua kwa kilimo kulisababishwa na sera za kilimo zisizofaa mikopo isiyotosha na vikwazo visiyofaa vya biashara ya kimataifa

Mnamo mwaka wa Serikali ya Kenya ilianzisha mpango mkuu wa kuimarisha uchumi na kuufanya huru Waziri mpya wa fedha na gavana mpya wa Benki Kuu ya Kenya walianza mikakati iliyofuatana kuimarisha uchumi kwa usaidizi wa Benki Ya Dunia na Shirika La Fedha la Kimataifa Kama sehemu ya mpango huu serikali iliondoa usimamizi wa bei za bidhaa leseni za uagizaji na uthibiti wa ubadilishaji fedha kubinafsisha kampuni nyingi zilizomilikiwa na umma kupunguza idadi ya wafanyi kazi wa serikali na kuanzisha sera madhubuti za kulinda fedha Kuanzia mwaka wa hadi ukuaji halisi wa uchumi wa Kenya ulikadiriwa juu kidogo ya asilimia kwa mwaka

Hata hivyo kati ya na uchumi uliingia kipindi cha kupungua au kutoimarika kwa sababu ya hali mbaya ya anga na kupungua kwa shughuli za kiuchumi Mwaka wa pato la taifa liliimarika kiasi kwani mvua ilirejea kunyesha karibu na viwango vya awali Ukuaji wa kiuchumi uliendelea kuimarika kiasi mwaka wa na kufikia asilimia mwaka wa asilimia mwaka wa kisha asilimia mwaka wa
Mandhari ya juu ya sehemu ya mizigo katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta ambao ndio mkubwa zaidi na wenye shughuli nyingi zaidi katika eneo la Afrika Mashariki

Mnamo Julai Serikali ya Kenya ilikataa kutimiza makubaliano ya awali na IMF kuhusu mabadiliko ya utawala wake Jambo hili lilisababisha kukatizwa kwa misaada kwa miaka nayo Benki ya Dunia ikaubana mkopo wa dola milioni za mpango wa kuufufua uchumi Ingawa mabadiliko mengi ya kiuchumi yaliyofanywa kati ya yalibakia wataalamu wa maswala ya kiuchumi wasiopendelea mabadiliko waliamini kuwa Kenya iliitaji mabadiliko zaidi hasa ya kiutawala ili kuongeza ukuaji wa pato la taifa GDP

Serikali ya Kenya ilichukua hatua yakini za mabadiliko pamoja na kuunda Tume ya Kupambana na Ufisadi KACA kuanzisha hatua za kuimarisha uwazi wa katika mikakati ya serikali kupata bidhaa na kupunguza fedha inayotumiwa na serikali kulipia mishahara Mnamo Julai shirika la IMF lilitia saini dola milioni za Poverty Reduction and Growth Facility PRGF nayo Benki ya Dunia ilifuatia na mkopo wa dola milioni kuimarisha uchumi na kuibadilisha sekta ya umma Mwezi wa Disemba iliamuliwa kuwa tume ya kupambana na ufisadi haikuwa ya kikatiba na sehemu za juhudi za mabadiliko kukatizwa mwaka Shirika la IMF na Benki ya Dunia zilikatiza mipango yao Juhudi zilizofanywa kuanzisha upya mipango hii katikati ya mwaka wa hazikufaulu

Chini ya uongozi wa Rais Kibaki aliyechukua hatamu za uongozi tarehe mwezi wa Disemba serikali ya Kenya ilianzisha mipango mipya na kabambe ya uimarishaji uchumi na imerejelea ushirikiano wake na Benki ya Dunia na IMF Serikali mpya ya National Rainbow Coalition NARC iliidhinisha Sheria dhidi ya Ufisadi na Uhalifu wa Kiuchumi pamoja na Sheria ya Maadili ya Watumishi wa Umma mnamo Mei iliyolenga kupiga vita ufisadi katika ofisi za umma Mabadiliko mengine hasa katika idara ya sheria kuagiza bidhaa za umma na kadhalika yamepelekea kurejelewa kwa misaada na matumaini ya kuimarisha uchumi Kufuatia kupitishwa kwa sheria muhimu za kupambana na ufisadi na serikali mpya wafadhili walirejelea ufadhili mwezi wa Novemba na IMF ikaidhinisha msaada wa miaka mitatu wa dola milion ili kupunguza umaskini na kuimarisha uchumi Wafadhili wakatoa dola bilioni kama msaada wa miaka minnne Kurejelewa kwa ufadhili na kujihusizisha upya kwao kumevutia imani ya wawekezaji

Mswada wa ubinafsishaji umeidhinishwa hata ingawa kuanzishwa kwa tume ya ubinafsishaji hakujakamilika mabadiliko katika utendakazi wa umma yametekelezwa na mwaka wa Kenya ilishinda tuzo la Umoja wa Kimataifa la Utenda kazi wa Umma Hata hivyo kazi nyingi inahitajika kufanywa ili kuiwezesha nchi hii kuyafikia mataifa yaliyoendelea sana kiuchumi hasa yale ya Mashariki ya Mbali Changamoto kuu ni pamoja na kuchukua hatua thabiti dhidi ya ufisadi kupitisha sheria zinazoshughulikia ugaidi na biashara haramu kutatua upungufu wa ufadhili wa bajeti kisha kurekebisha na kuunda miundo msingi Inaaminika haya yatasaidia kudumisha sera za kimsingi za kiuchumi na kuhakikisha ukuaji wa kasi wa kiuchumi uliofikia asilimia mwaka wa

Mwaka wa serikali ya Kenya ilizindua Ruwaza ambao ni mpango wa kiuchumi wenye matumaini makuu na ambao ikiwa utatekelezwa kikamilifu una uwezo wa kuifanya nchi hii kuwa katika kiwango sawa na mataifa yaliyoendelea kiuchumi ya Asia

Nairobi inaendelea kuwa kituo muhimu na cha kimsingi kwa mawasiliano na biashara cha Afrika Mashariki Kinajivuna kuwa na miundo msingi ya uchukuzi na mawasiliano bora zaidi katika eneo hili na wafanyi kazi wenye ujuzi Makampuni mengi ya kigeni hudumisha matawi yao katika eneo hili ama ofisi za kuyawakilisha mjini Nairobi Mnamo Machi Marais wa Kenya Tanzania na Uganda waliifufua Jumuia ya Afrika Mashariki EAC Shabaha za EAC ni pamoja na kasawazisha kodi na ada zinazotozwa bidhaa utembeaji huru wa watu na kuimarisha miundo msingi katika eneo hili Nchi hizi tatu za Afrika Mashariki zilitia saini mkataba wa Customs Union Agreement mwezi wa Machi

Mwanzoni mwa mwaka wa Raia wa Uchina Hu Jintao alitia saini kandarasi ya utafutaji wa mafuta na Kenya Haya ndiyo makubaliano ya hivi punde kati ya mfululizo wa mapatano yaliyopagwa kuelekeza maliasili ya Afrika huko Uchina ambako uchumi wake waendelea kukua kwa haraka

Kandarasi hii iliwezesha kampuni inayoongozwa na taifa la Uchina offshore oil and gas company CNOOC Ltd kutafuta mafuta Kenya ambayo imeanza kuchimba visima vya kwanza mpakani mwa Sudan na Somalia na katika maji ya upwa wake Hata hivyo hakuna mafuta yametolewa na pia hakuna makadirio rasmi ya visima vya mafuta

Kenya ni nchi yenye makabila mengi tofauti tofauti Wakenya wengi huzungumza lugha mbili Kingereza na Kiswahili na asilimia kubwa pia huzugumza lugha ya mama ya kabila yao

Makundi ya makabila
Wakikuyu Waluyia Wajaluo Wakalenjin Wakamba Wakisii Wameru makabila mengine ya Kiafrika wasioWaafrika Wahindi Waingereza na Waarabu

Mfumo wa elimu nchini Kenya unajumuisha elimu ya chekechea ya msingi ya sekondari na ya vyuo Elimu ya watoto wadogo aghalabu huchukua miaka mitatu ya msingi miaka minane sekondari minne na chuo kikuu miaka minne au sita kutegemea kozi Shule za chekechea ambazo ni za watoto wa umri wa miaka mitatu hadi mitano ni sehemu muhimu ya mfumo huu wa elimu na ni kigezo muhimu kabla ya kusajiliwa katika darasa la kwanza Gredi ya Kwanza Mwishoni mwa elimu ya msingi wanafunzi hufanya mtihani wa Cheti cha Kuhitimu Masomo ya Msingi Kenya KCPE ambao huamua watakaojiunga na shule ya sekondari au vyuo vya ufundi Umri wa shule ya msingi ni miaka hadi Wale wanaojiunga na shule ya upili hufanya mtihani wa kitaifa mwishoni mwa kidato cha nneMtihani wa Cheti cha Kuhitimu Masomo ya Shule ya Upili Kenya KCSE ambao huamua watakaojiunga na vyuo vikuu vyuo vya taatuma nyinginezo au kuajiriwa Baraza Kuu la Usajili JAB ndilo lenye jukumu la kuwachagua wanafunzi watakaojiunga na vyuo vikuu vya umma Mbali na shule za umma kuna shule nyingi za kibinafsi nchini hasa katika sehemu za miji Vilevile kuna shule kadhaa za kimataifa zinazofundisha mifumo mbalimbali ya elimu ya ngambo

Mfumo wa kwanza wa elimu nchini Kenya baada ya uhuru uliletwa na wakoloni Waingereza Baada ya Kenya kupata uhuru tarehe Disemba Tume ya Ominde iliundwa ili kuleta mabadiliko ya kielimu ambayo yangeakisi matarajio ya taifa huru la Kenya Tume hii ilimulika maswala ya usawa na umoja ambayo yalikuwa maswala muhimu wakati huo Mabadiliko ya kilichofundishwa katika historia na geografia yalifanywa ili kuakisi umoja wa kitaifa Kati ya na mfumo wa ulifuatwa miaka saba masomo ya msingi miaka minne sekondari ya daraja la chini miaka miwili sekondari ya daraja la juu na miaka mitatu masomo ya chuo kikuu Shule zote zilifuata mtalaa mmoja

Mwaka wa kamati iliyoteuliwa na rais kuratibu namna ya kuanzisha chuo kikuu cha pili nchini Kenya na pia kwa jumla kuubadilisha mfumo wa elimu ilianza kazi yake Kamati hii ilipendekeza kuwa mfumo ule wa ubadilishwe kuwa mfumo wa miaka minane shule ya msingi miaka minne shule ya upili miaka minne ya elimu ya chuo kikuu Jedwali lililo katika Elimu ya Sasa Nchini Kenya linaonyesha muundo wa mfumo wa Ingawa mfumo wa kinadharia ulifikia kikomo mfumo wa ulipoanzishwa mwaka wa kundi la mwisho la mfumo huo wa awali lilihitimu kutoka vyuo vikuu vya Kenya mwaka wa

Mfumo wa sasa wa ilizinduliwa Januari Ulitilia mkazo masomo ya kiufundi kwa matarajio kuwa muundo huu mpya utawawezesha wanaoacha shule katika viwango mbalimbali aidha kujiajiri wenyewe au kupata ajira katika sekta ya juakali

Mnamo Januari Serikali ya Kenya ilitangaza kuanzishwa kwa masomo ya shule za msingi bila malipo Hili lilipelekea kuongezeka kwa wanafunzi waliojiunga na shule za msingi kwa asilimia Hata hivyo idadi ya waliojiunga na shule za upili na vyuo haikuongezeka sana kwa sababu malipo bado yalihitajika ili kuhudhuria masomo

Mtihani wa kuhitimu cheti cha masomo ya msingi nchini Kenya KCPE hufanywa katika darasa la nane Matokeo ya mtihani huu huhitajika ili kusajiliwa katika shule ya upili Mtihani wa kuhitimu cheti cha masomo ya shule ya upili nchini Kenya KCSE hufanywa katika kidato cha nne Wanafunzi hufanya mtihani katika masomo nane

Mfumo wa kutuza Gredi za KCSE

Gredi ya wastani hutegemea jinsi mwanafunzi hupita masomo haya nane Endapo mtahiniwa atafanya zaidi ya masomo manane gredi ya wastani itategemea masomo manane ya kwanza anayopita vyema zaidi Kujiunga na chuo kikuu hutegemea masomo manane yanayopitwa zaidi na jinsi masomo fulani yamepitwa kutegemea kozi ya shahada fulani
Kwa mfano

Jumla ya pointi ni

Gredi ya wastani ni na ukiigawa mara ni sawa na hii ni karibu sawa na pointi ambayo ni B kwa mujibu wa mfumo wa gredi Mwanafunzi apataye gredi kama hii hufaulu kujiunga na mojawapo ya vyuo vya umma kwa kupata gredi nzuri Taasisi za mafunzo vitivo na idara huamua mahitaji ya kimsingi ya kujiunga navyo

Wanafunzi wanaopata gredi ya C hufaulu kusomea kozi ya shahada fulani katika chuo kikuu Kwa sababu ya ushindani mkubwa na nafasi chache katika vyuo vikuu wale wanaopata gredi ya B na wakati mwingine B na zaidi huchukuliwa kusomea shahada mbalimbali katika vyuo vya umma na hufaidi kwa kulipa karo iliyotolewa ruzuku na serikali Wale wengine hujiunga na vyuo vikuu vya kibinafsi au na vyuo vya kati

Jambo la kushangaza ni kuwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu vya umma kupitia JAB hutegemea jumla ya nafasi za kulala zinazopatikana katika vyuo vyote vya umma Hata hivyo wanaokosa nafasi hizi ingawa walipata gredi za chini zaidi za kujiunga na vyuo vikuu C au C wakiwa na cheti cha diploma fulani husajiliwa kupitia mpango wa kujilipia karo katika vyuo vikuu Module II ikiwa wanaweza kujilipia karo yote ya kozi husika

Jambo hili limezua mjadala mkali huku watu wakiuliza sababu na uadilifu wa kuwafungia nje wanafunzi waliofaulu kujiunga na vyuo vya umma kisha kuwasajili wanaotoka kwa familia zenye uwezo wa kifedha

Mfumo wa elimu wa Kenya umepitia mengi magumu katika kipindi cha miaka ulichodumu Punde tu baada ya kufuzu kwa kundi la kwanza la wanafunzi wa mfumo huu mwaka wa wananchi wengi walijitokeza kuilaumu na kuihukumu serikali kwa kuuanzisha mfumo huu Wakosoaji hawa walidai kuwa waliohitimu walikuwa hawajaandaliwa vyema na hawangeweza kushindana na wenzao kutoka sehemu nyingine za ulimwengu Wengine walihoji kuwa waliofuzu kupitia kwa mfumo huu walikuwa aidha wachanga sana au hawajaandaliwa vyema kwa nafasi za kazi zilizokuweko Serikali haikusikiza haya yote pengine kwa sababu uwezekano wa kuubadilisha na kuuunda upya kungeigharimu pesa nyingi

Hata hivyo kwa miaka mingi waliofuzu wamewaaibisha walioupinga kwa kufualu katika vyuo vya hapa nchini na ngambo Kwa hakika kuhama kwa wasomi na wafanyikazi wa afya hadi nchi zilizoendelea ni dhihirisho tosha la hali hii Wengi waliofuzu kupitia kwa mfumo huu wamefaulu katika vyuo vikuu vya ngambo

Mkazo uliotiliwa masomo ya kiufundi umefifia na mabadiliko ya hivi juzi katika mtaala yanasisitiza teknolojia ya ubadilishanaji habari sayansi hesabu na lugha Kwa vyovyote vile kazi ya kiakademia na kusisitizwa kwa kupita mitiani iliyoandikwa hakujaacha nafasi kwa useremala uashi upishi na mafunzo mengine ya kiufundi

Maasai warriors
A Wamaasai mtu katika jadi attire

Kenya ni nchi yenye tamaduni anuwai Tamaduni zinazotambulika ni pamoja na Waswahili walio katika eneo la pwani jamii za wafugaji katika eneo la kaskazini na jamii nyingine mbalimbali katika maeneo ya kati na magharibi Leo hii utamaduni wa Wamaasai unaajulikana sana kwa kuangaziwa vilivyo na utalii hata hivyo Wamaasai ni asilimia ndogo ya idadi ya Wakenya kwa jumla Wamaasai wanatambulika kwa kujipamba sehemu ya juu ya mwili na kwa vito

Kenya ina utajiri mwingi wa muziki vituo vya runinga na maonyesho ya sanaa

Kenya hushiriki katika michezo mbalimbali ikiwemo kriketi mbio za magari soka ragbi na ngumi Lakini nchi hii inajulikana hasa kwa kutawala katika mbio za masafa ya kadri na mbio za masafa marefu Kenya kwa muda mrefu imetoa mabingwa wa Olimpiki na michezo ya Jumuia ya Madola katika nyanja mbalimbali hasa katika mbio za mita mita mita kuruka viunzi na maji mita mita na mbio za masafa marefu Wanariadha wa Kenya hasa Wakalenjin wanaendelea kutawala mbio za masafa ulimwenguni ingawa ushindani kutoka nchi ya Morocco na Ethiopia umepunguza umaarufu huu Wanariadha wa Kenya wanaosifika sana ni pamoja na mshindi maranne wa mbio za masafa marefu za Boston kwa wanawake na mshindi marambili wa mbio za dunia Catherine Ndereba aliyeshikilia rekodi ya awali ya mbio za dunia Paul Tergat na John Ngugi

Kenya ilishinda medali kadhaa wakati wa michezo ya Olimpiki ya Beijing za dhahabu za fedha za shaba na kulifanya taifa lililofaulu sana barani Afrika katika michezo ya Olimpiki ya mwaka Wanariadha wapya walitambulikana kama Pamela Jelimo mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za mita kwa wanawake aliyejitahidi na kushinda tuzo la Golden League na Samuel Wajiru aliyeshinda mbio za masafa marefu kwa wanaume

Bingwa mstaafu wa mbio za Olimpiki na za Jumuia ya Madola Kipchoge Keino alisaidia kuanza ubingwa wa mbio za masafa marefu miaka ya na akafuatwa na Bingwa wa michezo ya Jumuia ya Madola Henry Rono aliyeshikilia rekodi kadhaa za dunia

Hivi majuzi kumekuwa na mzozo wa wanariadha wa Kenya kufuatia kusaliti nchi yao Kenya na kuwakilisha nchi nyingine hasa Bahrain na Qatar Wizara ya michezo ya Kenya imejaribu kuzuia usaliti huu lakini umeendelea tu Bernard Lagat akiwa wa mwisho akichagua kuiwakilisha Merekani Mizozo hii ilipelekea Kenya kupigwa marufuku na FIFA lakini marufuku hii iliondolewa mnamo Machi

Kwa upande wa mbio za magari Kenya ndio waandalizi wa mbio za magari maarufu za Safari Rally zinazotambulika kuwa ngumu zaidi ulimwenguni na ambazo ni sehemu ya Bingwa wa Mbio za Magari kwa miaka mingi hadi kuondolewa kwake baada ya mbio za kwa sababu ya matatizo ya kifedha Baadhi ya madereva maarufu wa mbio za magari ulimwenguni walioshiriki na kushinda mbio hizi ni kama Bjorn Waldegard Hannu MokkolaTommi Makinen Shekhar MehtaCarlos Sainz na Colin McRae Ingawa mbio hizi bado huendelea kila mwaka kama sehemu ya kutafuta Bingwa wa Mbio za Magari Afrika waandalizi wanatarajia kuruhusiwa kujiunga tena na Ubingwa wa Magari Ulimwenguni katika miaka michache ijayo

Ngugi wa Thiongo ni mmoja wa waandishi maarufu wa Kenya Kitabu chake Weep not Child ni ufafanuzi wa maisha yalivyokuwa Waingereza walipoitwaa Kenya Hii ni hadithi kuhusu athari za Mau Mau katika maisha ya Wakenya weusi Kinavyochanganya maudhui ukoloni elimu na mapenzi kunakifanya kuwa mojawapo wa vitabu bora vya hadithi barani Afrika

Kitabu cha hadithi cha MG Vassanjis The InBetween World of Vikram Lall kilishinda tuzo la Giller Prize mwaka Hii ni hadithi ya kubuni ya Mkenya mwenye asili ya Kihindi na familia yake wavyojizatiti na mabadiliko ya kisiasa wakati wa ukoloni na baada ya ukoloni nchini Kenya

Kuanzia mwaka wa jarida la fasihi Kwani limekuwa likichapisha fasihi ya kisasa ya Kenya

Serikali
Spokeperson serikali Ofisi Mnenaji wa Serikali ya Jamhuri ya Kenya
Serikali ya Kenya Official site
Kenya Law Reports Legislation Kenya Uchunguzi Sheria Official Gazette Notices na kisheria Info
State House Kenya Official site State House Kenya
httpswwwciagovlibrarypublicationsworldleadersworldleaderskkenyahtml Mkuu wa Nchi na Cabinet Members

Jumla

Maelezo ya nchi Country Profile kutoka BBC News
Kenya kutoka Encyclopaedia Britannica
Kenya kutoka UCB Libraries GovPubs

Vyombo vya habari
Vyombo vya habari Kenya orodha kutoka Chuo Kikuu cha Stanford

Utalii
Kenya Tourist Board Magical Kenya rasmi kusafiri na utalii kuongoza

Historia
Encyclopedia Britannica juu ya Kenya Colony
Encyclopedia Britannica juu wa Dermacation wa EthiopiaKenya Border

Zingine
Kenya Coast bibliography Academic bibliography hasa kwa Kiingereza compiled by Jan Hoorweg AfrikaStudiecentrum Leiden
Kamili Nakala ya kitabu saa zilizounganishwa

Vijijini umaskini katika Kenya IFAD
Kenya View A photographic mkabala na uzuri wa Kenya
UNESCO Nairobi Office Sekta ya Elimu Clearinghouse
Solar kupikia historia na maendeleo ya hivi karibuni nchini Kenya


Nchi za Afrika
Wanachama wa Umoja wa Afrika
Nchi za Bahari ya Hindi
Afrika Mashariki
Nchi na maeneo yanayozungumza Kingereza
Nchi na sehemu ambazo Kiswahili kinazungumzwa
Nchi na maeneo ya Wabantu
Mataifa ya G
Wanachama wa Jumuiya ya Madola
Majimbo na wilaya zilizoanzishwa mwaka

Mombasa
Mombasa ni mji mkubwa wa pili wa Kenya mwenye bandari muhimu zaidi ya Afrika Mashariki Iko kwenye mwambao wa Bahari Hindi Kuna wakazi kwenye kisiwa cha Mombasa pamoja na sehemu zake barani

Mombasa ni kitovu cha utalii wa pwani la Kenya Watalii walio wengi hufika kweye kiwanja cha ndege cha Moi

Kati ya ishara ya mji ni Boma la Yesu na pembe za Mombasa

Kiswahili cha Mombasa chaitwa Kimvita

Mombasa na Seattle ni mijindugu

Imombasa
Mombasa Online Kijerumani
Mombasa Polytechnic University College
Port of Mombasa

Miji ya Kenya
Kenya
Waswahili

Karte Togos
Togo ni nchi katika Afrika ya Magharibi kwenye mwambao wa Ghuba la Guinea ya Atlantiki ikipakana na Benin upande wa mashariki Burkina Faso kwa kaskazini na Ghana kwa mashariki
Idadi ya wakazi ilikuwa takriban milioni mwaka Mji mkuu ni Lome

Togo ni nchi ndogo katika Afrika yenye km pekee kwa umbo la pembenne yenye urefu wa km na upana wa takriban km Mwelekeo wa eneo la nchi ni kaskazini kusini kuna kanda zote za kijiografia ya Afrika ya Magharibi kuanzia pwani lenye machanga na misitu ya minazi kwenye kusini vilima vya nyanda za juu katikati na savana pamoja na maeneo yabisi zaidi ya Sahel kaskazini

Nchi ilianzishwa kama koloni ya Togo ya Kijerumani katika pengo kati ya maeneo ya Uingereza na Ufaransa

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia koloni ya Kijerumani iligawiwa kati ya majirani chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa na baadaye ya Umoja wa Mataifa

Katika Disemba ya wakazi wa Togo ya Kiingereza waliamua kwa kura kubaki na Ghana Hivyo ni Togo ya Kifaransa pekee iliyopata uhuru mwaka

Rais wa kwanza alikuwa Sylvanus Olympio
ya kuendelea

Serikali ya Togo

Nchi za Afrika


Mhanga au fundimchanga ni mnyama wa Afrika Wahanga hula chungu na mchwa Wanatokea pande nyingi za Afrika

Majina ya mamalia kwa Kiswahili
Wanyamapori

estimates vary
pop or
ref

Kazi kwa haki na kujitegemea kwa jamii kuendeleza Wamasai Watu
Mara Triangle Wamaasai Vijiji Association
Mtandao wa Change Shirika kwa Wamaasai
Wamaasai mawasiliano info kubadilishana noc Marafiki
Marafiki Kisaru Wamaasai Mradi
Massailand Website kuhusu Wamaasai watu na kusaidia miradi
Kujitolea kusaidia miradi katika Maasailand Kenya
Wamaasai Trust

Wamaasai
Makabila ya Afrika
Asili ya watu wa Afrika Mashariki

px
Ulaya
Ulaya
Ulaya
Ulaya ni bara eneo la Ulaya ni km na wakazi ni milioni
Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisationsmap

Baada ya vita kuu mbili nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali katika karne ya
Baraza ya Ulaya ina nchi wanachama
Mkutano wa usalama na ushirikiano katika Ulaya Marekani na Kanada ni wanachama pia
Umoja wa Ulaya mwenye nchi wanachama tangu mwaka

Mpangilio ufuatao unafuata ratiba ya Umoja wa Mataifa Lakini utaratibu huu haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati Wajerumani Waaustria Waswisi Wacheki Waslovakia na Wapoland hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki lakini Ulaya ya Kati Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado kwa mfano swali la Hungaria au Latvia

Notes
Kanda zinazotajwa Ulaya ya Kusini magharibi nk zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisationsmap Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine Asia Africa au Oceania Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao

Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee

Guernsey Kisiwa cha Man and Jersey ni maeneo ya kujitegema chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza

Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika

Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani la Marokko Afrika ya Kaskazini

Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini Bahari Hindi au Oceania

Uholanzi Idadi ya wakazi ni ya Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali

Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi kufuatana na kanda za UM na Ulaya ya Mashariki

Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi kufuatana na kanda za UM na Ulaya ya Mashariki idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee

Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi kufuatana na kanda za UM na Ulaya ya Kusini idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus

Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi kufuatana na kanda za UM na Ulaya ya Mashariki idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee

Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi kufuatana na kanda za UM na Ulaya ya Kusini namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul

Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi kufuatana na kanda za UM na Ulaya ya Mashariki idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee


Bara

Lituanya au pia Lituania ni nchi iliyoko Kaskazini Mashariki mwa Ulaya Inajulikana rasmi kama Jamhuri ya Lituania Mji mkuu wa Litwania ni Vilnius

Lituanya iko kwenye mwambao wa Bahari ya Baltiki

Vilnius

Kaunas
Vilnius

nchi ilikuwa jamhuri mwanachama wa Umoja wa Kisovyeti na kabla hayo sehemu ya Dola la Urusi

Nchi za Ulaya

Europa ni neno katika lugha mbalimbali lenye asili ya Kigiriki la kutaja

bara la Ulaya
Europa dini binti wa mfalme katika masimulizi ya dini ya Wagiriki wa Kale aliyekuwa mpenzi wa mungu mkuu Zeus
Europa mwezi mwezi wa pili kati ya miezi ya Mshtarii
Europa asteroidi katika mfumo wa jua
Europa kisiwa kisiwa ndogo cha Kifaransa katika bahari Hindi ni sehemu ya les parses
Europa kombora ilikuwa kombora la Kiulaya la kurusha vyombo angani kabla ya kupatikaka kwa makombora ya Ariane

Kuna pia nyimbo vitabu meli gari na michezo ya kompyuta na makampuni zinazoitwa Europa

Makala zinazotofautisha maana

Shilingi ni pesa inayotumika kwa malipo halali katika nchi za Tanzania Kenya Uganda na maeneo ya mipaka ya nchi za Maziwa Makuu Zambia Malawi na Msumbiji

Asili yake ni kitengo cha kihistoria cha pesa ya Uingereza iliyoitwa Shilling Hadi Pauni ya Kiingereza ilikuwa na shilling na kila shilling ilikuwa na penny

Uingereza ilitoa East African Shilling kuanzia kama pesa ya pamoja kwa ajili ya koloni zake za Kenya Uganda na Tanganyika Zanzibar ilijiunga na shilingi hii mwaka ilipoacha rupia zake Baada ya uhuru nchi hizi zilivunja umoja huu zikaanzisha pesa zao za pekee Zote zinaitwa shilingi lakini thamani ilianza kuwa tofauti haraka

Kuna majadiliano ya kurudisha shilingi ya pamoja kwa nchi za Afrika ya Mashariki

Pesa

Mlima Kilimanjaro unavyoonekana kutoka Moshi
Kilele cha Kibo kwenye mlima Kilimanjaro

Kilimanjaro ni mlima mrefu kuliko yote Afrika pia ni wa pili kwa urefu Duniani Mlima huu uko nchini Tanzania katika Mkoa wa Kilimanjaro Una urefu wa futi mita Hali halisi Kilimanjaro ni zaidi kuliko mlima tu ni kama safu ndogo ya milima mitatu Kibo Mawenzi na Shira Hii mitatu inaonekana kama vilele vitatu vya mlima mmoja hivyo si vibaya kusema Kilimanjaro ni mlima

Kilimanjaro ni volkeno iliyolala kwa sasa Kwenye kilele cha Kibo gesi bado inatoka Kumbukumbu ya wenyeji ina habari ya mlipuko takriban mnamo mwaka

Kilele cha juu cha Kibo kinaitwa Uhuru Peak Mtu wa kwanza wa kufika kileleni hapo alikuwa Johannes Kinyala Lauwo kutoka Marangu aliyewaongoza Wajerumani Hans Meyer na Ludwig Purtscheller tarehe Oktoba wakati wa ukoloni wa Ujerumani Wakati ule waliita ncha ya juu KaiserWilhelmSpitze kijerKilele cha Kaisari Wilhelm kwa heshima ya Kaisari wa Ujerumani

Kibo ina theluji na barafuto kadhaa ndogo

Milima ya Tanzania
Milima ya Afrika
Volkeno za Afrika

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa rais wa kwanza wa Tanzania Alizaliwa Butiama mkoani Mara pembezoni mwa Ziwa Nyanza tarehe Aprili Alifariki dunia Oktoba Aliiongoza Tanzania toka mwaka hadi mwaka

Yeye ni mwasisi wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea Kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa ni mwalimu Kazi hii ndiyo ilimpatia jina ambalo lilimkaa maisha yake yote la Mwalimu Mwalimu Nyerere ni kati ya viongozi wachache wa Afrika ambao wameacha madaraka kwa hiyari baada ya kutawala kwa muda mrefu Alipostaafu urais mwaka alirudi kijijini kwake Butiama ambako aliendesha shughuli za kilimo Aliendelea kuwa na athari kubwa katika siasa ya Tanzania hadi kifo chake

Julius Kambarage Nyerere alizaliwa mwaka katika kijiji cha Butiama wilaya ya Musoma mkoa wa Mara Tanzania wakati ule Tanganyika Alikuwa mojawapo kati watoto wa Nyerere Burito chifu wa kabila la Wazanaki Alipokuwa mtoto Nyerere alichunga mifugo ya babake katika umri wa miaka aliingia shule akitembea kilomita hadi Musoma Baada ya kumaliza shule ya msingi aliendelea kusoma shule ya wamisionari Wakatoliki huko Tabora Katika umri wa miaka alibatizwa akawa mkristo Mkatoliki hadi mwisho wa maisha yake

Mapadre wakaona akili yake wakamsaidia kusoma ualimu huko Makerere Kampala Uganda kuanzia Makerere akaanzisha tawi la Umoja wa wanafunzi Watanganyika pia amejihusisha na tawi la Tanganyika African Association TAA Baada ya kumaliza masomo ya ualimu alirudi Tabora akifundisha shule ya StMarys Mwaka alipata skolashipu ya kwenda kusoma kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh huko Uskoti Uingereza akasoma MA ya historia na uchumialikuwa mtanzania wa kwanza kusoma katika chuo kikuu cha Uingereza na mtanzania wa pili kupata shahada ya elimu ya juu nje ya Tanzania

Aliporejea Tanganyika kutoka masomoni Nyerere alifundisha Historia Kingereza na Kiswahili katika shule ya St Francis iliyo karibu na Dar es Salaam Mwaka alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African Association TAA chama ambacho alikisaidia kukijenga alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Makerere Mwaka alikibadilisha chama cha TAA kwenda katika chama cha Tanganyika African National Union TANU ambacho kilikuwa cha kisiasa zaidi kuliko TAA Ndani ya mwaka mmoja chama cha TANU kilikuwa tayari chama cha siasa kinachoongoza Tanganyika

Uwezo wa mwl Nyerere uliwashitua uongozi wa kikoloni na kumlazimisha Nyerere kuchagua kati ya siasa na kazi ya ualimu Nyerere alisikika akisema kuwa alikuwa mwalimu kwa kuchagua na mwanasiasa kwa bahati mbaya Alijiuzuru ualimu na kuzunguka nchini Tanganyika kuzungumza na watu wa kawaida na machifu ili kuleta muungano katika mapigano ya uhuru Pia alizungumza kwa niaba ya TANU katika Trusteeship council na Fourth committee ya Umoja wa Mataifa UN huko New York Uwezo wake wa kimaongezi na kuunganisha watu ulimwezesha kufanikisha Tanganyika kupata uhuru bila umwagaji wa damu Ushirikiano mzuri aliouonyesha aliyekuwa gavana wa wakati huo bwana Richard Turnbull ulisaidia pia kuharakisha upatikanaji wa uhuru Nyerere aliingia katika bunge la kikoloni mwaka na kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mwaka Mwaka Tanganyika ilipata uhuru wake na tarehe Nyerere alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika huru na mwaka mmoja baadae Nyerere alikuwa raisi wa kwanza wa jamhuri ya Tanganyika Nyerere alikuwa kiungo muhimu katika katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania baada ya mapinduzi ya Zanzibar mwaka yaliyomtoa madarakani sultani wa Zanzibar Jamshid bin Abdullah

Julius Nyerere mzee mnamo

aliongoza chama cha TANU katika tendo la kuungana na chama tawala cha Zanzibar ASP na kuanzisha chama kipya cha CCM Chama cha Mapinduzi akiwa mwenyekiti wake

Nyerere aliendelea kuongoza Taifa hadi alipomwachia nafasi raisi wa pili Ali Hassan Mwinyi Aliendelea kuongoza Chama cha CCM hadi na kuwa na athari kubwa katika siasa ya Tanzania hadi kifo chake Inasadikika kuwa Nyerere alishawishi uteuzi wa Benjamini WMkapa kama mgombea wa raisi wa mwaka na ambaye aliteuliwa kuwa raisi kwenye uchaguzi wa mwaka Nyerere alikaa muda mwingi kwake Butiama akilima shamba lake Pamoja na haya alianzisha taasisi yenye jina lake mwaka alionekana akiwa mpatanishi wa pande mbalimbali wa vita vya wenyewe kwa wenyewe huko Burundi Tar aliaga dunia katika hospitali ya St Thomas London baada ya kupambana na kansa ya damu

Makala hii bado inahitaji maelezo na utathmini zaidi kuhusu kazi ya Mwalimu Nyerere labda hivi
Nyerere akichanganya ardhi za Zanzibar na Tanganyika wakati wa muungano

kujenga umoja wa Taifa na utamaduni wa Kiafrika pamoja na lugha ya Kiswahili kushinda ubaguzi wa rangi kutetea usalama wa taifa katika vitani dhidi Idi Amin

Kutoa mchango kwa vyama vya ukombozi vya nchi za kusini ya Afrika kama Zimbabwe ZANU Afrika Kusini ANC na PAC Namibia SWAPO Angola MPLA na Msumbiji Frelimo

Siasa zake za ujamaa zilishindwa baada ya mwaka

Baada ya kuona kuwa uchumi wa Tanzania hautaweza kusimama kwa siasa za kijamaa na kutoweza kuvumilia kuendesha nchi kwa siasa ambazo yeye hakuwa muumini Nyerere kwa maamuzi yake mwenyewe aliamua kustaafu nafasi ya uraisi baada ya uchaguzi wa mwaka na kumwachia usukani kwa Ali Hassan Mwinyi aliyetawala kwa siasa za uchumi wa soko huria

Katika hali ya kukubali ukweli Nyerere alitamka katika tafrija ya kumwaga juu ya siasa yake kiuchumi Nimefeli Tukubali hivyo

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere MwlNyerere analaumiwa kwa siasa zake za kiujamaa kuwa zilichelewesha maendeleo ya kiuchumi wa Tanzania

Pia kuna makundi ya waislamu wanaomtuhumu kwa kuendesha kwa siri vita dhidi ya uislamu na upendeleo wa elimu na madaraka kwa wakristo

Nyerere akicheza bao kwake Butiama akitazamwa na mfuasi wake katika urais Ali Hassan Mwini mke wake Maria na kakaye chifu Burito

Bado anakumbukwa na watanzania hasa wa hali ya chini kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamuPia ataendelea kukumbukwa na waafrika kote barani hasa kwa mchango wake
mkubwa wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika

Ni mmoja wa viongozi wachache wanaokumbukwa kwa kutojilimbikizia mali pamoja na kutawala kwa miaka zaidi ya

Kaburi la Nyerere kijijini Butiama
Mwishoni mwa maisha yake Nyerere aliishi kama mkulima wa kawaida kijijini kwake Butiama Alipatwa na kansa ya damu leukemia na kufariki Uingereza wakati wa kutibiwa katika mji wa London tarehe Oktoba Alizikwa mahali pa kuzaliwa kwake kijiji cha Butiama

Freedom and SocialismMkusanyiko wa maandiko na hotuba

Freedom Development Uhuru Na Maendeleo

Ujamaa Essays on Socialism

Crusade for Liberation

Julius KaisariTafsiri ya mchezo wa William Shakespeare unaoitwa Julius Caesar

Taasisi ya Mwalimu Nyerere
Contemporary Africa Database People Nyerere

Mohamed Said Mwalimu in s Dar East African October

Waliozaliwa
Waliofariki
Wanasiasa wa Tanzania
N
N
N

Maziwa Makuu kutoka anga

Nchi za Maziwa Makuu ni nchi za Tanzania Rwanda Burundi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Kenya na Uganda Kati ya maziwa makubwa yaliyoko katika eneo hili ni Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyanza Vikitoria

Afrika

Fasihi ni sanaa inayotumia lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii husika Fasihi imegawanyika katika makundi makubwa mawili fasihi andishi na fasihi simulizi Fasihi simulizi ni fasihi iwasilishwayo kwa njia ya mdomo mazungumzo fasihi andishi ni fasihi iwasilishwayo kwa njia ya maandishi

Lugha



Picha ya njia mbalimbali katika sehemu ya Intaneti
Intaneti Internet pia mtandao ni mfumo wa kushirikiana kwa kompyuta unaowezesha kompyuta mbalimbali duniani kuwasiliana kati zao Kupitia mtandao huu watu huweza kutembelea tovuti mbalimbali kupiga gumzo na kuandikiana barua pepe

Ni ile mawasiliano ya tarakilishi pamoja na habari zinazotunzwa kwenye mashine na kupatikana kwa programu za kutafuta kama google au kwa kamusi kama wikipedia

Intaneti ni mfumo wa ulimwengu wa mitandao ya kompyuta inayotumia Itifaki inayokubalika ya intanet Suite TCP IP kutumikia mabilioni ya watumiaji duniani kote Ni mtandao wa mitandao ambayo ina mamilioni ya mitandao binafsi mitandao ya umma mitandao ya kielimu mitandao ya biashara na mitandao ya serikali zenye upana wa kimitaa na kiulimwengu ambazo zimeunganishwa na safu pana ya teknolijia za mtandao za elektroniki na za mwangaza Intanet hubeba safu kubwa ya huduma na rasilimali za habari hasa hati za HyperText zilizoshikanishwa za Mtandao wa ulimwengu nzima WWW na miundombinu ya kusaidia barua pepe

Mbinu nyingi za jadi za mawasiliano ya habari kama vile huduma za simu na televisheni zimeundwa upya kutumia teknolojia za intanet na kusababisha huduma kama vile itifaki ya kupitisha sauti kwa kutumia intanet VoIP na IPTV Uchapishaji magazeti umeundwa upya katika Tovuti ubadilishaji maoni na kupatiana habari zinapotokea Intanet imewezesha au kuharakisha uumbaji wa aina mpya za mwingiliano za kibinadamu kupitia ujumbe wa moja kwa moja jukwaa za Intanet na tovuti za kijamii

Asili ya mtandao ina mizizi katika mwongo wa wakati Marekani ilifadhili miradi ya utafiti wa wakala zake za kijeshi na kujenga mitandao iliyosambaa ya kompyuta ambazo zina uwezo wa kustahimili mabadiliko na ni vumilivu kwa makosa Kipindi hiki cha Utafiti na ufadhili wa raia wa Marekani wa uti mpya wa mgongo uliyofanywa na msingi wa kitaifa wa sayansi ulisababisha dunia yote kushiriki katika maendeleo ya teknolojia mpya na ukasababisha ufanyibiashara wa mtandao wa kimataifa katikati ya mwongo wa na kusababisha kujulikana kwa zana nyingi katika karibu kila nyanja ya maisha ya kisasa ya binadamu Kufikia mwaka wa wastani wa robo ya idadi ya watu duniani hutumia huduma ya Intanet

Intanet haina utawala wa kati katika utekelezaji wa kiteknolojia au sera ya upatikanaji na matumizi kila mtandao jumuishi unaweka masharti yake yenyewe Ufafanuzi tu wa jina mbili kuu katika Intanet Itifaki ya anwani za Intanet na mfumo wa makundi ya majina ndizo zinazongozwa na shirika iliyoagizwa ya Ushirika wa kupeana majina na nambari za intanetiICANN Msingi wa kiteknolojia na masharti ya itifaki misingi IPv na IPv ni shughuli ya kikundi maalum kilichoundwa kutekeleza kazi za uhandisi wa intanet IETF ambalo ni shirika la kimataifa lisilo la kutengeza faida ambalo washiriki wanaweza kuhusika nalo kwa kutoa mchango wa kitaalamu

Maneno intanet na matandao wa ulimwengu mzima mara nyingi hutumika katika hotuba za kila siku bila tofauti kubwa Hata hivyo Intanet na mtandao wa ulimwengu mzima si kitu kimoja na wala hazina maana sawa Internet ni mfumo wa kimataifa wa mawasiliano ya data Ni miundombinu ya vifaa na programu ambayo huwezesha mawasiliano kati ya kompyuta Kwa kulinganisha Mtandao ni mojawapo ya huduma inayowasilishwa na Intanet Ni mkusanyiko wa nyaraka zilizounganishwa na rasilimali zingine zilizoshikanishwa na viungo na URL Neno intanet wakati linapotumika kumaanisha intanet kiasili limekuwa likitumiwa kama nauni sahihi na kuanza na herufi kubwa Huu ni mwenendo kwa kuzingatia neno hili kama lenye matumizi ya aina nyingi au nauni ya kawaida na kwa hivyo liandikwe kama intanet bila kukianza na herufi kubwa mkuu


Uzinduzi wa Sputnik na USSR ulichochea Marekani kuanzisha shirika la utafiti wa juu wa miradi iliyojulikana kama ARPA katika mwezi wa Februari ili kuongoza kiteknolojia ARPA ilitengeneza afisi ya teknolijia za kuchambua habari IPTO ili kuendeleza utafiti wa programu inayojitekeleza ya mazingira ya chiniSage ambayo iliunganisha mifumo ya rada za nchi nzima pamoja kwa mara ya kwanza J C R Licklider alichaguliwa kuwa kiongozi wa IPTO Licklider alihama kutoka maabara ya masomo yanayochunguza jinsi ubongo wa binadamu unavyofasiri sauti katika Chuo Kikuu cha Harvard MIT mwaka wa baada ya kuvutiwa nateknolojia ya habari Akiwa MIT alikuwa kwenye kamati iliyoanzisha Maabara ya Lincoln na kufanya kazi ya mradi wa Sage Mwaka wa akawa Makamu wa Rais katika BBN ambapo alinunua kompyuta ya kwanza ya PDP na kuongoza maonyesho ya kwanza ya ugawanaji muda

Profesa Leonard Kleinrock pamoja na mmoja wa prosesa wa kwanza wa kionyesha ujumbe cha ARPANET huko UCLA
Wakati akiwa IPTO Licklider alimleta Lawrence Roberts ili aanzishe mradi wa kutengeneza mtandao na Roberts alikita msingi wa teknolojia katika kazi ya Paulo Baran ambaye alikuwa ameandika masomo kamili kwa Wanajeshi wa waangani wa Marekani akipendekeza ubadilishaji pakiti badala ya ubadilishaji mzunguko ili kupata mtandao bora unaobadilika na unaoweza stahimili janga Profesa wa UCLA Leonard Kleinrock alikuwa ametoa misingi wa nadharia ya pakiti za mitandao katika mwaka wa na baadaye katika mwaka wa wa upitishaji wa kiviwango dhana ambazo zimekuwa msingi wa maendeleo ya intanet ya leo

Baada ya kazi nyingi sehemu mbili za kwanza ambazo zingekuwa ARPANET ziliunganishwa kati ya Shule ya Uhandisi na Sayansi Tumizikizi ya UCLA na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti ya Stanford SRI katika bustani ya Menlo California tarehe Oktoba ARPANET ilikuwa moja ya mitandao tangulizi ya mtandao wa intanet ya leo Kufuatia maonyesho kuwa ubadilishaji pakiti ulifanya kazi kwa ARPANET kituo cha posta cha Uingereza Telenet TRANSPAC na DATAPAC zilishirikiana kuunda mtandao wa kwanza wa huduma ya ubadilishaji pakiti Nchini Uingereza hii ilikuwa inajulikana kama huduma ya kimataifa ya ubadilishaji pakiti IPSS mwaka wa Mkusanyiko wa mitandao yenye msingi wa X ilikua kutoka Ulaya na Marekani na kutanda Kanada Hong Kong na Australia kufikia mwaka wa Sheria ya ubadilishaji pakiti ya X ilitengenezwa katika CCITT sasa inaitwa ITUT takriban mwaka wa

X ilikuwa huru kutoka itifaki ya TCP IP ambayo iliinuka kutokana na kuwa kazi ya majaribio ya DARPA kwenye ARPANET mtandao wa Pakiti za Redio na Mtandao wa Pakiti ya Setilaiti wakati mmoja Vinton Cerf na Robert Kahn walitengeneza maelezo ya kwanza ya itifaki ya TCP mwaka wa na kuchapisha karatasi kuhusu mada hii katika mwezi wa Mei Matumizi ya neno Intanet kuelezea mtandao mmoja wa kiulimwengu wa TCP IP yalianza katika mwezi wa Desemba na uchapishaji wa RFC yakiwa maelezo kamili ya kwanza ya TCP iliyoandikwa na Vinton Cerf Yogen Dalal na Carl Sunshine waliokuwa katika Chuo Kikuu cha Stanford Katika miaka tisa iliyofuata kazi iliendelea kurekebisha itifaki hizo na kuzitekeleza katika mifumo ya oparesheni ya aina mbalimbali Mtandao wa Kwanza wenye upana mkubwa wa msingi wa TCP IP ulikuwa ukifanya kazi kufikia tarehe Januari wakati ambapo viwekaji vyote vya ARPANET vilibadilishwa kutoka itifaki za hapo awali za NCP Mwaka wa Wakfu wa Sayansi wa kitaifa Marekani NSF uliamuru ujenzi wa NSFNET uti wa mgongo wa mtandao wa chuo kikuu wenye kasi ya kilobiti kwa sekunde kwa kutumia kompyuta zilizoitwa fuzzballs na mvumbuzi wao David L Mills Mwaka uliofuata NSF ilifadhili ubadilishaji hadi mtandao wenye kasi ya juu zaidi ya megabiti kwa sekunde Maamuzi muhimu kutumia itifaki za DARPA TCP IP ulifanywa na Dennis Jennings aliyekuwa msimamizi wa programu ya kompyuta zenye nguvu huko NSF

Ufunguzi wa mtandao huo kwa maslahi ya kibiashara ulianza mwaka wa Baraza ya Mitandao ya Kimajimbo Marekani ilikubali ushikanishaji wa NSFNET na mfumo wa barua wa MCI katika mwaka huo kiungo kilifanywa katika msimu wa joto wa mwaka wa Huduma zingine za kielektroniki za kibiashara zilishikanishwa zikiwemo OnTyme Telemail na Compuserve Katika mwaka huo watoaji wa huduma ya Intanet watatu waliundwa UUNET PSINet na CERFNET Muhimu mitandao tofauti iliyotoa viingilio na baadaye kuungana na Intanet ilikuwa BITNET na Usenet Mitandao mingine ya kibiashara na elimu kama Telenet Tymnet Compuserve na JANET iliunganishwa na Intanet iliyokuwa ikikua Telenet iliyoitwa Sprintnet baadaye ulikuwa mtandao mkubwa wa kompyuta wa kitaifa uliofadhiliwa kibinafsi wenye upigaji simu ya intaneti bure katika miji kote Marekani na uliyokuwa ukifanya kazi tangu mwongo wa Hatimaye mtandao huu uliunganishwa na mingine katika mwongo wa wakati ambapo itifaki ya TCP IP iliendelea kuwa maarufu zaidi Uwezo wa TCP IP kufanya kazi kwa karibu mtandao wowote wa mawasiliano uliruhusu ukuaji rahisi ingawa ukuaji wa haraka wa Intanet ulikuwa juu ya upatikanaji rahisi wa safu ya vielekezi vya kibiashara kutoka makampuni mengi upatikanaji wa vifaa vya kibiashara vya Ethanet ya mitandao ya mitaa na kuenea kwa utekelezaji na uwekaji sheria mkali wa TCP IP katika UNIX na karibu kila mfumo mwingine wa oparesheni

Ingawa vifaa msingi na miongozo vinavyofanya uwezekanaji wa intanet vimekuwepo kwa karibu miongo miwili mtandao huo haukupata kuona nyuso za umma mpaka mwongo wa Tarehe Agosti CERN shirika ya Ulaya ya utafiti wa chembe ulieleza umma kuhusu mradi mpya wa matandao wa dunia nzima Mtandao ulizuliwa na mwanasayansi waKiingereza Tim BernersLee mwaka wa Kivinjari cha mtandao kilichokuwa cha kwanza na chenye umaarufu sana kilikuwa ViolaWWW iliyofuata mtindo wa HyperCard na kujengwa kwa kutumia mfumo wa X Window Hatimaye ilichujwa na umaarufu wa tovuti ya Mosaic Mwaka wa Kikao kikuu cha zana za kompyuta zenye nguvu katika Chuo Kikuu cha Illinois ilitoa aina ya kwanza ya Mosaic na mwisho wa mwaka wa hamu ya umma iliongezeka Intanet ambayo hapo awali ilikua ya taaluma na ufundi Kufikia mwaka wa matumizi ya neno Intanet ilikuwa kawaida na kwa hivyo hata matumizi yake kama neno yenye maana sawa na mtandao wa ulimwengu nzima

Wakati huo huo muongo huo ulipoendelea Intanet ilifanikiwa kushughulikia mitandao nyingi binafsi wa awali ingawa baadhi ya mitandao kama FidoNet vimebakia tofauti Katika miaka ya ilikuwa inakadiriwa kwamba Intanet ilikua kwa asilimia kila mwaka na kipindi kifupi cha mwaka wa na ambapo ukuaji wake ulilipuka Ukuaji huu ulitokana na ukosefu wa utawala kuu ambao unaruhusu ukuaji wa kikaboni wa mtandao na pia ukosaji ubinafsi na huru katika itifaki za Intanet ambao unahamasisha ubadilishaji wauzaji na kuzuia kampuni yoyote kuwa na udhibiti mkubwa wa mtandao Makadirio ya idadi ya watumiaji wa internet ni bilioni kufikai Juni

Ugumu wa miundombinu ya mawasiliano ya Intanet unahusisha vipengele vya vifaa vyake na sehemu za mfumo wa progamu inayodhibiti tabaka mbalimbali za usanifu Ingawa vifaa vinaweza kutumika kusaidia mifumo mingine ya programu ni urasimu na mifumo ya sheria za usanifu wa programu zinazoainisha Intanet na hutoa msingi wa ukubwa wake na mafanikio yake Wajibu wa urasimu wa usanifu wa mifumo ya programu za Intanet umepewa tume ya uhandis wa Intanet IETF IETF huongoza makundi ya kuweka sheria wazi kwa mtu yeyote kuhusu masuala mbalimbali ya usanifu wa Intanet Majadiliano yanayotokea na amri za mwisho huchapishwa katika mfululizo wa machapisho iitwayo Kuomba kwa Maoni RFCipatikanayo bure kwenye tovuti ya IETF Mbinu muhimu za utengenezaji wa mitandao zinazowezesha Intanet ziko katika RFC teule yenye sheria za Intanet

Sheria hizi hueleza msingi unaojulikana kama Itifaki ya Intanet Hii ni kielelezo cha usanifu unaogawanya huduma kuwa visehemu katika itifaki ya mfumoRFC RFC Visehemu hivi vina uhusiano na mazingira au upeo ambao huduma zao hufanya kazi Sehemu ya juu ni Sehemu ya zana nafasi iliyotengwa kwasababu ya mbinu za utenegnezaji mitandao zinazotumika katika zana za programu mfano kivinjari Chini ya sehemu hii ya juu kuna sehemu ya Usafiri iunganishayo zana katika kompyuta tofauti kupitia mtandao mfano clientserver na mbinu sahihi za kubadilishana takwimu Chini ya sehemu hizi ndipo kulipo na msingi wa teknolojia ya mitandao linalojumuisha sehemu mbili Sehemu ya Intanet inayowezesha kompyuta kutambuana kupitia anwani za Itifaki ya internetIP na huziwezesha kuungana pamoja kwa kutumia mitandao zilizo karibu Mwisho chini ya usanifu huu ni sehemu ya programu na sehemu ya uunganishaji ambayo huwezesha kuungana kwa kompyuta zilizo katika kiunganishi sawa wa mtandao ya mtaa kama vile mtandao wa eneoLAN au uunganishi wa kupiga Mfano huu ujulikanao pia kama TCP IP ni iliyoundwa isitegemee vifaa inavyotumia kwa hivyo mfano huu hauna haja ya kujishughulisha na maelezo yoyote Mifano mingine vimeundwa kama vile mfano wa mifumo ya kiunganishi kilichofunguka OSI lakini si sawa katika maelezo ya ufafanuzi wala utekelezaji lakini kufanana kupo n itifaki ya TCP IP hujumuishwa katika majadiliano ya mitandao ya OSI

Sehemu maarufu zaidi ya picha simamizi ya Intanet ni Itifaki ya Intanet IP ambayo hushughulikia upeanaji wa anwani za IP kwa kompyuta zilizo katika Intanet IP inawezesha ushikanishaji wa mitandao na kimsingi hujenga Intanet yenyewe Toleo ya ya IP IPv ni toleo lililotumiwa katika kizazi cha kwanza cha Intanet ya leo na bado yatumika vikubwa Iliundwa kushughulikia hadi watumiaji billioni wa intanet Hata hivyo kulipuka kwa ukuaji wa Intanet umesababisha kuisha kwa anwani za IPv ambayo inakadiriwa kuingia hatua yake ya mwisho katika takriban mwaka wa Toleo ya itifaki mpya IPv iliundwa katikati ya mwongo wa Toleo hili linauwezo mkubwa wa kupeana anwani na mbinu bora zaidi ya uelekezaji wa trafiki ya Intanet IPv kwa sasa ipo katika awamu ya kuachiliwa kibiashara duniani mashirika ya kuweka anwani za intanetRIR yameanza kuwahimiza mameneja wote wa rasilimali kupanga uchukuzi na uongofu wa haraka

IPv haishirikiani kikazi na IPv Kimsingi toleo la IPv hutengeneza toleo sambamba la Intanet ambalo halipatikani moja kwa moja na IPv Hii ina maanisha uboreshaji wa Programu au vifaa vya ukalimani ni muhimu kwa kila kifaa cha mtandao ambacho linahitaji kuwasiliana kupitia Intanet ya IPv Mifumo ya kuendesha kompyuta ya kompyta za kisasa tayari vimebadilishwa ili vifanye kazi na toleo zote za itifaki ya Intanet Miundombinu ya mtandao hata hivyo bado yamebaki nyuma katika maendeleo hayo Mbali na tata za viungo vinavyotengeneza miundombinu yake Intanet imewezeshwa na mikataba ya kibiashara mfano mkataba wa kujitakia na kwa ufundi maalum au itifaki zinazoeleza jinsi ya kubadilishana data kwa kupitia mtandao Hakika Intanet ina ainishwa na viungo vyake na sheria za uelekezaji

Muundo wa Intanet na sifa za matumizi yake vimekuwa vikisomwa kwa undani Imedhamiria kuwa muundo wa uelekezaji katika Intanet ya IP na viungo vya hypertext vya mtandao wa dunia nzima ni mifano ya mitandao isiyo na kipimo Sambamba na jinsi watoa huduma wa kibiashara za Intanet huwasiliana kwa kupitia sehemu za ubadilishanaji habari mitandao ya utafiti kwa kawaida huunganishwa kupitia mitandao mikubwa kama GEANT GLORIAD Internet halifa wa Mtandao wa Abilene na mtandao wa utafiti na kitaifa na elimu wa Uingereza JANET Mitandao hii imeundwa kutoka kwa mitandao mingine midogo pia tazama orodha ya mashirika ya kiakademia ya mitandao ya kompyuta

Wanasayansi wengi wa Kompyuta huelezea Intanet kama mfano halisi wa mfumo uliyo mkubwa wenye uhandisi wa hali ya juu lakini changamano zaidi Intanet ina tofauti nyingi mno kwa mfano kiwango cha kuhamisha data na sifa za kiumbo za uunganishaji vinatofautiana sana Intanet inaonyesha tukio ibuka linalotegemea muundo wake mkubwa Kwa mfano takwimu za viwango vya kuhamisha data vinaonyesha kufananakwa muda Kanuni za mbinu za uelekezaji na utoaji anwani kwa trafiki katika Intanet zinarejelea asili yake katika mwongo wa wakati ukubwa na umaarufu wa mtandao haukuweza kutarajiwa Kwa hivyo uwezekano wa kujenga miundo mbadalia unachunguzwa

Makao makuu ya ICANN huko Marina Del Rey California Marekani

Internet ni mtandao uliyosambaa duniani ulioundwa na mitandao mingi tofauti iliyoshikanishwa Hufanya kazi bila kitengo cha serikali kuu Hata hivyo ili kudumisha uwezo wa mifumo tofauti kufanya kazi pamoja nyanja zote za kifundi na sera ya msingi wa miundombinu na nafasi za jina kuu husimamiwa na Shirika la Intanet linalotoa majina na nambari ICANN lililo na makao makuu huko Marina del Rey California ICANN ndiyo yenye mamlaka ya kusitiri utaratibu wa utoaji wa vitambulisho vya kipekee kwa matumizi ya Intanet pamoja na majina ya vikundi anwani za Itifaki ya Intanet IP nambari ya vipenyezo katika itifaki ya usafiri na takwimu zingine nyingi Nafasi ya iliyounganishwa ya majina ya ulimwengu ambapo majina na nambari za kipekee hutolewa ni muhimu kwa mataifa katika kupata huduma za Intanet ICANN huongozwa na halmashauri ya wakurugenzi wa kimataifa wanaotolewa kutoka jamii za ufundi wa Intanet biashara elimu na mengine yasiyo ya kibiashara Serikali ya Marekani inaendelea kuwa na jukumu la msingi katika kuidhinisha mabadiliko katika shina la DNS lililoko katika kitovu cha mfumo wa eneo la majina Jukumu la ICANN katika kuratibu zoezi la utoaji vitambulisho vya kipekee hulitofautisha kama shirika la kipekee lenye madaraka ya kuratibu Intanet ya kimataifa Tarehe Novemba Mkutano wa Dunia juu ya Jamii ya Habari uliofanyika Tunis uliunda Fora ya Utawala wa Intanet IGF kujadili masuala yanayohusiana na Intanet

Intanet inaruhusu mabadiliko makubwa katika masaa na maeneo ya kufanyia kazi hasa kwa kuenea kwa viunganishi vya kasi visivyopimwa na zana za mtandao

Intanet kwa sasa yaweza kupatikana karibu popote kwa njia mbalimbali hasa kupitita vifaa vinavyobebwa mkononi Simu za mkononi kadi za data michezo ya video na vielekezaji vya mkononi vinaruhusu watumiaji kujiunganisha na intanet kutoka popote pale walipo na mtandao usiotumia waya unaoruhusu teknolojia ya kifaa hiki Ndani ya mipaka inayowekwa na skrini ndogo vifaa vingine pungufu kama vifaa vya mfukoni huduma za Intanet pamoja na barua pepe na mtandao huweza kupatikana Watoa huduma za Intanet huweza kuzuia huduma zinazotolewa na malipo ya usafirishaji wa data bila kutumia nyaya yaweza kuwa ya juu zaidi kuliko mbinu zingine za kupata intanet

Internet pia imekuwa soko kubwa kwa makampuni baadhi ya makampuni makubwa leo yamekua kwa kuchukua faida ya gharama nafuu ya matangazo na biasharakwa kupitia Intanet pia inajulikana kama biashara kupitia Intanetecommerce Ni njia ya haraka sana katika kueneza habari kwa idadi kubwa ya watu kwa ujumla Intanet pia imebadilisha ununuzikwa mfano mtu anaweza kuagiza CD kupitia intanet na kuipokea katika barua baada ya siku kadha au kuitoa kwa mtandao moja kwa moja katika baadhi ya kesi Intanet pia imewezesha uuzaji wa kibinafsi ambao unaruhusu kampuni kuuza bidhaa kwa mtu fulani au kundi maalum la watu zaidi ya njia zingine za matangazo Mifano ya uuzaji binafsi hujumuisha jamii zilizo katika Intanet kama vile MySpace Friendster Orkut Facebook na nyingine yznye maelfu ya watumizi wa Intanet ambao hujiunga kujitangaza wenyewe na kufanya urafiki kupitia Intanet Wengi wa watumiaji hawa ni vijana na waliobaleghe wenye kati ya miaka Kwa upande mwingine wakati wanapojitangaza wao wenyewe hao pia hutangaza maslahi na mazoea yao ambayo makampuni ya uuzaji katika Intanet yanaweza kutumia kama habari ili kujua kile ambacho watumiaji hawa watanunua kupitia Intanet na kutangaza bidhaa za makampuni kwa watumiaji hao

Gharama ya chini na ubadilishanaji wa haraka wa mawazo maarifa na ujuzi vimefanya kazi shirikishi kuwa rahisi sana kwa msaada wa programu shirikishi Makundi hayawezi tu kuwasiliana kwa bei ya chini bali upana wa Intanet unaruhusu makundi kama hayo kujiunda kwa urahisi Mfano wa makundi hayo ni harakati ya programu za bure ambazo zimetengeneza miongoni mwa programu nyingine Linux Mozilla Firefox na OpenOfficeorg Kuongea kupitia Intanet iwe katika fomu ya vyumba vya kuongea vya IRC au kupitia mfumo wa ujumbe wa moja kwa moja kunaruhusu mfanyikazi na wenzake kuwasiliana kwa njia rahisi sana wakati wanapofanya kazi katika kompyuta zao wakati wa mchana Ujumbe unaweza kubadilishwa kwa njia ya haraka na inayofaa zaidi kuliko barua pepe Maongezo katika mifumo hii huweza kuruhusu ubadilishanaji wa faili michoro ya ubao mweupe au mawasiliano ya sauti na video kati ya wanachama wa timu moja

Mifumo ya kudhibiti toleo unaruhusu timu zinazoshirikiana kufanya kazi kwa seti za hati zenye umiliki mmoja bila ajali ya kufuta kazi za timu nyingine au wanachama kusubiri hadi kupata hati zilizotumwa ili kuweza kutoa michango yao Biashara na timu za miradi zinaweza kushirikiana katika kalenda vilevile nyaraka na taarifa nyingine Ushirika kama huo hutokea katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na utafiti wa kisayansi maendeleo ya programu kupanga mikutano wanaharakati wa kisiasa na uandishi wa bunifu Ushirikiano wa kijamii na kisiasa pia unaenea wakati upatikanaji wa Intanet na idadi ya watu waliosoma kompyuta inapoongezeka Kutoka matukio ya makundi yanayoundwa haraka na watu mwanzo wa miaka ya na matumizi ya mitandao ya kijamii katika maandamano ya uchaguzi wa huko Iran Intanet inaruhusu watu kufanya kazi pamoja kwa ufanisi zaidi na kwa njia nyingi zaidi kuliko iwezekanavyo bila Intanet

Intanet inaruhusu watumiaji wa kompyuta kufikia kompyuta zingine na habari huhifadhiwa kwa urahisi popote walipo duniani Wanaweza kufanya hivi pamoja na au bila matumizi ya usalama kujitambulisha na teknolojia za kuficha kutegemea na mahitaji yao Hii inahimiza njia mpya ya kufanya kazi kutoka nyumbani kushirikiana na kubadilishana habari katika viwanda vingi Mhasibu aliyeketi nyumbani anaweza kukagua vitabu vya kampuni iliyo katika nchi nyingine kupitia kitumishi kilicho katika nchi nyingine ya tatu ambayo inahifadhiwa na wataalamu wa IT katika nchi ya nne Akaunti hizi zinaweza kuwa ziliundwa na waweka vitabu wafanyao kazi nyumbani katika maeneo mengine kwa kuzingatia habarie waliyopata kupitia barua pepe waliyotumiwa kutoka ofisi za duniani kote Baadhi ya mambo haya yalikuwa yanawezekana kabla ya kuenea kwa matumizi ya Intanet lakini gharama ya laini binafsi ya kukodisha ingefanya mamboo hayo yasiweze kufanyika Mfanyakazi wa ofisi akiwa mbali na dawati lake labda upande mwingine wa ulimwengu katika safari ya kibiahsara au likizo anaweza kufungua kikao katika kompyuta yake binafsi iliyoko ofisini mwake kwa kupitia mtandao binafsi wenye usalamaVPN kwa kupitia Intanet Hii inampa mfanyakazi upatikanaji kamili wa faili zake zote za kawaida na data pamoja na barua pepe na zana nyingine za matumizi wakati akiwa mbali na ofisi Dhana hii pia inajulikana na baadhi ya watu wa usalama wa mitandao kama mtandao binafsi wa kidhahania wenye ndoto za kutisha kwa sababu inapeleka mzunguko salama wa mtandao wa shirika ndani ya nyumba za wafanyakazi wa shirika hilo

Watu wengi hutumia maneno Intanet na mtandao wa dunia nzima au tu Web kama maneno yanayobadilishana lakini kama tulivyojadiliana awali maneno haya mawili si sawa Mtandao wa Dunia Nzima ni seti ya nyaraka za ulimwengu picha na rasilimali nyingine zinazotazamwa na kushikanishwa na kitafuta rasilimali sawa URL na viungo URL hizi huruhusu watumiaji kuvipatia anwani vijakazi vya mtandao na vifaa vingine vnavyohifadhi rasilimali hizi na kuvipata vinapohitajika kwa kutumia HyperText Transfer itifaki ya kupelekea hati HTTP HTTP ni itifaki ya kipekee ya mawasiliano inayotumika katika mtandao wa Intanet Huduma za mtandao huweza pia kutumia HTTP kuruhusu mifumo ya programu kuwasiliana ili kuweza kushiriki na kubadilishana mantiki ya biashara na data

Bidhaa za programu zinazoweza kupata rasilimali za Mtandao mara nyingi huitwa ajenti wa matumizi Katika matumizi ya kawaida tovuti za mtandao kama Internet Explorer Firefox Opera Apple Safari na Google Chrome huwaruhusu watumiaji kuvuka kutoka kurasa ya mtandao mmoja hadi nyingine kupitia viungo vya hyper Hati kwenye mtandao huweza kuwa na mchanganyiko wowote wa data ya kompyuta zikiwemo picha sauti maandishi video mchanganyiko wa picha na sauti na mambo yanayomhusisha mtumiaji wa Intanet kama michezo zana ofisi na maonyesho ya kisayansi Kupitia utafiti wa Intanet unaoendeshwa na maneno maalum kwa kutumia mitambo ya utafutaji kama Yahoo na Google watumiaji duniani kote huweza kupata habari nyingi kwa urahisi na moja kwa moja kutoka kwa Intanet Ikilinganishwa na kamusi elezi zilizochapishwa namaktaba za kawaida Mtandao wa Dunia Nzima umewezesha kusambaa ghafla kwa habari na data

Kwa kutumia mtandao pia ni rahisi kuliko awali kwa watu binafsi na mashirika kuchapisha mawazo na habari kwa watazamaji wengi wanaotarajiwa Kuchapisha kurasa ya mtandao kibadilishanaji maoni blogu au kujenga tovuti inahusisha gharama ndogo za awali na huleta kupatikana kwa huduma nyingi zisizo na gharama Kuchapisha na kudumisha idadi kubwa ya mitandao ya kitaalamu yenye kuvutia habari tofauti na ya moja kwa moja bado ni swala gumu na ghali hata hivyo Watu wengi na baadhi ya makampuni na vikundivitumizi hutumia mitandao ya ubadilishanaji maoni au blogu ambayo hutumika kama jarida zenye urahisi wakati wa kuongeza habari Baadhi ya mashirika ya kibiashara huwahimiza wafanyakazi kuwasilisha ushauri katika maeneo yao maalum katika matumaini ya kuwa wageni watafurahishwa na maarifa ya mtaalam na habari za bure na kuvutiwa kwa shirika hilo kama matokeo Mfano mmoja wa zoezi hili ni Microsoft ambayo watengenezaji bidhaa zake huchapisha mitandao ya ubadilishanaji binafsi katika blogu ili kuvutia umma kwa kazi zao Mikusanyo ya kurasa binafsi za mtandao zilizochapishwa na watoa huduma wakubwa hubakia maarufu na imeendelea kuwa ya kipekee Ingawa oparesheni kama vile Angelfire na GeoCities zimekuwepo tangu siku za mwanzo wa Tovuti oparesheni mpya kwa mfano Tovuti Facebook na MySpace kwa sasa vina wafuasi wengi Oparesheni hizi mara nyingi hujionyesha kama mtandao ya huduma za kijamii kuliko viwekaji vya kurasa za mtandao

Kuweka matangazo katika kurasa za tovuti pendwa huwa na faida biasharae biashara ya mtandaoecommerce au uuzaji wa bidhaa na huduma moja kwa moja kupitia tovuti inaendelea kukua Katika siku za mwanzo kurasa za mtandao kwa kawaida zilitengenezwa kama seti za faili za nakala kamilifu na zilizo peke za HTML zikihifadhiwa kwenye tovuti ya huduma Hivi karibuni tovuti hutengenezwa kwa kutumia kisimamizi cha yaliyomo au kifaa ororo cha wiki ambacho huwa na maudhui machache sana mwanzoni Wachangiaji wa mifumo hii ambao wanaweza kuwa wafanyakazi wanaolipwa wanachama wa klabu au shirika zingine au wanachama wa umma hujaza vihifadhidata na maudhui kutumia kurasa zilizoundwa kwa kusudi hilo ilhali wageni huangalia na kusoma yaliyomo katika ombo lake la mwisho la HTML Kuna uwezekano wa kuwa au kutokuwa na mifumo ya uhariri kibali na mifumo ya usalama iliyojengwa katika mchakato wa kuchukua maudhui mpya iliyoingizwa na kuifanya ipatikane na wageni wanaolengwa

Barua pepe ni huduma muhimu ya mawasiliano inayopatikana kwenye Intanet Dhana ya kutuma ujumbe wa kielektroniki wa maandishi kati ya wahusika kwa njia iliyosawa na kutuma barua au memo ilitangulia utengenezaji wa Intanet Leo inaweza kuwa muhimu kutofautisha kati ya Intanet na mifumo ya kindani ya barua pepe Barua pepe ya Intanet inaweza kusafiri na kuhifadhiwa kimaandishi katika mitandao mingine mingi na mashine zilizo nje ya udhibiti wa mtumaji na mpokeaji Kwa wakati huu kunauwezekano wa yaliyomo kusomwa na kubadilishwa na mhusika wa tatu ikiwa kuna mtu yeyote anayefikiri kuwa una umuhimu wa kutosha Mifumo ya barua za kindani ambapo habari haipaswi kamwe kutoka nje ya mtandao wa kampuni au shirika ni salama zaidi ingawa katika shirika lolote kutakuwa na wafanyikazi wa IT na wafanyakazi wengine ambao kazi yao inahusu ufuatiliaji na mara chache kufikia barua pepe za wafanyikazi wengine ambazo hawajatumiwa hao Picha nyaraka na faili nyingine zinaweza kutumwa kama viungo vya barua pepe Barua pepe zinaweza kutumwa kwa anwani nyingi za barua pepe

Telefoni ya intanet ni huduma nyingine la mawasiliano ya kawaida iliyowezekana kwa uundaji wa a Intanet VoIP husimamia itifaki ya kupitisha sauti kupitia Intanet ikirejelea itifaki msingi ya mawasiliano ya Intanet Wazo hili lilianza mwanzo wa mwongo wa na zana zilizofanana na simu za polisi za kompyuta binafsi Katika miaka ya hivi karibuni mifumo mingi ya VoIP imekuwa rahisi kutumia na kuwa na manufaa kama simu ya kawaida Faida ni kwamba Intanet inapobeba trafiki ya sauti VoIP inaweza kuwa bure au kuwa na gharama ndogo sana kuliko upigaji simu wa jadi hasa juu ya umbali mrefu na hasa kwa wale wenye viunganishi vinanvyowaka wakati wowote kama vile Cable au ADSL VoIP inapevuka na kujitokeza kama mshindani mbadalia wa huduma za simu za jadi Uwezo wa kubadilishana ujumbe kati ya watoa huduma mbalimbali imeboreshwa na uwezo wa kupiga au kupokea simu kutoka kwa simu ya jadi unapatikana Vibadilisha mtandao vya VoIP ambavyo ni rahisi na vya bei nafuu vinapatikana na vinaondoa haja ya kuwa na kompyuta binafsi

Ubora wa sauti unatofautiana kutoka wito moja hadi mwingine lakini mara nyingi ni sawa na huweza hata kuzidi ule wa simu za jadi Matatizo yaliyobakia kwa VoIP hujumuisha upigaji simu kwa nambari ya dharura na utumainikaji Hivi sasa watoa VoIP wachache hutoa huduma ya dharura lakini haipatikani na wote Simu za jadi huwezeshwa na nguvu za laini na hufanya kazi wakati stima zinapopotea VoIP haifanyi hivyo bila chanzo kingine cha nguvu kwa vifaa vya simu na vifaa vya upatikanaji wa Intanet VoIP pia imekuwa maarufu kwa zana za michezo kama njia ya mawasiliano kati ya wachezaji Wateja wa VoIP wanaojulikana katika michezo ni kama vile Ventrilo na Teamspeak Wii PlayStation na Xbox pia hutoa sifa za VoIP za kuongea kupitia mtandao

Kugawana faili ni mfano wa uhamishaji wa kiasi kikubwa cha data kupitia Intanet Faili ya kompyuta inaweza kutumwa kwa kutumia barua pepe kwa wateja waenzi na marafiki kama kiungo Inaweza kuwekwa kwenye tovuti au tumishi ya FTP kwa upakuaji rahisi na watu wengine Inaweza kuweka ndani ya eneo lenye wamiliki wengi au ndani ya tumishi ya faili kwa ajili ya matumizi ya haraka na washikadau Mzigo wa upakuaji mzito kwa watumiaji wengi unaweza kupunguzwa na matumizi ya vioo vya huduma au mitandao ya viwango aina moja Katika hali hizi zote upatikanaji wa faili unaweza kudhibitiwa na kujitambulisha kwa watumiaji usafiri wa faili katika ya Intanet unaweza kuborongwa kwa kupewa maana fiche na hongo ya pesa yaweza kutumiwa ili kuzipata faili Bei inaweza kulipwa kutoka eneo tofauti kwa njia isiyokuwa wazi kwa mfano kutoka kwa kadi ya denikrediti ambayo maelezo yake hupitishwa pia kwa kawaida hupewa maana fiche kabisa kupitia Intanet Asili na dhibitisho la faili iliyopokewa inaweza kuangaliwa kupitia saini za dijitali au kwa MD au aina nyingine ya ujumbe Sifa hizi rahisi za intanet juu ya msingi wa dunia nzima zinabadilisha uzalishaji mauzo na usambazaji wa kitu chochote ambacho kinaweza kupunguzwa na kuwa faili ya kompyuta kwa usafirishaji Hii ni pamoja na kila namna ya machapisho ya magazeti bidhaa za programu habari muziki filamu video picha grafiki na sanaa zingine Hili kwa upande mwingine limesababisha mabadiliko katika kila moja ya viwanda ambavyo awali vilidhibiti uzalishaji na usambazaji wa bidhaa hizi

Utabakishaji wa vyombo vya habari unahusu kitendo ambacho watangazaji wengi wa redio na televisheni wanatumia kukuza lishe ya Intanet ya habari za moja kwa moja kutumia sauti na tabaka za video kwa mfano BBC Wanaweza pia kuruhusu maonyesho na usikilizaji kulingana na mabadiliko ya wakati kama kuangalia mbele picha klasiki na sifa za kusikiliza tena Watoaji huduma hawa wameungwa na anuwai ya watangazaji halisi wa Intanet ambao kamwe hawakuwa na leseni za kutoa habari moja kwa moja Hii ina maanaisha kuwa kifaa kilichounganishwa na intanet kama vile kompyuta au kitu kingine maalum kinaweza kutumika kupata vyombo vya habari vilivyounganishwa na Intanet kwa njia ile ile kama ilivyowezekana tu na mpokezi wa televisheni au redio Aina ya matini ni pana sana kutoka kwa ponografia hadi tovuti za ufundi na utaaluma wa juu Podcasting ni aina fulani katika mada hii ambapo kwa kawaida ni sauti matini zinapakuliwa na kuchezwa tena kwenye kompyuta au kubadilishwa kwenye chombo cha habari kinachobebeka ili kisikilizwe matu anapotembea Hizi mbinu za kutumia vifaa rahisi vinaruhusu mtu yeyote aliye na udhibiti ufichaji au udhibiti wa leseni kutangaza picha muziki na video kote ulimwenguni

Kamera za mtandao zinaweza kuonekana kama ongezeko ya chini ya bajeti ya jambo hili Ingawa baadhi ya kamera za mtandao zinaweza kutoa video za kiima kizima picha huwa ndogo au hujiongeza pole pole Watumiaji wa intanet wanaweza kuangalia wanyama waliyozunguka kidimbwi cha maji huku Afrika meli katika kipisho cha Panama trafiki katika mzunguko wa barabara za mtaa au kufuatilia wanapoishi katika muda halisi Vyumba vya kuongea vya video na mikutano ya video pia ni maarufu matumizi mengi yakipatikana ya kamera kibinafsi za mtandao zilizo na au zisizo na sauti inayotamba pande zote mbili YouTube ilianzishwa tarehe Februari na sasa ni tovuti inayoongoza kwa maonyesho ya video za bure pamoja na idadi kubwa ya watumiaji Inatumia mtandao wenye msingi wa kichezaji cha flashi kuonyesha faili za video Watumiaji waliojiandikisha huweza kuongeza idadi isiyo na kipimo ya video na kutengeneza vitambulishi vyao binafsi YouTube inadai kuwa watumiaji wake hutazama mamia ya mamilioni na huongeza mamia ya maelfu ya video kila siku

Lugha ya iliyoenea katika mawasiliano ya Intanet ni Kiingereza Hii inayotumika zaidi katika intaneti ni Kiingereza Hili latokana na kuwa ndiyo lugha asilia ya intanet na pia nafasi yake kama lingufranca lugha sambazi Pia inaweza kuhusiana na upungufu wa utendaji wa kompyuta za awali kiasi kikubwa zikitoka Marekani kushughulikia maandishi mengine kuliko yale ya lahaja ya Kiingereza ya alfabeti ya Kilatin Baada ya Kiingereza asilimia ya wageni wa Tovuti lugha zilizohitajika zaidi katika Tovuti ya Dunia Nzima ni Kichina asilimia Kihispania asilimia Kijapani asilimia Kifaransa asilimia Kireno na Kijerumani kila moja asilimia Kiarabu asilimia na Kirusi na Kikorea kila moja asilimia Katika kanda asilimia ya watumiaji wa intaneti duniani wana makao Barahindi asilimia Ulaya asilimia Amerika ya Kaskazini asilimia Amerika Kusini na Caribbean zikichukuliwa kwa pamoja asilimia Afrika asilimia Mashariki ya Kati na asilimia Australia Oceania Teknolojia za Intanet zimeendelea ya kutosha katika miaka ya hivi karibuni hasa katika matumizi ya Unicode kwamba vifaa vizuri vinapatikana kwa maendeleo na mawasiliano katika lugha zinazotumiwa kwa wingi Hata hivyo baadhi ya matatizo kama mojibake uonyeshaji usiosahihi wa maandishi ya lugha za kigeni pia inajulikana kama kryakozyabry bado hubakia

Njia za kawaida za kupata Intaneti nyumbani ni kwa kupiga laini za broadband kupitia waya za koax nyuzinyuzi za optiki au waya za shaba WiFi setilaiti na teknolojia ya rununu yaG Maeneo ya umma kwa matumizi ya Intaneti ni maktaba na mikahawa ya Intaneti ambamo kompyuta zilizounganishwa na Intaneti hupatikana Pia kuna sehemu za kupata Intaneti katika maeneo mengi ya umma kama vile kumbi za uwanja wa ndege na maduka ya kahawa katika baadhi ya sehemu hizi kwa matumizi mafupi wakati umesimama Maneno mbalimbali hutumiwa kama vile kiosk za umma za interneti pahala pa upatikanaji intaneti pa umma na simu za kulipia za Mtandao Hoteli nyingi sasa pia huwa na pahala pa umma ingawa hizi hulipiwa kulingana na matumizi
Sehemu hizi hutumika kwa matumizi mbalimbali kama ununuzi tiketi amana za benki malipo kupitia mtandao nk WiFi hutoa upatikanaji usiotumia waya wa mitandao ya kompyuta na kwa hiyo yaweza kufanya hivyo kwa Intanet yenyewe Sehemu moto zinazotoa upatikanaji kama huo hujumuisha mikahawa ya WiFi ambapo watumiaji hupaswa kuleta vifaa vyao visivyotumia waya kufikia Intaneti kama vile Kompyuta za pajani au PDA Huduma hizi huweza kuwa bure kwa wote bure kwa wateja tu au waliolipishwa Eneo moto halina haja ya kuwa finyu katika eneo ndogo Kampasi nzima au bustani au hata mji mzima unaweza kuwezeshwa Juhudi za mashinani zimesababishamitandao ya kijamii isiyotumia waya Huduma za WiFi za kibiahsara zinazofunika maeneo ya miji mikubwa zinapatikana London Vienna Toronto San Francisco Philadelphia Chicago na Pittsburgh Intanet huweza kupatikana kutoka sehemu hizo kama kiti cha bustani Mbali na WiFi kumekuwa na majaribio na mitandao ya simu ya kibiashara isiyotumia waya kama Ricochet huduma mbalimbali za kasi za data kupitia mitandao ya simu za mkononi na huduma zisizotumia waya zisizobadilika Simu za mkononi za hali ya juu kama vile smartphone kwa ujumla huja na upatikanaji wa Intaneti kwa kupitia mtandao wa simu Vivinjari cha mitandao kama vile Opera hupatikana katika simu hizi za mkononi zilizoendelea ambazo pia huweza kutekeleza aina nyingie tofauti ya programu za Intaneti Simu nyingi za mkononi huweza kupata Intanet kuliko PC ingawa hii haitumiki kwa upana Kinachotoa huduma za upatikanaji wa Intaneti na muundo wa mfanyiko wa itifaki hutofautisha mbinu zinazotumika kupata Intaneti

Intanet imefanya kuwe na uwezekano mkubwa kabisa wa aina mpya za mahusiano ya kijamii shughuli na upangaji kutokana na sifa zake msingi kama vile kuenea katika matumizi na upatikanaji Tovuti za kijamii kama vile Facebook na MySpace vimetengeneza aina mpya ya ufahamianaji na mwingiliano Watumiaji wa tovuti hizi huweza kuongeza vitu mbalimbali kwa kurasa zao binafsi kuonyesha maslahi yao ya kawaida na kuungana na watu wengine Inawezekana kupata mzunguko mkubwa wa marafiki hasa kama tovuti inaruhusu watumiaji kutumia majina yao halisi na kuruhusu mawasiliano kati ya makundi makubwa ya watu waliomo Tovuti kama meetupcom zipo ili kuruhusu matangazo mapana ya makundi ambayo yanaweza kuwepo hasa kwa mikutano ya anakwaana lakini ambayo inaweza kuwa na mahusiano mbalimbali madogo katika tovuti ya kundi lao katika meetuporg au tovuti zingine zenye kufanana

Kizazi cha kwanza kwa sasa kinakuzwa na upatikanaji ulioenea wa kujiunga na Intaneti unaosababisha utovu wa faragha utambulisho na wasiwasi wa kimiliki Wenyeji wa dijitali hukumbwa na wasiwasi tofauti ambao haukuwa na vizazi vya mwanzoni

Katika jamii za kidemokrasia mtandao umepata uhusiano mpya kama chombo cha kisiasa kupelekea udhibiti wa Intaneti na baadhi ya nchi Kampeni ya urais wa Howard Dean mwaka huko Marekani ulikuwa mashuhuri kwa uwezo wake wa kutoa michango kupitia Intaneti Makundi mengi ya kisiasa hutumia interneti ili kufanikisha utaratibu mpya wa kujiandaa ili kutimiza wanaharakati wa Intaneti Baadhi ya serikali kama zile za Iran Korea ya Kaskazini Myanmar Jamhuri ya Watu wa China na Saudi Arabia zinaudhibiti wa juu wa yale watu katika nchi zao wanayoweza kupata kwenye Intanet hasa maudhui ya kisiasa na kidini Hii inakamilishwa kwa kupitia programu inayoficha makundi na maudhui ili yasipatikane kwa urahisi bila mbinu ya kitaaluma zaidi

Nchini Norway Denmark Finland na Uswidi watoa huduma za Intaneti kwa hiari yaopengine kuepuka mpangilio kama huo kuwa sheria walikubali kudhibiti upatikanaji wa tovuti zilizotajwa na polisi Ingawa orodha hii ya URL haramu inapaswa kuwa na anwani za tovuti zinazojulikana zenye kuonyesha ponografia ya watoto yaliyomo katika orodha hii ni siri Nchi nyingi ikiwemo Marekani zimepitisha sheria zinazofanya umiliki au usambazaji wa nyenzo fulani kama vile ponografia ya watoto iliyoharamu lakini hazitumii programu ya kuficha Kuna programu nyingi za bure na zinazouzwa ziitwayo programu za udhibiti wa maudhui na ambazo mtumiaji anaweza kuchagua kuzuia tovuti zinazokera katika kompyuta binafsi au mitandao kama kuzuia uwezekano wa mtoto kupata habari za kimapenzi au vurugu

Interneti imekuwa chanzo kikuu cha burudani tangu kabla ya mtandao wa dunia nzima kukiwa na majaribio ya kijamii yanayofurahisha kama vile MUD na MOOyaliyofanywa katika vitoa nhuduma vya vyuo vikuu ambapo makundi ya Usenetya vichekesho yalipokea kiasi kikubwa cha trafiki kuu Leo majukwaa mengi ya Intaneti yana sehemu ya michezo na video za kuchekesha katunivibonzo fupi katika mfano wa sinema za flashi pia ni maarufu Zaidi ya watu milioni hutumia vibadilishanaji maoni blogu au mbao za ujumbe kama njia ya mawasiliano na kwa ajili ya kubadilishana mawazo Viwanda vya sinema za watu wazima na kamari vimechukua faida kamili ya mtandao wa dunia nzima na mara nyingi hutoa chanzo muhimu ya mapato ya matangazo kwa tovuti zingine Ingawa serikali nyingi zimejaribu kuweka vikwazo katika matumizi ya Intaneti katika viwanda hivi zilishindwa kupunguza kuenea umaarufu wa viwanda hivi

Eneo moja kuu ya burudani kwenye interneti ni Michezo yenye wahusika wengi Aina hii ya burudani inajenga jamii kuwaleta watu wa umri fofauti na asili zote kufurahia mwendo wa kasi wa ulimwengu wa michezo ya wahusika wengi Hii inaanza kutoka MMORPG hadi mfyatua risasi wa kwanza kutoka michezo ya kusawiri mhusika hadi kamari ya Intaneti Hii imebadilisha njia ambayo watu wengi huweza kuingiliana na jinsi wao wanvyoweza kutumia muda wao wa bure katika Interneti Wakati michezo ya Intaneti imekuwapo tangu mwongo wa aina ya kisasa ya michezo ya Intaneti ilianza na huduma kama GameSpy na MPlayer ambayo wachezaji wa michezo kwa kawaida walijiunga nayo Wasiyojiunga walikubaliwa kucheza baadhi ya aina za mchezo iliyochezwa au baadhi ya michezo Wengi hutumia Intaneti kwa kupata na kuchukua muziki sinema na vitu vingine kwa starehe zao na utulivu Kama ilivyojadiliwa hapo awali kuna vyanzo za kulipia na vya bure kwa haya yote kwa kutumia vitoa huduma vikuu na teknolojia za viwango vinavyolingana Baadhi ya vyanzo hivi hujali zaidi haki za wasanii wa awali na juu ya sheria za kimiliki kuliko wengine

Wengi hutumia mtandao wa dunia nzima kupata habari taarifa za michezo na hali ya hewa na kupanga likizo na kujua zaidi kuhusu mawazo na maslahi yao Watu hutumia maongezi kupitia mtandao utumaji wa ujumbe na barua pepe kuwasiliana na marafiki duniani kote wakati mwingine kwa njia sawa na jinsi baadhi ya watu awali walivyokuwa na marafiki ambao walifahamiana kwa barua tu Mitandao ya kijamii kama MySpace Facebook na mingine mingi kama hiyo pia huwasaidia watu kubaki katika mawasiliana kwa starehe zao Intaneti imeshuhudia kuongezeka kwa idadi ya kopyuta binafsi za mtandao ambapo watumiaji wanaweza kupata faili zao folda na masharti kupitia Intaneti Matumizi ya Intaneti yamesababisha upungufu mkubwa kwenye rasilimali ya kampuni mfanyikazi wastani wa Uingereza hutumia dakika kwa siku akipitia mtandao wa dunia nzima wakati akifanyakazi kulingana na utafiti wa mwaka wa uliofanywa na Huduma za Kibiahsara za Peninsula

Blogu
Wiki
Tovuti
Web Design
Haki za dijitali
Uchapishaji wa kielektroniki
Uhuru wa habari
Uendelezi wa habari
Mapendeleo ya Intaneti
Demokrasia ya Intanet
Web Design
Intaneti Meme
Mashirika ya Intaneti
Faragha ya Intaneti
Orodha ya watoa huduma za kebo za Intaneti
Orodha ya mada za Intaneti
Inteneti isiyotegema mrengo mmoja
Muhtasari wa Intanet

Bibliography
Media Freedom internet Cookbook ulioandikwa na Mwakilishi wa OSCE kuhusu uhuru wa vyombo vya habari huko Vienna mwaka wa
Living Internet historia na habari inayohusiana na Intaneti pamoja na habari kutoka waundaji wengi wa Intaneti
First Monday Jarida lililochunguzwa na wasomi wa kiwango kimoja katika Intaneti
How Much Does The Internet WEIGH ulioandikwa na Stephen CASS Discover
Rehmeyer Julie J Mapping a medusa Intaneti inasambaza mizizi yake Science News Juni Inapatikana
Castells M Rise of the Network Society vols Vol Cambridge MA Wachapishaji wa Blackwell
Castells M Lessons from the History of Internet in The Internet Galaxy Ch ukurasa Uchapishaji wa Chuo Kikuu cha Oxford
RFC Requirements for Internet HostsCommunication Layers IETF R Braden Ed Oktoba
RFC Requirements for Internet HostsApplication and Support IETF R Braden Ed Oktoba

Orodha ya maneno ya tarakishi ya mradi wa Kilinux kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Kiingereza
Intanet Wakfu wa sayansi wa Kitaifa
Miaka iliyobadilisha dunia Wired anaangalia nyuma mageuzi katika Intanet kwa miaka iliyopita
Makao ya Intanet na jamii ya Berkman yaliyo Harvard
Hifadhi za Dijital za CDCUzushi wa umri wa Intanet
Jinsi Intanet ilikuja kuwa jinsi ilivyo
Kurasa ya nyumbani ya tovuti la Shirika la Intanet
RFC Upangaji wa ubadilishanaji katika TCPIP
Kutayarisha masuala ya dijital ya usoni ya Ulaya i Upitiaji tena wa kati ya muhula
Manjoo Farhad The Unrecognizable internet of Slate

Intaneti
Vyombo vya habari
Mawasiliano ya simu
Uvumbuzi vya Marekani
Mapinduzi ya kisayansi

Blogu ni teknolojia mpya inayowezesha watu binafsi kuchapa maoni na fikra zao katika mtandao wa tarakilishi Blogu inaweza kuchukuliwa kama ni shajara pepe Neno blogu ni tafsiri ya Kiswahili inayotokana na neno la kiingereza blog Neno blog limetokana na neno jingine weblog Kimsingi blogu ni aina ya tovuti ambayo huandikwa mara kwa mara na kwa mpangilio wa mambo mapya kutokea ukurasa wa mbele kuendana na tarehe na mwezi

Zipo blogu za aina mbalimbali Kwa mfano blogu za maandishi blogu za mkononi blogu za picha blogu za sauti na blogu za video

Blogu ya mradi wa Global Voices inaandika muhtasari wa majadiliano na habari zinazojitokeza katika blogu mbalimbali duniani hasa nje ya Marekani Mradi huu una wanablogu katika nchi mbalimbali duniani ambao wanaandika juu ya masuala muhimu yanayojitokeza katika blogu za nchini mwao au katika bara lao

Kikusanya Habari cha blogu za Afrika
Kikusanya Habari cha blogu za Afrika
Kikusanya Habari cha blogu za Afrika Kusini
Kikusanya Habari cha blogu za Nigeria
Kikusanya Habari cha blogu za Nigeria
Blogu za Kiswahili
Blogu za Watanzania
Blogu za Wakenya
Kikusanya habari cha blogu za KenyaUnlimited
Blogu za Wanawake Wanablogu wa Afrika
Kikusanya habari cha Blogu za Wanawake Wanablogu wa Afrika
Kikusanya Habari cha blogu za Kenya
Mradi wa Global Voices
Masomo kwa wanablogu wapya
Azimio la Dodoma
Jumuiya ya Wanablogu Tanzania

myBlogspotTemplates
MyXMLTemplates

SummerTemplates
Autumn Templates
WinterTemplates

ChristmasTemplates

Teknolojia
Blogu
Uandishi wa Raia

Jua
Jua ni nyota ambayo ni karibu yetu zaidi kuliko nyota nyingine Inazungukwa na sayari tisa Dunia yetu ni sehemu ya mfumo wa jua na sayari zake

Kutokana na myeyungano wa kinyuklia ndani yake jua hutoa nishati ambayo ni muhimu kwa maisha ya mimea na viumbe hai katika dunia Nishati hii inapatikana kama mwanga joto na aina mbalimbali za mnururisho

Mada yake ni katika hali ya utegili yaani kama gesi ya joto sana

astronomia
Nyota
Gimba la angani

Abedi Amani Karume
Sheikh Abeid Amani Karume alikuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar Alizaliwa mwaka na kufariki tarehe Aprili kwa kupigwa risasi

Karume aliongoza mapinduzi yaliyomwangusha Sultani aliyekuwa akitawala Zanzibar hapo mwaka Baada ya miezi mitatu Zanzibar iliungana na Tanganyika iliyokuwa ikiongozwa na Mwalimu Nyerere Baada ya muungano wa nchi hizi mbili uliozaa jina la Tanzania Karume alikuwa makamu wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Amani Abeid Karume ambaye ni mtoto wa Sheikh Karume ndiye rais wa sasa wa Zanzibar tangu mwaka

Waliozaliwa
Waliofariki
Wanasiasa wa Tanzania

px
Nelson Mandela

Nelson Rolihlahla Mandela alizaliwa tarehe Julai mwaka Ni rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini Afrika Kusini Alikuwa mwanasheria na mwanachama wa ANC aliyepinga siasa ya Apartheid katika Afrika Kusini Mandela alitumikia kifungo cha maisha kwa miaka kutokana na harakati zake za kuupinga ubaguzi wa rangi Alifungwa katika kisiwa cha Robben Baada ya kuachiliwa huru mwaka alianzisha sera ya maridhiano Mwaka wa pamoja na Frederik Willem de Klerk alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani

Waliozaliwa
Marais wa Afrika Kusini
Viongozi wa Afrika
Tuzo ya Nobel ya Amani

Mlima Kenya

Mlima Kenya ndio mlima mrefu kuliko yote nchini Kenya Mlima huu ambao hasa wenyeji waliuita Kirinyaga una urefu wa mita Mlima huu unatokana na volkeno iliyozimika ikikadiriwa ya kwamba mlipuko wake wa mwisho ulitokea mnamo miaka milioni hadi iliyopita

Vilele vyake vya juu vinaitwa Batian m Nelion m na Lenana m Kuna barafuto nane mlimani lakini zinapungua kila mwaka kutokana na kupanda kwa halijoto duniani na kupungukiwa kwa usimbishaji kwa sababu ya kukatwa kwa miti mingi

Milima ya Kenya
Milima ya Afrika
Volkeno za Afrika

Rosa Parks wakati alipokamatwa kwa kosa la kutomwachia kiti chake Mwamerika Mzungu

Rosa Louise McCauley Parks Februari Oktoba anakumbukwa kwa uamuzi wake wa kukataa kumpisha kiti Mmarekani mweupe kama alivyodaiwa na dereva wa basi Uamuzi wake huo hapo mwaka ulipelekea mzozo uliosababisha Mgomo wa Mabasi wa Montgomery na kuchangia katika Vuguvugu la Haki za Kiraia Marekani Baada ya kitendo chake cha kukataa kumpa mtu mweupe kiti ndani ya basi na Mgomo wa Montgomery uliodumu kwa mwaka Mahakama ya Marekani ilitamka kuwa sheria za ubaguzi ndani ya mabasi huko Alabama na Montgomery zilikiuka katiba

Makumbusho na Maktaba ya Rosa Parks
Taasisi ya Maendeleo Binafsi ya Rosa Raymond Parks
Picha na mahojian ya Rosa Parks

Waliozaliwa
Waliofariki
Watu wa Marekani

Kwame Nkrumah pamoja na Martin Luther King

Kwame Nkrumah alikuwa Rais wa kwanza wa Ghana Alizaliwa Septemba na kufariki Aprili Nkrumah alikuwa ni mmoja wa viongozi waliokuwa na nia ya kujenga Muungano wa Afrika na mchochezi wa falsafa ya umajinuni

Waliozaliwa
Waliofariki
Viongozi wa Afrika
Marais wa Ghana

kaskazini na magharibi mwa Ghana ya kisasa na ilitawala majimbo katika eneo la Mto Sngal na mashariki kuelekea Mito ya Niger katika maeneo ya sasa ya Senegal Mauritania na Mali Ghana lilichaguliwa kuwa jina rasmi la nchi ya Gold Coast nchi hii iliponyakua uhuru mnamo tarehe Machi hata hivyo Ghana haikuweza kutangaza uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza hadi tarehe Julai ambapo pia nchi ilianza kujulikana kama Jamhuri ya Ghana

Kuna ushahidi kutoka kwa maarifa ya mambo ya kale ambao unaonyesha kwamba watu wameishi katika eneo linalojulikana siku hizi kama Ghana kutoka karibu miaka ya Kabla ya KristoBC Licha ya hayo hakuna ushahidi wa kuonyesha kuwa wakazi hao wana uhusiano na wale wa eneo hili kwa sasa Kwa mujibu wa mapokezi simulizi mengi ya makabila ya Ghana leo kama vile watu wa chimbuko la makabila kadhaa kama Waakan Waga na Waewe walifika Ghana mnamo karne ya AD

Mengi ya maeneo ya Ghana yanajumuisha eneo lililokuwa la Himaya ya Ashanti mojawapo ya falme zilizokuwa na ushawishi mkubwa katika eneo la Afrika Kusini mwa Sahara kabla ya enzi za ukoloni Wahamiaji Waakan walihama kuelekea kusini na kuanzisha mataifa kadhaa likiwemo lile la kwanza la himaya kuu ya Akan ya Wabono ambayo kwa sasa inajulikana kama eneo la Brong Ahafo nchini Ghana Sehemu kubwa ya eneo la sasa la kusini na kati mwa Ghana ilikuwa imeungana chini ya Himaya ya Ashanti ya Waashanti tawi la Waakan wa karne ya

Sherehe ya Waashanti ya viazi vikuu karne ya kwa mujibu wa Thomas E Bowdich
Cape Coast Castle
Kasri la Elmina
Utawala wa Waashanti ilihudumu mwanzoni kama mtandao mlegevu kabla ya kuwa ufalme ulioungana huku ukiwa na urasimu ulioendelea na wenye uchanganuzi mkubwa uliokuwa na makao yake Kumasi Inasemekana kuwa katika kilele chake Waasantehene wangeweza kutuma askari vitani na kuwa walikuwa na ushawishi wa kijeshi wa kiwango fulani juu ya majirani wake wote Thuluthi moja ya Waashanti wote walikuwa watumwa Waga walianzisha muungano wenye ufanisi mnamo na Wagonja Wadagomba na Wamamprusi pia walipigania uwezo wa kisiasa katika miaka ya Baada ya Waholanzi kuondoka mnamo mwaka wa Uingereza iliiweka Gold Coast chini ya himaya yake Kufuatia ushindi wa Uingereza mnamo mwaka wa hadi unyakuzi wa uhuru mnamo Machi eneo la Ghana ya sasa ghairi ya sehemu ya Volta Region British Togoland lilikuwa likijulikana kama Gold Coast

Vita vingi vilitokea baina ya utawala wa kikoloni na baadhi ya mataifa ya eneo hilo vikiwemo Vita vya vya AshantiFante na mapambano ya kudumu ya Waashanti dhidi ya Waingereza ambayo yalikoma baada ya Vita vya Tatu baina ya Waashanti na Waingereza the third AshantiBritish War Hata chini ya utawala wa kikoloni machifu na watu walipinga mara kwa mara sera za Waingereza hata hivyo ushawishi wa kupinga ukoloni ulikolea baada ya Vita vya Pili vya Dunia Mnamo mwaka wa chama kipya cha United Gold Coast Convention UGCC kilitoa wito wa utawala wa kujitegemea katika wakati mfupi zaidi iwezekanavyo Baada ya kuongezeka kwa maandamano mnamo wanachama wa chama cha United Gold Coast Convention walikamatwa akiwemo Waziri Mkuu na Rais wa baadaye Kwame Nkrumah Baadaye Nkrumah aliunda chama chake mwenyewe the Convention Peoples Party CPP ambacho kiliongozwa na usemi serikali ya kujitegemea sasa self government now Alianzisha kampeni ya Vitendo Chanya na kupata ufuasi wa watu wa sehemu za mashambani na wa daraja la wafanyakazi

Huku ikiundwa kutoka kwa muungano wa maeneo ya Gold Coast na British Togoland kufuatia matokeo ya maono ya watu yaliyodhaminiwa na Umoja wa Mataifa mnamo Ghana ilikuwa nchi ya kwanza ya Afrika Kusini mwa Sahara kunyakua uhuru mnamo

Kwame Nkrumah Waziri Mkuu wa kwanza na baadaye Rais wa nchi ya sasa ya Ghana hakuwa tu kiongozi wa Kiafrika wa kupigana dhidi ya ukoloni ila alikuwa pia mtu aliyekuwa na ndoto ya muungano wa Afrika ambayo haingejipata katika ukoloni mamboleo Alikuwa kiongozi wa serikali wa kwanza Afrika kukuza Muungano wa Waafrika PanAfricanism wazo ambalo alilipata wakati wa masomo yake katika Chuo Kikuu Cha Lincoln lililo Pennsylvania Marekani wakati ambapo Marcus Garvey alikuwa anapata umaarufu kwa harakati zake za Back to Africa Movement Aliunganisha ndoto za Macus Garvey na zile za mwanachuo mashuhuri Mmarekani Mweusi WEB Du Bois ili kuandaa Ghana kisasa Kanuni za Ghana za uhuru na haki usawa na elimu ya bure kwa wote bila kujali kabila dini au mila zinatokana na utekelezaji wa wazo la PanAfricanism

Ingawa lengo lake la muungano wa Afrika halikuwahi kuafikiwa Osagyefo Dr Kwame Nkrumah kama ajulikanavyo sasa alishiriki kwa kiwango kikubwa katika kuzinduliwa kwa Shirika la Umoja wa Afrika ambalo lilifuatwa mnamo na Umoja wa Afrika African Union Kwa bahati mbaya ingawa Nkrumah aliheshimika sana ngambo hakuwa akipendwa katika maswala ya ndani ya nchi Hakufeli tu kuanzisha uchumi wa viwanda ila hata sera zake hukusu uchumi ziliishia kuifanya nchi ya Ghana kuwa maskini kuliko ilivyokuwa wakati wa ilipopata uhuru Mafanikio yake yalikuwa kutambuliwa na raia wa Ghana wakati wa maadhimisho ya kuzaliwa Centenary wake na siku aliliweka kama likizo umma nchini Ghana

Hatimaye Nkrumah aliondolewa mamlakani na jeshi alipokuwa ngambo mnamo Februari na mabadiliko hayo yalikaribishwa na wengi wa wakazi wa Ghana Inaaminika na wengi wa wachanganuzi wa maswala ya kisiasa kwamba shirika la Marekani la Central Intelligence Agency CIA lilihusika katika mapinduzi hayo lakini wazo hilo halijawahi kuthibitishwa

Mfululizo wa baadaye wa mapinduzi kati ya na uliishia kwa kuingia mamlakani kwa Liuteni wa Jeshi la Wanahewa Flight Lieutenant Jerry Rawlings mnamo mwaka wa Mabadiliko haya yalisababisha kusimamishwa kwa katiba ya nchi mnamo na kupigwa marufuku kwa vyama vya kisiasa Uchumi ulishuka sana punde baadaye na Waghana wengi walihamia nchi zingine Ingawa wengi wa Waghana waliohama walienda Nigeria serikali ya Nigeria iliwarudisha Ghana karibu Waghana milioni moja mnamo mwaka wa

Punde baadaye Rawlings aliafikiana na shirika la International Monetary Fund juu ya mkataba wa mpango wa maendeleo structural development plan na kubadili sera nyingi za awali za uchumi na hivyo uchumi ukaanza kukua Katiba mpya iliyorudisha mfumo wa siasa za vyama vingi ilitangazwa mnamo mwaka wa na Rawlings alichaguliwa kuwa Rais na tena mnamo mwaka wa Katiba ya mwaka wa ilimzuia kuwania kiti hicho kwa muhula wa tatu kwa hivyo chama chake National Democratic Congress kilimchagua Makamu wake wa Rais John Atta Mills kuwania urais dhidi ya vyama vya upinzani Huku akishinda uchaguzi wa mnamo John Kufuor wa Chama pinzani cha New Patriotic aliapishwa kama Rais mnamo Januari na kumshinda tena Mills mwaka wa hivyo kuhuduma kama Rais kwa mihula miwili

Mnamo mwaka wa John Atta Mills alichukua mamlaka huku kukiwa na tofauti ndogo sana ya kura ambazo ni kati ya chama chake National Democratic Congress na kile cha New Patriotic Party tukio hili likiwa la pili la ubadilishanaji wa mamlaka kutoka kwa kiongozi mmoja aliyechaguliwa kihalali kwa mwingine na hivyo kuimarisha hadhi ya Ghana kama demokrasia iliyo imara

Maeneo ya Ghana

Ghana imegawanywa katika maeneo ya utawala kumi ambayo yamegawanywa zaidi kwa jumla ya wilaya Maeneo haya ni

Jengo la Mahakama Kuu The Supreme Court Building Accra
Maadhimisho ya Ghana ya miaka ya utaifa

Kwa mujibu wa Fahirisi ya Mataifa Yameanguka Failed States Index Taifa la Ghana linaorodheshwa katika nambari ya baina ya mataifa ambayo hayajaanguka huku likiorodheshwa kwa nafasi ya pili baina ya mataifa ya Afrika baada ya Mauritius Taifa la Ghana liliorodheshwa katika nafasi ya baina ya nchi katika fahirisi hii na liliainishwa kama taifa la wastani Vilevile nchi ya Ghana imo katika nafasi ya baina ya nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Sahara katika fahirisi ya mwaka wa ya Ibrahim Index of African Governance ambayo ilitokana na hakiki za mwaka wa Fahirisi ya Ibrahim ni kipimo chenye uchanganuzi mwingi kuhusu maswala ya utawala barani Afrika kinachotokana na maswala ya mabadiliko tofautitofauti ambayo huashiria kufuzu kwa serikali wakati wa kutoa huduma muhimu za kisiasa kwa wananchi wao

Serikali Taifa la Ghana lilianzishwa kama demokrasia ya bunge wakati wa kupata uhuru mnamo mwaka wa ikifuatiwa na ubadilishanaji wa serikali za kijeshi na za kiraia Mnamo Januari serikali ya kijeshi iliondoka na kuipisha Jamhuri ya Nne baada ya uchaguzi wa urais na ubunge mnamo mwisho wa mwaka wa Katiba ya inagawa mamlaka kati ya Rais Bunge Baraza la Mawaziri Baraza la Taifa na mahakama huru Serikali huchaguliwa na upigaji kura wa haki kwa wote ingawa bunge halina uwiano kabisa kwani wilaya zilizo na watu wachache hupata wawakilishi wengi kwa kila mtu zikilinganishwa na wilaya ambazo zina idadi ya juu ya wakazi

Maeneo ya Utawala Kuna maeneo kumi ya utawala ambayo yamegawanywa katika wilaya kila moja ikiwa na Bunge la Wilaya District Assembly Chini ya wilaya kuna aina kadhaa za mabaraza yakiwemo mabaraza ya miji au maeneo mabaraza ya kanda na mabaraza ya maeneo Kamati za vitengo huwa katika daraja ya chini zaidi na kwa mujibu wa wa Benki ya Dunia kisio la mapato ya kila mtu per capita income ya Ghana yamekuwa mara dufu lakini kwa shida kwa miaka iliyopita

Nchi ya Ghana ikijulikana kwa dhahabu yake katika enzi za ukoloni bado ni kati ya wazalishaji wakuu ulimwenguni wa dhahabu Mauzo yake mengine nje ya nchi kama vile kakao mbao umeme almasi bauxiti na manganisi ni uzalishaji mkuu wa fedha za kigeni Kiwanja cha mafuta kinachoripotiwa kuwa na hadi pipa bilioni m za mafuta mepesi kiligunduliwa mnamo mwaka wa Utafutaji wa mafuta bado unaendelea na kiasi cha mafuta kinaendelea kuongezeka
Jumba la Kakao la Sunyani Bwawa la Akosombo ambalo lilijengwa juu ya Mto Volta mnamo mwaka wa linatoa umeme unaozalishwa na maji kwa nchi ya Ghana na nchi zinazoizunguka

Nguvukazi ya Ghana katika mwaka wa ilikuwa jumla ya watu milioni Uchumi unaendelea kutegemea sana kilimo ambacho huchangia ya Pato la Taifa na kutoa ajira kwa kwa ya watu wanaofanya kazi

Sera za kiuchumi zisizofaa za serikali za kijeshi zilizopita na masharti ya vikosi vya kulinda usalama katika maeneo ya kanda vimechangia mfumuko katika fedha za nakisi kushuka thamani kwa Sidi na kuongezeka kwa kutoridhika kwa umma katika maswala ya hatua za kupunguza ugumu wa maisha Hata hivyo Ghana inabakia kuwa mojawapo baina ya nchi za Afrika nzima ambazo zina ustawi wa kiuchumi

Mnamo Julai Benki ya Ghana ilianzisha shughuli ya kugeuza sarafu kutoka kwa Sidi hadi kwa sarafu mpya Sidi ya Ghana GH Kiwango cha ubadilishanaji ni Sidi moja ya Ghana kwa kila Sidi Benki ya Ghana ilizindua kampeni kabambe katika vyombo vya habari ili kuelimisha umma juu ya mageuzo haya

Sarafu mpya ya Sidi ya Ghana iko imara kwa kiwango kikubwa na katika mwaka wa ilibadilishwa kwa ujumla kwa thamani ya dola moja ya marekani kwa Sidi ya Ghana

Nchi hii ina maeneo tambarare vilima vya chini na mito michache Nchi ya Ghana inaweza kugawanywa katika maeneo matano tofauti ya kijiografia Eneo la pwani ni sehemu ambayo ni ya chini na iliyo na ufuo wa mchanga huku ikipakana na koko na kukingamana na mito na vijito kadha wa kadha huku sehemu ya kaskazini ikiwa na maeneo ya juu yaliyo tambarare Eneo la kusini magharibi na kusini ya kati mwa Ghana ni sehemu iliyoinuka sawa na pana yenye misitu ikiwa na vilima vya Ashanti na eneo sawa na pana plateau la Kwahu na safu ya vilima vya AkuapimTogo vinapatikana kwenye mpaka wa mashariki mwa nchi Bonde la Volta linachukua eneo la kati mwa Ghana Sehemu ya juu zaidi nchini Ghana ni Mlima Afadjato ulio na urefu wa mita futi na unaopatikana kwenye safu ya vilima vya AkwapimTogo
Hali ya hewa ni ile ya hari Kanda ya pwani ya mashariki ni ya joto na iliyokauka angalia Dahomey Gap pembe ya kusini magharibi huwa na joto jingi na unyevu hewani huku sehemu ya kaskazini ikiwa yenye joto jingi na iliyokauka Ziwa Volta ziwa lisilo la asili kubwa zaidi ulimwenguni linaenea kupitia katika mafungu makubwa mashariki mwa Ghana na ndicho chanzo kikuu cha vijito vingi kama vile vya Oti na Afram

Kuna misimu miwili mikuu nchini Ghana masika na kiangazi Kaskazini mwa Ghana huwa na msimu wa masika kutoka Machi hadi Novemba huku sehemu ya kusini ukiwemo mji mkuu wa Accra ikiwa na masika kutoka Aprili hadi Novemba katikati
Kusini mwa Ghana kuna misitu ambayo daima ni ya kijani kibichi na ile ambayo hupoteza majani yake wakati fulani wa mwaka ikiwa na miti kama mikangazi odumu na mipingo Sehemu hii inayo pia mingi ya mitende ya mafuta na mikoko Miti ya Shea mibuyu na mikakaya hupatikana kwa kawaida katika maeneo ya Volta na kaskazini mwa nchi

Barabara ya Bolga Tamale
Msikiti wa Larabanga uliojengwa katika karne ya Larabanga
Kanisa la Wesley Methodist Cathedral Kumasi
Nchi ya Ghana ina idadi ya watu inayokisiwa kuwa milioni Ghana ni kiambo cha zaidi ya makabila tofauti Kwa bahati nzuri nchi ya Ghana haijashuhudia migogoro ya kikabila ambayo imesababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi nyingi za Kiafrika Lugha rasmi ni Kingereza hata hivyo Waghana wengi pia huzungumza kwa kiasi lugha moja ya kabila
Makabila nchini Ghana ni Akan ambalo linajumuisha Fante Akyem Ashanti Kwahu Akuapem Nzema Bono Akwamu Ahanta na makabila mengine MoleDagbon Ewe GaDangme likijumuisha Ga Adangbe Ada Krobo na makabila mengine Guan Gurma Gurunsi MandeBusanga makabila mengine mengine Hausa Zabarema Fulbe sensa ya
Kwa mujibu wa sensa ya serikali ya migawiko ya kidini ni Wakristo Waislamu imani ya Kiafrika

Zaidi ya lugha na lugha ndogo huzungumzwa nchini Ghana Lugha ya Kingereza ndiyo lugha rasmi na hutumika sana katika maswala ya serikali na biashara Lugha hii vilevile ndiyo hutumika katika mafundisho ya kielimu Lugha za kiasili za Ghana zimegawanywa katika jamii mbili ndogo za kilugha kutokana na jamii ya lugha ya NigerCongo Lugha za jamii ndogo ya Kwa zinapatikana zaidi katika maeneo ya kusini mwa Mto Volta huku zile za jamii ya Gur zikipatikana katika eneo la kaskazini Kikundi cha Kwa lugha ambayo huzungumzwa na takribani ya wakazi wa nchi kinajumuisha lugha za Akan GaDangme na Ewe Kikundi cha Gur kinajumuisha lugha za Gurma Grusi na Dagbani

Lugha tisa zina hadhi ya kuwa lugha zinazodhaminiwa na serikali Akan hasa Ashanti Twi Fanti Akuapem Twi Akyem Kwahu Nzema DagaareWale Dagbani Dangme Ewe Ga Gonja na KasemIngawa si lugha rasmi Hausa ndiyo lugha ya mawasiliano inayozungumzwa na Waislamu wa Ghana ambo ni ya wakazi

Kufikia mwaka wa makadirio ya maisha life expectancy wakati wa kuzaliwa ni takribani miaka kwa wanaume na kwa wanawake huku makisio ya vifo vya watoto wachanga yakiwa kwa watoto waliozaliwa wakiwa hai Asilimia ya Pato la Taifa la nchi lilitumika kwa maswala ya afya katika mwaka wa
na aina ya awali zaidi ya muziki wa kidunia inayoitwa Highlife Highlife ni muziki uliochimbuka katika miaka ya mwisho ya na miaka ya mwanzo ya na kuenea kote Afrika Magharibi hasa Sierra Leone na Nigeria Katika miaka ya aina mpya ya muziki ilizinduliwa na vijana huku ikiunganisha jinsi za Highlife Afroreggae Dancehall na Hiphop Mchanganyiko huu huitwa Hiplife Wasanii wa Ghana kama vile mwimbaji wa RB na Soul Rhian Benson mwimbaji wa Highlife Kojo Antwi na msanii wa rap Tinchy Stryder Kwasi Danquah wamekuwa na ufanisi wa kimataifa

Ngoma densi ya Ghana ina tofauti mithili ya muziki wake Kila kabila lina ngoma zake za kitamaduni na kuna ngoma tofauti tofauti kwa hafla tofauti tofauti Kuna ngoma za mazishi sherehe za maadhimisho usimulizi wa hadithi sifa na kuabudu na kadhalika Baadhi ya ngoma hizi ni

Bamaya
Ngoma hii huchezwa na watu wa eneo la kaskazini mwa Ghana Inasimulia hekaya ya wakati wa ukame mkubwa Miungu iliwaambia watu kuwa ukame huo ulikuwa umeletwa na jinsi wanaume walikuwa wakiwakandamiza na kuwatweza wanawake Ilisema pia kwamba ukame ungeondolewa tu pale wanaume wangejizusha na kuchukua majukumu waliyokuwa wamewatwika wanawake kwa kuvaa marinda na kushiriki katika ngoma hii Wanaume walipofanya hivi mvua ilianza kunyesha Kwa sasa ngoma hii huchezwa wakati wa mavuno katika eneo la kaskazini magharibi mwa Ghana na wanaume pamoja na wanawake wa Dagbani
Wacheza ngoma wa Ghana
Adowa
Ngoma ya watu wa Ashanti wa Ghana Ngoma hii inatajika hasa kwa madaha na weledi wa mzunguko wa wachezaji Upigaji ngoma pia unasifika kwa weledi wa mfuatano wa sauti zinazochanganyika na ngoma mbili za atumpan ambazo zinatumika kama ngoma za kuongoza au ngoma simamizi Ngoma hii ilikuwa awali ikichezwa katika mazishi lakini kwa sasa inachezwa pia katika tamasha za kila mwaka na mikusanyiko ya kijamii

Kpanlongo
huchezwa na watu wa Ga wa Ghana Ngoma hii ya Kpanlongo ambayo mara nyingi huitwa ngoma ya vijana ilianza kuchezwa punde tu baada ya unyakuzi wa Uhuru wa Ghana kama aina ya muziki wa burudani jijini Accra Kpanlongo huchezwa kwa sasa kwa matukio yanayohusu maisha tamasha na mikutano ya kisiasa

Klama
Huu ni muziki na ngoma ambayo inahusishwa na ibada za kubalehe kati ya watu wa Krobo wa Ghana Inasisitiza kusonga kwa madaha kwa mikono na miguu Huku wakipiga hatua ndogo kuambatana na muziki na wakigeuza vichwa kwa utaratibu kuangalia chini wacheza ngoma huwa mfano wa madahiro tulivu Tofauti baina ya hatua za wachezaji zinanuiwa kuonyesha uzuri wa wacheza ngoma Mara kwa mara wachumba wanaotazama ngoma hii kutoka pembeni huzuru jamii ya msichana baada ya sherehe kwa madhumuni ya kumposa msichana huyo

Miss Ghana

Vyombo vya habari vya Ghana ni mojawapo ya vile vilivyo na uhuru zaidi barani Afrika Hapo awali vilikuwa vimewekewa vizuizi vingi wakati wa mfululizo wa mapinduzi ya serikali na viongozi wa jeshi Sura ya ya katiba ya ya Ghana inatoa hakikisho la uhuru na kujisimamia kwa vyombo vya habari huku Sura ya ikizuia uthibiti

Baada ya kujinyakulia uhuru serikali na vyombo vya habari vimekuwa mara kwa mara vikiwa na uhusiano ulio na mvutano huku mashirika ya kibinafsi yakifungwa wakati wa mapinduzi ya kijeshi na sheria kali ili kuzuia ukosoaji wa serikali Uhuru wa vyombo vya habari ulirejeshwa mnamo mwaka wa na baada ya uchaguzi wa wa John Kufuor mivutano kati ya vyombo vya habari vya kibinafsi na serikali ilipungua Kufuor alikuwa mtetezi mkubwa wa uhuru wa vyombo vya habari na alifuta sheria ya masingizio ingawa alisisitiza kuwa ni lazima vyombo vya habari vifanye kazi kwa uwajibikaji Vyombo vya habari vya Ghana vimeelezwa kuwa baadhi ya vile visivyo na uthibiti mkubwa na serikali mwingi barani Afrika huku vikifanya kazi vikiwa na masharti machache mno kwa vyombo vya habari vya kibinafsi Vyombo vya habari vya kibinafsi mara kwa mara hukosoa sera za serikali
Vyombo vya habari vilifanya kazi kwa bidii wakati wa uchaguzi wa rais wa Ghana wa mwaka wa na Chama cha Wanahabari wa Ghana Ghanaian Journalists Association GJA kilimpongeza John Atta Mills kwa ushindi wake huku kikinuia kukuza uhusiano mwema baina ya vyombo vya habari na serikali

Kikundi cha vitambaa cha Dora katika eneo la Nsawam
Chuo Kikuu cha Cape Coast
Kiwango cha kujua kusoma na kuandika kwa watu wazima kilikuwa mnamo huku wanaume wakiwa na wanawake wakiwa Nchi ya Ghana ina mfumo wa elimu ya msingi wa miaka kuanzia umri wa miaka sita na chini ya mageuzi ya elimu yaliyotekelezwa mnamo na kurekebishwa mnamo watoto huingia katika mfumo wa miaka mitatu wa elimu ya upili ya daraja la chini Mwishoni mwa mwaka wa tatu katika shule ya upili ya Junior High kuna mtihani wa lazima unaojulikana kama Basic Education Certificate Examination BECE Wale wanaoendelea na masomo ni lazima wamalize masomo ya miaka mitatu ya shule ya upili ya daraja ya juu senior high school SHS na kufanya mtihani wa kukubaliwa kuingia katika masomo ya chuo kikuu au taasisi yoyote ile

Kwa sasa Ghana ina shule za msingi shule za upili za daraja ya chini shule za upili za daraja ya juu vyuo vya mafunzo vya umma vyuo vya mafunzo vya kibinafsi Mbali na shule za msingi na za upili zinazofuata mfumo wa elimu wa Ghana kunazo shule za kimataifa kama vile Ghana International school Lincoln Community School na SOSHermann Gmeiner International College ambazo hufuata mfumo wa International Baccalaureat Advanced Level General Certificate of Education na International General Certificate of Secondary Education IGCSE

Huku ikiwa na asilimia ya watoto wake shuleni kwa sasa nchi ya Ghana ni baina ya nchi zilizo na viwango vya juu zaidi vya uandikishaji shuleni katika eneo la Afrika Magharibi Uwiano wa wasichana na wavulana katika ujumla wa mfumo wa elimu ni ambao kwa nchi ya Afrika Magahribi ni mafanikio makubwa Kadiri ya watoto hawaendi shuleni kwa sababu ya ukosefu wa mapato ya kuwezesha ujenzi wa shule kutoa vitabu vya kusoma vya kutosha na kutoa mafunzo kwa walimu wapya Tangu unyakuzi wa uhuru wa Ghana nchi hii imekuwa mojawapo ya vitovu vya elimu katika eneo la Afrika Kusini mwa Sahara na imekuwa mwenyeji wa watu maarufu kama vile Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe Alhaji Sir Dauda Jawara wa The Gambia na Cyprian Ekwensi wa Nigeria baina ya wengine Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Kwame Nkrumah ambacho ndicho chuo kikuu cha pili kuanzishwa nchini Ghana ndicho chuo cha kwanza cha masomo ya sayansi na teknolojia nchini humo na katika ukanda wa Afrika Magharibi

Jumuiya ya Madola
Orodha ya nafasi katika ngazi za kimataifa
Vidokezo kuhusu Afrika
Vidokezo kuhusu jiografia
Umoja wa Mataifa
Uchukuzi Ghana

Usafiri usio ghali kwenda Ghana

Serikali
Tovuti rasmi ya Ghana
Tovuti rasmi ya Bunge la Ghana
Tume ya Kitaifa ya Utamaduni
Mkuu wa serikali na Wanachama wa Baraza la Mawaziri

Habari za ujumla
Maelezo ya nchi Country Profile kutoka BBC News
Ghana kutoka Encyclopaedia Britannica

Ghana kutoka UCB Libraries GovPubs

Tovuti ya African Activist Archive Project ina picha za mkutano wa All Africa Peoples Conference uliofanyika Accra Ghana Disemba ikiwemo ile ya Kwame Nkrumah Waziri Mkuu wa Ghana akiuhutubia mkutano ujumbe wa American Committee on Africa ukikutana na Nkrumah na ya Patrick Duncan na Alfred Hutchinson wa Afrika Kusini katika mkutano huo

Vyombo vya habari
Shirika la Utangazaji la Ghana Ghana Broadcasting Corporation

Utalii

Utalii nchini Ghana Ghana Tourism Tovuti Rasmi ya Utalii wa Ghana

Picha za Ghana katika Bigfotocom
Picha za Ghana katika City photos

Geographic locale
list
Lat and Long Accra








Ghana
Nchi za Afrika
Wanachama wa Umoja wa Afrika
Nchi zinazopakana na Bahari ya Atlantiki
Shirika la Uchumi la Mataifa ya Africa Magharibi
Nchi na maeneo yanayozungumza Kingereza
Demokrasia huria
Wanachama wa Jumuiya ya Madola
Mataifa na maeneo yaliyoanzishwa

Wikipedia ni kamusi elezo huru ya lugha nyingi katika mtandao Inatumia taratibu wa wikiwiki Ni bure kabisa na inaweza kusomwa kuandikwa na kuhaririwa na mtu yeyote popote pale Yaani kila mtu anaweza kuchangia makala au kuwa na uhuru wa kuboresha makala zilizopo kwa kuzihariri

Kamusi hii inajengwa kwa utaratibu huria ambao umejengwa juu ya falsafa ya ushirikiano inayokuwa kwa kasi Falsafa hii inaonekana katika vuguvugu la programu huria ya tarakilishi mikutano huria demokrasia huria nk

Wikipedia ilianzishwa kwa Kiingereza mwezi wa kwanza mwaka Mwaka kamusi elezo hii ilianzishwa katika lugha ya Kiswahili

Wikimedia

Dar es Salaam ni jiji kubwa kuliko yote nchini Tanzania Ni pia jina la Mkoa wa Dar es Salaam Hali halisi ni pia mji mkuu wa Tanzania hata kama Dodoma imetangazwa kuwa mji mkuu tangu mwaka Lakini ofisi ya rais na wizara nyingi bado zinafanya kazi Dar es Salaam ambayo hali halisi ni makao makuu ya serikali

Jiji hili zamani liliitwa Mzizima Sultani Seyyid Majid wa Zanzibar ndiye aliyelipa jiji hili jina Dar es Salaam linalotoka kwenye Kiarabu Dr asSalm lenye kumaanisha nyumba ya amani Maelezo yanayopatikana mara nyingi kuwa maana ni bandari ya salama yachanganya maneno mawili yanayofanana katika Kiarabu yaani dar nyumba na bandar bandari

Dar es Salaam ilichaguliwa na wakoloni Wajerumani kuwa mji mkuu wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani kwa sababu ya bandari asilia kwenye mdomo pana ya mto Kurasini Kuanzia Dar es Salaam ilichukua nafasi ya Bagamoyo kama makao makuu ya utawala Bandari pamoja na ujenzi wa reli ya kati kwenda Kigoma tangu ziliimarisha nafasi ya mji ulioendelea kama mji mkuu baada ya Tanzania bara kuwa koloni ya Tanganyika chini ya Uingereza

Dar es Salaam inakadiriwa kuwa na wakazi wapatao milioni tatu Ingawa Dodoma inafahamika kama ndio mji mkuu wa Tanzania Dar es Salaam ndiko ziliko ofisi kuu za viongozi wa serikali mabalozi mashirika ya kimataifa nk

Uwanja wa ndege mkuu wa Tanzania uko pia mjini hii ni Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere
Bandari ya Dar es Salaam katika bahari ya Hindi ndio bandari kubwa nchini Tanzania inayojihusisha na usafirishaji na uingizaji wa bidhaa mbalimbali za kilimo ufugaji ujenzi magari madawa nk

Kiutawala Dar es Salaam imegawanywa katika wilaya za Temeke Ilala na Kinondoni

DAR ES SALAAM CITY PROFILE
Mohamed Said Mwalimu in s Dar East African October inasimulia maisha ya Nyerere katika Dar pamoja na habri nyingi za jiji wakati wa miaka ya

ImageDar IkulutzjpgIkulu Nyumba ya Rais huko DarEsSalaam
ImageDarEsSalaamSamoraMachelAvenuejpgSamora Machel Avenue with NIC House
ImageDarEsSalaamSkylinejpgFeri ya kuvuka Kigamboni nyumba za jiji zaonekana ngambo ya bandari asilia
ImageDar AskarijpgSanamu ya Askari kwa ajili ya maaskari Waafrika walioshiriki vita kuu ya kwanza upande wa Waingereza
ImageDar Po jpgUwanja wa Ndege wa kimataifa
ImageDar Jangwani jpgTimu ya mpira ya Yanga Young African Sports Club wanakaribishwa Dar
ImageDar MnazimmojajpgMnazi Mmoja

Miji ya Tanzania
Tanzania
Miji Mikuu Afrika

right
Bahari ya Hindi ni bahari kubwa ya tatu duniani ikiwa imechukua asilimia ya uso wa dunia Upande wa kaskazini imepakana na Asia ya Kusini magharibi imepakana na Ghuba ya Uajemi Bahari ya Shamu na Afrika mashariki imepakana na Ghuba ya Malay visiwa vya Sunda Indonesia na Australia na kusini imepakana na Bahari ya Kusini

Bahari hii ni njia muhimu ya usafirishaji na usafiri kwa meli kati ya Asia na Afrika

Bahari

Jomo Kenyatta
Nairobi ni mji mkuu wa Kenya na vilevile mojawapo ya mikoa ya Kenya Ni kati ya miji mikubwa ya Africa ukiwa na wakazi wapatao milioni katika eneo la km Jina Nairobi limetokana na neno la Kimaasai Enkarenairobi linalomaanisha mahali penye maji baridi

Lugha zote za Kenya huzungumzwa Nairobi lakini hasa ni Kiingereza na Kiswahili pamoja na Sheng

Nairobi imeanzishwa mahali ambako nchi tambarare ya Athi inakutana na mtelemko wa nyanda za juu zinazoongozana na Bonde la Ufa Kitovu cha Nairobi iko zipatao m juu ya UB Mahali pake ni kama km kusini mwa ekweta Hali ya hewa haina joto kali Halijoto ya wastani ni mwezi wa Machi na mwezi wa Julai Mvua nyingi hunyesha mwezi wa Machi mm kiangazi ina mm tu wakati wa Julai

Ndani ya jiji la Nairobi kuna mitaa mbalimbali kama vile Dandora Eastleigh Embakasi Highridge Huruma Jericho Karen Kariobangi Kiambiu Kibera Langata Lavington Mathare Parklands South C Westlands Kawangware Karen

Nairobi imeanzishwa mw na Waingereza kama kambi ya kujenga Reli ya Uganda Mahali ilikuwa karibu katikati ya Mombasa na Kampala palikuwa na maji ikaonekana ilifaa kwa kituo njiani Mwanzo wa Nairobi ilikuwa kambi kubwa ya hema na ghala za vifaa vya kujenga reli
Mwanzoni viongozi wengine walitaka kuacha eneo hili kwa sababu ya matope mengi Lakini makao iliendelea kukua nyumba za mawe zikajengwa Mw Waingereza walihamisha ofisi kuu ya serikali yao ya kikoloni kutoka Mombasa kwenda Nairobi ikawa makao makuu ya Afrika ya Mashariki ya Kiingereza British East Africa war baadaye Kenya Colony

ikawa mji mkuu wa nchi huru ya Kenya

Ikaendelea kukua haraka

Nairobi imeibuka kuwa mojawapo ya miji mikubwa katika bara la Africa Mashirika mengi makubwa duniani yamefungua ofisi zao zinazoshuhudia eneo la Afrika ya Mashariki na Afrika ya Kati Mojawapo ya mashirika haya ni ofisi za ya tawi la Umoja wa Mataifa United Nations UNEP Kunazo pia ofisi za mabalozi wa nchi mbali mbali duniani
Nairobi kama miji mingi mikubwa ina matatizo mengi yanayotokea kwa sababu ya ukubwa wake Watamaduni walioupanga mji wa nairobi hawakutegemea kuwa ungenenepa hivyo Wataalamu wengi wametoa maoonyo mengi kuhusu ukubwa wa mji huu na uwezo wake wa kuwahudumia waakaazi wote ambao wanazidi kuongezeka kila mwaka
Nairobi imewavutia waakaazi wengi wote wakiwa na hamu ya kujitafutia riziki yao Ijapokuwa kunao wanaofanikiwa wengi wao hujipata wameangulia patupu wakawachwa bila pesa au hali ya kujikimu Jambo hili limepelekea kuwepo kwa wakaazi wa maeneo yasiyotengwa wananchi maarufu kama slums kwa kimombo Eneo kubwa zaidi jijini Nairobi ni Kibera Eneo hili lina ukubwa wa kilomita kwa na wakaazi takribani milioni moja Eneo hili halina mipango yeyote ya kuruhusu binadamu kuishi lakini umaskini umewavutia wengi kuishi kule

Kunayo pia matatizo ya ujambazi wa kibinafsi ujambazi wa nyumba na utekaji nyara wa magari Matatizo haya yamesababisha watu wengi kutoupendelea mji wa Nairobi

valigntop



Tovuti rasmi ya Nairobi
Chuo Kikuu cha Nairobi

Mikoa ya Kenya
Miji ya Kenya
Miji Mikuu Afrika

Antaktiki
Antaktiki
Kituo cha Kisayansi katika Antaktiki
Antaktiki ni bara kwenye ncha ya kusini ya dunia Kwa sababu ya baridi kali katika bara hii ni bara ya pekee ambapo hawaishi binadamu wowote isipokuwa kuna wanasayansi wanaokaa kwa muda katika vituo vyao Jina Antaktiki latokana na lugha ya Kigiriki likimaanisha kinyume cha Aktiki na Aktiki ni eneo karibu na ncha ya kaskazini

Takriban za eneo la bara lafunikwa na theluji na barafu Bara liko kati ya bahari za Pasifiki Atlantiki na Bahari Hindi Eneo lake ni kubwa kushinda Ulaya lakini hakuna mti hata mmoja

Kuna volkeno hai moja inayotema moto barani ni mlima wa Mount Erebus

Antarctic Placenames Commission of Bulgaria
LL Ivanov et al Topographic map of Livingston Island and Greenwich Island

Jiografia
Bara

Ubaguzi wa rangi ni kitendo cha kuthamini au kutenga binadamu kwa misingi ya rangi za ngozi Ubaguzi wa rangi ulikuwa maarufu sana katika nchi kama Afrika Kusini kwa jina la apartheid na Marekani kwa jina la segregation ambapo huko Waafrika walikandamizwa kutokana na rangi yao katika kupata huduma mbalimbali za kijamii na kimaendeleo

Wakati wa ukoloni rangi ilitumika kama msingi wa utoaji huduma muhimu mfano shule matibabu na haki nyingine za kibinadamu Rangi nyeusi ilipewa hadhi ya chini zaidi

Siku hizi katika karibu nchi zote sheria zinapinga ubaguzi wa rangi Lakini katika nchi nyingi bado kuna wabaguzi wachache ambao wanavunja sheria kwa kuendelea kubagua Kwa mfano kuna wabaguzi wanaobagua Watu weusi nchini Marekani na katika nchi za Ulaya

Mkutano wa Kimataifa Dhidi ya Ubaguzi

Utumwa ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kummiliki binadamu mwenzake kama mali yake Binadamu anayemilikiwa anakuwa na hadhi sawa na chombo au kifaa chochote kinachoweza kuuzwa

Mfumo huu ulikuwa maarufu kabla ya harakati za ukoloni duniani mathalani karne ya ambapo watumwa walihitajika katika shughuli za kilimo na uchimbaji madini katika sehemu mbalimbali za ulimwengu

Mfumo huu uunda matabaka ya mabwana ambao humiliki watumwa na watwana ambao ni watumwa wenyewe

Katika historia zilitokea aina mbalimbali za utumwa

Kulikuwa na utumwa wa muda yaani mtu huwa mtumwa kwa miaka kadhaa au kwa maisha yote Kulikuwa na utaratibu ambako watoto wa mtumwa walikuwa watumwa tena hivyo kuzaliwa watumwa kulikuwa pia na utaratibu ya kwamba watoto wa watumwa waliazamiwa kama watu huru

Kulikuwa na jamii ambako watumwa hawakuwa na haki kabisa yaani mabwana waliweza kuwatendea jinsi walivyotaka hata kuwaua lakini kulikuwa pia na jamii zilizojua haki fulani za watumwa watumwa waliweza kuwa na mali ya binafsi na kwa njia hii hata kununua uhuru wao kutoka kwa mabwana

Watumwa katika utumishi wa watawala waliweza kupata nafasi muhimu katika jamii mfano ni wamameluki wa Misri waliokuwa watumwa wanajeshi wakatawala nchi hii kwa karne kadhaa

Chanzo cha utumwa kilikuwa mara nyingi ama vita ama madeni Vitani wafungwa wakauzwa kama watumwa wakihesabiwa kama sehemu ya uwindo wa washindi Sababu kuu nyingine ilikuwa madeni ya watu waliokamatwa na kuuzwa ili madeni yalipiwe kwa njia hii

Mahitaji wa kiuchumi kwa watumwa wengi yalisababisha biashara ya watumwa

Uchumi
Siasa
Utumwa

Ramani ya ukoloni duniani mwishoni mwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka

Ukoloni ni mfumo wa taifa moja kuvuka mipaka yake na kutawala taifa jingine katika nyanja za kiuchumi kiutamaduni na kijamii

Nchi za Afrika yaliwekwa chini ya ukoloni wa nchi za Ulaya mara baada ya Mkutano wa Berlin ulioitishwa na chansella wa Ujerumani Bismarck mwaka

Nchi zilizojenga ukoloni huu wa Afrika zilikuwa Uingereza Ufaransa Ureno Ujerumani Uhispania Italia na Ubelgiji

Ukoloni mamboleo ni aina ya nchi au kundi la nchi fulani kutawala nchi nyingine kinyemela kwa kuweka vikwazo na masharti yatakayowafanya watawaliwa waendelee kuwa na uchumi tegemezi ili wawatajirishe zaidi hao wanaowatawala kinyemela

Historia ya Afrika

Jamii

Map of Burundi
Satellite image of Burundi
NASA photo of Burundi

Jamhuri ya Burundi iliyojulikana zamani kama Urundi ni nchi ndogo ambayo iko karibu na Eneo la Maziwa Kubwa ya Afrika Burundi imepakana na Rwanda upande wa kaskazini Tanzania upande wa mashariki na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa magharibi Ingawa Burundi haina bahari sehemu ya mpaka wake eneo la mashariki uko karibu na Ziwa Tanganyika Jina lenyewe la nchi hii limetokana kwa msingi na kutanuka kwa lugha ya Kirundi ambacho ni lugha ya Kibantu

Burundi ni nchi ndogo iliyomo barani Afrika Mara kadhaa nchi hii imekuwa na misukosuko na machafuko ya kisiasa na kijamii Shida kubwa ni kuwa Burundi haina maliasili kutosheleza umma na kutosheleza ratili ya kisiasa kwa walio wengi Wahutu na walio wachache Watutsi na Watwa

Kwa orodha ya Marais wa nchi tangu uhuru angalia hapa

Kadanda Burundi
orodha ya waandishi kutoka Burundi
Muziki wa Burundi

Mawasiliano nchini Burundi
Mahusiano ya Kimataifa Burundi
Jeshi la Burundi
Usafiri nchini Burundi

Mambo mengi ya Burundi yamepatikana kutoka CIA World Factbook na US Department of State website

Burundi Ethnic Conflict and Genocide Reni Lemarchand and Lee H Hamilton

Orodha ya miji ya Burundi
Orodha ya mikoa ya Burundi

Tovuti ya serikali ya Burundi

Agence Burundaise de Presse ABP
Habari za Burundi toka tovuti ya habari ya allAfrica Burundi
Radio Isanganiro Radio binafsi nchini Burundi kwa Kifaransa na Kirundi na Kiswahili
umucocom Habari kuhusu Burundi kwa Kifaransa
Burundi Ralits Habari na Uchambuzi kwa Kiingerenza na Kifaransa

BBC News Country Profile Burundi
CIA World Factbook Burundi

Open Directory Project Burundi directory category
Stanford University Africa South of the Sahara Burundi directory category
University of Pennsylvania African Studies Center Burundi directory category
Yahoo Burundi directory category

Burundian Human Rights Organisation Ligue Iteka with uptodate news in English and French
Campaign for the prosecution of FNL leader Agathon Rwasa
Human Rights Watch reports on Burundi
Woodrow Wilson Center Reports on Burundi
Human Rights Watch special report on the August Gatumba massacre
Links to political analyses from on by the International Crisis Group
Reuters Alertnet Burundi humanitarian news
Updated humanitarian news from the United Nations Office for the Coordination of Humanitarian Affairs


Nchi za Afrika


aligncenter colspan Hadabu ya Taifa Nie nie

aligncenter colspan Location of Eritrea

Lugha za Taifa
Tigrinya Kiarabu na Kiingereza

Mji Mkuu
Asmara

Rais
Isaias Afewerki

Eneo Total Maji
Kadiriwa th kmsup Acha

Idadi ya Watu Makadirio Jumla Chumo cha Umma kugawa na Eneo
Kadiriwa th kmsup th

GDP PPP Jumla Kwa Kila Raia Per capita
estimate th th

Uhuru Kadirifu Barabara
Kutoka Ethiopia Uhebeshi Mai Mai

Fedha
Nakfa

Saa za Eneo
UTC

Wimbo wa Taifa
Ertra Ertra Ertra

Intaneti TLD
er

Kodi ya simu


Eritrea ni nchi ya Afrika kaskazinimashariki Upande wa Magharibi imepakana na Sudan upande wa Kusini imepakana na Ethiopia na KusiniMashariki kuna nchi ya Djibouti Mashariki na KusiniMashariki Eritrea ina pwani ndefu ya Bahari ya Shamu Eneo hili hujulikana pia kama Pembe ya Afrika

Jina la nchi limetungwa mnamo mwaka na wakoloni wa Italia kutokana na neno la Kigiriki erythraa linalomaanisha bahari nyekundu Hii ni kwa sababu Bahari ya Shamu iliitwa Sinus Erythraeus na mabaharia Wagiriki au Mare Erythraeum kwa Kilatini na Waroma wa kale maana yake ni bahari nyekundu tazama Kiingereza Red Sea

Angalia makala Historia ya Eritrea

Historia ya Eritrea kama eneo la pekee jinsi lilivyopata uhuru mwisho wa karne ya ilianza na ukoloni wa Italia Hadi karne ya maeneo ya Eritrea yalikuwa sehemu ya Ethiopia Pwani ilikaa karne nyingi chini ya utawala wa Uturuki au baadaye Misri zilizokuwa nchi zenye nguvu kwenye Bahari ya Shamu

kampuni la Kiitalia lilinunua bandari ya Assab ambayo ikawa koloni la serikali ya Italia mwaka Italia ilipanua utawala wake kwa kutwaa mji wa Massawa mwaka na kuchukua pia pwani yote kati ya miji hiyo miwili Baadaye Waitalia walianza kuelekea nyanda za juu na Ethiopia yote Mwendo huu ulisimamishwa na Ethiopia katika mapigano ya Adowa mwaka Italia ilikubali uhuru wa Ethiopia nayo ilikubali koloni la Italia katika Eritrea

Koloni lilianzishwa rasmi mwaka kwa jina la Eritrea kutokana na jina la kale la Mare Erytraeum au Bahari ya Eritrea

Utawala wa Italia ulileta mabadiliko mengi kati ya watu wa koloni na kujenga jamii mpya na tofauti na wakazi wa Ethiopia hivyo kuweka msingi wa taifa la pekee

Tangu mwaka serikali mpya ya Italia ya Mussolini ilianzisha siasa ya ubaguzi wa rangi na kuwatendea wenyeji kwa dharau

Kuanzia Eritrea ilikuwa mahali pa kuanzisha vita mpya ya Italia dhidi ya Ethiopia

Katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia jeshi la Italia katika Ethiopia lilishindwa na Waingereza na Eritrea ikaja kutawaliwa na Uingereza tangu mpaka Eritrea ilipokabidhiwa na Umoja wa Mataifa kwa Ethiopia kama eneo la pekee

Serikali ya Haile Selassie ililenga kuunganisha tena Eritrea na Ethiopia na kwa mbinu mbalimabli ilipata kura ya bunge la Eritrea ya kujivunja na kuwa jimbo la Ethiopia

Baada ya tukio hili vikundi vya wanamigambo walienda porini kupigania uhuru ya Eritrea kwa silaha Baada ya vita ya miaka harakati ya Eritrean Peoples Liberation Front EPLF ilishinda jeshi la Ethiopia mwaka Usindi huu ulikuwa baadaye sababu kuu ya kuanguka kwa serikali ya Ukomunisti ya Ethiopia

Baada YA kura ya wakazi wa Eritrea uhuru wa nchi ilitangazwa tarehe Mei Awali uhusiano na serikali mpya ya Ethiopia ulikuwa mzuri lakini baada ya miaka ya kwanza ulizorota

Mwaka kulitokea vita kati ya Eritrea na Ethiopia vilivyokwisha na ushindi wa Ethiopia Wanajeshi wa kulinda amani wa UM wanajaribu kutunza hali ya kutopigana

Kifungu chenyewe Siasa za Eritrea
Rais wa Eritrea Isaias Afewerki kulia na Waziri wa Marekani wa Ulinzi Donald Rumsfeld
Bunge la Taifa la viti iliyo tekezwa mwaka baada ya Uhuru Bunge hiyo ilimchagua Rais wa sasa Isaias Afewerki Kura za Nchi huwa zinapagwa na kupanguliwa Shina za taarifa madaraka za kutangaza habari kwa siasa za nyumbani Eritrea haziko na September serikali ilifunga wataarifi midia zakibinafsi na watu wanaopinga serikali kufugwa bila kushtakiwa hii yote ni kutoka taarifa ya washufu wa ulimwengu kama Waangalizi wa haki za Kibinadamu Human Rights Watch and Wakobozi wa Kimataifa Amnesty International Mwaka wa Idara ya jimbo ya marekani US State Department iliamua kwamba Eritrea ni Nchi maksusi Kujalisha Country of Particular Concern au CPC ya kufinyilia Dini Ona chini hapa

Mambo ya inje yanahusu vita na Ethiopia na Sudan Baada ya wajumbe wa serikali ya Eritrea wa Idara ya mambo za kigeni kuenda Sudani ushirikiano umeanza kuwa wakawaida Bishano na Ethiopia bado ni mawazo makubwa ya chuki abayo imemfanya Rais kuiambia Muungano wa Kimataifa UN ichukua hatua Uagizaji huu umelezwa kwa barua kumi na moja uadishi wa Rais

Kifungu chenyewe Eneo za Eritrea
Eritrea Mgao Eneo

Kati Maekel
Anseba
Kisini ziwa lekundu DebubawiKeihBahri
Kaskazini ziwa lekundu SemienawiKeihBahri
Kusini Debub
GashBarka

Eritrea
Kifungu chenyewe Jiografia ya Eritrea

Eritrea iko kwa eneo la Pembe la Afrika na imepakana na Bahari ya Shamu kaskazini mashariki Kwa mchanga wa pwani uliyo Eneo Kame pahali pa kutega samaki ni Dahlak Achipelago Eneo ambayo iko kwa milima kusini si kame vile lakini hali ya hewa ni poa Mlima juu zaidi ni Soira ambao huko kati ya Nchi Eritrea m Juu ya bahari

Mji mkuu wa Eritrea ni Asmara na miji mingine ni kama mji wa bandari Assab kusini mashariki na pia miji kama Massawa na Keren

Kifungu chenyewe Uchumi wa Eritrea

Nchi za Afrika
Bahari ya Shamu

thumb

Umoja wa Mataifa UM ni umoja wa nchi karibu zote duniani ulianzishwa mwaka na nchi washindi wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia Umoja huu ulianzishwa na nchi na kufikia mwaka kuna nchi ambazo ni wanachama wa umoja huu Dhumuni la umoja huu ni kuratibu mahusiano ya kimataifa kupitia sheria na mikataba ya kimataifa kwenye maeneo kama usalama amani maendeleo ya jamii haki za binadamu nk

Makao makuu ya Umoja wa Mataifa yako New York nchini Marekani

Umoja huu ulichukua nafasi ya Shirikisho la Mataifa

Nchi za pekee zisizo wanachama wa UM ni Dola la Vatikano lililokataa uanachama Palestina ambayo haijatangaza hali ya dola la kujitegemea bado na Taiwan isiyotambuliwa kuwa nchi ya kujitegemea bali sehemu ya Uchina

Katibu Mkuu wa UM ni Ban Kimoon kutoka Korea ya Kusini Ban Kimoon alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu mwaka akachukua nafasi ya Kofi Annan

UM una vyombo sita
Mkutano Mkuu wa UM United Nations General Assembly
Baraza la Usalama la UM United Nations Security Council
Ofisi Kuu ya UM United Nations Secretariat
Mahakama Kuu ya Kimataifa International Court Of Justice
Baraza la Uchumi na Ustawi wa Jamii la UM ECOSOCEconomic And Social Council

Baraza la Wafadhili la UM Trusteeship Councilimesimamisha kazi yake

UNICEF United Nations Childrens Fund
WHO World Health Organization
FAO Food and Agriculture Organization
UNESCO United Nations Educational Scientific and Cultural Organization Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni
ILO International Labour Organization
IMF International Monetary Fund

UNCTAD United Nations Conference on Trade and Development
ITC International Trade Centre UNCTADWTO
UNDCP United Nations Drug Control Programme
UNDP United Nations Development Programme
UNIFEM United Nations Development Fund for Women
UNV United Nations Volunteers
UNEP United Nations Environment Programme
UNFPA United Nations Fund for Population Activities
UNHCR Office of the United Nations High Commissioner for Refugees
UNHABITAT United Nations Human Settlements Programme
UNRWA United Nations Relief and Works Agency for Palestine Refugees in the Near East

IAEA Shirika la Kimataifa la Nishati ya Nyuklia inashirikiana na UM na kutoa taarifa mbele ya Baraza la Usalama hata kama si chini ya katiba ya UM

UNDIO United Nations Data and Information Organization

United Nations tovuti rasmi
UN Works
UN Chronicle Magazine
About the United Nations
United Nations Charter Charter text
United Nations Security Council Resolutions
United Nations Webcasts
United Nations Volunteers
Universal Declaration of Human Rights
UN Organisation Chart
Global Issues on the UN Agenda
World Map of UN websites and locations
Journal of the United Nations Programme of meetings and agenda
Highlevel Panel on United Nations Systemwide Coherence
The United Nations Regional Information Centre UNRIC


Mashirika ya kimataifa

Uchoraji kwenye mwamba kwenye mapango karibu na Kondoa Tanzania
Uchoraji ni sanaa ya kupaka rangi kwenye uso wa karatasi kitambaa ubao metali mwamba au penginepo Tokeo la uchoraji huitwa picha

Ni sanaa wakilishi inayotumika kuwakilisha ujumbe kwa jamii kuna aina tofauti za uchoraji

Hii inategemea na mchoraji mwenyewe anapenda aina gani ya uchoraji pia wakati mwingine sanaa hii ya uchoraji si kuwakilisha ujumbe tu pia kumvutia mtamzamaji kwa rangi za kupendeza bila kujali ujumbe uliobebwa na picha hiyo au wakati mwingine inawezekana picha isiwe na ujumbe kabisa lakini ikawa imechorwa kwa ustadi mkubwa na kupakwa rangi za kuvutia sana

Uchoraji wa Misri ya Kale Kaburi la Nakht

Picha za kale kabisa zinaonyesha uchoraji kwenye miamba katika mapango Katika Afrika ni Wasan au watu waliokuwa karibu nao waliochora wanyama kwenye kuta za mipango walipopumzika Picha zao zinapatikana kote katika Afrika ya Kusini hadi Tanzania ambako kuna mifano mbalimbali karibu na Kondoa Mifano ya uchoraji wa aina hii imepatikana pia Ulaya Asia na Australia

Hatujui mengi kuhusu namna nyingine za uchoraji wa kale kwa sababu vifaa vingine vilivyotumiwa havikudumu

Kutoka tamaduni ya juu kama Misri bonde la Indus au China tunajua mifano mingine ya uchoraji inayoonyesha hali ya juu zaidi Katika ustaarabu wa madola ya kwanza wachoraji walikuwa tayari watu waliokuwa na nafasi ya kufuata sanaa yao bila haja ya kuwinda au kulima wenyewe kwa sababu mtu mkubwa kama mfalme au kuhani aliwapa ridhiki ya maisha

Katika makaburi ya NubiaUfalume wa Kush kuna picha zilizohifadhiwa ukutani Makaburi ya Wamisri yalijengwa mara nyingi kwenye jangwa kando la bonde la Naili Ukavu wa mazingira pamoja na giza ulitunza rangi vema Wamisri wa Kale walichora watu bila kutofautisha mandharimbele au mandharinyuma Wati muhimu waliochorwa wakubwa kuliko wale waliokuwa na cheo kidogo Mwili ulionyeshwa mara nyingi kwa mbele lakini kichwa na uso kwa kando

Katika Ugiriki ya Kale uchoraji na wasanii wake uliheshimiwa sana Philostrates aliandika mnamo mwaka KK ya kwamba uchoraji ulibuniwa na miungu Kuna taarifa juu ya picha lakini ni machache tu yaliyohifadhiwa kwa sababu ya hali ya hewa na kwa sababu picha nyingi zilichorwa juu ya ubao au matofali

Waroma wa Kale walituachia mifano mingi ya uchoraji wa ukutani nje ya makaburi ni hasa nyumba za miji Pompei na Herkulaneo zilizofunikwa na majivu ya volkeno Vesuvio ambako picha nzuri zimehifadhiwa tangu mwaka BK Wakati ule wasanii walitofautisha tayari kati ya mandharimbele na mandharinyuma

Uchoraji wa China uliendelea sana kufuatana na utamaduni wake mnamo mwaka kuna picha za mandhari zinazoonyesha nchi na milima msanii wa kwanza anayejulikana alitumia mbinu huu alikuwa Zhan Ziqian

Sanaa

Kamusi elezo pia ensiklopedia ni kitabu kinachojaribu kukusanya ujuzi wote wa ubinadamu Siku hizi Wikipedia ni kamusi elezo kubwa zaidi duniani Zamani kabla ya uumbaji wa Wikipedia Encyclopedia Britannica ilikuwa kati ya kamusi elezo kubwa zaidi duniani

Katika historia zilikuwepo majaribio mbalimbali kukusanya ujuzi wote wa dunia Mfano bora wa kale ni kamusi ya Yongle kutoka China iliyotungwa karne ya na wataalamu na kundikwa kwa mkono katika vitabu

Lakini kamusi elezo au ensiklopedia zilikuwa na athari kubwa sana tangu Johannes Gutenberg na kupatikana kwa uchapisho vitabu iliyoshusha kabisa bei ya vitabu kwa watu wengi

Ensiklopedia ya kwanza ya kisasa iliyokuwa na athira kubwa sana ilikuwa Encyclopdie ou Dictionnaire raisonn des sciences des arts et des mtiers ya Denis Diderot pamoja na Jean Baptiste le Rond dAlembert pamoja na waandishi zaidi ya katika karne ya Kamusi elezo hili likawa kati ya vyanzo vya harakati ya Zama za Nuru

Ellen JohnsonSirleaf

Ellen JohnsonSirleaf alizaliwa Oktoba nchini Liberia amekuwa rais wa kwanza mwanamke barani Afrika baada ya kushinda katika uchaguzi wa mwaka JohnsonSirleaf ameshika nyadhifa mbalimbali serikalini na katika mashirika ya kimataifa Baada ya kumaliza masomo katika chuo kikuu cha Harvard alifanya kazi katika serikali ya Rais William Tolbert mwaka wa akiwa ni Waziri wa Fedha

Johnson amekuwa Rais wa kwanza mwanamke barani Afrika Hata hivyo yeye sio mwanamke wa kwanza kuongoza nchi barani Afrika Malikia Zauditu wa Ethiopia aliongoza nchi yake kwa miaka toka mwaka hadi Ruth Perry ni mwanamke wa kwanza Afrika kuwa mkuu wa nchi pale alipokuwa mwenyekiti wa urais wa pamoja wa jamhuri ya Liberia toka mwaka hadi

JohnsonSirleaf alihukumiwa kifungo cha miaka kumi jela mwaka baada ya kushutumu utawala wa kijeshi nchini humo katika kampeni zake za kugombea ubunge Alitumia kifungo hicho kwa muda mfupi kabla ya kuachiliwa na baadaye kukimbilia uhamishoni hadi aliporudi mwaka akiwa anafanyia kazi Benki ya Dunia na Citibank

JohnsonSirleaf alimuunga mkono Charles Taylor wakati wa mapinduzi yake dhidi ya Jenerali Samuel Doe lakini baadaye alikuja kuwa mpinzani wake mkubwa na hata kugombea urais dhidi yake mwaka Taylor alimwandana na hata kumpeleka mahakamani kwa madai ya kuhusika na hujuma za kihaini

Uchaguzi wa urais mwaka ulirudiwa baada wagombea urais kutopata kura za kutosha Katika raundi ya kwanza JohnsonSirleaf alikuwa wa pili wa kwanza alikuwa ni mpinzani wake mkubwa George Weah Katika raundi ya pili ya uchaguzi JohnsonSirleaf alitangazwa kuwa mshindi Hata hivyo George Weah amepeleka mashtaka mahakama kuu akidai kuwa uchaguzi haukuwa wa haki

Ellen Johnson Sirleaf alizaliwa mjini Monrovia mji mkuu wa Liberia na elimu ya wazazi Kabila lake ni nusu Gola kutoka upande wa baba yake na robo Kru na robo Kijerumani kutoka upande wa mama yake
Babake Sirleaf Jahmale Carney Johnson alikuwa mzaliwa wa Liberia wa kwanza kuweza kukaa katika mbunge la taifa
Sirleaf alisoma maswala ya uchumi na akaunti katika Chuo Afrika Magharibi mjini Monrovia Aliolewa na James Sirleaf akiwa na miaka tu na kuhamia Marekani katika mwaka wa ambapo aliendelea na masomo yake katika chuo kikuu cha Colorado na kuhitimu na shahada ya digri Alisomea maswala ya uchumi na sera za umma katika chuo Chuo Cha Maswala Ya Serikali ya John F Kennedy mjini Harvard katika miaka ya na na kupata shahada ya maswala ya serikali Kisha alirudi Liberia na kufanya kazi chini ya rais William Tolbert
Alikuwa naibu waziri wa fedha kati ya mwaka wa na Alikuwa waziri wa fedha toka mwaka wa hadi Aprili
Aliweza kuwa naibu mwenyekiti wa benki ya CitiBank mjini Nairobi Kenya kutoka mwaka wa Aliwahi kufungwa mafungo ya nyumbani na Samule Doe aliyepindua serikali kwa kutangaza nia ya kugombea urais
Baadaye alienda uhamishoni
Kati ya miaka ya alikuwa makamu wa rais na mwanachama wa bodi ya benki ya Equator Washington DC Kati ya miaka ya alikuwa mbunge wa bodi ya wakurugenzi wa Taasisi ya Synergos ALigombea urais kwa tiketi ya chama ya maunganoUnity Party katika mwaka wa na kuwa

Ndiye rais wa sasa wa Liberia Alimshinda alikuwa mwanasoka mashuhuri George Weah na zaidi ya asilimia ishirini katika uchaguzi wa mwaka wa Uzinduzi ulifanyika tarehe Januari na ulihudhuriwa na wageni mashuhuri wakiwemo aliyekuwa waziri ya maswala ya kigeni wa Marekani Condeleeza Rice Laura Bush na Mitchelle Jean
Katika mwaka wa alianzisha tume ya ukweli na maridhiano ambayo ilitoa ripoti yake katika mwaka wa

Naibu Waziri wa Fedha wa Liberia
Waziri wa Fedha wa Liberia
Makamu wa Rais wa Kanda ya Afrika Ofisi ya Citibank Nairobi
Makamu wa Rais na mwanachama wa bodi ya beni ya Ikweta Washington DC
Mbunge wa bodi ya wakurugenzi wa Taasisi ya Synergos
Mkurugenzi wa Mpango wa Maendeleo ya Umoja wa mataifa Ofisi za bara Afrika
Rais mgombea wa chama cha UmojaUnity Party
Mwenyekiti wa Tume ya Mageuzi ya Utawala Bora
Mgombea urais kwa tikiti ya chama ya umoja
hadi leo Rais wa Liberia

Mwanachama mwanzilishi wa Taasisi ya Kimataifa kwa Wanawake katika uongozi wa kisiasa
Mwanachama wa bodi ya ushauri wa kisasa wa Kukuza Uchumi na Uwekezaji Afrika Kampuni
Afisa mwandamizi wa mkopo wa Benki ya Dunia

Liberia

George Weah ni mwanakandanda mashuhuri duniani na mwanasiasa aliyegombea urais wa Liberia mwaka Weah alizaliwa Oktoba katika jiji la Monrovia Alikulia katika kitongoji cha masikini cha Clara Kabla ya kujiunga na soka la kulipwa Weah alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Mawasiliano la Liberia kama fundi simu

Kielimu Weah ana Shahada ya Kwanza ya Uendeshaji Michezo toka Chuo Kikuu cha Parkwood Londo Uingereza Mwkaa alipata shahada ya Udakitari ya Heshima toka Chuo Kikuu cha AME Zion nchini Liberia

Mwaka Weah alipewa tuzo na Shirikisho la Soka Duniani FIFA kuwa Mwanasoka Bora Duniani Yeye ni mwanasoka pekee toka Afrika aliyewahi kupewa tuzo hiyo Mwaka huo huo alichaguliwa pia kuwa Mwanasoka Bora Ulaya na Mwanasoka Bora Afrika

Weah alianza safari yake ya soka katika timu ya Liberia ya Incincible Eleven na Tonnerre Yaounde ya Cameroon Baada ya hapo alikwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya mwaka Alijiunga na timu ya Monaco ambapo aliiongoza kushinda kombe la Ufaransa mwaka Baadaye alijiunga na Paris Saint Germain mwaka Aliiongoza timu hii kuchukua kombe la ligi ya Ufaransa mwaka Mwaka alikuwa akiichezea timu ya AC Milan ambayo ilishinda ligi ya Italia mwaka na Mwaka aliondoka AC Milan na kujiunga na Chelsea baada ya muda mfupi alijiungana Manchester City na baadaye Marseille mwaka Alimaliza soka la kulipwa akiwa na timu ya Al JAzira ya Falme ya Nchi za Kiarabu

Weah amekuwa akitoa misaada kusaidia wananchi wa Liberia Mwaka alipewa tuzo ya Arthur Ashe kwa juhudi zake za kusaidia kujenga nchi yake

Liberia
Wachezaji Mpira wa Afrika ya Magharibi

Monrovia ni mji mkuu wa Liberia Eneo uliko mji huu mwanzoni liliitwa Cape Mesurado na Wareno katika miaka ya Eneo hili lilianzwa kujenga mji mwaka na chama cha
American Colonization Society ikiwa ni makazi ya watu waliokombolewa toka utumwani nchini Marekani Jina Monrovia lilitokana na jina la Rais wa Marekani James Monroe Kwa mujibu wa sensa ya mwaka Mji huu una wakazi wapatao

Uchumi wa Monrovia unategemea zaidi bandari yake na madini ya chuma Bidhaa kama vile saruji mafuta matofali vigae samani na kemikali zinatengenezwa Monrovia

Wakati mabaharia Wareno walipowasilia Monrovia na kuuita mji huu Cape Mesurado tayari kulikuwa na wakazi wakiishi hapo Watu wa kwanza kuhamia Monrovia toka nchini Marekani waliwasili mwaka katika Kisiwa cha Sherboro nchini Sierra Leone Wahamiaji wengi walifariki baada ya kuwasili Monrovia

Mkutano wa kutunga katiba ya Liberia wa American Colonization Society ulifanyikia Monrovia mwaka

Liberia
Miji ya Liberia
Miji Mikuu Afrika

Ngoma djembe
Ngoma inaoweza kumaanisha muziki unaochezwana na ala ya muziki inayoitwa ngoma pia

Ngoma ni muziki na lugha ya pekee inayotumika kwa kuelezea utamaduni na historia ya nchi fulani tunatumia lugha ya ngoma katika kuelezea hali mbalimbali za maisha yetu kama vile huzuni furaha mapenzi kutia moyo vitisho shukurani na ushindi

Babu zetu walikuwa na lugha hii ya ngoma ambayo tumeirithi kwa mapokeo Ngoma pia ilitumika na jamii mbalimbali kama njia ya kuita watu kwenye kusanyiko muhimu kama vile vita mikutano nk ilipigwa kwa milio tofauti kulingana na tukio

Ala za muziki

Bombwe ni sanaa ya urembo wa kuchora mwilini kama kuchora kwa hina na kuchora kwa piko sanaa hii hutumika zaidi na wanawake
Vile vile ni kiumbe anayeishi kwenye maji baridi ama ya chumvi hasa sehemu za bahari zilizoingia ndani ya ardhi ambako pia kuna makutano na maji baridi

Sanaa

Togwa ni kinywaji baridi kinachotengenezwa kwa nafaka au maji ya matunda Namna ya kutengeneza ni sawa na pombe ya kawaida ila tu haikubadilika bado kuwa na alikoholi

Togwa ndiyo itakuwa pombe ikikaa Kwa mfano togwa ya ulanzi ni utomvu kutoka mianzi baada ya masaa kadhaa na ulanzi wenye pombe ni utomvu uleule kutoka mianzi baada ya siku mbili hivi

Nafaka zinazotumika kutengenezea zaidi huwa ni mtama au mahindi

Chemsha mtama mpaka uive kama uji halafu uvumbike kwa siku mbili tia sukari ni tayari kwa kunywewa

Vinywaji

Liberia ni nchi iliyoko Afrika ya Kaskazini Imepakana na nchi za Ivory Coast Guinea na Sierra Leone

Liberia ni nchi iliyoundwa na makabila mbalimbali ya asili nchini humo na wahamiaji weusi toka Marekani Wamarekani Weusi hawa walikuwa ni watumwa waliopata uhuru ambao kwa kushirikiana na chama cha American Colonization Society waliunda taifa hili na kutangaza uhuru wa nchi hiyo Julai Wamarekani Weusi hawa waliichukulia nchi hiyo kama nchi ya ahadi kutokana na asili yao kuwa ni Afrika ambako ndiko mababu zao walikotokea kabla ya kupelekwa utumwani Marekani Hata hivyo wahamiaji hawa waliendelea kujitambulisha kama Wamarekani na hawakujenga mahusiano ya karibu na wenyeji

Alama za taifa hili bendera kauli mbiu na nembo ya taifa na hata muundo wa serikali vilikuwa vikionyesha mahusiano ya karibu kati ya nchi hizi mbili

Liberia imekuwa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya mwaka na Hivi karibuni imefanya uchaguzi uliofanyika kwa amani na kuweza kumchagua mwanamke wa kwanza kuwa Rais barani Afrika Ellen JohnsonSirleaf

Serikali ya Liberia


Nchi za Afrika

Mwai Kibaki ni rais wa tatu wa Jamhuri ya Kenya akiwa ametanguliwa na Rais wa Kwanza wa KenyaMzee Jomo Kenyatta na Daniel Arap Moi Jina lake la kubatizwa ni Emilio Stanley

Kibaki alisoma uchumi historia na sayansi ya siasa katika chuo kikuu cha Makerere Kampala Uganda Akiwa mwanafunzi Makerere Kibaki alikuwa ni mwenyekiti wa chama cha wanafunzi toka Kenya Kenya Students Association Alipomaliza masomo yake mwaka alipewa tuzo kutokana na kufanya vyema katika mitihani Tuzo hiyo ilimwezesha kwenda kusoma katika chuo cha London School of Economics Alipomaliza masomo alikwenda kufundisha katika chuo kikuu cha Makerere Baadaye aliacha kazi ya kufundisha na kuwa mtendaji mkuu wa chama cha Kenya African National Union

Kibaki licha ya kuwa mbunge amewahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha Mwenyekiti wa Tume ya Mipango Waziri wa Biashara na Viwanda na Waziri wa Fedha Moi alipoingia madarakani baada ya kifo cha Jomo Kenyatta Kibaki aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais

Mwaka Kibaki alianza kuwa na mgongano na Rais Moi Mwaka huo alivuliwa Umakamu wa Rais na kupelekwa Wizara ya Afya

Mwaka Kibaki aliondoka chama cha KANU na kuanzisha chama cha Democratic Party Katika uchaguzi wa Urais wa mwaka Kibaki alikuwa wa tatu na mwaka alikuwa wa pili

Katika uchaguzi wa Kibaki alishinda na kutangazwa kuwa Rais wa Kenya Alikuwa mgombea wa maungano wa vikundi vingi vya upinzani vilivyoshirikiana kwa jina la NARC

Kibaki ameweka historia mwezi Novemba baada ya kuwa Rais wa kwanza nchini Kenya kuondoa baraza lote la mawaziri kufuatia kura ya maoni ambayo ilikuwa inahusu katiba mpya ya Kenya Kibaki alikuwa upande wa kundi lililokuwa likiunga mkono katiba hiyo kambi ya ndizi Kundi lililokuwa likiipinga katiba hiyo kambi ya machungwa lilipata ushindi

Uchaguzi wa Desemba ulimrudisha Kibaki kwa kipindi cha pili kama rais Uchaguzi huu ulipingwa na chama cha upinzaniODM na watazamaji wa kimataifa kuwa matokeo hayo hayakuwakilisha matakwa ya Wakenya Mpinzani wake mkuu Raila Odinga alikuwa mbele katika hesabu za kura hadi Kamati ya Uchaguzi iliposimamisha kuhesabu baada ya kuendelea na matanganzo Kibaki alionekana kuwa mbele Kulikuwa na hofu ya kwamba matokeo ya majimbo ya uchaguzi kadhaa yalibadilishwa yakiegemea upande wake kwa kumwongezea kura Hisia hizi zilisababisha ghasia kuibuka Nairobi Kisumu Eldoret Kericho Mombasa na sehemu zinginezo nchini Kibaki aliapishwa upya kuwa rais wa Kenya masaa machache tu baada ya kutangazwa kuwa mshindi hafla ilifanywa katika Bustani ya Ikulu ya Nairobi mbele ya waalikwa wachache walioruhusiwa kushuhudia

Kamati iliyobuniwa tutathmini ukweli wa mambo katika uchaguzi huo wa urais iliyoongozwa na jaji mstaafu kutoka Africa Kusini Johann Kriegler iliripoti kwamba mshindi katika uchaguzi huo wa urais wa hangeweza kujulikana Hii ni kwa sababu wizi wa kura ulifanyika katika sehemu nyingi nchini na ulitekelezwa kule mashinani na wafuasi wa wapinzani wote katika kinyanganyiro cha Urais Kriegler pia alielekeza lawama kwa Tume ya Uchaguzi ya Kenya kwa kutowajibika katika utendakazi na ripoti hiyo ya Krieger ilipendekeza tume hiyo ivunjwe na ibadilishwe na ingine iliyo huru

Kinyume cha uchaguzi wa rais uchaguzi wa Bunge la Kenya uliendelea bila matatizo makubwa

Baada ya kutangazwa kuwa rais mpya Kibaki aliteua mawaziri kama awamu ya kwanza ya serikali akiacha nafasi nyingine serikalini kando kwa muda
Makamu wa Rais na waziri wa mambo ya ndani Stephen Kalonzo Musyoka
Waziri wa utawala wa mikoa na usalama wa ndani katika Ofisi ya Rais George Saitoti
Waziri wa ulinzi katika Ofisi ya Rais Yussuf Mohamed Haji
Waziri wa mipango maalumu katika Ofisi ya Rais Dr Naomi Namsi Shaban
Waziri wa utumishi wa serikali katika Ofisi ya Rais Asman Abongotum Kamama
Waziri wa fedha Amos Muhinga Kimunya
Waziri wa elimu Sam Ongeri
Waziri wa mambo ya nje Moses Wetangula
Waziri wa serikali ya mitaa Uhuru Kenyatta
Waziri wa habari na mawasiliano Samuel Lesuron Poghisio
Waziri wa maji na umwagiliaji John Munyes
Waziri wa nishati Kiraitu Murungi
Waziri wa barabara na kazi za umma John Njoroge Michuki
Waziri wa sayansi na teknolojia Noah M Wekesa
Waziri wa sheria na mambo ya katiba Martha Karua
Waziri wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki Dr Wilfred Machage
Waziri wa usafiri Chirau Ali Mwakwere

The Kibaki Legacy EAStandard juu ya Kibaki kabla ya uchaguzi

Wanasiasa wa Kenya
Marais wa Kenya
Waliozaliwa
Watu walio hai

Kura ya maoni zinatumika katika demokrasia ili kuchagua viongozi wa nchi au kuamua kama sheria fulani itumike Kawaida kura ya maoni hupigwa na wale wote wenye umri halali wa kupiga kura ili kukubali au kukataa pendekezo sera sheria mabadiliko ya katiba katiba mpya kukataa au kumuunga mkono kiongozi fulani Kura ya maoni huchukuliwa kuwa ni aina mojawapo ya demokrasia ya moja kwa moja

Siasa

Demokrasia ya moja kwa moja ni aina ya demokrasia ambayo wananchi wote wanaweza kushiriki katika kuamua masuala ya kisiasa kijamii kisheria na kiuchumi bila kutumia chombo cha uwakilishi kama vile bunge

Uwezo huu wa wananchi kutoa maamuzi unaweza kuwapa wananchi hata uwezo wa kimahakama ingawa mara nyingi wananchi hupewa uwezo wa kutunga au kupitisha sheria tu

Muundo wa demokrasia ya asili uwezo huu wa kutunga au kupitisha sheria na kupitisha maamuzi ulikuwa uko mikononi mwa wananchi wenyewe na sio wawakilishi wao
Kutegemeana na mfumo wenyewe wa demokrasia ya moja kwa moja wananchi huwa wana uwezo wa kutunga sheria kupitisha sera kuwaweka madarakani na pia kuwaondoa madarakani viongozi

Demokrasia ya moja kwa moja ni tofauti na demokrasia inayofuatwa katika nchi nyingi duniani hivi sasa ambapo wananchi huchagua wawakilishi wao katika uchaguzi

Siasa

Bunge ni chombo cha kutunga sheria na pia ni mmoja wa mihimili mitatu inayounda mfumo wa utawala kulingana na mfumo wa mgawanyo wa madaraka Mihimili mingine ni mahakama na serikali

Bunge ni chombo kinachotokana na mfumo wa utawala wa Westminster Mfumo huu ambao umerithiwa na nchi nyingi duniani umetoka nchini Uingereza Kutokana na mfumo huu kutoka nchini Uingereza mara nyingi Bunge la Uingereza huitwa Mama wa Bunge duniani Bunge la kwanza nchini Uingereza liliundwa wakati wa utawala wa Mfalme Henry III katika karne ya Bunge hilo lina sehemu mbili Bunge la Makabwela na Bunge la Mabwanyeye

Katika nchi nyingi zinazofuata mfumo wa Westminster Waziri Mkuu huwa ndio kiongozi mkuu wa serikali bungeni

Shughuli za bunge husimamiwa na mbunge aliyechaguliwa kuwa mwenyekiti wake akiwa na vyeo kama mwenyekiti rais aus spika wa bunge

Orodha ya Wabunge wa Tanzania

Bunge la Tanzania
Bunge la Afrika Kusini
Bunge la Umoja wa Afrika
Bunge la Ghana
Bunge la Uingereza
Bunge la Ulaya

Siasa

Mahakama ni mfumo wa wataalamu na kamati maalumu ambao unatafsiri na kutumia sheria katika jina la wananchi la jamhuri au la mfalme

Mahakama pia inatoa mfumo wa kutatua migogoro Chini ya mfumo wa mgawanyo wa madaraka mahakama kwa ujumla haitungi wala haiundi sheria ambayo ni kazi ya bunge wala kutekeleza sheria ambayo ni wajibu wa serikali bali inatafsiri sheria na kutumia na kutekeleza katika ukweli wa kila kesi

Mahakama ina kazi ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria kwa watu wote

Kwa kawaida kuna mahakama za ngazi mbalimbali mahakama za juu zinapokea rufaa dhidi ya kesi za ngazi za chini hadi mahakama ya rufaa ya mwisho inayoitwa mahakama kuu au mahakama ya katiba Tawi hili la mahakama lina uwezo wa kubatilisha sheria zisizolingana na katiba ya nchi

Neno mahakama pia hutumika kumaanisha kwa pamoja maafisa ndani yake kama vile majaji mahakimu na makarani wengine

Kimsingi mahakama ina kazi ya kutumia sheria zilizopo na kuamua juu ya matumizi yao Hali halisi sheria haziwezi kutaja kila kitu kinachoweza kutokea hivyo ni mahakama zinazoamua kwa njia ya kulinganisha kesi sheria na maazimio ya mahakama yaliyotangulia

Kwa hiyo mahakama zinashiriki kiasi katika kazi ya kutunga haki hasa pale ambako sheria za bunge zinaacha pengo

Kidesturi muundo wa haki na sheria katika Uingereza na Marekani unaziachia mahakama nafasi kubwa zaidi kuendeleza tratibu za kisheria

Mgawanyo wa madaraka
Serikali
Bunge

Cardozo Benjamin N mwaka wa The Nature wa mchakato wa kimahakam New Haven Yale University Press
Feinberg Kenneth Jack Kress Gary McDowell na Warren E Burger The High Cost and Effect of Litigation matoleo
Frank Jerome Law and the Modern Mind Birmingham AL Legal Classics Library
Lawi Edward H An Introduction to Legal Reasoning Chicago University of Chicago Press
Marshall Thurgood Thurgood Marshall His Speeches Writings Arg maoni na Reminiscences Chicago Lawrence Hill Books
McCloskey Robert G na Sanford Levinson The American Supreme Court toleo la Chicago University of Chicago Press
Miller Arthur S PoliticsDemocracyand the Supreme CourtEssays on the Future of Constitutional Theory Westport CT Greenwood Press
Tribe Laurence God Save This Honorable Court How the Choice of Supreme Court Justices Shapes our History New York Random House
Zelermyer William The Legal System in Operation St Paul MN West Publishing

Sheria


Katiba ni sheria au kanuni zinazoanisha jinsi ambavyo nchi chama au shirika vitakavyoendesha shuguli zao Kwa upande wa nchi katiba ni sheria mama inayoainisha misingi mikuu ya kisiasa na kuonyesha madaraka na majukumu ya serikali Katiba za nchi pia huanisha haki za msingi za wananchi
Constitution laws

Siasa
Sheria

Upungufu wa Kinga Mwilini UKIMWI kifupi cha Kiingereza AIDS ni ugonjwa unaotokana na virusi vinavyoshambulia mwili kwa kuondoa nguvu za mwili kupambana na magonjwa Ugonjwa huu umeua watu zaidi ya milioni hasa wanaoishi Kusini mwa Afrika kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani Kwa mwaka pekee watu milioni wamefariki na kati ya hao ni watoto Ukimwi hadi hivi sasa hauna dawa

Tarehe kwanza mwezi kumi na mbili kila mwaka ni siku ya Ukimwi duniani

Tovuti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Ukimwi UNAIDS
HIV InSite
sidafr un centre pour les malades du SIDA infos tmoingnages actualits

Ukimwi
Magonjwa

Desemba ni mwezi wa kumi na mbili katika kalenda ya Gregori na ni kati ya miezi saba katika kalenda hiyo yenye siku Neno Desemba limetokana na neno la Kilatini decem linalomaanisha kumi Desemba ulikuwa ni mwezi wa kumi katika kalenda ya Kirumi

Miezi
Kalenda

Mimea
Mimea ni moja ya kundi la viumbe hai duniani ikijumuisha miti maua mitishambank Kuna zaidi ya aina ya mimea

Sayansi inayochunguza mimea huitwa botania ni kitengo cha biolojia Kwenye uainishaji wa kisayansi Mimea hujumlishwa katika himaya ya planta kwenye milki ya Eukaryota

Kwa jumla mimea huwa na uwezo wa usanisinuru yaani hujilisha kwa msaada wa nuru

FileBorassus flabelliferjpgBorassus flabellifer
FileGntTaatiFruitjpgThe fruits of Palmyra Palm tree Borassus flabellifer locally called Thaati Munjelu sold in a market at Guntur India
FileTurmericrootjpgTurmeric rhizome
FileStarr Ipomoea batatasjpgSweet potato Ipomoea batatas Maui Nui Botanical Garden
FilePandan wangiJPGPandanus amaryllifolius
FileCalifornia Papaya IDjpgCalifornia Papaya
FilePapaya sunsetjpgCarica papaya cultivar Sunset
FilePrepared lemon grassJPGCymbopogon citratus lemon grass oil grass
FileBangkuang stgdjpgPachyrhizus erosus bulbroot Situgede Bogor West Java Indonesia
FileKIKU brakontreeJPGFuji apple
FileSauropusAndrogynusjpgSprouting shoots of Sauropus androgynus
FileIlaneerjpgCocos nucifera


Mimea

Mipango miji ni sayansi na sera kuhusu maendeleo ya kijamii kiuchumi kimazingira katika miji na vitongoji vyake Mgiriki Hippodamus anasemekana kuwa ndiye baba wa mipango miji kutokana na ubunifu wake wa mji wa Miletus ingawa kumekuwa na miji iliyopangwa kabla yake

Taaluma ya mipango miji imechipuka toka kwenye taaluma za usanifu majengo na uhandisi

Miji
Ujenzi
Sayansi ya Jamii

Internet Relay Chat IRC ni aina ya mawasiliano ya papo kwa hapo kupitia mtandao wa Intaneti Teknolojia hii imeundwa hususan kwa ajili ya mawasiliano ya watu wengi kwa wakati mmoja lakini pia mawasiliano ya mtu mmoja kwa mmoja yanawezekana

Teknolojia hii ilitengenezwa na Jarkko Oikarinen Agosti ili kuchukua nafasi ya teknolojia nyingine kama hii iliyokuwa ikiitwa MUT huko Ufini

IRC ilipata umaarufu pale ilipotumika kuripoti jaribio la kuipindua serikali ya Urusi mwaka Teknolojia hii ilitumiwa pia kuripoti uvamizi wa Kuwait na nchi ya Iraki

Tovuti ya IRC

Intaneti

Blogu za mkononi ni aina ya blogu zinazotumia zana zinazoshikika mkononi kama vile simu za mkononi Kwahiyo habari maoni au visa vinatolewa katika mtandao wa kompyuta kwa kutumia zana hizi Teknolojia hii ilianza huko Japan ambapo simu za mkono zenye kamera zilianza kupatikana kwa urahisi

Inasemekana utumaji wa habari kwenye mtandao wa kompyuta toka katika zana za mkononi ulifanywa na Steven Mann hapo mwaka alipotumia kompyuta inayovalika Mwaka ndipo utumaji wa habari katika mtandao wa kompyuta toka katika simu ya mkono ulifanywa na Tom Paamand nchini Udeni

Adam Greenfield ndiye aliyeanzisha matumizi ya neno blogu za mkononi Aliandaa Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Blogu za Mkononi jijini Tokyo Japani mwaka

Teknolojia
Blogu
Uandishi wa Raia

Paul Simon
Paul Simon ni mwanamuziki wa country anaimba na kupiga gitaa Amewahi kushirikiana na wanamuziki wengi moja ya makundi hayo ni Ladysmith Black Mambazo Nyimbo alizowahi kuimba ni Homeless Mother and child reunion na Diamond in the sole of her shoes

Paul Simon alizaliwa tarehe Oktoba katika mji wa Newark Height New Jersey Huko alifahamika kama muimbaji na mtunzi mwenye asili ya kiyahudi Aliwahi kufunga ndoa mara tatu ana watoto wanne Mmojawapo ni mpigaji gitaa kama baba yake

Waliozaliwa
Wanamuziki wa Marekani
New York City

Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa ya Tanzania ikipakana na Zambia na Malawi halafu na mikoa ya Rukwa Tabora Singida na Iringa

Kuna wilaya zifuatazo Mbeya Mjini Mbeya Vijijini Rungwe Kyela Ileje Mbozi Chunya na Mbarali

Mbeya ni kati ya maeneo yanayopendeza kabisa ndani ya Tanzania ikiwa na sehemu za Ziwa la Nyasa Ziwa Rukwa milima ya Mbeya milima ya Rungwe Uwanja wa juu wa Uporoto Uwanja wa Usangu ingawa haukufikiwa bado na utalii

Wenyeji wa wilaya ya Chunya ni Wabungu na waishio huko zaidi ni Wanyiha

Wilaya ya Rungwe ni eneo penye mvua nyingi katika Tanzania Mkoa wa ujumla ni mojawapo kati ya mikoa yenye kilimo kizuri inayotoa mazao ya kulisha taifa Lakini maeneo makubwa ya Wilaya ya Chunya ni makavu

Wilaya ya Chunya ina madini mbalimbali hasa dhahabu
Mbeya na Mbozi kahawa hupandwa Rungwe pana chai nyingi pamoja na Rungwe na Chimala hulimwa mpunga Nyanda za juu kuna nafaka na viazi

Kijiolojia mkoa wa Mbeya ni eneo la kukutana kwa mikono miwili ya Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki inayoendelaea hapa katika ziwa Nyasa

Mkoa wa Mbeya inapakana na maziwa mawili makubwa ndiyo Ziwa Nyasa na Ziwa Rukwa Hasa milima yenye asili ya volkeno ya wilaya ya Rungwe inyajaa maziwa ya kasoko

Mito mikubwa ni Songwe na Kiwira Chanzo ya mto Ruvuma iko pia Mbeya katika tambarare ya Usangu

Mbeya Region Socioeconomic Profile katika TZOnline

M


Ladysmith Black Mambazo
Ladysmith Black Mambazo ni kundi la muziki ambalo linaimba bila kutumia ala za muziki Kundi hili lipo Afrika ya Kusini Neno Mambazo linamaanisha shoka kwa Kizulu Na Ladysmith ni kitongoji katika jimbo la Natal alichotoka Joseph Shabalala kiongozi na mwanzilishi wa kundi hili

Ladysmith Black Mambazo lina albamu zaidi ya Kundi hili lilipata umaarufu mkubwa liliposhirikiana na mwanamuziki wa Marekani Paul Simon kutoa albamu ya Graceland ambayo iliwashirikisha pia wanamuziki maarufu duniani kama Miriam Makeba na Hugh Masekela

Wanamuziki wa Afrika Kusini

Mkoa wa Arusha ni moja kati ya mikoa ya Tanzania Imepakana na Kenya upande wa kaskazini Mikoa ya jirani ni kufuatana na mwendo wa saa Kilimanjaro Manyara Shinyanga na Mara

Wilaya zake ni Monduli Longido Arumeru Arusha Ngorongoro na Karatu Makao makuu yapo Arusha mjini

Eneo lake ni km za mraba zikiwemo km za maji Kati ya milima yake Oldoinyo Lengai m bado ni volkeno hai Arusha ni volkeno ya kulala tangu mw Mvua hunyesha kati ya millimita mm kwa mwaka mlimani Arusha hadi mm kwa mwaka katika maeneo makavu

Mkoa wa Arusha ndio kitovu cha utalii Tanzania Bara Barabara ya lami DaressalaamNairobi inavuka eneo lake Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro wahudumia miji ya Arusha na Moshi Kuna mbuga za taifa na hifadhi za wanyamapori Ngorongoro Serengeti Olduvai Arusha Tarangire na Ziwa Manyara Hifadhi ya Mlima Kilimajaro iko karibu

Arusha hulimwa kahawa nafaka pareto katani pamba alizeti Fosfati inachimbuliwa Minjingu Mkoani Arusha na takribani tani kwa mwaka hutumiwa katika uzalishaji wa mbolea

Kati ya wakazi wa mkoa kiasili ndio Waarusha Wameru Wairaqw na Wamassai

Tovuti ya Mkoa wa Arusha

Arusha

wwwdwworldde
Deutsche Welle Bonn
Redio Deutsche Welle DW au Sauti ya Ujerumani ni kituo cha Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani kwa ajili ya matangazo ya nje

Kituo kimeanzishwa mw kilitoa matangazo ya Kijerumani kwa ajili ya Wajerumani kote duniani kwa njia ya SW
Leo kituo hutangaza kwa redio za SM na FM kwa lugha halafu kwa TV kwa lugha
Makao makuu ndipo Kln ofisi za DWTV ziko Bonn na Berlin

Kwa wwwdwworldde ratiba na matangazo hupatikana pia katika mtandao

Ukurasa wa matangazo ya Kiswahili upo Sauti ya Ujerumani

Ujerumani
Redio
Kiswahili

Usawa wa wastani wa maji ya bahari hutumika kama kipimo cha kulinganisha kimo cha mahali duniani toka usawa wa bahari Kimo cha bahari hubadilika muda hadi muda Wastani wa vimo hivi ni usawa bahari wastani

Kawaida hutumika katika sentensi kama Nairobi iko mita juu ya usawa wa bahari
Au Ndege inatembea mita juu ya usawa wa bahari
Kifupi chake UB

Jiografia
Bahari
Vipimo

Kitabu cha Alfu Lela U Lela au Usiku Elfu na Moja kwa Kiarabu au kwa Kiajemi ni mkusanyiko wa fasihi katika muundo wa visa kutoka Mashariki ya Kati
Alfu Lela u Lela kwa maandishi ya Kiarabu

Visa hivi vinatokana na kitabu cha zamani cha Kiajemi kiitwacho Hazr Afsna Visa vya Ngano Elfu Moja Inaaminika kuwa mtu aliyekusanya visa hivi na kutafsiri kwa Kiarabu ni mtambaji hadithi maarufu Abu abdAllah Muhammed elGahshigar katika karne ya Tafsiri ya kwanza ya Kiarabu ya kisasa ilichapwa Cairo Misri mwaka

Inasadikika kuwa visa hivi vilianza kukusanywa wakati Baghdad ilipokuwa kitovu cha biashara na siasa Mashariki ya Kati Wafanyabiashara toka Uajemi Persia China India Afrika na Ulaya walikuwa wakitembelea Baghdad kwa ajili ya biashara
Sharyari na Shahrazadi

Mwanzo wa visa hivi ni kuudhiwa kwa mfalme Shahryar wa kisiwa kilichoko kati ya India na China na kitendo cha mke wake kuwa na mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa Shahryar aliamua kumuua mke wake Kwa kuamini kuwa wanawake wote wako kama mke wake aliyemuua yaani sio waaminifu anamwamuru mtumishi wake awe anampatia mke kila usiku Baada ya kulala na mke wake mpya usiku kunapokucha anaamuru mke huyo auawe

Hali hii inaendelea hadi pale binti wa huyo mtumishi wake anapounda mbinu maalum na kuamua kujitolea kuwa mke wa mfalme Binti huyo jina lake ni Shahrazad Scheherazade au Shahrastini katika vitabu vya Kiingereza Kila usiku baada ya ndoa yao binti huyo anatumia masaa na masaa kumsimulia mfalme visa vitamu na vya kusisimua ambapo utamu wake unakuwa umekolea inapofika alfajiri ule wakati wa kuuawa kwa mke wa mfalme Kwa nia ya kujua mwisho wa kisa mfalme alikuwa akiahirisha mauaji ya Shahrazad Aliendelea kuahirisha kuuawa kwa mke wake hadi akapata naye watoto watatu Ulipofika wakati huo aliamini kuwa mke wake huyo ni mwaminifu hivyo akabadili uamuzi wa kuua wake zake

Visa vyenyewe ni mchanganyiko wa mapenzi misiba ucheshi mashairi na visa vya dini ya Kiislamu Visa hivi vinajumuisha pia wanamazingaombwe na majiniVisa maarufu ni pamoja na Taa ya Alladin Baharia Sindbad Ali Baba na Wezi Arobaini Kati ya majina mengi inayotajwa kuna pia majina ya Khalifa Harun arRashid na mshairi Abu Nuwas Inaaminika kuwa visa vya Alladin na Ali Baba viliingizwa katika mkusanyiko huo karne ya na Antoine Galland ambaye alisikia visa hivyo toka kwa mtambaji hadithi wa Kimaroni tokea nchini Syria

Tafsiri mbalimbali za Alfu Lela U Lela pamoja na tafsiri ya Sir Francis Burton na John Payne

Project Bartleby edition Tafsiri ya Lane na Poole

Tafsiri ya Jonathan Scott

Kipindi cha luninga

Sinema ya Sinbad Legend of the Seven Seas

Fasihi

Karne ni miaka mia moja Karne ni milenia moja Inawezekana kugawa karne kwa miongo

Neno hili limetokana na Kiarabu linamaanisha kipindi cha miaka mia moja Kwa kawaida karne si miaka yoyote inayofuatana lakini kipindi kati ya miaka kama vile au

Karne inakwisha katika mwaka yenye mwishoni yaani Sababu yake ni ya kwamba hakuna mwaka ya kuanzisha hesabu hivyo karne ya kwanza ya hesabu ilianza kwa mwaka Hali hii huleta kila karne majadiliano kwa sababu watu wengi husikia karne mpya inaanza wakati namba ya mbele waliyozoea muda mrefu inabadilika

Hivyo watu wengi walisheherekea karne mpya mwanzoni wa mwaka iliyokuwa mwaka wa mwisho wa karne ya si mwaka wa kwanza wa karne ya Ingawa maoni ya wataalamu hayakueleweka au hayakupokelewa watu wengine walisema haidhuru

Vipimo vya wakati

Bendera ya Tanzania
Bendera ya Zanzibar mwaka iliyotangulia kuundwa kwa bendera ya Tanzania
Bendera ya Jamhuri ya Tanganyika hadi iliyotangulia kuundwa kwa bendera ya Tanzania

Bendera ya Tanzania ni ya mstatili unaokatwa pembe kwa pembe na kanda nyeusi yenye milia za njano dhahabu kando

Pembetatu ya juu ina rangi ya majani pembetatu ya chini ni ya buluu

Bendera hii imepatikana tangu kutokana na muungano wa Tanganyika na Zanzibar Bendera ya Tanganyika ilikuwa na rangi ya kijani ikiwa na kanda nyeusi katikati yenye milia za njano dhahabu kando Buluu imepatikana kutokana na bendera ya Zanzibar ya ikimaanisha bahari Hata hivyo toka mwaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilianza kutumia rasmi bendera ya Zanzibar Hii ni mara ya kwanza toka kuungana kwa Tangantika na Zanzibar kwa kisiwa cha Zanzibar kuwa na bendera yake yenyewe

Rangi zinasemekana kuwa na maana yafuatayo Kijani kwa ajili ya mashamba kilimo na misitu Kijani ni pia rangi ya bendera ya chama cha TANU kilichokuwa chama tawala tangu uhuru Buluu kwa ajili ya bahari na visiwa Nyeusi ni rangi ya watu Waafrika Njano dhahabu inakumbusha juu ya utajiri wa madini

Tanzania
Tanzania

Jakaya Mrisho Kikwete tangu tarehe Desemba ni rais wa nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jakaya Kikwete pamoja na marais waliostaafu Benjamin Mkapa na Alhaji Ali Hassan Mwinyi

Amezaliwa Oktoba katika kijiji cha Msoga kata ya Lugoba tarafa ya Msoga Jimbo la Chalinze Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani Lugha ya mama ilikuwa Kikwere

Alizaliwa katika familia ya wanasiasa Babu yake Mzee Mrisho Kikwete alikuwa chifu wa Wakwere Baba yake alikuwa Mkuu wa Wilaya Pangani Same na Tanga Jakaya Kikwete amesimulia hadithi ya kifamilia ya kuwa wakati mama yake alipokuwa mja mzito naye Babu alitamka kuwa ikiwa mtoto atakuwa wa kiume atampatia urithi wa cheo chake

akasoma Shule ya Msingi Msoga halafu Shule ya Middle School Lusonga halafu Shule ya Sekondari Kibaha akiongeza Alevel huko Shule ya Sekondari Tanga Kuanzia mwaka alisoma uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akimaliza digrii yake mwaka Akajiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ

Jakaya aliposoma Shule ya Sekondari ya Kibaha alikuwa mwenyekiti wa wanafunzi na pia wa Vijana wa TANU Shule ya Sekondari Tanga alikuwa Kiranja Mkuu na pia kiongozi wa timu ya mpira UDS alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya wanafunzi

left

akateuliwa kuwa mbunge na waziri msaidizi alichaguliwa kuwa mbunge wa BagamoyoChalinze akirudishwa kila uchaguzi hadi mw Akawa waziri akipita katika wizara za maji na fedha

alijaribu kuchaguliwa kuwa mgombea wa uraisi upande wa CCM Inasemekana ya kwamba Mwl Julius Nyerere alimwomba wakati ule kumwachia Benjamin Mkapa nafasi aliyeteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Kikwete akawa Waziri ya Mambo ya Nje katika serikali zote mbili za Mkapa

Mwaka alifaulu kuteuliwa mgombea wa CCM kwa nafasi ya raisi na akashinda uchaguzi wa Desemba akizoa za kura zote

Jakaya Kikwete Fans Website
Government of Tanzania
Ippmedia Interview with Col Kikwete
BBC Profile
Jakaya Kikwete SwearingIn Ceremony

Waliozaliwa
Marais wa Tanzania
Watu walio hai

Victoria lake and the Rift
Density growth around Lake Victoria
Lacal languages around lake Victoria
Lake Victoria height variation
right
Ziwa Victoria pia Viktoria Nyanza Ziwa Nyanza ni ziwa kubwa Afrika pia ni chanzo cha mto Nile hili ni ziwa la pili kwa ukubwa Duniani Ziwa la kwanza ni Ziwa Superior ambalo lipo Amerika ya Kaskazini Ziwa Victoria lipo futi kutoka usawa wa bahari na lina eneo la maili za mraba zaidi ya Maji ya ziwa Victoria yanamiminika kwenye mto Nile na kuelekea bahari ya Mediteranea kwa umbali wa maili Ziwa Victoria limekuwa ni kiunganisho na mpaka kwa nchi tatu za Afrika ya mashariki ambazo ni Tanzania Kenya na Uganda

Watersheds of Africa A Nile Lake Victoria

Maziwa ya Afrika
Maziwa ya Tanzania
Maziwa ya Uganda
Maziwa ya Kenya
Nile

Jens FinkJensen
Bwana Jens FinkJensen alizaliwa tarehe Desemba katika mji wa Copenhagen nchini Denmark Yeye ni mwandishi katika lugha ya Kidenishi katika nyanja mbalimbali kama vile semi za kawaida na mashairi Vile vile yeye ni mpiga picha na mwandishi wa vitabu hasa vya muziki na nyimbo

Alianza maisha yake kama mwandishi wa vitabu vya hadidhi Juni wakati alipoandika hadithi fupi ijulikanayo kama Juni Kitabu hicho kilichapishwa kwenye gazeti la kila siku kwa lugha ya Kidenish lijulikanalo kama Nipashe Habari Hatimaye kwenye mwezi wa Mei katika mwaka wa Elfu Moja na Mia Tisa na Sabini na Sita akawa mwandishi wa mashairi kwanza kwa kuandika tunzi nne za mashairi zilizo chapishwa kwenye jarida nambari sabini na sita mkwaju moja na ambalo hujulikana kama Mbegu ya Ngano Hvedekorn

Tunzi zake za mwanzo kwenye nyanja ya mashairi zilichapishwa kwa mara ya kwanza kunako Mwaka wa Elfu Moja Mia Nane na Dhemaanini na Moja na zikajulikana kwa kupewa kicwa cha maneno Dunia Kwenye Jicho Alianza kukusanya mashairi yalio kua yameandikwa na washairi wengine na kuyaweka katika hali ya vitabu kwenye mwaka wa Elfu Moja Mia Tisa na Dhemanini na Sita Vitabu vyenyewe vilichapishwa vikiwa katika hali ya mkusanyiko wa hadidhi fupifupi na vikatambulika kwa jina la Wanyama mwitu Hatimae kunako mwaka wa Elfu Moja Mia Tisa na Tisini na Nne akaanza kuandika vitabu kwa watoto baadhi yavyo kikiwa ni kile kiitwacho Jonas na Konokono

Alihitimu masomo yake kwenye shule ya upili kidato cha sita na kupita vizuri katika masomo ya lugha mbalimbale akiwa katika shule ya bweni ya Herlufsholm kunako mwaka wa Elfu Moja mia Tisa na Sabini na Sita Baadae alifanya mafunzo ya kijeshi na kuhitimu kwa kutunukiwa cheo cha Kamanda kwenye kikosi kiitwacho Walinzi Hai wa Kifalme Royal Life Guards Hatimae kwenye mwaka wa Elfumoja na Mia Tisa na Dhemaanini na Sita akajiunga na chuo kitoacho masomo kwenye fani ya ujenzi kilichoko mjini Conpenhagen amboko alitunukiwa shahada ya Mastas katika uchoraji na ujenzi Katika mwaka wa Elfu moja Mia Tisa na Tisini na Saba akiwa bado angali kwenye chuo hichohicho aliyaendeleza masomo yake kwa kushiriki kwenye masomo ya ukusanyaji na utoaji wa habari katika misingi inayo husisha matumizu ya mbinu mbalimbali

Na akiwa kama mojawapo wa waandishi wakongwe walio vuma katika miaka ya Dhemaanini na ambao walipenda kua na uhusiano wa karibu sana na bwana Poul Borum mhariri wa Hvedekorn yeye pamoja na wenzake wengine kama vile Michael Strunge walichangia katika kubuni onyesho la kusisimua ambalo lilijulikana kama Kizazi Kipya na ambalo liliandaliwa katika ukumbi wa Huset ulioko mjini Copenhagen Hii ilikua ni kwenye mwaka wa Elfu Moja mia Tisa na Dhemaanini

Vilevile alijishirikisha kwenye maonyesho ya tunzi mbalimbali na alishikilia nafasi maalum ya kusoma mashairi yenye kuelezea hali ya furaha na huzuni huku akionyesha picha zinazo onyeshwa kwenye kuta kwa kutumia miale ya mwangaza Mengine alio jihusisha nayo yalikua ni Kuleta hali ya uuwiyano katika tunzi mbalimbali zilizo tungwa na shule mbalimbali za upili na kwenye sherehe zingine mbalimbali zilizo wahi kufanyika wakati huo Hii ikiwa ni baadhi ya matukio mengine alio jihusisha nayo Wengine walio shiriki nae ni mwana mziki Fredrik Mellqvist ambae ana uhodari wa kucheza chombo kiitwacho Keyboard Wengine alio shiriki nao ni pamoja na yule mchezaji wa chombo kiitwacho Saksafoni aitwae Jens Severin

Mwana sanaa huyu Jens FinkJensen amewahi vilevile kuandaa maonyesho ya picha kwamfano yale yaliyo julikana kama Meli za Kusini pamoja na Uso wa Beijing Mengine yalikua ni pamoja na maonyesho yalio julikana kama Picha za Neno ambazo ziliandamana na picha ambazo huonyeshwa kwa kutumia miyale ya mwangaza na ambazo hushirikisha sauti Mfano ukiwa ni ile ijulikanayo kama Jicho limulikalo Ulimwengu likiwa ni onyesho lililokua linasimulia kuhusu malighafi inayo tumika ndani ya vitabu

Mashairi ya Verden i et je Dunia kwenye jicho
Mashairi ya Sorgrejser Safari za kufadhaisha
Mashairi ya Dans under galgen Kucheza densi kwenye miti ya kunyongea watu
Hadidhi Fupi za Bsterne Wanyama mwitu
Mashairi ya Nr afstanden Karibu ya mwendo yalio chapishwa kwa lugha ya Kiarabu
Vitabu kwa Watoto Jonas og konkylien Jonas na konokono ambamo picha za tafsiri zimechorwa na msanii Mads Stage
Mashairi ya Forvandlingshavet Bahari ya mageuzi
Kitabu Kwa Watoto Jonas og himmelteltet Jonas na hema ipepeayo kwenye mawingu ambamo picha za tafsiri zimechorwa na msanii Mads Stage
Mashairi ya Alt er en bning Kila kitu ni ufunguo mpya
Chaguo Maalum la Mashairi Mia Moja ya kimapenzi ya Syd for mit hjerte Kusini ya moyo wangu

Jens FinkJensen Online

Waliozaliwa
Waandishi wa Denmark

Uchoraji wa Kiorthodoksi unaoonyesha kuzaliwa kwake Kristo Yesu anaonekana amevikwa sanda na kulazwa kaburini kwa maana alizaliwa ili atukomboe kwa kifo chake
Krismasi pia Noeli ni sikukuu ambako Wakristo husheherekea kuzaliwa kwake Yesu Kristo zaidi ya miaka iliyopita Kwa kawaida husheherekewa tarehe Desemba katika Ukristo wa magharibi na tarehe Januari katika ule wa mashariki

Tarehe halisi ya kuzaliwa kwake Yesu haijulikani kwa sababu utamaduni wa Wayahudi wa wakati ule haukuwa na sherehe au kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa

Lakini baadaye Ukristo ulienea katika Dola la Roma na kati ya mataifa yaliyokuwa na kawaida ya kuzingatia siku ya kuzaliwa Hivyo ilijitokeza hamu ya kusheherekea pia sikukuu ya kuzaliwa kwake Kristo Ndiyo asili ya Sikukuu ya Krismasi

Tangu mwanzo wa karne ya BK kuna kumbukumbu ya waandishi mbalimbali waliojadili tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo

Habari za kwanza kabisa za makadirio ya tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu zinapatikana kutoka Misri mnamo mwaka Mwandishi Mkristo Klemens wa Alexandria kitabu cha Stromateis I xxi alilalamikia udadisi wa wataalamu kadhaa wa Misri waliodai kwamba wamekadiria tarehe hiyo katika mwezi Mei wengine katika Aprili Alisema pia kuwa kikundi cha Kikristo cha wafuasi wa Basilides huko Misri walisheherekea Epifania pamoja na kuzaliwa kwake Yesu tarehe Januari

Labda kadirio la tarehe ya Desemba pia lina asili katika Misri Kuanzia mwaka kwa mara ya kwanza katika maandishi ya Sixtus Julius Africanus tunasikia kwamba wataalamu wa Misri walifikiri tarehe Machi ilikuwa tarehe ya kufa kwake Kristo na pia siku ya kuzaliwa kwake Kwa kuongeza miezi tisa ya mimba inajitokeza Desemba kama tarehe ya kuzaliwa

Inaonekana tarehe Desemba ilijitokeza wakati huo Kuna taarifa ya mwaka kutoka Ipolito wa Roma kwamba tarehe Desemba ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo

Wataalamu mbalimbali walidai kwamba Kanisa lilipachika sikukuu ya Kristo kwenye tarehe hiyo kwa nia ya kuchukua nafasi ya sikukuu ya jua kama mungu Sol invictus Lakini pengine mambo yalikwenda kinyume yaani kwamba Makaisari walianzisha sikukuu hiyo halafu wakaipanga tarehe ya Krismasi ili kushindana na Ukristo uliokuwa bado chini ya dhuluma

Aliyeingiza sikukuu ya Kuzaliwa Jua Mitra huko Roma ni Eliogabalus kaisari kuanzia hadi Baadaye Aurelianus akaithibitisha rasmi mwaka hatimate ikahamishiwa tarehe Desemba Wakati wa Licinius sikukuu hiyo ilikuwa ikiadhimishwa bado tarehe Desemba Taz maandishi yaliyotajwa na Allan S Hoey katika ukurasa rejeo wa Official Policy towards Oriental Cults in the Roman Army Transactions and Proceedings of the American Philological Association pp

Kutoka Roma uliokuwa mji mkuu wa Dola la Roma sherehe ya Desemba ilienea kote katika Ukristo

Wakristo wengi husheherekea tarehe Desemba Wakatoliki Waprotestanti sehemu ya Waorthodoksi Kati ya Waorthodoksi kuna tarehe nyingine hasa Januari kutokana na tofauti katika kalenda

Habari za Krismasi kama sherehe hazipatikani katika Biblia kwa sababu zilizotajwa hapa juu

Lakini hasa vitabu viwili vya Agano Jipya vina habari za kuzaliwa kwake Yesu yaani Injili za Mathayo na Luka

Mathayo anasimulia habari hizo katika mlango wa kwanza kuanzia aya na katika mlango wa pili

Bikira Maria alipata mimba wakati alipokuwa mchumba wa Yosefu Yosefu alitaka kumwacha lakini aliambiwa na malaika aanze kuishi naye na kumkubali mtoto kama wake kwa kumpa jina Yesu

Mamajusi kutoka mashariki waliwatembelea na kuwaletea zawadi kwa sababu waliona nyota ya pekee iliyokuwa kwao alama ya kuzaliwa kwa mfalme mpya katika Uyahudi ikawaongoza hadi Yerusalemu Lakini walipompitia mfalme Herode Mkuu huyo alikasirika akimwogopa mfalme mpya Hata hivyo aliwaelekeza Bethehemu kadiri ya utabiri wa nabii Mika

Yosefu alipata tena ujumbe kutoka kwa malaika akaondoka na mtoto na Maria kukimbilia Misri kabla ya askari wa Herode hawajaweza kumuua Yesu

Baada ya kifo cha Herode walirudi kutoka Misri lakini hawakuenda tena Bethlehemu bali kuhamia Nazareti katika mkoa wa Galilaya

Katika taarifa ya Luka mlango wa na Maria alipokea huko Nazareti ujumbe wa malaika mkuu Gabrieli kwamba atapata mimba na mtoto wa pekee

Yosefu na Maria walikwenda Bethlehemu kwa sababu ya sensa iliyowataka kwenda katika mji alikotokea Yosefu Hapo Yesu alizaliwa katika hori la kulishia wanyama wachungaji mabondeni walitangaziwa na malaika habari hiyo wakaja kumwona mtoto

Baada ya kuzaliwa wazazi walimpeleka Yesu Yerusalemu katika hekalu kufuatana na sheria ya Agano la Kale Kitabu cha Kutoka halafu wakarudi kwao Nazareti

Korani pia ina habari za kuzaliwa kwake Yesu nabii Isa

Sura ya tatu Al Imran ina habari za tangazo la malaika kwa Bikira Mariamu zinazofanana na Luka

Sura ya Mariamu inarudia tangazo la malaika kwa Mariamu na inasimulia kuzaliwa kwake Yesu chini ya mti wa mtende halafu majadiliano kati ya Mariamu na ndugu zake Mtoto mchanga Yesu akaanza kusema wakati wa kuzaliwa akimtetea mama yake dhidi ya ndugu zake

Watu wote ni wakosefu na kujenga mazingira maovu hata wanayakinai na kutamani wamuone mtu tofauti yaani mwema na mtakatifu Pengine wanadhani fulani ni mwema kabisa kumbe siyo

Haja hiyo inaturudia sisi kwa nini nisiwe mimi mtu wa namna hiyo Kwa nini nisianze na moja kama kwa kuzaliwa upya kabla sijawadai wengine Zaidi tena haja kuu ya binadamu ni kumuona Mungu mwenyewe lakini wapi lini namna gani

Kama kawaida imani na liturujia ya Kikristo zinaitikia haja za binadamu Kipindi cha Noeli kinatimiza haja tulizozitaja kwa kuwa anazaliwa mtu mpya kabisa ambaye anatuvutia kwa wema wake na ambaye tukimuona tumemuona Mungu tena tukimpokea tunazaliwa upya kama wana wa Mungu

Leo amezaliwa kwa ajili yenu Mwokozi ndiye Kristo Bwana Tunapoadhimisha Noeli tangazo hilo la malaika kwa wachungaji linatufikia sisi Si kujidanganya kana kwamba Yesu angezaliwa leo wala hatukumbuki tu tukio la zamani bali fumbo la kuzaliwa Bwana linatufikia leo katika liturujia na kutuletea neema zake Hivyo tunaweza tukazaliwa upya kwa kushiriki kuzaliwa kwa kichwa chetu

Liturujia inashangilia hivi Lo Mabadilishano ya ajabu Mwana wa Mungu anakuwa mtu kusudi mtu awe mwana wa Mungu Tena si binadamu tu bali viumbe vyote vinapata heshima mpya kwa Neno wa milele kujifanya kiumbe

Liturujia
Sikukuu za Ukristo

Mkoa wa Kagera ni mkoa wa kaskazinimagharibi kabisa katika Tanzania Jina lake linatokana na mto Kagera

Mkoa wa Kagera umepakana na Burundi Rwanda na Uganda upande wa Magharibi na Kaskazini Upande wa Kusini umepakana na mikoa mengine ya Tanzania ya Kigoma Shinyanga na Mwanza Eneo lake ni km za nchi kavu na km za maji hasa ya Viktoria Nyanza jumla km

Mkoa wa Kagera uko mnamo m juu ya uwiano wa bahari

Makao makuu ya mkoa ni mji wa Bukoba

Kuna wilaya saba za Bukoba Mjini Bukoba Vijijini wilaya ya Misenyi wilaya ya Muleba wilaya ya Karagwe wilaya ya Ngara wilaya ya Biharamulo na wilaya ya Chato Misenyi na Chato ni wilaya mpya zilizoanzishwa mwaka

Sensa ya mw imeonyesha idadi ya wakazi kuwa inayoendelea kuongezeka asilimia kwa mwaka

Tovuti wa Mkoa wa Kagera
Kagera Bukoba the official webguide
Tourist Office Bukoba Kagera
United Republic of Tanzania Kagera Region
Utamaduni wa Kagera en

K

Yesu Kristo

Yesu alikuwa Myahudi mwanamume aliyeishi miaka hivi iliyopita labda KK BK Kutokana na umuhimu wake katika historia ya binadamu kwa kawaida miaka yote inahesabiwa kwanzia ujio wake ulivyokadiriwa kimakosa katika karne ya

Nchi ambayo Yesu alizaliwa akafundisha ni nchi ileile ambayo Mungu aliwaahidia Waisraeli tangu zamani za Abrahamu ni nchi ileile waliyoiteka chini ya Yoshua ni nchi ileile waliyoirudia kutoka utumwani Babeli

Lakini wakati wote wa Agano Jipya yaani tangu Yesu alipozaliwa hadi mwisho wa maisha ya mitume wake nchi hiyo haikuwa huru bali chini ya himaya ya Warumi ingawa pengine hao waliwakabidhi vibaraka yaani watawala wenyeji waliowekwa na wakoloni

Vibaraka hao ni Herode Mkuu KK KK na wazawa wake ambao tena hawakuwa Waisraeli halisi bali Waedomu ingawa kabila lao lililazimishwa kuingia dini ya Kiyahudi karne iliyotangulia Ukoo huo unajulikana kwa ukatili uchu wa madaraka na uzinifu wake

Vilevile maliwali wa Kirumi waliowekwa pengine kutawala nchi au sehemu fulani walionyesha mara nyingi ukatili na dharau kwa Waisraeli na dini yao hata kusababisha chuki na mapigano kati ya jeshi na wananchi Mfano mmojawapo ni Ponsyo Pilato aliyesimamia Uyahudi kuanzia mwaka hadi BK

Mbali na hayo utawala wa Roma ulioenea Ulaya Magharibi na Kusini Afrika Kaskazini na nchi za Mashariki ya Kati kupakana na Iraq ya leo kwa jumla ulihakikisha hali ya amani kwa muda wote wa Agano Jipya na karne za kwanza za Kanisa Hali hiyo pamoja na umoja wa dola hilo lote na urahisi wa mawasiliano kwa njia ya barabara zilizotengenezwa na Warumi na uenezi wa lugha ya kimataifa Kiyunani yaani Kigiriki cha zamani ilichangia kasi ya uenezaji wa habari njema Injili Lugha hiyo ndiyo iliyotumiwa na waandishi wote wa Agano Jipya ili vitabu vyao viwafaidishe watu wengi zaidi ingawa baadhi yao hawakuijua vizuri

Lugha asili ya Yesu na ya Mitume ilikuwa Kiaramu ambacho ni jamii ya Kiyahudi na ambacho polepole kilishika nafasi yake kati ya Wayahudi kuanzia karne ya sita KK Hao wote walitokea mkoa wa Galilaya uliokuwa na mchanganyiko wa watu Waisraeli na mataifa kiasi kwamba huko Wayahudi wenyewe walifuata kwa urahisi desturi za Kiyunani hata wakadharauliwa na wenzao wa Kusini Yerusalemu na mkoa wa Yudea

Kati ya mikoa hiyo miwili ulienea mkoa wa Samaria ambao wakazi wake walijenga uadui mkubwa na Wayahudi baada ya uhamisho wa Babeli walipokataliwa kuchangia ujenzi wa hekalu la pili la Yerusalemu

Dionisi Mdogo mmonaki aliyeanzisha mwaka hivi mtindo wa kuhesabu miaka kuanzia kuzaliwa Yesu kurudi nyuma KK au kwenda mbele BK alikosea hesabu zake Leo tunakisia Yesu alizaliwa mwaka hivi KK kwa sababu alizaliwa Bethlehemu chini ya Herode Mkuu aliyefariki mwaka KK

Huyo alipojaribu kumuua mtoto Yesu familia takatifu ilikimbilia Misri mpaka baada ya kufa kwake Hapo ikarudi Galilaya hata Yesu akajulikana kwa jina la kijiji cha Nazareti kilichodharauliwa na Wagalilaya pia Ndipo alipokulia na kuishi akifanya kazi ya ufundi

Mwaka hivi BK ndugu yake Yohane Mbatizaji aliacha maisha ya jangwani na kuanza kuhubiri toba kandokando ya mto Yordani Kwa kuwa Waisraeli walikosa manabii kwa muda mrefu na walitamani sana ukombozi walimuendea kwa wingi hata wakamtia hofu Herode Antipa

Ingawa huyo akamfunga mapema akamuua kazi ya Yohane ilikuwa imetimia kwa sababu aliweza kuwaandaa Waisraeli wengi hasa watu wadogo na wakosefu wampokee Yesu aliyebatizwa naye Katika nafasi hiyo Yohane alimtambulisha kama Mwanakondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu

Ndipo Yesu naye alipoanza kuhubiri lakini pia kutenda miujiza ya kila aina akapata haraka wafuasi wengi Kati yao akachagua Mitume wake kama msingi mpya wa taifa la Mungu Alifanya kazi hizo kuanzia Galilaya akitangaza ujio wa ufalme wa Mungu kwa maana ya kwamba ufalme uliotazamiwa na Wayahudi umewajia kwa njia yake

Ingawa hakupitia shule yoyote ya Biblia Yesu alionekana anafundisha vizuri kuliko walimu wa sheria wa kawaida kama mtu mwenye mamlaka juu ya Torati Mafundisho yake yalilingana na yale ya Mafarisayo kuliko na yale ya Masadukayo lakini alishindana pia na hao wa kwanza

Kijicho na upinzani vikazidi hasa Yerusalemu walipoanza kufanya njama za kumuua Ingawa Yesu alijua hayo alijikaza kwenda katika mji mtakatifu autangazie habari njema na kufia huko Baada ya kupokewa kwa shangwe kabla ya sherehe ya Pasaka ya mwaka au akakamatwa na baraza la Israeli kwa tuhuma ya kufuru ya kujilinganisha na Mungu halafu akakabidhiwa kwa liwali wa Kirumi aliyekuwa na mamlaka ya kutoa adhabu ya kifo Baada ya kikao ambapo Wayahudi walitafuta kisingizio cha kisiasa Ponsyo Pilato akalazimika kuagiza Yesu asulubiwe na kisha kufa kwake kaburi lilindwe na askari

Hata hivyo siku ya tatu kaburi likaonekana tupu na Yesu akaanza kuwatokea wanafunzi wake wa kike na wa kiume kwa muda wa siku arubaini halafu akapaa mbinguni mbele ya macho yao

Habari hizo zikatangazwa kwa sauti tu kwa miaka kadhaa halafu zikaanza kuandikwa Kanisa linaheshimu kwa namna ya pekee kama ushuhuda mkuu juu ya maisha na mafundisho ya Yesu na kama moyo wa Maandiko matakatifu yote Injili nne zilizoandikwa na Marko Mathayo Mwinjili Luka na Yohane kati ya mwaka na hivi

Waumini wake wanaunda Kanisa la Kikristo ambalo linapatikana leo katika madhehebu mengi Karibu wote wanamwamini kuwa Mungu aliyechukua umbile la mwanadamu au kwa lugha nyingine kuwa Mwana wa Mungu Wakristo wengine wanaamini kuwa yeye ni mtume wa pekee wa Mungu ila sio Mungu

Katika dini ya Uislamu Yesu anajulikana kama Nabii Isa Waislamu wanaamini kuwa yeye alikuwa ni nabii wa Mungu ila hakuwa mwana wa Mungu wala Mungu

Maisha yake yamekuwa msingi wa sikukuu mbalimbali zinazosheherekewa katika nchi nyingi duniani kama vile Noeli auKrismasi kuzaliwa kwake Epifania kuonekana kwake na kubatizwa kwake Majilio kuandaliwa ujio wake Kwaresima mafungo na mateso yake Ijumaa Kuu kifo chake muhimu kuliko zote ni Pasaka kufufuka kwake

Papyrus P iliyoandikwa kwa Kigiriki mwaka hivi inahesabika kuwa andiko la zamani zaidi kutufikia kuhusu Yesu Ina sehemu za Injili ya Yohane mbele nyuma

Yesu hakuacha maandiko yoyote Habari zake zinapatikana hasa katika Biblia kwa namna ya pekee katika Injili

Nje ya Ukristo kuna habari fupi kuhusu Yesu katika maandiko ya waandishi Waroma Wagiriki na Wayahudi Habari hizi zinaangaliwa sana kwa sababu zimetungwa na watu wasiomwamini Yesu Kwa ujumla zinathibitisha ya kwamba Yesu alikuwepo alikuwa na wafuasi huko Roma na ya kwamba awali Waroma hawakuelewa tofauti kati ya wafuasi wake na Wayahudi Muhimu ni hasa

Mtaalamu Myahudi Flavius Josephus aliandika mnamo BK kitabu cha Antiquitates Judaicae Habari za historia ya Kiyahudi akitaja kifo cha Yakobo ndugu wa Yesu sura ya

Mwandishi Mroma Tacitus aliandika mnamo mwaka ya kwamba Kaisari Nero alishtaki kikundi cha Chrestiani ya kuwa wamechoma moto mji wa Roma Aliongeza Mtu ambaye ni asili ya jina hili ni Chrestus aliyeuawa wakati wa Tiberio kwa amri ya Pontio Pilato Annales XV

Mwandishi Mroma Svetonius alimtaja Chrestos katika kitabu chake juu ya maisha ya Kaisari Claudius ya kwamba huyu amesababisha fujo kati ya Wayahudi wa Roma hivyo Kaisari aliwafukuza mjini

Mwanasiasa Mroma Gaius Plinius Caecilius Secundus aliacha barua kadhaa zinazotaja Wakristo mnamo mwaka BK Alimwuliza Kaisari Traianus jinsi ya kushughulikia Wakristo waliokataa kutoa sadaka mbele ya sanamu za Kaisari

Makala Yesu Kristo mafundisho ya Kikristo kuhusu Yesu
Makala Isa mafundisho ya Uislamu kuhusu Yesu

Waliozaliwa KK
Waliofariki
Yesu Kristo
Ukristo
Watu wa Biblia
Watu wa Israel

Jumuiya ya Madola jina la Kiingereza ni Commonwealth of Nations inaunganisha nchi mbalimbali hasa Uingereza na nchi zilizokuwa koloni zake

Umoja huu umeanzishwa mw kama Jumuiya ya Kibritania British Commonwealth na kupewa jina lake la sasa tangu Inafuatana na Dola la Kibritania au Dola la Kiingereza ambayo ilikuwa dola kubwa kabisa katika historia ya dunia lakini maeneo yake yalianza kuachana baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia kutokana na kudhoofishwa kwa Uingereza vitani na miendo ya kupigania uhuru katika nchi mbalimbali hasa Uhindi

Leo zipatao asilimia ya watu wote duniani watu huishi katika nchi wanachama za Jumuiya ya Madola Nchi za jumuiya hii wenye wakazi wengi ni hasa Uhindi Pakistan Bangladesh na Nigeria Kuna pia nchi ndogo sana kama Tuvalu yenye wakazi pekee

Nchi kadhaa zilisimamishwa uanachama au kuondoka kwa hiari zao Mfano Tanganyika na Zanzibar ziliungana kwa hiyo hazipo tena lakini mpya ya Tanzania imekuwa nchi mwanachama Vilevile Newfoundland iliondoka katika jumuiya baada ya kujiunga na Kanada kama jimbo

Pakistan ilisimamishwa uanachama mara kadhaa kwa sababu serikali yake ilipinduliwa na wanajeshi walioanzisha serikali ya kijeshi Imerudishwa tena

Zimbabwe ilisimamishwa uanachama baada ya uchaguzi bandia ikaamua kujiondoa kabisa mwaka

Jamhuri ya Ueire iliamua mwaka kuacha viungo vyote na Uingereza ikajitangaza kuwa jamhuri isiyokubali athira ya nje kama hali ya malkia wa Uingereza kuwa mkuuw a dola hivyo ikaondoka katika jumuiya

Afrika Kusini ilijiondoa kwa sababu ya upinzani wa jumuiya dhidi ya sheria za apartheid Baada mwisho wa ubaguzi wa rangi nchi ilirudi katika jumuiya

Fiji imesimamishwa mara kadhaa baada ya uasi wa kijeshi uliopindua serikali Kwa sasa ni nchi ya pekee iliyosimamishwa uanachama

iliondoka ikajiunga tena ikasimamishwa ikakubaliwa tena ikasimamishwa tena kwa sababu ya mapinduzi ya kijeshi ya

Mashirika ya kimataifa

Majina mahali na njia za biashara katika Periplus
Periplus ya Bahari ya Eritrea ni kitabu cha mwongozo kwa ajili ya mabaharia kilichoandikwa mn mw bK Periplus ni neno la Kigiriki linalomaanisha tendo la kuzunguka baharini kwa merikebu Bahari ya Eritrea ni jina la kale kwa ajili ya Bahari ya Shamu pamoja na Bahari Hindi Jina limeundwa na watu wa nchi za mashariki ya Bahari ya Mediteraneo na Misri waliotumia lugha ya Kigiriki wakati wa miaka iliyopita

Kitabu hiki kimeandikwa na mwenyeji wa Aleksandria Misri iliyokuwa mji mkubwa wakati ule na kitovu cha biashara ya kimataifa kati ya Dola la Roma Afrika ya Mashariki na Bara Hindi

Kitabu cha Periplus kinaeleza mabandari kuanzia Misri hadi Afrika ya Mashariki kwa upande moja na hadi Bara Hindi kwa upande mwingine Kinataja majina ya mabandari bidhaa zilizopelekwa huko na bidhaa zilizopatikana kila mahali Pia kuna habari za kando juu ya watu watawala ni mila zao

Maelezo ni mengi kuhusu pwani la Eritrea na Somalia hadi Pembe la Afrika kuelekea kusini majina ya mabandari ni machache mwisho wa eneo lililojulikana ni mji wa Rhapta katika nchi za Azania

Bahari ya Hindi
Historia ya Afrika ya Mashariki

Bahari ya Eritrea Kigiriki erythr thlassa ni jina la kale kwa ajili ya Bahari ya Shamu pamoja na Bahari Hindi Neno erythra katika lugha ya Kigiriki inamaanisha rangi nyekundu thalassa bahari Hivyo bahari ile iliitwa kwa jina kama Bahari Nyekundu linganisha Kiing Red Sea Inasemekana ya kwamba jina hili limetokana na aina ya mwani unaoonyesha rangi hiyo wakati mwingine

Inaonekana ya kwamba waandishi wa kale hawakutofautisha kati ya Bahari ya Shamu na Bahari Hindi Merikebu za zamani zile zilitembea muda wote karibu na pwani kwa sababu dira haikulikana bado nje ya Uchina Hivyo haikuwa rahisi kuvuka bahari moja kwa moja na kupata picha kamili ya umbo la bahari

Nahodha wa merikebu hizi walitumia maandiko kama Periplus ya Bahari ya Eritrea wakipanga safari zao

Bahari ya Hindi

Eneo la Bahari ya Shamu Red Sea
Bahari ya Shamu Kiingereza Red Sea Kiarabu Bar alAmar alBaru lAmar Kiebrania Yam Suf Kitigrigna QeyH baHri ni ghuba kubwa ya Bahari Hindi Jina la kihistoria katika lugha ya Kigiriki ilikuwa Bahari ya Eritrea erythr thlassa

Kaskazini ni rasi ya Sinai pamoja ghuba ndogo za Aqaba na Suez halafu imeunganika na Mediteranea kwa njia ya Mfereji wa Suez Kusini Bahari ya Shamu imeunganika na Bahari Hindi kwa njia ya mlango wa bahari wa Bab el Mandeb

Ghuba yote ina urefu wa takriban km upana wake ni kati ya km na km tu kwenye Bab el Mandeb Eneo lake ni km Vilindi vyake vinaelekea hadi m chini ya uwiano wa bahari Vilindi hivi ni sehemu ya Bonde la Ufa Halijoto ya maji ni kati ya C

Nchi zinazopakana na Bahari ya Shamu ni

Upande wa Kaskazini
Misri
Israeli
Yordani
Upande wa Magharibi
Sudan
Misri
Upande wa Mashariki
Uarabuni Saudi
Yemen
Upande wa Kusini
Djibouti
Eritrea
Somalia

Bahari ya Hindi
Bahari ya pembeni

Ramani

Visiwa vya Zanzibar Unguja na Pemba
Visiwa vya Unguja na Pemba ramani haionyeshi umbali kati ya visiwa hali halisi

Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayojitawala katika mambo yake ya ndani Eneo lake ni sawa na funguvisiwa ya Zanzibar iliyopo mbele ya mwambao wa Afrika ya Mashariki karibu na Tanganyika au Tanzania bara Inajumuisha visiwa vikubwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogovidogo

Kwa jumla mikoa mitano ya Tanzania imo ndani ya Zanzibar ikiwa mitatu iko Unguja na miwili Pemba Hadi mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka sehemu hizi zilijulikana kama Usultani wa Zanzibar

Zanzibar inatawaliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar SMZ Raisi Amani Abeid Karume aliyekuwa mgombea wa CCM amechaguliwa mara ya pili na wananchi wote tar katika kura iliyopingwa na chama cha Upinzani CUF

Zanzibar ina Bunge lake lenye wabunge wanaochaguliwa kwa muda wa miaka mitano

Mji mkuu na makao makuu ya serikali ni Jiji la Zanzibar ambalo liko kisiwa cha Unguja Mji mkuu wa kisiwa cha Pemba ni Chake Chake
Idadi ya wakazi wote ilikuwa mwaka wakiwa wakazi wa Unguja na wakazi wa Pemba

Biashara ya Zanzibar ni kilimo na utalii Mazao yanayouzwa nje ni hasa karafuu basibasi mdalasini na pilipili

Jamhuri ya watu wa Zanzibar ilianzishwa baada ya mapinduzi ya iliyomaliza Usultani wa Zanzibar Rais wa kwanza alikuwa Abeid Amani Karume hadi aliyefuatwa na Aboud Jumbe Rais wa tatu aliyemfuata alikuwa Ali Hassan Mwinyi aliyeendelea kuwa pia rais wa Tanzania tangu

Rais wa sasa ni Amani Abeid Karume ambaye ni mwana wa rais wa kwanza

Historia inajionesha ya kwamba kiasi cha miaka kumekuwepo makazi ya bidadamu katika visiwa vya Zanzibar Visiwa hivi ni sehemu ya kumbukumbu ya kihistoria ya ulimwengu wakati waajemi wafanyabiashara waliigundua na kufanya ndio makao makuu kwa safari kati ya Mashariki ya Kati India Na Afrika

Katika karne ya mwanzo AD Zanzibar pamoja na mwambao wa Afrika ya Mashariki ulikua katika ufalme wa SabaKatika kipindi cha karne ya na ADWabantu walianza biashara na Waarabu waliokuja Afrika ya Mashariki
Katika karne ya ADwaarabu walikuja Zanzibar kibiashara pia kusambaza Dini ya KiislamWaarabu ndio waliyoipa jina ZANZIBAR kutokana na neno la Kiarabu ZINJI BAR yaani sehemu ya watu weusi

Lugha ya kiswahili imeanza kutumika kiasi cha karne ya ADLugha ya kiswahili ilitokana na kuchanganyika lugha ya kiarabu na lugha za kiafrika

Karne ya AD wareno walikuja Zanzibar lakini utawala wao ulifuatiwa na kutokuwepo utulivulakini biashara ya Utumwa iliwaweka watu pamoja
Waarabu kutoka Oman walichukua utawala Zanzibar katika karne ya ADNa Zanzibar ilikua ni makao makuu ya utawala wa Waomani

Zanzibar ilifaidi matunda mazuri ya kiuchumi na maendeleo yaliyosababishwa na utawala wa kisultani na hivyo kupelekea Zanzibar kuwa na mwakilishi nchini marekani na kupelekea kuenea kwa Dini ya wa kiislam
Katika karne ya AD Zanzibar ilikua chini ya utawala wa Omanmwaka Zanzibar ilikua inaongoza kwa kilimo cha karafuu na hiyo kupelekea mahitaji ya watumwa kuongezeka kutumika katika kilimo
kamisheni kutoka Uengereza na Ujerumani iliamua kuigawa Zanzibar kutoka katika utawala wa Kisultani na ndio ulikua mwisho wa utawala wa kujitegemea kwa Zanzibar na mnamo mwaka sultani alikubali maridhiano hayo

Zanzibar ilikua chini ya uangalizi wa waingereza rasmi lakini uchaguzi wa mwanzo ulifanyika mwaka na miaka iliyofuata kukakuwepo fujo na machafuko kutoka kwa waafrika wanaodai uhuru dhidi ya utawala wa kiarabu
Mwezi wa mwaka Waingereza waliipa uhuru Zanzibar chini ya jumuiya ya madolana mwezi wa mwaka Zanzibar ilifanya mapinduzi kujikomboa kutoka katika utawala wa kisultanimuda mchache baadae iliungana na Tanganyika kuunda Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA

Uchumi wa Zanzibar ni uchumi wa hali ya chini kabisa ambao mwananchi wa kawaida anaishi chini ya dola moja kwa siku au kutokua na uhakika wa kupata chochote
Hilo linatokana na viongozi wa vyama kutoonesha mori katika kutatua matatizo au kuweka mbinu za kuleta maendeleobadala yake ni kujadili siasa kwa muda mwingi
Zanzibar ni nchi yenye matumaini katika uchumi lakini kutokana na migogoro ya kisiasa imekua katika hali duni kabisani hivi majuzi tu balozi wa Marekani alisisitiza kuwa umuhimu wa kuwepo mashirikiano katika siasa ili kuiwezesha Zanzibar kuinuka katika hali ya kiuchumi

dadi ya Watu na Makazi

Watu wa Zanzibar ni wa asili mbalimbali hasa watu wa asili ya Afrika Bantu Waasia awali kutoka India na nchi za Kiarabu Idadi ya wakazi wa Zanzibar ilikuwa mwaka tarehe ya sensa ya mwisho kwa kiwango cha ukuaji wa Hii karibu theluthi mbili ya watu wanaishi Kisiwa cha ZanzibarUnguja
Mkoa wa mjini magharibi ndio wenye idadi kubwa ya wakaazi kiasi cha watu

Pemba ina jumla ya makazi sawa Mji mkubwa ni Chake Chake na idadi ya mengine ni Wete na Mkoani Kuna tofauti kubwa katika kiwango cha maisha kati ya wakazi wa Pemba na Unguja na kati ya wakazi wa mijini na vijijini Wastani wa mapato ya kila mwaka ya US na ukweli kwamba karibu nusu ya maisha ya wakazi wanaishi chini ya mstari wa umaskini Huduma ya afya vifo vya watoto wachanga bado ni katika Waliozaliwa na inakadiriwa kuwa utapiamlo huathiri moja katika tatu ya watu wa visiwa matarajio ya maisha wakati wa kuzaliwa ni Wakati matukio ya VVU UKIMWI ni ndogo mno kwa Zanzibar kuliko Tanzania kwa ujumla ya idadi ya watu kama dhidi ya wastani wa kitaifa wa

Dini ya Uislamu ni kiasi cha Mchanganyiko iliyobaki ni mchanganyiko wa Hindu na wa kikristo

Dini za kihindi pia zipo katika visiwa hivyo lakini wengi wao walikimbilia nchi au kuuawa wakati wa mapinduzi ya Wakristo walikuja baadaye wakati wa kipindi cha utawala wa Kireno na ukoloni wa Uingereza

Kuna misikiti ambaye waadhini hugongana kwa kila mmoja wakati wa maombi pamoja na Majumba ya Hindu sita mahekalu na Kanisa Kuu Katoliki kama vile Kanisa Kuu Anglican katika mji wa Zanzibar Stonetown

wwwtanzabradfordwebscomumoja wa watanzania Bradford
wwwtzgrewebsitecomUmoja wa Watanzania Greece
Tovuti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Takwimu
Picha za Zanzibar
Ramani ya Zanzibar na Tanganyika
Makala ya BBC kuhusu bendera mpya
Historia na utamaduni wa Zanzibar
Zanzibar links
Zanzibar Network kwa Utalii wa Ushirika NGO Umoja

Tanzania
Zanzibar

Watu walikimbia wimbi la tsunami tar Desemba lilipogonga mwambao wa Ao Nang nchini Uthai
Uenezaji wa mawimbi ya tsunami wa Krismasi katika Bara Hindi

Tsunami ni wimbi kubwa sana katika bahari inayosababishwa na tetemeko la ardhi mlipuko wa volkano au matokeo mengine yanayosababisha mshtuko wa ghafla chini ya maji Mshtuko huu unasababisha kutokea kwa wimbi kali linaloanza kupaa juu likifika katika maji kame

Neno tsunami linatokana na lugha ya Kijapani likimaanisha bandari ya mawimbi

Tsunami huweza kutokea na kusababisha vifo vya maelfu ya watu Wakati mwingine inaweza kutokea bila kuleta madhara yoyote

Tar Disemba lilitokea tetemeko la ardhi chini ya Bahari Hindi karibu na pembe ya kaskazini ya Sumatra kwenye mstari ambako bamba la Uhindi linajisukuma chini ya bamba ndogo la Burma Siku ile km za pembizo la bamba la Uhindi zilisogea mbele katika muda wa dakika chache kwa urefu wa takriban m chini ya bamba la Burma Bamba la juu lilisukumwa na kupaa juu hadi mita Mshtuko huu ulianzisha wimbi kubwa chini ya bahari lililotokea juu kwa umbo la tsunami lililoua takriban watu

Katika maji marefu ya bahari wimbi halikuwa na hasara likaonekana kuwa na cm pekee Lakini ilifika mwambaoni kwenye maji kama likaanza kupaa juu kufikia hadi m

Kutoka kitovu cha tetemeko la ardhi mawimbi ya tsunami yalienea kote Yalipiga vikali sana pwani za Indonesia Sri Lanka Thailand na India Mawimbi yalifikia hadi pwani la Afrika na kusababisha vifo katika Somalia Kenya Tanzania na Afrika Kusini

Madhara ya ongezeko la joto Duniani

Bahari
Tsunami